Sehemu za kivuko wanawekaga alama!Hata kuweka tuta moja sehemu hatarishi ni mpaka watu wafe na waandamane
Samahani Naomba Uzi huo niusome kiungoziyAsije yakamkuta kama ya ile story tuliokuwa tunasoma humu jf,jamaa wakazurumiwa mali na baba mkubwa mwisho wa siku kijana mkubwa akawa jambazi
Kama Mkono wa MUNGU umeweza kumuokoa huyu mtoto bas hakika najua atakuja kuwa na mafanikio ingawa atapitia changamoto nyingi sana.Watu wawili mke na mume wamefariki dunia kwenye ajali iliyohusisha gari ndogo na treni katika makutano ya reli, Kata ya Tambukareli, Dodoma.
Akizungumzia marehemu hao Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Ibenzi Ernest amesema walipokea mwili wa mwanamke Furaha Rashid huku mume wake Hussein Chilala akiwa katika hali mbaya.
“Ilikuwa majira ya saa tatu usiku mwanamke tulimpokea akiwa tayari amefariki, lakini mwanaume alikuwa na hali mbaya na wakati anapatiwa huduma akafariki muda mfupi baadaye,” amesema Ibenzi.
Ibenzi amesema marehemu waliumia zaidi kichwani hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kupoteza maisha.
Hata hivyo, katika ajali hiyo ambapo marehemu walikuwa na mtoto wao anayekadiriwa kuwa na mwaka mmoja, Ibenzi amesema walimpokea mtoto huyo akiwa mzima na alisema amechukuliwa na mama yake mdogo kwani hakuumia sehemu yoyote.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema atamrudia mwandishi baada ya kumaliza kikao.
MWANANCHI
Kweli kabisa hawanaga jema wanajiangalia wao tu na familia zaoKapoteza ndoto zake zote,waliobaki watagawana kila kitu na kumsahau dogo
Halafu hii Njia ndio Kuelekea Zile Nyumba Walipo Wabunge na baadhi ya MawaziriTena sikuiz Kuna automated system za kila namna... ndio hivo tena labda kiongozi mkubwa yamkute ndio tupate hiyo neema...
Eeh! AC ni Ulimbukeni Kumbe?Watu wengi ulimbukeni wa AC kwenye Gari ndiyo unawaponzaga! Hata Kama kuna hatari mbele,hata wakipigiwa kelelee hawasiki maana vio vyote vimefungwa hadi juu!!
Dah! Jumbe Kama hizi Zinanitisha! Namuangalia Dogo tu HapaMtoto huenda asikatize miaka 5 mana wataona ni kero.
Wazazi tujitahidi kuwa makini barabarani
Innah lillah waina ilayh rajioonEngineer Hussein chilala na mkewe wote wamefariki. Wameacha kichanga chao, inauma sana
Hiyo ni ajali ndugu ya usije ukashanga na wewe ukafa kwa ajali ya train hiyo hiyo mungu hadhihakiwiHawa wanao kufa kwa kugonga treni wana kufaga kwa ujinga wao tu na mahalaka ya kijinga
Huo ndo uhalisia, Afrika ukifa ndo imekula kwako labda Babu yake awe tajiriDah! Jumbe Kama hizi Zinanitisha! Namuangalia Dogo tu Hapa
Haya maisha kuna wakati yanaumiza na kutafakarisha sana.Engineer Hussein chilala na mkewe wote wamefariki. Wameacha kichanga chao, inauma sana
Acha tu maisha bana haya eleweki.Jamaa kavuta gar na wife na mtt tayr kumbe ndo history inashia hapo.Haya maisha kuna wakati yanaumiza na kutafakarisha sana.
Seems jamaa ndiyo alikuwa ameshaji-set aanze kula mema ya nchi lakini ndani ya dakika tu amepotea na mpendwa wake,Mungu awarehemu marehemu hako katoto akalinde kakue salama hakuna lingine tunaweza kusema kwa sasa.
Mwamba alichomoka salama?Kuna ajali moja staff mwenzetu amebeba milipuko ya migodini(baruti na fataki zake) kwenye hilux halafu kagonga treni .Mungu saidia kichwa cha gari tu ndo kilibamizwa vilipuzi havikuguswa .
Kama vingepata friction na impact yoyote ingekuwa historia duniani , hiyo shimo ingechimbwa hapo ni balaa.
Hakutoka ,safari iliishia hapo hapoMwamba alichomoka salama?
Tatizo tunafunga vioo vyote ili tufaidi AC na hapo mziki upo sayti ya juu sana hio treni tutaisikia saa ngapKivuko cha reli sio siri kama ni driver makini unajua nini cha kufanya iwe treni ipo au haipo. Mtu anaesema treni imemshtukiza, na kelele na muungurumo wote ule sio rahisi uwe hujaskia unless hauko makini.
Siku hzi hayupoNimemsikia mwanasheria wa PT usalama barabarani akidai madereva wote nchini wawe wanatembea na vyeti vyao vya kuhitimu mafunzo ya udereva pamoja na leseni zao.
Tunakoelekea watataka watu tutembee na madaftari ya notisi za driving schools.
BTW😛ale Isaka (Bandari kavu) palikuwepo na kizuizi (barrier) pamoja na kibanda cha mfanyakazi anayefunga na kufungua barabara.
Na ukute ndani ya gari wameaachia sound kubwa!!Watu wengi ulimbukeni wa AC kwenye Gari ndiyo unawaponzaga! Hata Kama kuna hatari mbele,hata wakipigiwa kelelee hawasiki maana vio vyote vimefungwa hadi juu!!