Alikiba sio wa kufa kimziki leo, bado sana

Alikiba sio wa kufa kimziki leo, bado sana

Its Pancho

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
15,966
Reaction score
26,404
1686857643787.png

Wakuu,

Alikiba huyu ni mkongwe kama tujuavyo. Kadri muda ulivyosogea watu walitabiri kifo chake cha kimziki, ingawaje wale alioanza nao kuimba wengi wamepotea.

Nimesikiliza hizi nyimbo mbili latest; Mahaba na On fire, niseme tu huyu mtu bado sana kupotea, sio leo wala kesho, hii on fire niliiona huko tiktok tu!

Anajitahidi sana.
 
Mie sijui unaongelea nini...Kipindi Ali kiba ametoa seduce me kuna jamaa yangu mmoja alinipigia simu muda huo huo ngoma ilipoachiwa na mimi nikaipakua muda huo huo,from there nikawa ninaicheza non stop kwenye simu yangu.

Kipindi hiko Ali kiba alikuwa anabembelezwa aachie ngoma,watu wanakaa wanasubiri ngoma za Ali Kiba.Hapa katikati sijui nini kimetokea,nahisi pumzi ya Kiba imekata,au uwezo ndio umeisha,au labda yeye ameridhika na amechoka kusukumwa na mashabiki zake kwenda kule ambako yeye hataki kufika.

Mimi pia nilichoka kumfuatilia Kiba. Juzi nipo kwenye gari natoka town,nasikia kwenye radio ya gari presenter anasema nyimbo ya Kiba imeshuka kwenye chat.

Niliwaza kiasi,Kiba anatoa ngoma siju? Inaingia top ten sijui?inapanda na kushuka chat sijui? Jamaa yangu aliyekuwa ananipigia simu Kiba akitoa ngoma nae hapigi siku hizi,wala sijui kama anafahamu kuwa Kiba katoa ngoma.
 
Mie sijui unaongelea nini...Kipindi Ali kiba ametoa seduce me kuna jamaa yangu mmoja alinipigia simu muda huo huo ngoma ilipoachiwa na mimi nikaipakua muda huo huo...
Useme hapo tatizo ni kuwa anakaa muda bila kutoa ngoma ila kusema sijui ameshuka chat sio kweli nenda kaangalie mbona anatrend?

Kuhusu kupenda wimbo hapo tunatofautiana ladha na sikio.
 
Ulikuwemo humu jukwaani kipindi cha Ali Kiba VS Diamond?
Useme hapo tatizo ni kuwa anakaa muda bila kutoa ngoma ila kusema sijui ameshuka chat sio kweli nenda kaangalie mbona anatrend?

Kuhusu kupenda wimbo hapo tunatofautiana ladha na sikio.
 
Ulikuwemo humu jukwaani kipindi cha Ali Kiba VS Diamond?
Halafu mkuu ni lazima alikiba ashindane na diamond?

Mambo haya haya ndo yamempoteza aslay.

Anafanya mziki wake basi
 
Halafu mkuu ni lazima alikiba ashindane na diamond?

Mambo haya haya ndo yamempoteza aslay.

Anafanya mziki wake basi
siongelei ushindani wa Ali kiba na Diamond,naongelea kipindi ambacho Ali Kiba alikuwa katika kilele cha mashabiki. Nyuzi kama hii uliyoleta nilitegemea kuiona kipindi hiko.Watu walimpenda Ali Kiba wakachoka. Mada yako ya kisasa lakini humu inaweza kuonekana ipo nyuma ya wakati sababu watu walisha-move on.
 
Niliwahi ona clip Ali Kiba anaimba bila beat ule wimbo alioimba na Ommy Dimpoz...ilikuwa balaa sana ...
Sijawahi ona mwanamuziki anaimba bila beat Tz nikafurahia zaidi ya Ali Kiba na Christia Bella
 
siongelei ushindani wa Ali kiba na Diamond,naongelea kipindi ambacho Ali Kiba alikuwa katika kilele cha mashabiki. Nyuzi kama hii uliyoleta nilitegemea kuiona kipindi hiko.Watu walimpenda Ali Kiba wakachoka. Mada yako ya kisasa lakini humu inaweza kuonekana ipo nyuma ya wakati sababu watu walisha-move on.
Mbona unaongelea opinion za watu mkuu?
Sema wewe umechoka sio watu mbona Mimi sijachoka.

Wewe umechoka wapo ambao hawajachoka.
Kwahiyo zile trending kule inakuwaje hapo?
 
Niliwahi ona clip Ali Kiba anaimba bila beat ule wimbo alioimba na Ommy Dimpoz...ilikuwa balaa sana ...
Sijawahi ona mwanamuziki anaimba bila beat Tz nikafurahia zaidi ya Ali Kiba na Christia Bella
Mkuu alikiba ni msanii complete.

Huwa hata live anaimba pia hata huyo ommy dimpoz yuko vizuri shida hawa wanatoa nyimbo Mara moja moja japo ali ana project yake sasa hivi nadhani.
 
Niliwahi ona clip Ali Kiba anaimba bila beat ule wimbo alioimba na Ommy Dimpoz...ilikuwa balaa sana ...
Sijawahi ona mwanamuziki anaimba bila beat Tz nikafurahia zaidi ya Ali Kiba na Christia Bella
Long live the king😍😍😍
 
siongelei ushindani wa Ali kiba na Diamond,naongelea kipindi ambacho Ali Kiba alikuwa katika kilele cha mashabiki. Nyuzi kama hii uliyoleta nilitegemea kuiona kipindi hiko.Watu walimpenda Ali Kiba wakachoka. Mada yako ya kisasa lakini humu inaweza kuonekana ipo nyuma ya wakati sababu watu walisha-move on.
Watu wamemove on wapi au ww ndo umemove on ?
 
Back
Top Bottom