Akumbukwe John Okello, Baba wa Taifa la Zanzibar. Bila huyu leo Zanzibar wangekuwa bado Utumwani

Akumbukwe John Okello, Baba wa Taifa la Zanzibar. Bila huyu leo Zanzibar wangekuwa bado Utumwani

Chizi...
Nimeeleza hapa kuwa mapinduzi ya Zanzibar huwezi kuyaeleza kwa kuanza na usiku wa tarehe 11 Januari kuamkia tarehe 12 na kufika asubuhi serikali ya Mohamed Shamte ikawa imeanguka.

Mipango ya kupindua serikali ilianza nyuma sana na sehemiu kubwa ya kufanikisha mapinduzi imetoka Tanganyika ikihusisha vyombo vyake vya usalama.

Unaijua Kambi ya Kipumbwi?
Unaujua mchango wa Kassim Hanga na Kambona?

Vipi kuhusu Engen au Aboud MmasaI?

Soma kitabu cha Harith Ghassany, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' kitabu hiki kitakufungulia mengi.

Kitabu hiki kitakupeleka kwa walioshiriki mapinduzi ambo wewe majina yao hujapata kuyasikia hata siku moja.

Ali Mwinyi Tambwe kapewa nishani ya mapinduzi baada ye kufa kwake.

Wapo walioshtuka kusikia kuwa alishiriki katika mapinduzi kwa kuwa hakuna popote katika historia ya mapinduzi ambako ametajwa.

Hawa wako wengi sana.
Ovyoo...
Sawa uhusika wake ni upi hata kupewa radio kutangaza mapinduzi?.
 
kwa ushahidi upi wakati kwa uchache tu nimekueleza kuwa kulikuwa na wamwera pia? Unajua kuna mazoea ya wengi kuwa mtu akitoka kusini maana yake ni mmakonde kitu ambacho sio kweli je wewe si muumini wa hivyo?
Mna...
Mimi siko hapa kushinda mjadala.

Niko hapo kufundisha kile ambacho wengi hawakijui.

Ingekuwa kambi ya Kipumbwi ilitawaliwa na Wamwera ningeeleza.

Ukisoma kitabu cha Dr. Ghassany utawasoma Wamakonde wenyewe wakieleza mchango wao katika mapinduzi.
 
Frank...
Sijapatapo kuhangaika na Nyerere ila nimeandika historia yake kwa kadri ya uwezo wangu.

Kuhusu Okello historia yake naifahamu vizuri kwa utafiti kwani nilikuwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany wakati anaandika, "Kwaheri Uhuru Kwaheri Ukoloni.''

Siwezi kumlazimisha mtu kuniamini anaweza kuamini atakacho.
Sawa tuambie wewe ilikuwaje John Okello akapewa radio kutangaza mapinduzi matukufu ya Zanzibar ilihali si mhusika?.
 
Ovyoo...
Sawa uhusika wake ni upi hata kupewa radio kutangaza mapinduzi?.
Frank...
Ilitakiwa apatikane mtu mgeni mwenye lafidhi ngeni masikioni mwa Wazanzibari ili ipatikane picha kuwa ASP imeleta wapiganaji kutoka nje hivyo kuzidisha hofu kwa wapinzani wao ZNP na ZPPP.
 
Huyu ni Mmoja wa Mashujaa wa miaka ile aliyeshiriki kuwaondoa Makoloni huko Zanzibar. Kama ambavyo Bara nao walikuwa wameondoa wao.

Anasimulia mzee wangu ambaye alikuwa Mwalimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka hiyo Che Guavera alikuja Tanzania mwaka 1965. Anasema Che alijaribu kuulizia habari za Mwanamapinduzi aliyesaidia kuipatia Zanzibar Uhuru wake John Okello.

Kwa his disappointment alishtuka kuambiwa the Man alifukuzwa mara baada ya kumaliza jukumu lililomleta Zanzibar kuwaondoa Waarabu waliokuwa wakiitawala Zanzibar.Aliwaokoa Waafrika kutoka kutawaliwa walipopata tu uhuru wakamfukuza.

John Okello Baba wa Taifa la Zanzibar ataendelea kukumbukwa kila tutakapoadhimisha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Baada ya hapo John Okello alirudi kwao kwenda kuendeleza mapambano dhidi ya udhalimu na hatimaye alikuwa kama mtu wa kawaida tu pasipo makuu. Hakulipwa yeye wala familia yake. Kabla ya Mwaka 1967 Che Guevara kufariki aliwahi mtumia mzee wangu barua akimtaka amtafute John Okello wajiunge naye kwenye harakati huko Msumbiji na Angola.

Mzee hakujua aanzie wapi.
Wakt mwingine uchizi unafanya kazi vzr

UMUGHAKA njoo jamaa ako leo Yuko kimataifa Zaid

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Sasa we ulitaka Mkisto awe baba wa Taifa la Zanzibar huoni Mohamed Said anavyo angaika na Mwalimu Nyerere kwa nini awe baba wa Taifa mwenye macho na akili haambiwi tazama watu wa Pwani kutetea uongo ni sahihi kwa imani yao maadamu lina maslahi kwao.

Mzee Said haaminiki tena kwa sababu akili yake ameiruhusu itawaliwe na illusion za dini ya waarabu anawatukuza waarabu na dini yao kuliko uafrika na utanganyika wake. Hovyo kabisa.
 
