Ajira 6,000 za walimu zagubikwa na utapeli. Waziri Ummy amuagiza Katibu Mkuu kufanya uchunguzi

Ajira 6,000 za walimu zagubikwa na utapeli. Waziri Ummy amuagiza Katibu Mkuu kufanya uchunguzi

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amesema kuna Watu wamejitokeza mitaani ambao wanawadanganya Walimu ambao hawajaajiriwa kuwa wanatakiwa kutoa Tsh. Milioni moja ili wapate ajira kwa haraka kwani nafasi hizo hazitatangazwa na Serikali bali zitatolewa kisirisiri.

Waziri Ummy ameyasema hayo mapema hii leo wakati akiwa katika ziara ya kikazi katika Shule ya Sekondari Zingibari Wilayani Mkinga, Tanga.

Waziri Ummy amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kufanya uchunguzi ili kujua kama Watu hao wapo ndani ya Wizara au nje na kuwachukulia hatua za kisheria haraka.

Ummy pia amesema ajira hizo zikiwa tayari basi watatangaza kwa utaratibu unaotakiwa na kila mmoja anayehitaji atafuata utaratibu na hakuna atakayependelewa.

Chanzo: MillardAyoUPDATES

Pia soma,
1. TAMISEMI ninyi ndio chanzo cha rushwa na utapeli ajira za walimu

2. Anton Mtweve ni nani huko TAMISEMI?

3. TAMISEMI: Acheni kuajiri kimya kimya, mchakato wa ajira 6000 za walimu ufanyike kwa uwazi
 
Rushwa lazima maana watu zaidi ya laki moja kugombea nafasi 6000 unategemea sampling gan kutumika! WTF.
 
Mama yangu anapenda ziara za Tanga huyu!

Mama Samia kama kuna kitu unatakiwa kupambana nacho kimoja wapo ni hii ya kila kiongozi kuweka kwao mbele. Awamu ya 5 viongozi walizoea sana makwao, Majaliwa na Magu walikuwa hawaishi Ruangwa na Chato respectively
 
Mama yangu anapenda ziara za Tanga huyu!

Mama Samia kama kuna kitu unatakiwa kupambana nacho kimoja wapo ni hii ya kila kiongozi kuweka kwao mbele. Awamu ya 5 viongozi walizoea sana makwao, Majaliwa na Magu walikuwa hawaishi Ruangwa na Chato respectively
Hakuna ubaya ila ziara zake ziwe na tija co aje ademke
 
Afanye kazi na atatue kero kimya kimya wananchi tutaona tu kuliko anaongea ongea lakini mabadiriko hatuyaoni mkuu.
Sasa huoni kwamba alivyoliweka public inasaidia zaidi kutatua hizo kero kuliko kukaa kimya? Akikaa kimya watendaji watamsikiaje?
 
Mama yangu anapenda ziara za Tanga huyu!

Mama Samia kama kuna kitu unatakiwa kupambana nacho kimoja wapo ni hii ya kila kiongozi kuweka kwao mbele. Awamu ya 5 viongozi walizoea sana makwao, Majaliwa na Magu walikuwa hawaishi Ruangwa na Chato respectively
Karibu Tanga Sheikh! Tanga ni kutamu kama sukari. Mkataa kwao ni mtumwa. Hata mama nae muda si mrefu atakuwa anaibukia Zenj!!
 
Huyu Waziri kila siku vyombo vya habari!, tunakoelekea itakuwa afadhari Jaffo.
Wewe vipi bhana!! Sasa watu wanatapeliwa kupitia kivuli cha Wizara yake, halafu unataka anyamaze tu kimya! Si huo utapeli utaonekana una ukweli ndani yake?
 
Hili suala wanapewa ajira kwa wanaojitolea tu ni rushwa hili mama angalia hili.inakuwaje mnasema ambao hawana ajira wajiajiri wenyewe.watu wamejiajiri wakisubiria ajira ,na sasa wanaambiwa ajira hakuna ila kwa wanaojitolea tu.hili suala litasababisha rushwa kufanyika.
 
Back
Top Bottom