Aliniacha kwa fedheha, lakini leo anahitaji msaada wangu

Aliniacha kwa fedheha, lakini leo anahitaji msaada wangu

Jina lake linaanzia na M ni binti wa kaskazini mwa Tanzania mwenye level ya diploma katika upande wa elimu.

Ni binti nilie mpenda kutoka moyoni, shida zake zote zilikuwa zangu niliakikisha anakuwa happy muda wote.

Nikaenda kujitambulisha kwa wazazi wake ndugu na jamaa zake, nikaanza kuweka mikakati ya kutaka kumuoa.

Mwaka jana binti akadai anataka kwenda kusoma (kuongeza elimu) nikakubali kwa shingo upande sana sana sana (maana ada sikuwa nalipa mimi, ni wazazi wake), nilikubali uku nikiwa naona penzi na mipango ya ndoa ndio inaingia mchanga (kwa waliopita vyuoni nadhani mnaelewa ofu iliyokuwa inanitawala),

Binti akafika chuo mwaka wa kwanza hapa hapa jijini DASILAMU mabadiliko yakaanza kwenye semieter ya kwanza katikati, kiburi kikaanza, binti hakawa tena hataki mawasiliano na mimi, nikaanza kupata wakati mgumu sana maumivu ya kichwa juu ya penzi ilo yakaanza, ikabidi niingie chimbo kuanza kuchunguza ili niwe na majibu ya uhakika.

Kumbe alishapata mtu mpya chuoni, binti nikawa simuambii kitu tena akanisikiliza, binti nikawa simpigii simu akapokea, simtumii sms ikajibiwa, siku ya tarehe 14/02/2021 aliniambi ivi "Wewe nini umesahau kwangu mbona ujiongezi, ebu sema kuna ulicho acha nikupatie ili usiwe unanitumia sms na kunitafuta kwa simu zako, naomba niseme ivi sikutaki ili uelewe kama umeshindwa kujiongeza na waambie wote wanaojua mahusiano yetu its over now na waambie ndugu zako wasinisumbue pia" nilibaki nimebungaa kama nimepigwa na shoti za umeme.

Nikatamka neno moja tu moyoni "mungu najua ntapita kwenye tanuru ili, na kila kitu juu ya aya maisha yangu unayo wewe, nashukuru umenibariki sana kufika hapa ngoja nifanye kazi kwa bidii ntapata wa kunifaa" Mawasiliano yakaishia hapo japo kwa maumivu makali mnooo.

Ilipita miezi kadhaa.

Napokea simu kutoka kwa M akidai anataka tuongee, nikamsikiliza ilikuwa ni simu ya kutaka kuniomba msamaa kwa kilicho tokea, anadai ata yeye haelewi nini kilimpata (nikaona izi ni soud tu za mabinti wa kileo) nikamuambia tu sawa nilisha kusamehe muda tu na nakutakia kila lenye heri kwenye maisha yako na mtu wako mpya..

Ni binti ambaye maumivu yake bado yanaishi kwenye kumbukumbu ya maisha yangu mpaka ivi sasa,

Nadahani mnaelewa dunia ya sasa bila connection mambo yanakuwa magumu sana, nashukuru mungu mimi naishi vizuri sana na watu tofauti tofauti kwenye sector nyingi nina watu ambao kama ikitokea changamoto falani naweza wafata wakanisaidia kwa uharaka zaidi, na uyo binti analielewa ilo kabisa ameshapata changamoto nyingi uko nyuma ila nilikuwa natumia connection za watu nilio nao kusolve kwa uharaka kabisa.

Sasa uyu binti kwa sasa anasumbuliwa na changamoto flani flani amabyo anadai kama isipokuwa solved kuendelea kwakwe kwa shule kutakuwa na changamoto kubwa sana, iyo changamoto yake kwangu haitachukua ata siku mbili kuisolve kama nikichukua jukumu ilo la kumsaidia,

Baada ya kupata changamoto iyo kwa sasa ndio amekuwa akinitafuta na kuniomba niwe msaada wake.... sijawai kujibu sms zake ambazo kila akituma lazima aniombe nimsaidie kwenye ilo tatizo, sijawai pokea simu zake maana najua ataanza tu kunielezea ilo tatizo na mimi sikutaka kushughulika na mambo yake kwa sasa maana yupo kwenye mahusiano mengine.

Je wangwana wana jamiiforum wenzangu, watu wangu wa nguvu ambao tumeshawai kupitia changamoto za kuumizwa na walio tuumiza kesho wanataka msaada wetu mnashaurije kwenye ili maana bado nina kidonda moyoni

Note: nilikaa nae kwenye mahusiano miaka 4.

Karibuni kwa mawazo yenu wana JF.
Show the character of a gentleman. Kama ulivyosema kuwa unaishi vizuri na watu hata yeye ni mtu pia. KAMA UNA UWEZO WA KUMSAIDIA MSAIDIE ILA SI KWA MANUFAA YAKO. YAANI MSAIDIE HATA KAMA HUNA NIA YA KUMRUDIA.

You never know your tomorrow. So don't set barriers.
 