Kwa hili Mzee wangu Mohamed Said anapata kigugumizi kukiri ushujaa wa Okello katika Mapinduzi.

Mzee wangu!
Kama ambavyo umekuwa ukifundisha kuwa Historia ya Uhuru wa Tanganyika imepindishwa, kubali na hili kuwa historia ya Mapinduzi pia imepotoshwa.

Ukweli ni kitu rahisi sana kuutetea.
 
Sela...
Okello alichaguliwa kutoa tangazo la kuanguka kwa serikali ya Mohamed Shamte kwa sababu ya lafidh yake ambayo si ya Kiunguja.

Karume, Babu na Hanga wote walikuwa Dar es Salaam.

Sauti ngeni kwa Wazanzibari oliwatia wananchi hofu.
Karume, Hanga na Babu kwanini hawakuwepo katika mapinduzi?
Na kwanini waitwe wao?
 
End justifies the begining. Wengine walifeli hadi mpaka hapo okelo alipo oongoza mapinduzi na yakafanikiwa huku hao unaosema maplanner wakiwa wamejificha gest house tanganyika kama panya wajifichavyo mafichoni.

All in all okello apewe heshima yake katika mapinduzi ya zenji bila yeye yaaingetokea.

Kwanini hamtaki kumpa heshima yake badala yake wanapewa heshima waliojificha mashimoni wakati mwanaume akiongoza mapambano. ?
View attachment 2478861
Mojamed Said anatudanganya na historia yake ya kuchonga eti hakuwemo huyu mnyama John Ok..
Hivi asiye mwanamapinduzi anaweza kukaa mbele ya lmg na AK 47 hivyo?
 
Yaani haiingii akilini eti wengine wafanye mapinduzi ila kwenye kutangaza kuwa wameshinda wanaogopa mpaka wakaenda mitaani kumtafuta Okello aje awatangazie. Huyu mzee side boi anatuona sisi kama watoto wadogo sana kwamba hatuwezi kuhoji wala kufikiri.

Sasa swali linakuja kwanini hao anaosema wapigania mapinduzi waliogopa kukaa front?mpaka wakakimbilia tanganyika.
Huyo Mzee Said wa ajabu Sana eti okelo aliitwa kuwatisha watu kwa sauti yake!

Huyu mzee ndie huyu hulialia kuhusu kufichwa kwa historia ya Wanaharakati wa Uhuru wa Tanganyika but ni yeye anayepinga na kuficha ukweli juu ya kijana huyu wa zamani.
 
Frank...
Ilitakiwa apatikane mtu mgeni mwenye lafidhi ngeni masikioni mwa Wazanzibari ili ipatikane picha kuwa ASP imeleta wapiganaji kutoka nje hivyo kuzidisha hofu kwa wapinzani wao ZNP na ZPPP.
Mzee wa kushangaza Sana huyu yaani John O anaonekana katika picha akiwa na silaha na mwenye kujiamini sana mbele ya wafuasi wake we watueleza eti aliitwa tu kutangaza Jambo Hilo kwa lafudhi yake ya kutishia watu!
Mzee unatuonaje.

Eti utafiti!
Leo unaificha historia ya umuhimu wa Okelo waziwazi lakini unalilia kutambulika kwa Wanaharakati wa Kiislam wa uhuru Tanganyika.

NB.
Naunga mkono hoja ya kutambulika kwa Wanaharakati wa uhuru wa nchi hii Bill kujali itikadi zao za kidini, tamaduni Wala kingine chochote.
 
Ingawa alisaidia lakini pia alitaka kupinuda...
 
Mzee wa kushangaza Sana huyu yaani John O anaonekana katika picha akiwa na silaha na mwenye kujiamini sana mbele ya wafuasi wake we watueleza eti aliitwa tu kutangaza Jambo Hilo kwa lafudhi yake ya kutishia watu!
Mzee unatuonaje.
Eti utafiti!
Leo unaificha historia ya umuhimu wa Okelo waziwazi lakini unalilia kutambulika kwa Wanaharakati wa Kiislam wa uhuru Tanganyika.
Nb.
Naunga mkono hoja ya kutambulika kwa Wanaharakati wa uhuru wa nchi hii Bill kujali itikadi zao za kidini, tamaduni Wala kingine chochote.
Umemaliza kila kitu hapa. Kila kitu.
 
Huyo mzee sideboy wa ajabu Sana eti okelo aliitwa kuwatisha watu kwa sauti yake!
Huyu mzee side ndie huyu hulialia kuhusu kufichwa kw historia ya Wanaharakati was Uhuru wa Tanganyika but Ni yeye anayepinga na kuficha ukweli juu ya kijana huyu wa zamani.
Anataka John Okello afichwe sababu ya Dini yake. Huyu John aliwakomboa Wazanzibar pasipo kujali dini na kabila zao. BABA WA TAIFA HILI LA ZANZIBAR.
 
Dingi...
Siko hapa kubishana.

Mimi namweleza Okello kama nilivyomjua kutokana na utafiti.

Unaweza kuamini utakacho hata bila ya kutafiti.

Hakuna wa kukuzuia.
Kuna tofauti kati ya kubishana na kujengeana uelewa ndg.
Elezea tu hata kidogo kuwa J.Okello alitolewa wapi mpaka kutumika kutoa matangazo ?
 
Back
Top Bottom