Ajira za Uhasibu (Accountant), Store Keeper na Personal Assistant

Ajira za Uhasibu (Accountant), Store Keeper na Personal Assistant

Tapeli huyu
Juzi nilimcheck nikamtumia cv yangu ya kazi ya uhasibu, akaniomba laki 1 ili tu eti anipe kazi. Nikamwambia simpi hata mia mbovu. Akaniblock.

Kuweni makini sana na huyu mtu.
 
Tapeli huyu
Juzi nilimcheck nikamtumia cv yangu ya kazi ya uhasibu,akaniomba laki 1 ili tu eti anipe kazi..nikamwambia simpi hata mia mbovu.akaniblock.
Kuweni makini sana na huyu mtu.
Noma sana
 
Tapeli huyu
Juzi nilimcheck nikamtumia cv yangu ya kazi ya uhasibu,akaniomba laki 1 ili tu eti anipe kazi..nikamwambia simpi hata mia mbovu.akaniblock.
Kuweni makini sana na huyu mtu.
Labda sio Abdul Ghafur uliyekumbana nae?

Kwanza sisi hatuulizi CV ya mtu, sijui ni nani alikudanganya kuwa inayoajiriwa ni cv? Pili, nakumbuka kuna mtu katuma cv nikamuuliza nani kakuambia utume cv? akanambia "just ignore", nikamjibu "ignored" akaniita "tapeli" Nahisi ni wewe na hilo la kuambiwa utume l;aki moja ni uongo wa wazi kabisa, labda ulipigiwa na matapeli.

Kama huyo ni wewe, kweli kabisa nime ku block. You were just wasting precious time and you've asked yourself to be ignored. I did better to block you.


Niianike namba yangu JF kwa miaka sasa, picha yangu halisi, niandike humu mpaka anuani za nilipo halafu nikutapeli laki moja.

Kijana kama ndio hizo njia zako za kuomba kazi, basi nakutakia mema.

Wengi wa vijana hamna muelekeo wala hamja fundishwa namna ya kutafuta kazi, sio makosa yenu, faiza Foxy anasema tatizo ni shule za "kusomea ujinga".
 
Mkuu kwa kazi kama store keeper na personal assistant zinatrainika hata mtu akikosa uzoefu na ubobezi.
Wape nafasi vijana
Ndivyo tufanyavyo hivyo. Tusome vizuri post zetu.

Hata wewe kama unaweza kutrain vijana, toa ujuzi wako kwa faida ya wengi. Unangoja nini?

Unaonesha hujapitia uzi vizuri, hili si jukwaa la siasa. Soma...

Tunaitwa Madrassatul Abraar.

Kipaumbele kwa sasa ni watu wa IT, wahasibu, wahasibu wasaidizi, watu wa logistics and supplies, site foreman wa ujenzi. Mafundi ujenzi wenye uzoefu na wasio na uzoefu lakini wenye Nia na wataopenda kujifundisha ujenzi Kwa vitendo. Wake kwa Waume.

Wasiliana nasi kwa WhatsApp 0625249605.

Tupo mtaa wa Vitendo, kata ya Misugusugu, wilaya ya Kibaha, mkoa wa Pwani.

Stendi inaitwa Miyomboni Shule au Misugusugu Shule ya msingi.

Ukija unakuja na barua ya utambulisho wa Serikali ya mtaa.
 
Acha siasa,weka details za kampuni yako watu tuijue kiundani.
Unaonesha hujapitia uzi vizuri, hili si jukwaa la siasa. Soma...

Tunaitwa Madrassatul Abraar.

Kipaumbele kwa sasa ni watu wa IT, wahasibu, wahasibu wasaidizi, watu wa logistics and supplies, site foreman wa ujenzi. Mafundi ujenzi wenye uzoefu na wasio na uzoefu lakini wenye Nia na wataopenda kujifundisha ujenzi Kwa vitendo. Wake kwa Waume.

Wasiliana nasi kwa WhatsApp 0625249605.

