Ajira Serikalini iwe miaka 10 tu, baada ya hapo watu wastaafishwe

Ajira Serikalini iwe miaka 10 tu, baada ya hapo watu wastaafishwe

Hacha kupoteza muda hicho kitu hakiwezekani, serikali haina hella ya kuwalipa na kwenye hesabu za uchumi hilo haliwezekani. Wewe tia juhudi na muombe Mungu upate ajira.
Inshallah nakubaliana na wewe. Ila avarice inalea adversity kwenye taifa na ndy chanzo cha rushwa, nyie ni kuwakomalia tu hadi kwenye makongamano ya vyuo vikuu mada itafika mtatambua uongozi tu.

Thank you Mtoa mada hii mada nimeipenda nitapita nayo hadi kwa walengwa wahanga wahitimu wa vyuo vikuu.

Si mnasema haliwezekani ngoja tu liwafikie gen Z, litawezekana tu.
 
Hakika watu tupeane nafasi za ajira bana watu wanakula cake 🍰 ya taifa wenyewe mtu anakaa miaka 30+ kazini wengine waajiriwe lini sasa 😡
serikali inapaswa kusimamia uwajibikaji ili kukuza ufanisi, ajira za serikali si kwa ajili ya kula keki ya taifa.

Huwezi kubadili wafanyakazi kila baada ya miaka 10 unaleta wapya, itakuwa nchi ya kipuuzi mno. Experience ndo kila kitu katika ufanisi. Ni usimamisi na uwajibikaji uongezwe.
 
Kwamba tusomeshe experts kwa kodi zetu na gharama kubwa ili waje watufanyie kazi kwa miaka kumi tu ili waingie wengine watumie miaka mitatu kupata experience ili baada ya miaka saba mingine waingie wengine ? Na hapo watakuwa pensionable au hatuwapi pensions ? Sababu mpaka dakika hii hata hizo pension zinapumulia mashine...

In short nishasema na kila siku nasema capitalism as we know it haiwezi kufanya kazi kwenye hii technological advancement ambapo nguvu kazi haina uhitaji tena we can create more with less manpower....
1730537682346.png
 
Hii kauli sitoiacha nitaplead sana tu na nitazisema waajiriwa wapewe mda specific wa kufanya kazi tupishane, we unataka kuhold possession kwa zaidi ya miaka 30+ kwani hiyo office ulijengewa wewe na familia yako?

If ni kwaajili ya public lets public be benefited kwa wote.

Kama ni uzoefu na utaalam ndy mana kuna interviews na selection ya wafanyakazi.

Kila mwenye criteria zinazohitajika kupata kazi apewe kazi kulingana na utaalam wake, tupishaneni kwenye hizo offices wote ni watanzania asee 🇹🇿
Do you have qualifications to serve in those public offices you're talking about?

Being in office for 30+ years is something fair,there is no way we invest on someone for 17+ years and you want them to produce for ten years only(never)

Acha ubinafsi man,muda wako utafika utapata na wewe ila sio uwe na chuki na waliopata kwamba itakusaidia kufika unapotaka.Maisha ni yako mwenyewe,ulitoka tumboni mwa mama yako mzazi mwenyewe bila kujua utakutana na wenzako(take this responsibility,there is no one coming to save you)
 
serikali inapaswa kusimamia uwajibikaji ili kukuza ufanisi, ajira za serikali si kwa ajili ya kula keki ya taifa.

Huwezi kubadili wafanyakazi kila baada ya miaka 10 unaleta wapya, itakuwa nchi ya kipuuzi mno. Experience ndo kila kitu katika ufanisi. Ni usimamisi na uwajibikaji uongezwe.

Kitu hamjaelewa ni kwamba tunachokitaka ni kuwe na muda maalumu wa kuwa katika office, baada ya hapo wale ambao wanakuwa wamestaafu na ujuzi mkubwa na utaalam wa kutosha katika hiyo sector wanaweza kupewa nafasi ya kuwa wakufunzi katika vyuo vyetu vikuu ili kuendelea kuzalisha wataalam wengine watakaotumika ndani ya nchi kwa maendeleo ya nchi.

Ila hapo ili upate nafasi ya kuwa mkufunzi lazma uwe na kitu kinaitwa legacy katika office uliyokuwa Unafanya kazi, uwe na umri usiozidi miaka 60-65. Zaidi ya miaka 70 we kapumzike nyumbani na wajukuu tu.

Tatizo ni kuweka mfumo utakaopunguza wimbi la unemployment japo huwezi kulimaliza kwa ukubwa wake kutokana na population ya nchi rasilimali pamoja na idadi ya wasomi unayozidi kuongezeka kila mwaka.

Tukubali tukatae lazma tuwe wabunifu katika kulikabili hili tatizo la unemployment ni janga la dunia ila Haifai kufumba macho katika hili.
 
Do you have qualifications to serve in those public offices you're talking about?

