Alexander Mnyeti Maji ya Shingo, miradi yake yaanza kufa mmoja baada ya mwingine

Alexander Mnyeti Maji ya Shingo, miradi yake yaanza kufa mmoja baada ya mwingine

Huyu ni miongoni mwa wale waliokuwa wanafaidi matunda ya nchi kwenye utawala wa Awamu ya 5, ni mmoja wa wale viongozi wa ngazi ya chini waliokuwa na Kiburi kilichopitiliza , inadaiwa alikuwa na uhusiano wa Kindugu na John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania .

Mnyeti aliokotwa kutoka kwenye ualimu na kupewa Ukuu wa Wilaya , ghafla akaanza kuwa Tajiri wa kutupwa na dharau na kejeli vikamwingia ( ulevi wa madaraka ) , akapandishwa cheo na kuwa RC , akaanza kumiliki miradi kadhaa ikiwemo timu ya soka inayoitwa Gwambina , akapewa na TCC CLUB na kuiita Gwambina , ili ajenge hostel kwa ajili ya timu yake , akajenga na uwanja wa soka , yaani RC anajenga uwanja wa soka ambao Taasisi nyingi za nchi hii hazina , alikopata hela anajua mwenyewe , japo inadaiwa alikuwa na kolabo na mkubwa kwenye mashimo ya madini (tetesi) , kukawa na mpango wa kupewa Uwaziri , ikabidi kwanza aanzie kwenye ubunge wa Misungwi , wapinzani wakahujumiwa , akapita bila kupingwa .

Waswahili wanasema ukiona ngedere mjini basi ufahamu kwamba kafugwa , mfugaji akifa huyo ngedere atarudi mwituni au atakufa njaa , Sasa kwa kufupisha ni kwamba , Timu ya soka ya Gwambina inayomiliki uwanja wake , ambayo ni Mali ya Mnyeti ,
sasa IMEJIONDOA KWENYE CHAMPIONSHIP kwa kile kinachodaiwa ni kuelemewa na gharama za uendeshaji , Yaani baada ya Magufuli kufa Mnyeti anashindwa kuendesha Timu ! Hivi mnanielewa lakini jamani ?

Neno la leo linatoka kwenye kitabu cha YEREMIA 17 : 5-8

View attachment 2457682

Itaendelea ........
Alexander Mnyeti ni mtoto wa dada wa Magufuli. Huyu ndiyo mtu pekee ambaye wakati wa Magufuli alikuwa na uwezo wa kutaka chochote kwa mjomba wake na mjomba asipindue. Mnyeti akiwa RC Manyara alikuwa ana njia yake ya chini kwa chini ya kutorosha Tanzanite Kyle Mererani, huku Magufuli akituzuga kwa kujenga ukuta.


tuzuga
 
Hakuna aliyeishi kwa kumtegemea mtu isipokuwa mifumo ya kazi iliwalazimu kutegemeana.

Lakini wao walichofanya ni kutimiza wajibu wao kulingana na wakati waliokuwa nao. Kama uliona wamekugonga kwa namna moja au nyingine basi ilikuwa sehemu ya utendaji wao.

Hata Magufuli kilichombeba 2015 ni rekodi ya utendaji wake pamoja na kutofautiana na baadhi ya watu alipokuwa akitimiza wajibu wake kama waziri.

Usipotimiza wajibu utaitwa dhaifu kama mnavyomuita huyu mama kwa sasa kwa staili yake ya nendeni mkalitizame na ukitimiza wajibu utaitwa dikteta. Sasa kazi kwako.

But I am sure about one thing. Hujaelewa mantiki ya andiko hilo...!!

Hata hivyo kwa namna yako unavyoeleza maana ya kutegemeana, basi fahamu haya vilevile;

1. Hata majambazi na watenda uovu mwingine wowote ktk syndicates na mifumo yao ya kihalifu wako very organized na hutegemeana wanapotimiza ajenda zao za ujambazi/uovu...

2. Walimgonga kila mtu direct au indirect so long as mtu huyo ni Mtanzania na raia wa nchi hii. Wewe nawe uligongwa unless uwe "mjinga" hujui athari za ufisadi na rushwa ktk taifa ambalo wewe umo ndani yake...

3. Kiongozi hapaswi kuwa dhaifu (mradi liende) na wala hapaswi kuwa katili mvunja taratibu, kanuni na sheria ktk kutenda wajibu wake kuendesha mambo ya nchi. Aina hii ya viongozi, wote hawafai..!