Tupo mtaa wa Vitendo, kata ya Misugusugu, wilaya ya Kibaha,mkoa wa pwani.

Stendi inaitwa Miyomboni Shule au Misugusugu Shule ya msingi.

Ukija unakuja na barua ya utambulisho wa Serikali ya mtaa.
 
Shaka lipo sana hapo, company bila kuwa scale maalum ya ulipaji inatia shaka.
Kama una shaka usije. Ukishaanza kuwa na mashaka basi utakuwa ni mtu wa mashaka mashaka, ukiwa na shaka na kitu usikifanye. Unachotakiwa uulize kwa usilolijua, usiwe na mashaka. Muono wako ni mwengine na hatuwezi kufanana miono yetu kama vile ambavyo DNA zetu haziwezi kufanana.

Unaonesha unahitaji mafunzo zaidi za namna ya malipo yaliopo dunia ya leo. Hata marehemu Magufuli amelisema mara chungu nzima, "utalipwa kwa uwezo wako" (performance) sio kwa jina lako au jina la kazi.

Unaonesha haufahamu maana ya "performance-based payments". Tunacholipa ni kwa kazi aifanyayo mtu si kwa jina la kazi aifanyayo.

Unaweza kuwa mhasibu lakini wakati huo huo huo unafanya na kazi za utawala, procurement, operations, sasa tukulipe kama mhasibu ambae anafanya data entry tu?

Hata wahasibu, wapo wa uwezo tofauti na ujuzi na uzoefu tofauti, unataka wote walipwe namna moja?

Nikuulize maswali? Umeshafanya kazi zipi na wapi na kwa miaka mingapi?
 
Tapeli huyu
Juzi nilimcheck nikamtumia cv yangu ya kazi ya uhasibu,akaniomba laki 1 ili tu eti anipe kazi..nikamwambia simpi hata mia mbovu.akaniblock.
Kuweni makini sana na huyu mtu.
Acha uongo, kama umeshindwa hizo nafasi waachie wengine watakaoweza. Mzee Abdul namfahamu hawezi kukutapeli hata senti yako hana shida hizo na pia hahitaji cv sasa imekauje wewe ukaombwa cv. Nakushauri kuwa hili jukwaa lina watu wa aina tofautitofauti sio kila unayemuona ni muhuni au tapeli, kuna watu wamepata kazi za mishahara mikubwa kupitia wanachama wa hilihili jukwaa. Jifunze heshima mkuu.
 
Tunawapa tahadhari.

Kama umeombwa CV au pesa basi elewa hao sio sisi, tumedukuliwa au umedukuliwa. Hatuombi cv ya mtu kwenye simu wala mtandao kwa sasa, hiyo ni kizamanni. CV siyo ifanyayo kazi, cv ni
introduction" tu. Mbadala wa cv unapotutumia message ya whatsapp (usitume cv) tunabadilishana maswali mawili matatu ya introduction tunakupa anuanu zetu, ukija tunaongea ana kwa ana, kwa kuongea tunapata kuelewaana vizuri sana, cv unaweza kuandikiwa na mjomba, ndugu au rafiki. Lakini ana kwa ana hakuna hayo, wewe unapata kutuelewa sisi na sisi tunapata kukuelewa wewe na unapata kuyaona mazingira ya kazi na kuishi. Ana kwa ana.
 
Labda sio Abdul Ghafur uliyekumbana nae?

Kwanza sisi hatuulizi CV ya mtu, sijui ni nani alikudanganya kuwa inayoajiriwa ni cv? Pili, nakumbuka kuna mtu katuma cv nikamuuliza nani kakuambia utume cv? akanambia "just ignore", nikamjibu "ignored" akaniita "tapeli" Nahisi ni wewe na hilo la kuambiwa utume l;aki moja ni uongo wa wazi kabisa, labda ulipigiwa na matapeli.

Kama huyo ni wewe, kweli kabisa nime ku block. You were just wasting precious time and you've asked yourself to be ignored. I did better to block you.


