Ajali ya MV Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe bado Mawaziri?

Ajali ya MV Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe bado Mawaziri?

Ni kweli kwa sababu Kangi Lugola, Jenista ni Captains wa MV Nyerere
Hata Alhaj Ali hassan Mwinyi alimuandikia barua J.K Nyerere mwaka 1976 kujiuzulu baada ya kutokea mauaji shinyanga maana yeye ndio aliyetekeleza hayo mauaji au siyo Troll?
 
Mkuu ni bora sana kueshimu taalamu sio kwa kuwa wewe mwana siasa ndio ukajiona bora na mwenye akili hata kwa fani usizozijua kusema watu wamesitisha uokoaji kwa ajili ya giza ni nonsense huwatendi haki if you don't know nothing kwenye rescue at sea bora ukae kipya ni kweli tuna jeshi la uokozi lakini uokozi wa nini? rescue at sea ni tafauti sana na rescue za aridhini je kuna sheria au taasisi mahususi ya ukoaji wa majini tz na kama hakuna nyie kam wabunge mmechukua hatua gani?
 
Ajali ya Mv Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe Bado mawaziri?

Ni masikitiko makubwa kwamba, Serikali ya wanyonge imeokoa mtu mmoja, wakati wananchi wenyewe wameweza kuokoa watu 40..... hii ni aibu kubwa sana. Watu 225 wamepoteza maisha sababu ya uzembe.

Tuache kujidanganya na mapenzi ya Mungu. Mungu katupa akili, namna ya kuzitumia ni sisi wenyewe. Huwezi kupata Habari ya ajali saa nane mchana halafu ukaitisha Kamati ya Usalama mkoa saa 11 jioni ( yaani mwendo wa Dreamliner Dar-Mwanza mara 4 ). Rais naye hakuitisha Cabinet ya dharura wala Baraza la Ulinzi na Usalama Taifa kuratibu uokoaji. Uokoaji unasitishwa sababu ya GIZA? Tukihoji mnasema tunaleta Siasa? Nonsense!

Kwa nchi zilizoendelea Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Waziri wa Ujenzi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu walitakiwa wawe wamekwishafutwa kazi au wamejiuzulu wenyewe.

Miaka 57 baada ya uhuru...Jeshi la uokozi linapoishia kuwa jeshi la UOPOZI, ni wakati wa rafiki nyangu Kangi Lugola kupumzika. Waziri Kamwelwe, Jenista na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wanapaswa kufukuzwa kazi mara moja. Bahati mbaya sana Rais amechoka na hivyo hajali tena. Wazembe Ndio wameongoza mazishi ya ndugu zetu leo.
Nasikitika sana kiongozi mkubwa kama wewe huna ufahamu jinsi gani Kamati za maafa zinavyofanya kazi au labda unaenjoy kukashifu Serikali na kuichonganisha Serikali na wananchi.

Naomba nikuulize maswali muhimu kwa niaba ya umma wa wapenda ukweli.

1-Unafahamu kamati ya maafa ya mkoa inaundwa na nani ?Mwenyekiti wa kamati hiyo ni nani?wajumbe wake ni kina nani?

2-Unafahamu ni wakati gani au kwa tukio gani kamati ya maafa ya wilaya inaitishwa?

3-Unafahamu ni wakati gani kamati ya maafa ya mkoa inaitishwa au kwa lugha ya kitaalamu inakuwa activated?
4-Je ni wakati upi kamati ya maafa ya kitaifa inaitishwa?kwa vigezo vipi?
unawafahamu wajumbe wake?
Furthemore bwana mdogo Zitto
5-Unafahamu ni wakati gani kamati za maafa za kikanda au kimataifa zinaundwa?ni matukio ya aina gani yana-activate kamati tajwa?

Acha kupotosha umma kijana huu sio ushabiki wa liverpool na Southampton haya ni maafa na Taifa lipo msibani...
Eti unasema Serikali imeokoa mtu mmoja tu?...Hii ni insanity....hivi watu walinusurika walitibiwa na yule babu yako unayetishiaga naye watu au ACT Wazalendo?

Zitto do you know ABCs za uokoaji kwenye maji?Je una thamini usalama wa wataalamu wa uokozi au wataalamu wa kukabiliana na majanga?
Kwa nini basi kama uliona mambo hayaendi vizuri hukutoka huko majuu ulipo ili kuja kusaidia uokoaji Gizani?

Hivi Zitto nikuulize je pale Katika jimbo lako au wilaya yako wewe sio mjumbe wa kamati ya maafa ya wilaya au hata mkoa wenu? Je hufahamu au hujawahi kuhusishwa kwenye Maandalizi ya Disaster Management and preparedness.
Hakuna contigency plan ya kupambana na majanga katika wilaya yako?

Kama ipo kwa nini unaisema Serikali ni zembe?

Kama hakuna je tukulaumu kwa kukaa kimya?

Zitto ni kama vile unalazimishia kukamatwa na kuhojiwa ili upate kiki ya aina mpya yaani eti umekamatwa kwa kuhoji...huu ni utoto na sio siasa bali ni ubaradhuli na roho mbaya kwa wafiwa na waathirika wa tukio hili.

