Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
😂😂😂😂😂 hapo inakuwa jino kwa jino dereva kashapagawa anataka amuwahi mkewe ww unaleta mambo ya kitotoMadereva wa malori ni wababe si mchezo japo madereva wa mabasi nao ni watu wa kuforce sana wakiwa barabarani.
Dereva wa bus anaona kabisa gari la mbele yake limekaribia lakini anavuta moto hadi apenye sasa wakati mwingine hesabu zinafeli tena akikutana na wa lori ndo kabisa wa roli anaweza kuona mwenzake kapiga hesabu vibaya lakini anakanyaga moto wakutane au bus lipenye kwa shida ilimradi liwalo na liwe yaan ni jeuri kweli kweliqs
Hizo Gari madereva wake huwa wanalaana fulani.Fuso
Hamna bifu mkuu wangu! Ni uzembe tu..Hili bifu la madreva mabasi na Malori litaisha lini kwenye hizi highway[emoji848][emoji22]
wazee wa kafara walikua mzigoni. 😎Mabasi yanasifa sana anakuletea bodi ili umpisha sasa akikutana na dereva kichaa ndio haya yanatokea huwa always wanaharaka na wanafhani wana hatimiliki ya barabara
Yani uso kwa uso useme ni udhembe !!!????
binafsi nasema wazee wa kafara walikua mzigoni.
Trafiki sio suluhu ya ajali, huko barabarani kuna vipande vingi tu hawakai hao trafiki...
Mara nyingi sababu ya ajali za kugongana uso kwa uso ni uzembe katika kuendesha au mechanical failure, hivi vitu havizuiwi na uwepo wa askari barabarani bali uduni wa mifumo ya uukagu
Nashukuru mkuu nimefika salama nimeanza safari SAA 3 asubuhi na nimeingia DAR SAA 12 jioni...Safiri salama ukirudi Dom tutafutane, mi ntaenda jumanne Dar, kikubwa Dua na TOBA
Pamoja mkuu hata hivyo nimefika salama nashukuru MUNGUUsiogope Muamini Mungu ,ajali nyingi zinasababishwa na nguvu za Giza ajali halisi aiwezi kuuwa inajeruhi tu,Mungu sio katili kama wengi wanavyofikiri.kwenye basi inahitajika mwenye mamlaka mmoja tu dhidi ya nguvu za Giza ajali haiwezi kutokea .Muamini Mungu utabaki salama.Zaburi 91:3,16 .Mimi nasafiri Kila week mara mbili safari za dar -mwz-arsh lazima nifike namjua Mungu ninaye mwamini.
Magari ya serikali ndiyo balaa hawa madereva wanachojua ni kukanyaga Tu mafutaTena iyo njia ya Dom to Dar ...Ni balaa naa nusu ..inakuwaga na ajali Sana.
Ulifika salama?Ninasoma habari hii nikiwa hapa Dodoma nikianza safari ya kuelekea DAR hakika hizi safari ndefu ni MUNGU mwenyewe Tu anahitajika....namwomba MUNGU anifunike Kwa mikono yake na mimi
Nimefika salama nashukuru MUNGU nikiwa na familia yangu wote tumefika poa kabisaaUlifika salama?
Breaking News
Watu watano wamepoteza maisha hapo hapo na wengine 36 wamejeruhiwa vibaya kwenye ajali iliyohusisha basi la kampuni ya Najmunisa T 413 DAY kugongana uso kwa uso na Fuso T 123 DJH katika eneo la Ibadakuli Shinyanga.
Mzee Kinana kama nakuona vile
Chanzo: ITV
====
Update
Watu watano wamepoteza maisha na wengine 36 kujeruhiwa vibaya katika ajali iliyohusisha basi la Kampuni ya Najmunisa T 413 DAY kugongana uso kwa uso na Fuso T 123 DJH katika eneo la Ibadakuli Shinyanga, leo Septemba 3, 2022.-
Majeruhi wote wamekimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga na miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Leonard Nyandahu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Taarifa zaidi kuhusu ajali hii zitazidi kukujia.
Umenikumba Jana tupo kwenye Costa ya abiria aisee ilipita tanker moja ina over take , adi nikaogopa ,nadhani ilikuwa empty inawahi mzigo uko daresalamu.Omba usikutane na Tanker inawahi beba mzigo na dereva ana kimeo cha deni la mafuta