Akumbukwe John Okello, Baba wa Taifa la Zanzibar. Bila huyu leo Zanzibar wangekuwa bado Utumwani

Akumbukwe John Okello, Baba wa Taifa la Zanzibar. Bila huyu leo Zanzibar wangekuwa bado Utumwani

Mgeni,
ASP na Umma Party walikuwako wababe si Okello.

Okello alivuna kwenye "Mob Psychology."

Alikuwa mfano wa Musiba aliyekuwa anazungumza kwenye mitandao ya kijamii.

Ushamsikia tena Musiba?

Okello alipokutana na Hashil Seif (huyu ni comrade kasoma Cuba) ndani ya ndege Okello hakuweza kufanya lolote alisalimu amri.

Hakuweza kumkabili Hashil.

Wako wababe kutoka ASP ukihadithiwa unyama wao mwili utakusisimka.

Watu wenye uwezo wa kumzika mtu yu hai.

Nilikuwa nataka kuandika kuhusu kubakwa kwa binti mdogo wa Kihindi wakati mama yake anabakwa....

Nashindwa kuandika maneno ya huyu mama kuomba salama ya mwanae...

Aliyenihadithia ni kati ya hao washenzi...

Wengi mnaandika msiyoyajua.
Mzee Mohamed andika tujifunze.
 
Cuba na nchi nyingine ambazo Chegu wa 1 alishiriki kuzipa uhuru wanatambua nafasi yake, ni huku kwetu tu ndo tunatambua huyu Chegu wa EA kwa sauti yake redioni. Jokes!
 
Niwekee link mzee wangu.
Being...

Ni kweli, nilimuuliza Sheikh Said ikiwa Mapinduzi ni halali au ni haramu. Sijawahi kupata jibu zaidi ya ku'dance'

Kuna ''Mwarabu wa London'' Bw Rajab, yeye alijaribu lakini pia hakuwa na jibu la moja kwa moja.
Katika gazeti la Raia mwema, alisema ' kwamba ni halali au haramu inatagemea mtu yupo upande gani''

Ni nadra kumsikia Jussa akitamka neno Mapinduzi lakini ni kawaida sana kumsikia Mansour Himid akitamka.
Mifano hiyo inaonyesha sensitivity ya jambo zima na linavyowagawa Wazanzibar hasa kwa rangi na nywele

Niliwahi kumuuliza Mo ikiwa Mapinduzi ni haramu na yalifanywa na Watu kutoka Tanganyika kambi ya Kipumbwi, je, Wazanzibar wanaosherehekea wanafanya makosa kutukuza haramu?
Hakuna jibu hadi kesho, ana 'dance' tu

Kwa bahati mbaya katika wale 12 wa Baraza la Mapinduzi wengi wametangulia mbele ya haki, waliobaki wachache ni A.H.Mwinyi sina habari za Kanali S.Bakar. @JokaKuu kama una taarifa zaidi tafadhali

Wanamapinduzi 12 hawakuacha nyaraka kwa kimaandishi kama vitabu vya kueleza nini kilijiri, sijui kama walikatazwa au la. Tunabaki na simulizi za upande mmoja kutoka Oman au mrengo wa Kiimani.

Kinachosikitisha ni chombo kama TBC kinachoendeshwa kwa kodi zetu kinatumiwa 'kiharamia'

Tido alilipa gharama pia kwa kutaka kuiweka TBC huru. Aliahidi kuonyesha chaguzi mubashara. CCM hawakubaliani na mambo ya kwenye mwanga, wanapenda mambo kizani, Tido akalipia gharama.

Lakini pia kuna kauli nimeisikia na hapa Mohamed atanisahihisha kwamba ' kuna nyakati heri inafichwa ndani ya shari'' kule Buckingham palace wanasema '' a blessing in disguise' , Tido is better off today.
Nguruvi...
Bahati mbaya unaandika kwa kukejeli.
Umemkejeli Ahmed Rajab na umenikejeli mimi pia.

Laiti ungeandika kwa ustaarabu ningeweza kushawishika kuchangia.
Nimejifunza mengi kutoka kwa Ahmed Rajab katika historia ya Zanzibar.

Si mtu wa kuvunjiwa heshima yake hapa.

1705780111905.png

Mwandishi na Ahmed Rajab, Mhariri wa Africa Analysis, Barbican London 1991​
 
Being...
Asante mzee wangu mohamed upumzike sasa au unaangalia mechi?
 
City...
City...
Okello anabebeshwa mzigo si wake.

ASP haikuwa na uwezo wa kupindua serikali.

Mipango yote ilifanyika Dar es Salaam ikisimamiwa na Oscar Kambona na Abdullah Kassim Hanga.

Waliweka kambi Kipumbwi ambako waliwaweka Wamakonde kutoka shamba la Mkonge la Sakura kwa ajili ya kuwavusha kuingia Zanzibar kuIpigIa kura ASP na kushiriki katika mapinduzi.

Kambi hii ilikuwa chini ya Ali Mwinyi Tambwe akiwa District Commissioner wa Tanga na Regional Commissioner Jumanne Abdallah.

Waliopewa kazi ya kuchagua vijana wa kuletwa kambini Kipumbwi walikuwa Victor Mkello kiongozi wa chama cha wakata mkonge na Mohamed Omar Mkwawa kijana wa Kidigo kutoka Tanga aliyepatakuwa mwanachama hodari wa ASP.

Ali Mwinyi Tambwe wakati wa ukoloni aliwatumikia Waingereza kama "mole" wao ndani ya TAA kisha TANU.

Mkwawa yeye ndiye aliyekuwa akiwavusha hawa Wamakonde kuwaingiza Zanzibar usiku kwa majahazi wote wamevaa kama wavuvi wa Kidigo.

Kipumbwi yote ilikuwa imezuiwa kwa watu kuingia ovyo.

Hawa Wamakonde ndiyo walioua Waarabu wengi wakulima wa kawaida tu waliokuwa mashambani Zanzibar.

Mpango huu ulifanyika kwa siri kubwa sana.

Mzanzibari aliyepata kufika Kipumbwi inasemekana ni Jimmy Ringo ambae aliuliwa baada ya mapinduzi kama walivyouliwa wana ASP wengine.

John Okello hakuwa katika mipango hii.

Kilichompa umaarufu ni kule yeye kupewa radio kutangaza kuwa serikali imepinduliwa na Karume arejee Zanzibar kukalia kiti chake.
Weka chanzo cha habari
 
Mzee sijui anatuonaje.
Magnifico,
Unapokejeli mjadala unaharibika.

Mimi nilikuwa Research Assistant wa Dr. Ghassany wakati wa utafiti wa historia ya mapinduzi na kitabu kimeandikwa.

Hapa nimeeleza yale tuliyoona katika utafiti.

Ikiwa hutaki kuamini sikulazimishi lakini wapangaji wa mapinduzi wanafahamika na John Okello hakuwa mmoja wapo.
 
Back
Top Bottom