Ajali ya MV Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe bado Mawaziri?

Ajali ya MV Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe bado Mawaziri?

Watu 100 * 2 si mchezo tukumbuke wanaokufa kwenye majanga haya wana wategemezi lundo ingekuwa busara sasa kuangalia namna ya kuwasupport
Ndugulai mpka saiv wameshavuka iyo number saivi ni 200+, na kuhusu wategemezi kuna mamlaka naona imeamua laki tano zitolewe kwao, ni mpka pale watakapo waza haya yangetokea kwao wenyewe nadhani ndo wangeyatenda kwa uzalendo wanao utaja taja kirahisi tu, watanzania kuna mindset ya kipuuzii sana inakuaa kwa speed
 
Ajali ya Mv Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe Bado mawaziri?

Ni masikitiko makubwa kwamba, Serikali ya wanyonge imeokoa mtu mmoja, wakati wananchi wenyewe wameweza kuokoa watu 40..... hii ni aibu kubwa sana. Watu 225 wamepoteza maisha sababu ya uzembe.

Tuache kujidanganya na mapenzi ya Mungu. Mungu katupa akili, namna ya kuzitumia ni sisi wenyewe. Huwezi kupata Habari ya ajali saa nane mchana halafu ukaitisha Kamati ya Usalama mkoa saa 11 jioni ( yaani mwendo wa Dreamliner Dar-Mwanza mara 4 ). Rais naye hakuitisha Cabinet ya dharura wala Baraza la Ulinzi na Usalama Taifa kuratibu uokoaji. Uokoaji unasitishwa sababu ya GIZA? Tukihoji mnasema tunaleta Siasa? Nonsense!

Kwa nchi zilizoendelea Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Waziri wa Ujenzi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu walitakiwa wawe wamekwishafutwa kazi au wamejiuzulu wenyewe.

Miaka 57 baada ya uhuru...Jeshi la uokozi linapoishia kuwa jeshi la UOPOZI, ni wakati wa rafiki nyangu Kangi Lugola kupumzika. Waziri Kamwelwe, Jenista na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wanapaswa kufukuzwa kazi mara moja. Bahati mbaya sana Rais amechoka na hivyo hajali tena. Wazembe Ndio wameongoza mazishi ya ndugu zetu leo.
utawala wa sheeria
 
Ajali ya Mv Nyerere: Kangi, Jenista na Kamwelwe Bado mawaziri?

Ni masikitiko makubwa kwamba, Serikali ya wanyonge imeokoa mtu mmoja, wakati wananchi wenyewe wameweza kuokoa watu 40..... hii ni aibu kubwa sana. Watu 225 wamepoteza maisha sababu ya uzembe.

Tuache kujidanganya na mapenzi ya Mungu. Mungu katupa akili, namna ya kuzitumia ni sisi wenyewe. Huwezi kupata Habari ya ajali saa nane mchana halafu ukaitisha Kamati ya Usalama mkoa saa 11 jioni ( yaani mwendo wa Dreamliner Dar-Mwanza mara 4 ). Rais naye hakuitisha Cabinet ya dharura wala Baraza la Ulinzi na Usalama Taifa kuratibu uokoaji. Uokoaji unasitishwa sababu ya GIZA? Tukihoji mnasema tunaleta Siasa? Nonsense!

Kwa nchi zilizoendelea Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Waziri wa Ujenzi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu walitakiwa wawe wamekwishafutwa kazi au wamejiuzulu wenyewe.

Miaka 57 baada ya uhuru...Jeshi la uokozi linapoishia kuwa jeshi la UOPOZI, ni wakati wa rafiki nyangu Kangi Lugola kupumzika. Waziri Kamwelwe, Jenista na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wanapaswa kufukuzwa kazi mara moja. Bahati mbaya sana Rais amechoka na hivyo hajali tena. Wazembe Ndio wameongoza mazishi ya ndugu zetu leo.
Mkuu ZZK Navy iko chini ya Hussein Mwinyi,mbona umem skip ?
 
Hakuna hoja fikirishi hapa zaidi ya kutugeuza sisi wajinga, Huyu "Mpelesi" ni Mbunge, Kiongozi kila kitu anachofanya ni kwa Kodi yetu hata hii posti aliyotuma ametumia Kodi zetu, narudia Zitto ni Kiongozi Kama walivyo hao anaowataka wajiuzuru, ni ujinga kutuaminisha eti they are not part of this simply because they are from opposition, ukweli unabaki wote ni viongozi, Kama ni serikali imekwama yeye hawezi kujiondoa, unless otherwise aje hapa atueleze kwanini analipwa mshahara na Serikali!
Una hoja nyepesi hata robo kilo hazifiki yaani! Kwa hiyo hapo napo unasubiri bk 7? Fedha nyingine bora kununua kondom.
 