Natumai umeelewa..
 
Hakuna aliyeishi kwa kumtegemea mtu isipokuwa mifumo ya kazi iliwalazimu kutegemeana.

Lakini wao walichofanya ni kutimiza wajibu wao kulingana na wakati waliokuwa nao. Kama uliona wamekugonga kwa namna moja au nyingine basi ilikuwa sehemu ya utendaji wao.

Hata Magufuli kilichombeba 2015 ni rekodi ya utendaji wake pamoja na kutofautiana na baadhi ya watu alipokuwa akitimiza wajibu wake kama waziri.

Usipotimiza wajibu utaitwa dhaifu kama mnavyomuita huyu mama kwa sasa kwa staili yake ya nendeni mkalitizame na ukitimiza wajibu utaitwa dikteta. Sasa kazi kwako.

Taratibu ziko wazi, tuliona utawala wa ulevi wa madaraka, na uonevu wa wazi. Kama huyo mnyeti alikuwa anafanya kama team work, mbona sasa hivi hafanyi hivyo, au sheria zimebadilika?

Usidhani hatujui tofauti ya utendaji na kiburi cha madaraka. Magu alikuwa ni muhalifu aliyepata madaraka. Kama mama Samia hafanyi anavyopaswa, hilo ni kosa lake kiutendaji, lakini huwezi kuhalalisha utawala wa mabavu na uonevu, eti kisa kuna anayetawala kwa udhaifu. Hatutaki kiongozi mwenye kiburi cha madaraka wala dhaifu.
 
Actually huyu jamaa madaraka yalimlevya sana. Wakati ni RC alikuwa akitoka Mkoani kwake kwenda kunywa wine Mwanza, hiyo wine ilikuwa ni lazima itokee Dodoma. Alikuwa na msafara ambao gari moja ilikuwa inabeba walimbwende wakumfurahisha.Akiwa RC wa mkoa wake alikuwa anatawala pia vituo vya polisi Mwanza, askari wa baadhi ya vituo pale walikuwa wanamuogopa kuliko hata mkuu wa mkoa wa Mwanza. Mtu kama huyu akifilisika sio rahisi watu kumhurumia.
SOURCE. Shemeji wa mhusika.
 
Huyu ni miongoni mwa wale waliokuwa wanafaidi matunda ya nchi kwenye utawala wa Awamu ya 5, ni mmoja wa wale viongozi wa ngazi ya chini waliokuwa na Kiburi kilichopitiliza , inadaiwa alikuwa na uhusiano wa Kindugu na John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania .

Mnyeti aliokotwa kutoka kwenye ualimu na kupewa Ukuu wa Wilaya , ghafla akaanza kuwa Tajiri wa kutupwa na dharau na kejeli vikamwingia ( ulevi wa madaraka ) , akapandishwa cheo na kuwa RC , akaanza kumiliki miradi kadhaa ikiwemo timu ya soka inayoitwa Gwambina , akapewa na TCC CLUB na kuiita Gwambina , ili ajenge hostel kwa ajili ya timu yake , akajenga na uwanja wa soka , yaani RC anajenga uwanja wa soka ambao Taasisi nyingi za nchi hii hazina , alikopata hela anajua mwenyewe , japo inadaiwa alikuwa na kolabo na mkubwa kwenye mashimo ya madini (tetesi) , kukawa na mpango wa kupewa Uwaziri , ikabidi kwanza aanzie kwenye ubunge wa Misungwi , wapinzani wakahujumiwa , akapita bila kupingwa .

Waswahili wanasema ukiona ngedere mjini basi ufahamu kwamba kafugwa , mfugaji akifa huyo ngedere atarudi mwituni au atakufa njaa , Sasa kwa kufupisha ni kwamba , Timu ya soka ya Gwambina inayomiliki uwanja wake , ambayo ni Mali ya Mnyeti ,
sasa IMEJIONDOA KWENYE CHAMPIONSHIP kwa kile kinachodaiwa ni kuelemewa na gharama za uendeshaji , Yaani baada ya Magufuli kufa Mnyeti anashindwa kuendesha Timu ! Hivi mnanielewa lakini jamani ?

Neno la leo linatoka kwenye kitabu cha YEREMIA 17 : 5-8

View attachment 2457682

Itaendelea ........
Nayakumbuka haya majitu ya hovyo yaliyookotwa na mwendazake na kuyaacha sasa yanalia. Makonda, Mnyeti, Byakanwa na mapigaji mengine acha yaanza kuoja joto ya jiwe. Aliyeko juu mngoje chini.
 
