Ajira Serikalini iwe miaka 10 tu, baada ya hapo watu wastaafishwe

Ajira Serikalini iwe miaka 10 tu, baada ya hapo watu wastaafishwe

Kwani huyo expert akifa dunia au nchi itasimama?
Unaangalia mambo kwa mafungu.., jiulize kwanini tunasomesha watu kama Taifa ? Ili tuje tuwape pesa baadae au ili wakidhi haja fulani ? Kwahio tunasomesha waalimu madaktari n.k. au watendaji ili tu wapate pesa na sio kwamba kuna need fulani inayotakiwa ?

Pili unadhani kwanini umri wa pensheni, dunia nzima unaongezwa ?, Ni kwamba nguvu kazi inayochangia ni ndogo kuliko watu wanaopokea; Kwahio naweza kusema badala ya kuhangahika na kugawana kidogo kilichopo watu wenye busara wanawaza ni jinsi gani wanaweza kuongeza kilichopo...
Watu wanajipa umuhimu mno kwenye maisha... Walikuwepo mascientist mwenye akili na sasa hawapo na dunia inaendelea tu. Ajira ziwe za mikataba tu vijana nao wapate ajira.
Kwahio wanasayansi wakifa tulishangilia ? Ni kwamba watendaji wala usiwaone kama mzigo bali watu muhimu wa kutenda kitu husika kwahio kama mwalimu yupo na ana knowledge cha muhimu ni kuona ni jinsi gani mnatumia ujuzi wake kuhamishia wengine na sio jinsi gani utakatiza ujuzi wake..., In short perception yako ni myopic... Ni sawa sawa unasema sababu maji kwenye ndoo ni mazito, utoboe matundu ili yavuje na kukupunguzia ule uzito (badala ya kuangalia ni jinsi gani unaweza kusaidiana na wengine kubeba kwa pamoja).....

In short cha maana ni kuangalia ni vipi tunaweza kuongeza ujira kwa watu ukizingatia hata huko Serikalini ni watu wachache sana wanakuwa absorbed..., Kwahio kuondoa tatizo ni kuhakikisha kila mwenye nguvu zake anapata ujira; Kama alivyosea Nyerere kwenye Mkutano wa TANU....

  • CHAMA CHETU KINASEMA - mtu mwenye Afya ambaye tumeshindwa kumpa njia halali ya kujipatia riziki yake. Nawaomba ardhi - hakuna ardhi; hamnipi ardhi, Mnasema "Ardhi hakuna". Naomba kazi ya kibarua basi, Nipeni basi ya kibarua, "Hamnipi kazi ya kibarua. Mimi niko tayari kabisa kufanya kazi au ya kulima au ya kibarua chochote nipeni. Hamnipi Chama Chetu kinasema MTANILISHA.
 
Wazee watastaafu, watafariki. Unakuja ulimwengu wa AI isiyokufa. Kwa huu mtazamo wako yajayo siyapatii picha.
Mtaongea yote mtajitetea ila inapaswa muachie vijana nao wapate ajira wazazi wanasubiri na wao waone matunda ya uzao wao nyie mnabana tu mnashikilia wenyewe tu, mnapeana viti wenyewe tu mnakuwa na mambo ya hierarchical systems kwenye public offices.

It’s your era to end up all of these oppressive deeds.

Wacha vijana tutafute njia bana.
 
Watapewa mkataba mwingine kama kuna ulazima wa wao kuhitajika. Waende wakajiajiri sasa, walishapata mitaji
Kama kujiajiri ni rahisi kwanini hata mtu usumbuke kwanza kufanya kazi kwa miaka kumi ? Si uende Benki ukachukue mikopo ? Au tuongelee ni jinsi gani ya kutoa mikopo...

In short kumekuwa na Utopian ideas kana kwamba kila mtu anaweza akajiajiri tena kwa nchi kama yetu yenye madalali na wachuuzi kuanzia Viongozi wa nchi mpaka chinga mtaani ni wangapi tutauza bidhaa za mchina na tutamuuzia nani ?

Watunga Sera wamekuwa na majibu rahisi sana na mbaya zaidi watu wa kuwahoji nao wamekuwa wakiridhika na mediocrity....; Na hapo bado Technology inazidi ku kick in ambapo nguvu kazi haina maana tena...
 
Kuna kada nyingine sio za kuongelea tu eti kwa sababu baba yako hana ajira

Madaktari bingwa wanapatikana kwa njia ngumu sana sio rahisi kuwastaafisha kwa miaka 10 tu kijana

thats wastage of precious materials

Mtaalam wa mionzi mfano yuko mmoja tu katika hospitali flani, umstaafishe ili iweje?

waalimu wa Sayansi hawatoshi kabisa huko katika idara za Elimu msingi na sekondari, bado uwastaafishe, ili iweje?

SERIKALI INAPASWA KUPAMBANA NA HILI TATIZO LA AJIRA KWA NAMNA YA TOFAUTI, sio hivi ulivyoandika
Nafasi za serikalini sio udaktari tu. Zipo nafasi kibao za kisiasa ambazo watu wanaweza temwa hata baada ya miaka 5 tu
 
Kama kujiajiri ni rahisi kwanini hata mtu usumbuke kwanza kufanya kazi kwa miaka kumi ? Si uende Benki ukachukue mikopo ? Au tuongelee ni jinsi gani ya kutoa mikopo...