Hakuna wa kumzuru huyu, lakini anachokifanya ni kutumia huu msiba kuiprovoke Serikali ili aakamatwe and it is for his own gain, political stunts, and nothing else, vijana wa umri wake Europe wapo busy kubuni vitu vya msingi kwa ajiri ya Nchi zao, yeye yupo busy kuitumia elimu yake na akili yake kupigania Maslahi ya tumbo lake!
Wewe hadi umri huo wa uzeeni umeifanyia nini Tanzania???
 
1, Na swali ile ajari ya Moto iliyotokea kwenye ile nnchi ya ulaya mawazili walijiuzuru? Au mamlaka husika inayosimamia?
2, Jitaidi utumie ujana wako kama kweli unawapenda Watanzania vijana waweze kupata fursa za ajira au buni kitu cha msingi umekaa attention mda wote kukosoa ni sawa na unajikita kutafuta mabaya ya mwenzio kwa staili hii tutafika? Ndo maana wabongo wamtoendelea
3, waliosababisha ajali ni Mawazili? au mamlaka husika ndo washughulikiwe?Aseee kuwa Makini
Hizo ni siasa tu,hamna kitu
Huyo Mwenyekiti wa bodi aliyefukuzwa alikuwa Ukara?
 
Hakuna hoja fikirishi hapa zaidi ya kutugeuza sisi wajinga, Huyu "Mpelesi" ni Mbunge, Kiongozi kila kitu anachofanya ni kwa Kodi yetu hata hii posti aliyotuma ametumia Kodi zetu, narudia Zitto ni Kiongozi Kama walivyo hao anaowataka wajiuzuru, ni ujinga kutuaminisha eti they are not part of this simply because they are from opposition, ukweli unabaki wote ni viongozi, Kama ni serikali imekwama yeye hawezi kujiondoa, unless otherwise aje hapa atueleze kwanini analipwa mshahara na Serikali!

Kama hoja ni kulipwa mshahara na serikali vipi walimu,manesi, madaktari, wao wamehusikaje katika hii ajali? Mkuu ungejenga hoja nzuri kumpinga zzk si kihoja hiki cha kulipwa mshahara na serikali maana hata madereva wa serikali nao wanalipwa na serikali japo sioni kwa vipi wanahusika na hii ajali.
 
Hakuna hoja ya msingi

Nahodha kamkabidhi Chombo day worker Waziri anahusikaje?
Hata Yeye Zitto Basi angejiuzulu Kwa Matokeo ya chama chake 2015
Nani kakwambia ni day worker? Kumbe na wewe ni walewale mnaoshadadia utetezi wa kijinga kama huo wa kujificha kwenye shamba la karanga? Kwa taarifa yako aliyeendesha kivuko ndiye nahodha wa siku zote ila alikuwa amesimamishwa kwa takribani miezi minne kwa tuhuma (za kimahusiano) na akaletwa huyo mnayedanganywa ndiye nahodha.
 
Nasikitika sana kiongozi mkubwa kama wewe huna ufahamu jinsi gani Kamati za maafa zinavyofanya kazi au labda unaenjoy kukashifu Serikali na kuichonganisha Serikali na wananchi.

Naomba nikuulize maswali muhimu kwa niaba ya umma wa wapenda ukweli.

1-Unafahamu kamati ya maafa ya mkoa inaundwa na nani ?Mwenyekiti wa kamati hiyo ni nani?wajumbe wake ni kina nani?

2-Unafahamu ni wakati gani au kwa tukio gani kamati ya maafa ya wilaya inaitishwa?

3-Unafahamu ni wakati gani kamati ya maafa ya mkoa inaitishwa au kwa lugha ya kitaalamu inakuwa activated?
4-Je ni wakati upi kamati ya maafa ya kitaifa inaitishwa?kwa vigezo vipi?
unawafahamu wajumbe wake?
Furthemore bwana mdogo Zitto
5-Unafahamu ni wakati gani kamati za maafa za kikanda au kimataifa zinaundwa?ni matukio ya aina gani yana-activate kamati tajwa?

Acha kupotosha umma kijana huu sio ushabiki wa liverpool na Southampton haya ni maafa na Taifa lipo msibani...
Eti unasema Serikali imeokoa mtu mmoja tu?...Hii ni insanity....hivi watu walinusurika walitibiwa na yule babu yako unayetishiaga naye watu au ACT Wazalendo?

Zitto do you know ABCs za uokoaji kwenye maji?Je una thamini usalama wa wataalamu wa uokozi au wataalamu wa kukabiliana na majanga?
Kwa nini basi kama uliona mambo hayaendi vizuri hukutoka huko majuu ulipo ili kuja kusaidia uokoaji Gizani?

Hivi Zitto nikuulize je pale Katika jimbo lako au wilaya yako wewe sio mjumbe wa kamati ya maafa ya wilaya au hata mkoa wenu? Je hufahamu au hujawahi kuhusishwa kwenye Maandalizi ya Disaster Management and preparedness.
Hakuna contigency plan ya kupambana na majanga katika wilaya yako?

