Akili za watanzania wengi bado hazipo tayari kupata maendeleo

Akili za watanzania wengi bado hazipo tayari kupata maendeleo

Naanto Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,236
Reaction score
15,677
Sijui shida ni elimu au vip. Mfano mdogo sana nilijaribu kwenda kununua kiwanja maeneo mawili tofauti katika mikoa miwili tofauti.

Kilichonishangaza ni kwamba, unakuta muuzaji wa kiwanja, au mmiliki amegawa hivo viwanja kwa style ambayo mpaka unaweza kujiuliza 'hivi huyu mtu ni kichaa?'

Unakuta viwanja vimegawanywa mara kingine unakuta kina shape ya pembetatu, kingine cha pembeni kina shape ya trapeza, kingine ni mraba ambao haujakaa sawa pande zote.

20221221_161548.jpg


Matokeo yake watu wanakuja kujenga, unashangaa nyumba zimepangana kama kikao cha nzi. Yaani mpaka ukipaangalua hivi unapata kichefuchefu.

Nikakaa chini nikajiuliza 'Hivi hata hili nalo linahitaji uwepo wa serikali? Kwanini hawa wauzaji wa viwanja wasigawanye maeneo kwa kufuata mpangilio unaovutia?
 
Upo sahihi kabisa tena kwa 💯. Watanzania bado sana tena sana. Rais Samia 2025 inamhusu. Hatuhutaji mwingine.
 
Upo sahihi kabisa tena kwa 💯. Watanzania bado sana tena sana. Rais Samia 2025 inamhusu. Hatuhutaji mwingine.
Ni sawa mkuu..... kampeni ikifika unioe tenda na mimi nipige hela
 
Mtwara nyumba ni za kiswahili lakini mitaa imenyooka balaa. Nyumba zimetengeneza mstari kama imepigwa rula vile. Ni ustaarabu tu
Ni kweli kabisa mkuu.. naona ni utaratibu... pia maeneo kama Moshi mashamba na viwanja vinagawiwa kwa viboksi...

Ila kuna eneo moja Morogoro nilienda.. aisee ni uchafu.. nilichanganyikiwa.. nilikuta plot ina shape ya Sambusa.. Mahali ni pazuri ila kuona tu shape ya kiwanja nikaogopa
 
Serikali ya mtaa ikisimamia haya mambo vizuri, kutakuwa na mpangilio unaoeleweka. Kujenga chochote kile ni lazima serikali ya mtaa ihusishwe.
 
Mimi nadhani kwa mwanaume kosa yote ispokuwa nguvu za kiume.
Unaweza kuwa na nguvu za kiume lakini ukakoswa na akili
asikudanganye mtu hakuna mwanamke atakayekukubali maana utakuwa ni chizi/mwehu.

Nguvu za kiume ni muhimu sana lakini bila ya kuwa na akili hazitatumika popote
 
Sijui shida ni elimu au vip. Mfano mdogo sana nilijaribu kwenda kununua kiwanja maeneo mawili tofauti katika mikoa miwili tofauti.

Kilichonishangaza ni kwamba, unakuta muuzaji wa kiwanja, au mmiliki amegawa hivo viwanja kwa style ambayo mpaka unaweza kujiuliza 'hivi huyu mtu ni kichaa?'

Unakuta viwanja vimegawanywa mara kingine unakuta kina shape ya pembetatu, kingine cha pembeni kina shape ya trapeza, kingine ni mraba ambao haujakaa sawa pande zote.

Matokeo yake watu wanakuja kujenga, unashangaa nyumba zimepangana kama kikao cha nzi. Yaani mpaka ukipaangalua hivi unapata kichefuchefu.

Nikakaa chini nikajiuliza 'Hivi hata hili nalo linahitaji uwepo wa serikali? Kwanini hawa wauzaji wa viwanja wasigawanye maeneo kwa kufuata mpangilio unaovutia?
Naona unawasema watu wa Kwa Moromboo Muriet Arusha,yaani nyumba kama kichuguu cha Siafu ili hali ni mji mpya..NI AIBU KWA KWELI!
 
Nikakaa chini nikajiuliza 'Hivi hata hili nalo linahitaji uwepo wa serikali? Kwanini hawa wauzaji wa viwanja wasigawanye maeneo kwa kufuata mpangilio unaovutia?
Mfumo wa elimu dunia na uelewa wa mambo mbali mbali uko nyuma kutokana fikra zilizodumaa, ambapo serikali haiwezi kuepuka lawama ya kuwa chanzo cha hili.....

Tumeshataniwa sana kwa hili na majirani zetu wakenya. Kuna wakati wakituita 'imbeciles'

Iko katika sura nyingi, ikiwemo kuabudu kiswahili na kudharau kiingereza, ilhali uwezekano mkubwa wa kuijua dunia nje ya mfumo rasmi wa elimu ni pale unapojua kiingereza. Watakuambia "....mbona wachina wameendelea na hawajui kiingereza??!! 😂
 
Serikali ya mtaa ikisimamia haya mambo vizuri, kutakuwa na mpangilio unaoeleweka. Kujenga chochote kile ni lazima serikali ya mtaa ihusishwe.
Nakuunga mkono.. lakini shida ndo hiyo unakuta mwenyekiti wa serikali za mitaa hajaenda shule na hana exposure yeyote matokeo yake unakuta ... yeye anaona ni sawa tu viwanja vikiwa vinauzwa kwa mfumo huo
 
Mfumo wa elimu dunia na uelewa wa mambo mbali mbali uko nyuma kutokana fikra zilizodumaa, ambapo serikali haiwezi kuepuka lawama ya kuwa chanzo cha hili.....

Tumeshataniwa sana kwa hili na majirani zetu wakenya. Kuna wakati wakituita 'imbeciles'

Iko katika sura nyingi, ikiwemo kuabudu kiswahili na kudharau kiingereza, ilhali uwezekano mkubwa wa kuijua dunia nje ya mfumo rasmi wa elimu ni pale unapojua kiingereza. Watakuambia "....mbona wachina wameendelea na hawajui kiingereza??!! 😂
Una hoja.. ila nadhani haya mambo yangeweza kurekebishika ikiwa wenyeviti wa mitaa ambao ndio huwa wanasimamia uuzwaji wa viwanja wangekuwa kidogo na elimu.

Ila shida unakuta wenyeviti wa mitaa wameishia lasaba.. kwahiyo uwezo wa kuelewa kwamba mpangilio ni muhimu kuwepo.. kwake ni shida
 
Back
Top Bottom