In short kumekuwa na Utopian ideas kana kwamba kila mtu anaweza akajiajiri tena kwa nchi kama yetu yenye madalali na wachuuzi kuanzia Viongozi wa nchi mpaka chinga mtaani ni wangapi tutauza bidhaa za mchina na tutamuuzia nani ?

Watunga Sera wamekuwa na majibu rahisi sana na mbaya zaidi watu wa kuwahoji nao wamekuwa wakiridhika na mediocrity....; Na hapo bado Technology inazidi ku kick in ambapo nguvu kazi haina maana tena...
Kujiajiri ni kugumu na ni kipaji pia; ndio maana wengi wanategemea kuajiriwa mpaka wanakufa.

Mtaji unaweza usiwe sababu, sababu wapo wanaolipwa pesa nyingi kwenye kuajiriwa lakini hawawezi kujiajiri.

Kuhusu sera, unategemea alie ajiriwa akutengenezee wewe sera ya kujiajiri wakati yeye mwenyewe amefeli kujiajiri?​
 
Kuna kada nyingine sio za kuongelea tu eti kwa sababu baba yako hana ajira

Madaktari bingwa wanapatikana kwa njia ngumu sana sio rahisi kuwastaafisha kwa miaka 10 tu kijana

thats wastage of precious materials

Mtaalam wa mionzi mfano yuko mmoja tu katika hospitali flani, umstaafishe ili iweje?

waalimu wa Sayansi hawatoshi kabisa huko katika idara za Elimu msingi na sekondari, bado uwastaafishe, ili iweje?

SERIKALI INAPASWA KUPAMBANA NA HILI TATIZO LA AJIRA KWA NAMNA YA TOFAUTI, sio hivi ulivyoandika
Walimu wa sayansi hawatoshi wakati mtaani wamejaa kibao?
 
kwamba serikali iandae bajeti ya kulipa mafao ya watumishi kila miaka 10 ,itafilisika
Mafao ya watumishi si michango yao. Halafu unapoitetea serikali kwamba haina hela za kulipa watu hao wakati kuna kundi dogo la watu linaweza likakwapua zaidi ya trillion 1 ndani ya mwaka kwenye mfumo wa serikali na maisha yakaendelea. Mbona usiseme serikali itafilisika?
 
Tafuta kazi ya kufanya achana hizi fikra za kibinafsi ,acha aliyepata afanye kazi.Hizi habari za tugawane keki ya taifa unajidanganya

Anyway,wewe unamchango gani katika hili taifa tofauti na hiyo indirect tax(VAT) unalipa?Sasa kama kodi yenyewe unalipa hii ya added value tax,hii keki unayotaka mgawane ni hipi?
Kiburi cha Check number hiki🤣
 
Hilo sio sawa, huwezi kuwatoa watu wenye uzoefu.
Ni bora wafanyakazi wote wa serikali wawe na mikataba ya miaka mitano mitano.
Kupata mkataba mpya wa kuendelea na mitano mingine itategenea na uadilifu, ufanisi, uchapa kazi, uzalendo na uzalishaji na matokeo chanya. Vinginevyo chukua mafao yako ukapambane mtaani.
Itasaidia kuleta ubunifu, japo kwa upande mwingine ushirikina utashamiri na uchawa utakuwa mkubwa sanaa
 
Hakika watu tupeane nafasi za ajira bana watu wanakula cake 🍰 ya taifa wenyewe mtu anakaa miaka 30+ kazini wengine waajiriwe lini sasa 😡
Kama keki kiduchu Wote wapate hicho hicho kiduchu sio? Hata kama ni Harufu kuliko kuwapa watoto watatu unaacha wengine unasema keki ndogo. Bila kujua wale watatu umewapa Dhuluma.

Asikiaye na afahamu.
 
Tafuta kazi ya kufanya achana hizi fikra za kibinafsi ,acha aliyepata afanye kazi.Hizi habari za tugawane keki ya taifa unajidanganya

Anyway,wewe unamchango gani katika hili taifa tofauti na hiyo indirect tax(VAT) unalipa?Sasa kama kodi yenyewe unalipa hii ya added value tax,hii keki unayotaka mgawane ni hipi?
Kiburi cha Check number hiki
Hapa lengo ni lipi kwamba ufanisi?, Wote tupate? Au nini?

Kama umechukulia kama njia ya kuongeza ufanisi kiutendaji ni kwambie hakuna positive impact utapata

Kama ni kusema wote tupate? Jibu ni jepesi,hakuna taifa lolote chini ya jua ambalo watu wake wako katika madaraja sawa.Wapo ambao watapata na wakukosa pia.

Sijui uliwaza nini, lakini hakuna uwiano sawa kati ya mda uliowekeza kwa huyo mtu na time uliyoweka mtu huyo kuproduce(Someone has to spend 17+ years in training and ask them to produce for 10 years only.Don't you see mismatch here?Will you profit from your investment?) Au mada yako ni kuongelea ubinafsi wa mtu nasio kwa malengo ya wengi
Hizi ni siasa za waliojiriwa 😂 utaskia jiajirini.. Mara uzoefu sijui blaah blaah. Hivi Tanzania hii wafanyakazi wanaofanya kazi na kuwa audited na measures kama KPI ni % ngapi serikalini? Gavo Imekuwa ni sehemu ya watu kupumzikia maana hamna productivity yoyote zaidi ya kusaini mshahara tu😄 ukiachana na nafasi za udaktari na za ma technicians.
 
Back
Top Bottom