Being in office for 30+ years is something fair,there is no way we invest on someone for 17+ years and you want them to produce for ten years only(never)

Acha ubinafsi man,muda wako utafika utapata na wewe ila sio uwe na chuki na waliopata kwamba itakusaidia kufika unapotaka.Maisha ni yako mwenyewe,ulitoka tumboni mwa mama yako mzazi mwenyewe bila kujua utakutana na wenzako(take this responsibility,there is no one coming to save you)
I’m not avarice person I just need to find a good way for all of us, ila nimekuelewa mkuu it’s so fine, thank you 🙏🏻
 
Kwamba tusomeshe experts kwa kodi zetu na gharama kubwa ili waje watufanyie kazi kwa miaka kumi tu ili waingie wengine watumie miaka mitatu kupata experience ili baada ya miaka saba mingine waingie wengine ? Na hapo watakuwa pensionable au hatuwapi pensions ? Sababu mpaka dakika hii hata hizo pension zinapumulia mashine...

In short nishasema na kila siku nasema capitalism as we know it haiwezi kufanya kazi kwenye hii technological advancement ambapo nguvu kazi haina uhitaji tena we can create more with less manpower....
View attachment 3141346
Kwani huyo expert akifa dunia au nchi itasimama? Watu wanajipa umuhimu mno kwenye maisha... Walikuwepo mascientist mwenye akili na sasa hawapo na dunia inaendelea tu. Ajira ziwe za mikataba tu vijana nao wapate ajira.
 
At least
Kwani huyo expert akifa dunia au nchi itasimama? Watu wanajipa umuhimu mno kwenye maisha... Walikuwepo mascientist mwenye akili na sasa hawapo na dunia inaendelea tu. Ajira ziwe za mikataba tu vijana nao wapate ajira.
wewe umeongea fact ya maana mno kama wasipokuelewa na wewe there must be something wrong inside their medulla.
 
Kuna kada nyingine sio za kuongelea tu eti kwa sababu baba yako hana ajira

Madaktari bingwa wanapatikana kwa njia ngumu sana sio rahisi kuwastaafisha kwa miaka 10 tu kijana

thats wastage of precious materials

Mtaalam wa mionzi mfano yuko mmoja tu katika hospitali flani, umstaafishe ili iweje?

waalimu wa Sayansi hawatoshi kabisa huko katika idara za Elimu msingi na sekondari, bado uwastaafishe, ili iweje?

SERIKALI INAPASWA KUPAMBANA NA HILI TATIZO LA AJIRA KWA NAMNA YA TOFAUTI, sio hivi ulivyoandika
Hivi hapa Tanzania doctors wote wameajiriwa?
Je walimu wote wa sayansi wameajiriwa?
 
Kitu hamjaelewa ni kwamba tunachokitaka ni kuwe na muda maalumu wa kuwa katika office, baada ya hapo wale ambao wanakuwa wamestaafu na ujuzi mkubwa na utaalam wa kutosha katika hiyo sector wanaweza kupewa nafasi ya kuwa wakufunzi katika vyuo vyetu vikuu ili kuendelea kuzalisha wataalam wengine watakaotumika ndani ya nchi kwa maendeleo ya nchi.
Mkuu, Miaka 10 bado hajawa na ujuzi mkubwa. Ndo kaanza kuwa na manufaa katika sekta aliyopo. Daktari mwenye miaka 10 kazini bado kijana, ndo jamii inaanza kula matunda ya uwepo wake, huwezi mfananisha na daktari mwenye miaka 20/25 hadi 30 kazini. Haiwezekani kila baada ya miaka 10 tuna madaktari wapya. Halafu ualimu ni prof pia, ni utaalam pia kama utaalam mwingine.
Ila hapo ili upate nafasi ya kuwa mkufunzi lazma uwe na kitu kinaitwa legacy katika office uliyokuwa Unafanya kazi, uwe na umri usiozidi miaka 60-65. Zaidi ya miaka 70 we kapumzike nyumbani na wajukuu tu.
Umri wa kustaafu ni sahihi kuwa miaka 60 unless kuna ulazima sana.
Tatizo ni kuweka mfumo utakaopunguza wimbi la unemployment japo huwezi kulimaliza kwa ukubwa wake kutokana na population ya nchi rasilimali pamoja na idadi ya wasomi unayozidi kuongezeka kila mwaka.
Huwezi kuondoa tatizo la ajira kwa kuleta tatizo jingine kubwa zaidi. Halafu tatizo la ajira mbona bado, tunapoelekea litashamiri, subiri tech iongezeke Ai iingie kazini 100% . Utashuhudia ongezeko la ukosefu wa ajira.
Tukubali tukatae lazma tuwe wabunifu katika kulikabili hili tatizo la unemployment ni janga la dunia ila Haifai kufumba macho katika hili.
Ubunifu unahitajika ila si kwa kuondoa watendaji kila baada ya miaka 10. Tutazalisha jambo la ajabu hutoamini boss.
 
Kuna kada nyingine sio za kuongelea tu eti kwa sababu baba yako hana ajira

Madaktari bingwa wanapatikana kwa njia ngumu sana sio rahisi kuwastaafisha kwa miaka 10 tu kijana

thats wastage of precious materials

Mtaalam wa mionzi mfano yuko mmoja tu katika hospitali flani, umstaafishe ili iweje?

waalimu wa Sayansi hawatoshi kabisa huko katika idara za Elimu msingi na sekondari, bado uwastaafishe, ili iweje?

SERIKALI INAPASWA KUPAMBANA NA HILI TATIZO LA AJIRA KWA NAMNA YA TOFAUTI, sio hivi ulivyoandika
Watapewa mkataba mwingine kama kuna ulazima wa wao kuhitajika. Waende wakajiajiri sasa, walishapata mitaji
 
Back
Top Bottom