Ali Kiba: Diamond Platnumz unikome, Nikuweke uchi watu wajue unayonifanyia?

Ali Kiba: Diamond Platnumz unikome, Nikuweke uchi watu wajue unayonifanyia?

Ukikosea maisha unahisi kila mtu mbaya wako kama wote waliosema Ruge anawanyonya leo Ruge kafariki bado wapo pale pale wanagundua mchawi wao ni wao wenyewe.
Kiba kakosea maisha?basi watanzania matajiri sana
 
"Ukitaka nikuweke uchi na hata kwenye hilo tamasha hatokuja mtu"

Sijaelewa hapa!! au kwamba utatokea msiba!!! Watu wasihudhulie
 
Alikiba kazingua sana sio kidogo, japo kuna upande wa pili wa sarafu ambayo bado haijawa revealed huenda kukawa kuna jambo kubwa liliopelekea yeye kuandika hivyo.

Lakini kwa hii script alikiba ameonesha panic, na sidhani kama kutakua hakuna sababu ya msingi ya yeye kufanya hivyo.

Binadamu tumetofautiana, kila mtu ana hasira ila utofauti unakuja kwenye namna ya kui control hasira yako (kufikiria kabla ya kufanya maamuzi).

Diamond inaonekana hana panic ya haraka hiyo ni kutokana na uwezo wa kuimudu hasira yake pale anapokwazika

Alikiba namuweka kwenye kundi la watu ambao wanaathiriwa na hasira zao wenyewe, anaweza akawakweli amekosewa ila namna ya kuelezea hizo feelings zake akatumia ghadhabu na panic ya juu


Lakini hata hivyo sio alikiba tu ambaye kaongea kauli zisizo na adabu, hata mhasimu wake alishawahi kuimba kua "kumfananisha yeye na sinderela haiwezikua freshi" lakini hakuna mtu hata mmoja hapa aliyegusia hilo kua diamond alishawahi kutoa maneno ya shombo bali karibia wadau wote mmemu attack alikiba kua katoa maneno ya kashfa.

Naona watu wamekomaa kusema neno UNIKOME hutumiwa na wanawake, lakini siwaoni wakisema kua eleni, wanja, vikuku nk hutumiwa na wanawake.

Fid Q Alisema

Hawaamini kwenye kuunda diamond na kiba wawe wawili, wanachoamini nikumshusha mmoja ili mmoja awe dili/

cha kupewa hakishibishi ukipewa lazima ukumbushwe, dunia mwendo wa ngisi kung'aa so lazima staa ashushwe/

Nikki mbishi naye alisema kama unatafuta kiki basi Mdisi alikiba ama timu simba uone, unavyokua staa kesho early in the morning.
 
Kipindi kile Kiba anarudi kwenye game,mtu ambaye alikuwa mdomoni kwake ni Diamond,katafuta kiki kwa Mondi ,kila akihojiwa mara hoo dogo aniheshimu,mara dogo amefuta verse yangu mara sijui nini,kila interview yake alikuwa akimponda Mondi alikaa kimya.Nakumbuka alijibu issue ya hiyo kufuta verse ya kiba ktk nyimbo ya lala salama,baada ya kiba kufuta verse yake ktk single boy(kwa sababu hii kwangu mimi beef lao naona ni la kitoto).Kaendelea kumwongelea mwenzake -ve kweli akafanikiwa kusimama tena kwenye game.

Zikaja kampeni za KILI MUSIC AWARDS baadhi ya media plus team, team Wema,Team Jokate na Team Kiba (Team ndipo zilipozaliwa kwenye mziki) zikaaungana ktk tuzo za KILI,kweli Diamond kuna baadhi ya tuzo wakambania,Mungu si Athuman mwaka huo huo MTV MAMA wakampa tuzo ya Best entertainer.

Jamaa baada zile team,chuki zilizosambazwa na Kiba na team za ma-ex wake ,Diamond akazomewa Fiesta.Mungu si Athumani akapambana we ,mwaka 2015 kwa mujibu wa EMC Kenya ,Mondi akaendeleza record ya kuwa msanii anayesikilizwa sana kwenye Radio na TV,hii ilimfanya apate zaidi ya mil 600.Mpaka sasa jama ana utitiri wa show,ubalozi kwenye kampuni mbalimbali na kila anachogusa kinakuwa almasi kama jina lake.

Ukiyaangalia haya matukio utakuja kugundua,alieanza maswala ya kumungelea mwenzie kwa kumpaka matope ni Kiba na hali kama hii iliyomkuta Mondi kama ingemkuta kiba nahisi angedata.

Zamani Mondi alikuwa akipayuka akiulizwa maswala ya kiba,ila siku hizi anavyo react kama hakuna kitu.Ila WCB wana kauli yao mbiu,kama ukijaribu kutengeza beef ,wao lile BEEF wanaligeuza linakuwa BIASHARA kwao.WCB hapa wanacheza mind game.
 
Nimeona mpaka nikashangaa kwamba ni yeye kweli, nimeingia akaunti ni ya kwake. Ameandika kwa uchungu sana kama ni yeye. Hawakawii kusema akaunti ilikuwa hacked.
Dah kweli kaandika kwa uchungu mpk kamtag jamaa kwa mara ya kwanza kabisa
 
.
FB_IMG_15725172525969903.jpeg
 
Back
Top Bottom