Akina Jemedari wamenawishwa kazi ya uwakala wa wachezaji

Akina Jemedari wamenawishwa kazi ya uwakala wa wachezaji

YUKO mchambuzi mmoja anaitwa job ndugai sijui nani pale Wasafi, kila siku na kila mara lazima ajimwambafai na kusema "mimi wachezaji wangu" ninaowasimamia wana hiki na kile!!! hivi nae yumo kwenye shajala ya TFF ya mawakala?
Mimi radio zenyewe huwa sisikilizi.
 
Football ya Tanzania imekuwa sana ghafla, uwekezaji kwenye mpira ni mkubwa sana kiasi Cha timu zetu kugombania wachezaji na mabenchi ya ufundi na timu kubwa Africa. Hii ni ishara na indicator kuwa Sasa lazima mpira wetu professionalism kwenye nyanja zote. Itakuwa aibu na kusababisha hasira kubwa kuona mambo kama:
1. Mchambuzi anakuwa wakala
2. Mchezaji anamrukia na kumuumiza kipumbavu mchezaji ghali wa timu ya taifa ya nchi fulani.
3. Refa anachezesha mechi kwa kupendelea timu fulani kwa sababu yoyote Ile. Tuwe na waamuzi hodari kabisa wanaochezesha kwa kufuata kanuni za mpira.
4. Kiongozi wa mpira/TFF anakuwa na mahaba na upendeleo na timu fulani kwa sababu zake.
5. Mdhamini wa hovyo asiyetimiza mkataba.
6. Wachambuzi wa mpira wasiokuwa na weledi, wanaokatisha tamaa wachezaji na wadhamini kipumbavu utadhani wanachangia uendeshaji wa timu.
7. Viwanja vya hovyo vinavyohatarisha afya za wachezaji ghali wanaotegemewa na timu za mataifa Yao.
8. Kuwa na kanuni za ligi na ratiba ya ligi ya hovyo inayopendelea timu fulani TU au unsporting.
9. Zawadi ndogo za mashindano na wadhamini zisizofanana na gharama halisi za uendeshaji wa timu.
hiyo namba 5 inamhusu Karia na likatibu lake Kidau!
 
Kumwembe anafanya uchambuzi au anapiga story za mpira!?
Hivi IPO kozi ya uchambuzi wa mpira au ni janjajanja TU? Mbona salama ngare anaonekana anajua kuliko kazumari na jeflea? Kwenda hewani lazima kuwe na maadili yake.
 
Kuna wakati nikahisi kama vile wachambuzi wengi wa mpira ni washabiki wa simba. Hawapendi kuikosoa vibaya Simba hata pale inapokosea wakidhani kuwa wanaisaidia kumbe wanaipa kile wazungu wanachokiita false hope/matumaini bandia. Mchambuzi wa mpira huwa anauchambua mpira kwa mapana yote. Mchambuzi anatakiwa kuwa kioo cha wadau wote wa mpira kujitazama. Kioo kinaonyesha tu ulivyo lakini hakihukumu kuwa wewe ni mbaya, mzuri au umechafuka. Ni Kazi yako mwenyewe kutafsiri ulichokiona kwenye kioo na hatua utakazochukua. Kazi ya kioo sio kukuonya, kukupongeza au kukutuma ni chakufanya. Wachambuzi wetu ni kama matawi hai ya timu wanazozipenda. Kazi ambayo ilipaswa kufanywa na wasemaji wa timu husika wanaifanya wao.
 
Hivi IPO kozi ya uchambuzi wa mpira au ni janjajanja TU? Mbona salama ngare anaonekana anajua kuliko kazumari na jeflea? Kwenda hewani lazima kuwe na maadili yake.
Inabidi uwe unaijua mpira,kwa waliocheza kwa viwango vya juu wanakua na uelewa wa mpira,siyo kuangalia mpira kwa muda mrefu Kama akina Edo kumwembe,zamani alipokuwepo marehemu mziray,shafi dauda alikua haendi,maana ilikua akiongea mziray anamkosoa
 
Back
Top Bottom