Niianike namba yangu JF kwa miaka sasa, picha yangu halisi, niandike humu mpaka anuani za nilipo halafu nikutapeli laki moja.

Kijana kama ndio hizo njia zako za kuomba kazi, basi nakutakia mema.

Wengi wa vijana hamna muelekeo wala hamja fundishwa namna ya kutafuta kazi, sio makosa yenu, faiza Foxy anasema tatizo ni shule za "kusomea ujinga".
We jamaa unashangaza sana, unataka mzoefu wa kazi, mtu ameweka CV hutaki, sasa utajuaje kwamba ni mzoefu? au hujui maana ya CV?

Umeulizwa mshahara unazugazuga tu, si useme tu kwamba ni commission watu waelewe?
Au kweli wewe ni Tapeli, hata kama ni wale watu wa kuuza vyombo mitaani, haiwezekani kusiwe na jina la kampuni! Anyway sikulaumu, maisha ni magumu. Wapige hela hao watakaokubali kupigika.
 
Acha uongo, kama umeshindwa hizo nafasi waachie wengine watakaoweza. Mzee Abdul namfahamu hawezi kukutapeli hata senti yako hana shida hizo na pia hahitaji cv sasa imekauje wewe ukaombwa cv. Nakushauri kuwa hili jukwaa lina watu wa aina tofautitofauti sio kila unayemuona ni muhuni au tapeli, kuna watu wamepata kazi za mishahara mikubwa kupitia wanachama wa hilihili jukwaa. Jifunze heshima mkuu.
Kama unamfahamu sio tapeli basi hawezi kabisa kujieleza, tangazo liko hovyo mno. Awaachie watu wanaoweza kujieleza vizuri.
 
Kama unamfahamu sio tapeli basi hawezi kabisa kujieleza, tangazo liko hovyo mno. Awaachie watu wanaoweza kujieleza vizuri.
Usemacho ni sahihi labda tuseme mzee huwa haelezi mambo yakanyooka na hii ni kutokana na kwamba huwa anaandika mara nyingi humu kuhusu hayo mambo. Ukienda utajionea mengi sana vijana wanajifunza ufundi mbalimbali kwa vitendo tena bure na wanafundishwa na vijana wenzao ambao ndio hao wanatafutwa kwa malipo yaani mshahara kabisa. Hiyo ni taasisi ya dini yenye lengo la kusaidia vijana kupata ujuzi nje ya mfumo rasmi.
 
Kama una shaka usije. Ukishaanza kuwa na mashaka basi utakuwa ni mtu wa mashaka mashaka, ukiwa na shaka na kitu usikifanye. Unachotakiwa uulize kwa usilolijua, usiwe na mashaka. Muonowako ni mwengine na hatuwezi kufanana miono yetu kama vile ambavyo DNA zetu haziwezi kufanana.

Unaonesha unahitaji mafunzo zaidi za namna ya malipo yaliopo dunia ya leo. Hata marehemu Magufuli amelisema mara chungu nzima, "utalipwa kwa uwezo wako" sio kwa jina lako au jina la kazi.

Unaonesha haufahamu maana ya "performance-based payments". Tunacholipa ni kwa kazi aifanyayo mtu si kwa jina la kazi aifanyayo.

Unaweza kuwa mhasibu lakini wakati huo huo huo u8nafanya na kazi za utawala, procurement, operations, sasa tukuloipe kama mhasibu ambae anafanya data entry tu?

Hata wahasibu, wapo wa uwezo tofauti na ujuzi na uzoefu tofauti, unataka wote walipwe namna moja?

Nikuulize maswali? Umeshafanya kazi zipi na wapi na kwa miaka mingapi?
Nimekuelewa sana tu ila nataka kujua, je hao wahasibu unaohitaji kwa majukumu unaowahitajia mnawalipa Tsh ngapi endapo wataperform kama unavyotaraji?
 
We jamaa unashangaza sana, unataka mzoefu wa kazi, mtu ameweka CV hutaki, sasa utajuaje kwamba ni mzoefu? au hujui maana ya CV?

