Ali Kiba atambulisha rasmi label yake(Kingmusic) aachia nyimbo mpya "SINA".

Ali Kiba atambulisha rasmi label yake(Kingmusic) aachia nyimbo mpya "SINA".

Mkuu alikiba namuonea huruma sana naomba niwanufaishe na wengine kwa USHAURI HUU,kwenye level ya familia yangu ninachakumjuza huyu bwana ,tukiwa kwetu marangu tulizaliwa watoto 4 wa familia moja tukiwa wadogo tulianza biashara ndogo ndogo wenzangu walikuwa na hulka ya kushindana sana ,mimi nilijitenga na ushindani huo kabisa leo hii mimi namaisha ya kawaida mazuri nyumba mbili tatu vigari vya kutembelea na tulodge ,sasa wenzangu wako so active ,so competitive wote ni matajiri sana wana misemi kibao maghorofa uchafu ,lakini nimewazidi kitu kimoja na wanakili AMANI YA MOYO,wote kwanza hawaongei kabisa wao kwa wao na hata wake zao wamerithi wanaendeana hadi kwa waganga ,wote walevi wa kutupwa na wawili wanavisukari ,wote wananipenda sana na huwa hawamalizi mwezi huja kulala na wake zao kwangu ,ila wao kwa wao hawakaribishani na husemana vibaya sana ,imerithi hata watoto wao ni wa hivyo hivyo walevi na wakorofi ,mimi namaisha ya kushinda kanisani na kushukuru kwa kidogo kinachonitosha nina amani sana...SOMO maishani usikubali kuwekwa kwenye trap ya kushindana mbio ni kweli utaweza fika mbali ila utakuwa restless maisha yote maana daima wakukuzidi atakuwepo pangilia unataka ufike wapi kadiria spidi iendee ndoto yako .UTAKUWA NA AMANI ...Haka kawimbo hakafai hata kuimbwa na beka flavor ni kakawaida sana imagine presha anayoipata kiba akipita mitaa ya Dar kila mahali jibebebebe
Hii story ya ushindani kwa wachaga ni kawaida sana.
Anyway, mmojawapo wa kaka zako ni yule aliyeoa msilamu nini?
 
Kazi nzuri vijana, endeleeni kuleta vitu vizuri zaidi.

Kuna vijana wanachuki za ajabu hadi unashangaa. Wasanii mbalimbali wanatoa nyimbo kila siku, baadhi nzuri nyingine mbaya, lakini huwezi kuona comment za chuki kama Kiba anapotoa nyimbo zake
 
Kazi nzuri vijana, endeleeni kuleta vitu vizuri zaidi.

Kuna vijana wanachuki za ajabu hadi unashangaa. Wasanii mbalimbali wanatoa nyimbo kila siku, baadhi nzuri nyingine mbaya, lakini huwezi kuona comment za chuki kama Kiba anapotoa nyimbo zake
Upumbavu eti ndio nyimbo kwendraaa
 
Upumbavu eti ndio nyimbo kwendraaa
Kwanini matusi, huwezi kutoa maoni yako bila kutumia lugha ya kuudhi?

"Nyimbo" ndiyo nini? Umesoma kiswahili kweli wewe shuleni?

Kama kitu hujakipenda, unataka kulazimisha kila mmoja asikipende?
 
Kwa wimbo huu naona hata Harmonize nae kamuacha mbali kiba. Bora hata mack muga kuliko hii nyimbo
 
Ali Kiba kama anataka afanye muziki wa kipekee basi atafute muziki wa pekee yake sio huu wa ushindani, atajikuta anakimbia mbio ambazo hawezi.

Sijawahi kupenda wimbo wa Ali Kiba mbali na Karim, kama unajua vyema na una sikio la kusikiliza utagundua Ali Kiba ni mzuri sana kwenye Rumba/Zuku tena akiimba kwa sauti original sio hii ya Yooooooo!


Sikiliza kwenye wimbo wa Karim kuna baadhi ya maneno Ali alikuwa anapachika kwa sauti yake halisi na kufanya ule wimbo kuwa mzuri kwangu sijajua kwa wengine.

Ali hawezi kuimba bongofleva siku zote atapuyanga anabana sauti akijua ndio ataimba vizuri kumbe utumbo tu.

Producer wake amshauri jamaa ajikite kwenye rumba au Zuku na aimbe kwa uhalisia wa sauti yake sio kulialia yoooo kama Mbuzi jike anataka kupandwa.
Duh
 
Msanii nguli nchini Tanzania Alike a maarufu KingKiba ametambulisha rasmi lebal yake ya King Music kwa kuachia nyimbo mpya ya pamoja akiwa na wasanii wake. Enjoy
Huyu jamaa,nyimbo yake niliyoipenda ni Cinderella,dushelele,nakshi nakshi,zingine zote huwa naona hamna kitu,
 
Bila ushabiki nyimbo nzur
Video safi
Location nzur
W
Wasanii wote wako poa kama ww unaweza katoe yako tuone
 
Naona kama wote wana sound kama Kiba

Yaani sauti za hawa bongo fleva ni kama ile ile. Ukisikiliza audio huwezi kujua yupi ni yupi!
Tuleteeni sauti tofauti jamani. Hii moja sasa inaboa..
 
music ni sawa na fashion ni muhimu kuzingatia muda. Hata mababu zetu walitembea uchi zama zilizopita,
 
Msanii nguli nchini Tanzania Alike a maarufu KingKiba ametambulisha rasmi lebal yake ya King Music kwa kuachia nyimbo mpya ya pamoja akiwa na wasanii wake. Enjoy

Ameachia NYIMBO Mpya au Wimbo Mpya?
 
Back
Top Bottom