cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 96,456
- 156,324
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pole sanaSiku tatu hizi hajarudi anapoishi, wamemtafuta simu hapatikani, kazini kwake nao hawampati mwisho akakutwa mortuary hafai Aliopolewa akiwa tayari kaenda.
Unajua nilivyopata taarifa ya ile ajali mida ya asubuhi nilishinda siku yote najisikia hatia, mpaka nakajiuliza kwanini lakini sikupata jibu. Nikawa najisikia vibaya tu na uzito ndani yangu.
Tumekua wote, tumecheza wote, tumekula wote, moments nyingi tumeshea tukiwa karibu, tabasamu lake, ni mtu asiyejua kukasirika labda awe pissed off kwa sana, mizaha na utani wake. 30 good years tupo wote, now mwendo kaumaliza.
Mtu mnaongea mnacheka muda wote, anakwambia baadae basi kumbe ndio kwaheri. Hakujua nini kitatokea usiku ule, hakuna aliyejua ile barabara na kituo ndio njia ya uelekeo kazini. Akajikuta mmoja wa wahanga bila kutarajia. Sitamuona tena! Waliosema hakuna ajuae kesho yake hawakukosea!
Ushauri: Ishini kwa upendo sana guys, kuwa chanzo cha furaha na tabasamu kwa wote unaokutana nao. Usimdharau mtu yeyote, alienacho asie nacho wote wape heshima.
Usijivune.
Usipungukiwe upendo.
Usimsahau Mwenyezi Mungu.
Moyo wangu unauma.