Umeulizwa mshahara unazugazuga tu, si useme tu kwamba ni commission watu waelewe?
Au kweli wewe ni Tapeli, hata kama ni wale watu wa kuuza vyombo mitaani, haiwezekani kusiwe na jina la kampuni! Anyway sikulaumu, maisha ni magumu. Wapige hela hao watakaokubali kupigika.
Lazima unishangae sana, kwa sababu mawazo yako na mawazo yangu ni tofauti, muono wako na muono wangu ni tofauti. Badala ya kunishangaa niulize kwanini sihitaji CV za watu. Kuhusu CV, kuna uwezekano mkubwa maana ya CV uijuavyo wewe na niijuavyo mimi tunatofautiana, kwa kuwa hata herufi CV ni kifupisho cha maneno ya lugha za kigeni. Nijuavyo mimi maana ya "CV" ni utambulisho wako binafsi, kama ulivyouandika au kuandikiwa. Utambulisho wetu tunaufanya kwa kutambuana ana kwa ana. Uzoefu wa kazi huonekana ufanyapo kiazi, kwetu kuna "orientation" ya wiki mbili itayotudhirishia uzoefu wako wa kazi. CV sio uzoefu wa kazi.

Uzoefu wetu umetufundisha kuwa wengi wanaandikiwa CV na hawaandiki wenyewe na wengi hawaelewi hata kilichoandikwa humo ni nini.

Ngoja nikupe kisa kimoja cha CV kati ya vingi nilivyonavyo; Kuna kijana alikuja kwetu na kitu cha kwanza kanipa bahasha, nikamuuliza ina nini? akanambia CV na kopi za vyeti vyangu, nikamwambia baki na bahasha yako, nipe CV tu, akanitolea CV ina page 3. Nikaipitia haraka haraka, nikakutana na kipengele kinachosema kuwa yeye ni mwanamichezo na anapenda sana kucheza mpira wa kikapu (basket ball) na amekua kwenye mchezo huo kuanzia shule ya msingi. Nikaona safi sana, hapa tumepata kijana ataetufundishia vijana wengine kucheza mpira wa kikapu. Bahati, hapa kwetu tulikua na mpira wa kikapu kati ya vifaa vingi vya michezo tulivyo navyo kwa ajili ya watoto, wanafunzi wetu wa madarasa ya Qur'an. Tukampa mpira tukamwambia tuoneshe uwezo kidogo hapo uwanjani. Akabaki anatutazama kama mjusi anavizia nzi ukutani. Nikamuuliza, vipi, tuoneshe mambo. Akasema yeye aliikopi tu cv na kubadili jina na mambo mengine, hilo la mpira wa kikapu lilimpita.


Mambo kama hayo na mengine mengi yametufanya tusiulize cv ya mtu ya maandishi mpaka awe kamaliza orientation ya wiki mbili na sisi, na ndani ya hizo wiki mbili, kama itahitajika, huwa tunamuelekeza namna ya kuipangilia CV yake kwa namna ya sisi tuwekavyo kumbukumbu zake kwenye files zetu za kielektroniki.
 
Nimekuelewa sana tu ila nataka kujua, je hao wahasibu unaohitaji kwa majukumu unaowahitajia mnawalipa Tsh ngapi endapo wataperform kama unavyotaraji?
Hakuna kikomo cha malipo kwenye system yetu ya "performace based". Ukifika hapa kufanya orientation utayaelewa yote. Ni vigumu sana kukufahamisha kwa maandishi kwa upande wangu, Sisi hupendelea zaidi kufanya vitu kwa vitendo.
 
Hakuna kikomo cha malipo kwenye system yetu ya "performace based". Ukifika hapa kufanya orientation utayaelewa yote. Ni vigumu sana kukufahamisha kwa maandishi kwa upande wangu, Sisi hupendelea zaidi kufanya vitu kwa vitendo.
Na mnachukua wakristo kweli, maana naona ni taasisi yenye jina la kiislamu?
 
Back
Top Bottom