Kama ipo kwa nini unaisema Serikali ni zembe?

Kama hakuna je tukulaumu kwa kukaa kimya?

Zitto ni kama vile unalazimishia kukamatwa na kuhojiwa ili upate kiki ya aina mpya yaani eti umekamatwa kwa kuhoji...huu ni utoto na sio siasa bali ni ubaradhuli na roho mbaya kwa wafiwa na waathirika wa tukio hili.

Hivi ukihojiwa na sisi wananchi utupe makosa specific kwa kila unayemlaumu utaweza kujibu?

Nakushauri utulie na usisake kiki ya kisiasa ...wananchi wa Ukara ndio wanaojua kilichotokea ...wanaelewa uzembe upo wapi na wanajua nani awajibike ndio maana kwa sasa wapo msibani na wanaomboleza.

You have been shifting your line of attack yaani mara urukie kwa Rais,Mara JWTZ,Mara mawaziri Mwisho utataka hadi kumtusi Mwenyezi Mungu.

Zitto hebu tumia busara kidogo na ujaribu kukumbuka tweet yako mojawapo ya tarehe 1 juni 2014 na ulinganishe walioyasema watanzania siku hiyo kwako na kwa umma.
Ukiikumbuka siku hii vyema basi utaelewa thamani ya Mtu mmoja kuokolewa na Serikali.
Mkuu tusaidie majibu hayo maswali ili nasisi tujue..
 
Hakuna hoja fikirishi hapa zaidi ya kutugeuza sisi wajinga, Huyu "Mpelesi" ni Mbunge, Kiongozi kila kitu anachofanya ni kwa Kodi yetu hata hii posti aliyotuma ametumia Kodi zetu, narudia Zitto ni Kiongozi Kama walivyo hao anaowataka wajiuzuru, ni ujinga kutuaminisha eti they are not part of this simply because they are from opposition, ukweli unabaki wote ni viongozi, Kama ni serikali imekwama yeye hawezi kujiondoa, unless otherwise aje hapa atueleze kwanini analipwa mshahara na Serikali!
Kwa hiyo unajua wapinzani wanakusanya kodi za wananchi ili wazitumie kuleta maendeleo?
 
Nani kakwambia ni day worker? Kumbe na wewe ni walewale mnaoshadadia utetezi wa kijinga kama huo wa kujificha kwenye shamba la karanga? Kwa taarifa yako aliyeendesha kivuko ndiye nahodha wa siku zote ila alikuwa amesimamishwa kwa takribani miezi minne kwa tuhuma (za kimahusiano) na akaletwa huyo mnayedanganywa ndiye nahodha.

Mbona hiyo taarifa yako nayo Ni nyepesi Kama Yangu Kwa Kuwa haijaambatana Na ushahidi zaid ya blaa blaa tu
 
Duh,kwa akili hizi acha tuendelee kuwa mazuzu daima
Sijakuelewa mazuzu kwa namna ipi,kama mtu unashindwa kuongea vizuri basi bora kuwa Mtulivu tu yani bora kunyamaza tu maana sipendagi Matusi hayo ni mawazo yangu nayaheshimu Mwenyewe kadri ya mtazamo Wangu
 
Kujiuzulu ni njia moja katika nyingi za kuonesha uwajibikaji ila sio njia pekee; hivyo sio lazima kila linapotokea janga basi kila mhusika ajiuzulu.
 
Kwa nn hampend kukosolewa nyie ccm? Mbona mkisifiwa huwa mnafurai sana? Kwan mwinyi alivyo jiudhuru kwa mauaji yaliyo fanywa na polisi kipind akiwa wazir wa mambo ya ndan alikua ameusika na mauaji? Kujiudhuru ni kuonyesha uajibikaji tuu...mm siungi mkono wajiudhuru sema nlitaka kuweka kumbu kumbu sawa pale unapotaka kutuaminisha watu wanajiudhuru kwa kuusika moja kwa moja ila sio lazma wauske moja kwa moja
Unajuaje kama mimi Ni ccm au sio ccm na swala la ccm limeingiaje hapa Wakati tunajadili hii Mada
 
Nani kakwambia ni day worker? Kumbe na wewe ni walewale mnaoshadadia utetezi wa kijinga kama huo wa kujificha kwenye shamba la karanga? Kwa taarifa yako aliyeendesha kivuko ndiye nahodha wa siku zote ila alikuwa amesimamishwa kwa takribani miezi minne kwa tuhuma (za kimahusiano) na akaletwa huyo mnayedanganywa ndiye nahodha.
Nenda mahakamani uwashitaki wanaosema uongo kwa vile wewe unaujua ukweli..
 
Back
Top Bottom