Nayakumbuka haya majitu ya hovyo yaliyookotwa na mwendazake na kuyaacha sasa yanalia. Makonda, Mnyeti, Byakanwa na mapigaji mengine acha yaanza kuoja joto ya jiwe. Aliyeko juu mngoje chini.
Yaani huyu Byakanwa natamani hukumu ya Mahakama ya kuharibu shamba la Mh Mbowe Hai,itoke..nakumbuka Mbowe alimshtaki yeye binafsi na si kama DC wa Hai

Yaani nchi ilikuwa ikiendeshwa kama genge la WAHUNI
 
Unathibitisha vipi kama ni mchongo? Vipi kama ana nyaraka kamili za kumiliki?

Kama ni biashara kuna kiongozi gani chadema asiye na biashara pamoja na dili za michongo? na juzi Sugu akiwa iringa akamshabikia Samia kuzuia TRA kukusanya kodi na bado akakiri ni sheria hivyo Samia aifute hiyo sheria ya TRA kukusanya kodi walizozikwepa nyuma.
Ni kazi yako kuthibitisha kama Mnyeti hayo aliyofanya yalikuwa sahihi ili unizodoe , hatuandiki kibwege
 
kilichotokea uwanja wa gwambina umefungiwa hivyo kuwalazimu timu kutafuta uwanja sehemu nyingine na kupelekea gharama kupanda

sio porojo unazo sema
Sasa Mnyeti ni wa kushindwa kusafirisha timu kwa Coaster kweli ?

Hakuna nisichokijua katika hayo unayosema , ila wewe kuna kitu hukijui kwenye andiko langu
 
Namnukuu;

".....5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA. 6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. 7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake. 8 Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda...."

YEREMIAH 17:5 - 8


That's means, Mnyeti aliishi kwa kumtegemea mtu na haya yanayomtokea ni matokeo yake maana tegemeo lake (mwanadamu) aitwaye Magufuli hayupo tena..

Si huyu tu. Wako wengi mno. Mfano yupo mwingine maarufu sana wakati ule kwa matendo maovu na ya kikatili tena kijana mdogo sana anaitwa Ole Lengai Sabaya, naye kosa hili la kuishi kwa kumtegemea mtu/mwanadamu kama kiini cha uhai wake kifedha na kimwili linamtafuna kwelikweli...

Na yupo mwingine vilevile maarufu sana nyakati hizo kwa matendo maovu na ya kikatili dhidi ya binadamu wenzake Paul Christian Makonda a.k.a Albert Bashite naye anacheza kwenye moto huu huu kwa kosa la kumtegemea binadamu kama kiini cha uhai wake kifedha na kimwili...
Amen
 
Ni kazi yako kuthibitisha kama Mnyeti hayo aliyofanya yalikuwa sahihi ili unizodoe , hatuandiki kibwege
Unapomtuhumu mtu kwa tuhuma nzito kama hizi jitahidi pia kuweka na evidence. Usisahau we unatokea kikundi cha watu waliomtuhumu lowasa kwa miaka nane kuwa ni fisadi na mwizi na ilipofika 2015 kikundi hicho hicho kilipokuwa na lowasa kikasema mwenye ushahidi wa ufisadi wa lowasa aende mahakamani.
Kwa hiyo tupo makini kwa sasa na tuhuma zozote nzito zinazotolewa na watu wa karba yenu.
 
Alexander Mnyeti ni mtoto wa dada wa Magufuli. Huyu ndiyo mtu pekee ambaye wakati wa Magufuli alikuwa na uwezo wa kutaka chochote kwa mjomba wake na mjomba asipindue. Mnyeti akiwa RC Manyara alikuwa ana njia yake ya chini kwa chini ya kutorosha Tanzanite Kyle Mererani, huku Magufuli akituzuga kwa kujenga ukuta.


tuzuga
Asante kwa taarifa hii muhimu
 
Magufuli hakua tajiri
Ila huu huu wizi hapa alifanya mama yako au? 👇
Screenshot_20220415-072852.jpg
Screenshot_20220415-140726_1.jpg
Screenshot_20220520-171316.jpg
1650491737485.png
Screenshot_20221105-124332.png
Screenshot_20220719-125637.png
Screenshot_20220719-125655.png
 
Back
Top Bottom