TANZIA Ajali yaua 5 na kujeruhi 36 Shinyanga

Nasema Uongo Ndugu Zangu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
279
Reaction score
779
Breaking News

Watu watano wamepoteza maisha hapo hapo na wengine 36 wamejeruhiwa vibaya kwenye ajali iliyohusisha basi la kampuni ya Najmunisa T 413 DAY kugongana uso kwa uso na Fuso T 123 DJH katika eneo la Ibadakuli Shinyanga.

Mzee Kinana kama nakuona vile

Chanzo: ITV

====

Update

Watu watano wamepoteza maisha na wengine 36 kujeruhiwa vibaya katika ajali iliyohusisha basi la Kampuni ya Najmunisa T 413 DAY kugongana uso kwa uso na Fuso T 123 DJH katika eneo la Ibadakuli Shinyanga, leo Septemba 3, 2022.-

Majeruhi wote wamekimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga na miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Leonard Nyandahu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Taarifa zaidi kuhusu ajali hii zitazidi kukujia.
 
What a pitful loss.

Mungu awapokee marehemu wetu.

nimeshangazwa kuona umemalizia post yako in bias manner. Ina maana zile ajali nyingi za kutisha huko nyuma zilitokea wakati Trafiki polisi hawapo barabarani?
 
What a pitful loss.

Mungu awapokee marehemu wetu.

nimeshangazwa kuona umemalizia post yako in bias manner. Ina maana zile ajali nyingi za kutisha huko nyuma zilitokea wakati Trafiki polisi hawapo barabarani?
Endeleeni kusubiri
 
Ajali imetokea lini na muda gani?

Kama ni usiku basi Kinana atoe tamko magari yasitembee usiku.
 
Trafiki sio suluhu ya ajali, huko barabarani kuna vipande vingi tu hawakai hao trafiki...

Mara nyingi sababu ya ajali za kugongana uso kwa uso ni uzembe katika kuendesha au mechanical failure, hivi vitu havizuiwi na uwepo wa askari barabarani bali uduni wa mifumo ya ukaguzi
 

Polisi traffic mnaonekana mnavyorukaruka kwa furaha. Lini mlieahi kuzuia ajali ipi?
 
Hilo basi laonekana bovu
Malori yatafutiwe sehemu ya kupita
 
Ulipomuhusisha tu kinana na ajari nikaacha kusoma huo utumbo....🙄🙄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…