Kwa kipindi kirefu jamii ya kitanzania hasa uwanja wa siasa na dini zilibugukiwa na sintofahamu ya mtu anayeitwa Daudi Albert Bashite. Tuhuma nyingi na nzito zilielekezwa kwa mkuu wa Mkoa Dar-es-Salaam aka Paul Maonda akituhumiwa kuwa alitumia majina na vyeti vya kugushi (Criminal offence) huku majina yake kamili yakiwa ni Daudi Albert Bashite
Jana akiwa Kisarawe, Bwana Makonda alifanya kitendo cha ajabu sana kwa kumuita mlevi wetu wa Taifa, Pierre Gambo “Perre Konki Liquid” kuwa mtu wa hovyo. Ilhali Pierre anatumia umaharufu alioupata kujipatia riziki yake kihalali. Huku Makonda ambaye anatuhumiwa kugushi vyeti kujipatia ajira kwa udanganyifu. Kati ya hawa watu wawili, nani ni mtu wa hovyo? Makonda ni mtu wa kukaa jela siyo mtu wa kunyoosha kidole kwa mwingine na kujiona malaika
Hakuna binadamu wa hovyo mbele za muumba. Ndugu Makonda hana haki ya kumuita mtu yeyote kuwa wa hovyo. Nadhani jamii; wanasiasa, viongozi wa kidini na kijamii wafike sehemu wakemee hii tabia aina ya Makonda. Yeye mwenye tuhuma nzito ambazo ni criminal in nature, anamhukumu mtu anayetumia jasho lake kujipatia rizki. Makonda must be condemned by every sane minded human being.
Makonda asiwe kama nyumbu. Anasahau vitu kirahisi hivyo.......Unamcheka mwenzio kuwa na kengeza wakati una jicho moja? Huu udhalilishaji usiruhusiwe katika jamii ya kitanzania