Hivi ukihojiwa na sisi wananchi utupe makosa specific kwa kila unayemlaumu utaweza kujibu?

Nakushauri utulie na usisake kiki ya kisiasa ...wananchi wa Ukara ndio wanaojua kilichotokea ...wanaelewa uzembe upo wapi na wanajua nani awajibike ndio maana kwa sasa wapo msibani na wanaomboleza.

You have been shifting your line of attack yaani mara urukie kwa Rais,Mara JWTZ,Mara mawaziri Mwisho utataka hadi kumtusi Mwenyezi Mungu.

Zitto hebu tumia busara kidogo na ujaribu kukumbuka tweet yako mojawapo ya tarehe 1 juni 2014 na ulinganishe walioyasema watanzania siku hiyo kwako na kwa umma.
Ukiikumbuka siku hii vyema basi utaelewa thamani ya Mtu mmoja kuokolewa na Serikali.
 
Uongo wa huyo jamaa upo wapi? Je si kweli kuwa wananchi waliokoa wahanga wengi zaidi? Tujibu hoja badala ya kumshambulia mtoa hoja..
 
Uongo wa huyo jamaa upo wapi? Je si kweli kuwa wananchi waliokoa wahanga wengi zaidi? Tujibu hoja badala ya kumshambulia mtoa hoja..
Kuna janga lolote duniani ambalo wananchi hawashiriki na kuokoa wahanga wengi zaidi ya Serikali?Tupe mfano.
 
Live TBC jioni ya leo,Kuna kauli katoa waziri uchukuzi,wakiwa na CDF,sio njema kabisa .... Shughuli inagaramiwa na serikali,vifaa nk asiwepo yeyote wa kudai malipo huduma yeyote hata cent....!!!! ....mfano mtambo kufua upepo umeletwa Jeshi!!!!....serikali mkoa na kuu tumejipanga vizuri...... Sijui lugha hii ya kibabe kaitoa wapi!!! Nijuavyo katika janga tunathamini msaada wowote kwa garama yeyote ili mradi kuokoa maisha kwanza.
 
Lengo la zitto ni kutaka akamatwe au ajibiwe na serikali ili apate kiki. Bahati mbaya haitakua hivyo.
Nashukuru wananchi tumeanza kulitambua hili. Jamaa anafanya kila awezalo akamatwe.
Alafu pia inafurahisha anadai uhuru wa kujieleza umebanwa.
 
Hakuna wa kumzuru huyu, lakini anachokifanya ni kutumia huu msiba kuiprovoke Serikali ili aakamatwe and it is for his own gain, political stunts, and nothing else, vijana wa umri wake Europe wapo busy kubuni vitu vya msingi kwa ajiri ya Nchi zao, yeye yupo busy kuitumia elimu yake na akili yake kupigania Maslahi ya tumbo lake!
Mkuu tupe vitu hapa, Zitto anaelimu gani
 
Masikini Tanzania.
System yote imeparalyze inasubiri rais aseme nini kifanyike, rais akiona easy na watendaji nao wanaona easy hadi wamezika watu kwenye mabanzi waliyoyafunika kwa mashuka.
Na waziri mkuu kasema pesa mnazochanga kwa ajili ya rambirambi zitatumika kugharamia mnara wa kumbukumbu hapo ziwani.
 
Mi nadhan badala ya kuwataka wakina kangi na wenzake kujiuzuru huu ungekuwa muda sasa wa kujitathmini nini tufanye kama taifa kukabiliana na majanga kabla na baada ya kutokea
 
Watu 100 * 2 si mchezo tukumbuke wanaokufa kwenye majanga haya wana wategemezi lundo ingekuwa busara sasa kuangalia namna ya kuwasupport
 
Mkuu wa Mkoa anapaswa kuwajibika kwa majibu zake zisizo
ridhisha wala kufufua Mishipa yetu inayovuja damu ya kupoteza Ndugu zetu!
 
Mkuu ni bora sana kueshimu taalamu sio kwa kuwa wewe mwana siasa ndio ukajiona bora na mwenye akili hata kwa fani usizozijua kusema watu wamesitisha uokoaji kwa ajili ya giza ni nonsense huwatendi haki if you know nothing kwenye rescue at sea bora ukae kipya ni kweli tuna jeshi la uokozi lakini uokozi wa nini? rescue at sea ni tafauti sana na rescue za aridhini je kuna sheria au taasisi mahususi ya ukoaji wa majini tz na kama hakuna nyie kam wabunge mmechukua hatua gani?
Dah kweli kuna watu mna roho mbaya yaani ww huelewi ata ni nn kimetokea umeamua kutetea tu,ipo siku zamu yako wataahirisha kukuokoa namuomba Mungu kesho yake uokolewe ukiwa hai apo nadhani utaijua thamani ya uhai, yaani uzembe wote huo tokea usimamizi wake mpka janga lenyewe na uokoaji wa kizembe kabisa huoni?
 
Back
Top Bottom