Isafishe nafsi yako kwa kuachia msamaha na alama ya mtu aliyesamehe ni kuwatendea wema wale waliotukosea......

Wanadamu ni viumbe wenye kubadilika badilika ndio maana hata Mungu anatuasa kuwa tunakubaliana jambo basi kuwe na mashahidi kwa kuwa kiumbe mwanadamu ana kawaida ya kubadili maamuzi......

Kama yeye amekubadilikia ndivyo ambavyo pengine na wewe ungembadilikia.....

Kama umeamua kumsamehe na kuendelea na maisha mengine basi hupaswi kumuwekea kinyongo na kama jambo lipo ndani ya uwezo wako wewe msaidie kwani Mungu pekee ndiye anayelipa wema na sio mwanadamu........

Kukubali kumsaidia kutatoa tafsiri kuwa umesamehe na kumsahau na umeamua kuendelea na maisha yako bila ya yeye na uwepo wako mbele ya macho yako haukupi shida...

Kukataa kumsaidia kunakutafsiri kuwa bado una kinyongo na upo kwenye mateso makali baada ya kuvunjika kwa mahusiano yenu...........

Vaa uanaume, jitoe kwenye tope la visasi na chuki achia upendo na ubinadamu na hiyo ndio fimbo na funzo kwa watesi wako.......
Ushauri mzuri ila ulitakiwa kutolewa kuanzia miaka ya 1990 kurudi nyuma. Hawa wa kuanzia miaka ya 1990 kuja leo tunadeal nao kiume kama vile wao wanavyodeal kiume.

Wanawake wenye busara na hekima huwa hawafanyi huu upuuzi. Mtu wa namna hii akisaidiwa tabia ya kiburi na mapembe ya jeuri huwa vinakuwa maradufu na hatoweza kujifunza kwa matendo yake.

So be it, hakuna mtu anaehukumiwa sababu alichagua kumpotezea mtu aliyemdhuru kwa kusudi sababu hata maneno ya hekima yanatuagiza kuachana na kuwakalia mbali wale wanaotukorofisha kwa makusudi kisha wanapaza sauti zao kulalamika tusipowarudi.
 
mkuu kama hiyo aya yote ni neno moja basi nikusalim tuu kwa jina la jamhuri ya muungano wa tanzania

Sent from my M2101K7AI using JamiiForums mobile app
Hahahahahhahahahahahahahaha mzee baba hunaga baya 😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅
 
Show the character of a gentleman. Kama ulivyosema kuwa unaishi vizuri na watu hata yeye ni mtu pia. KAMA UNA UWEZO WA KUMSAIDIA MSAIDIE ILA SI KWA MANUFAA YAKO. YAANI MSAIDIE HATA KAMA HUNA NIA YA KUMRUDIA.

You never know your tomorrow. So don't set barriers.
Yeye hawezi kuwa mtu! Ili neno naomba lisitumike vibaya. Ukiskia yule jamaa “mtu” kweli yani jua kabisa ana character zote za kibinadamu zikitawaliwa na huruma na hekima!

Tabia ya usaliti ni tabia ovu haikubaliki popote duniani wala mbinguni. Na ndio maana shetani yupo duniani anapuyanga tu baada ya kutimuliwa peponi!
 
msaidie hiyo changamoto yake,
ILA MAMBO YA MAPENZI NAYE PAMOJA NA NDOA ACHANA NAYO.......

Tnda wema nenda zako.
Hakuna mnamtetea nini huyo mpuuzi😅 she must taste the blood of her own flesh! Itamsaidia wakati mwengine akiwa na mtu aache tabia ya kuangalia maslahi yake tu.
 
Yeye hawezi kuwa mtu! Ili neno naomba lisitumike vibaya. Ukiskia yule jamaa “mtu” kweli yani jua kabisa ana character zote za kibinadamu zikitawaliwa na huruma na hekima!

Tabia ya usaliti ni tabia ovu haikubaliki popote duniani wala mbinguni. Na ndio maana shetani yupo duniani anapuyanga tu baada ya kutimuliwa peponi!
noted
 
Ushauri mzuri ila ulitakiwa kutolewa kuanzia miaka ya 1990 kurudi nyuma. Hawa wa kuanzia miaka ya 1990 kuja leo tunadeal nao kiume kama vile wao wanavyodeal kiume.

Wanawake wenye busara na hekima huwa hawafanyi huu upuuzi. Mtu wa namna hii akisaidiwa tabia ya kiburi na mapembe ya jeuri huwa vinakuwa maradufu na hatoweza kujifunza kwa matendo yake.

So be it, hakuna mtu anaehukumiwa sababu alichagua kumpotezea mtu aliyemdhuru kwa kusudi sababu hata maneno ya hekima yanatuagiza kuachana na kuwakalia mbali wale wanaotukorofisha kwa makusudi kisha wanapaza sauti zao kulalamika tusipowarudi.
noted
 
Songa mbele kurudi nyuma mwiko achana nae asaidiwe na huyo nsomi mwenzake. Dawa ya moto ni moto.
 
Hakunaga hio [emoji28] hilo alilofanya huyo mwenzenu ni kusaliti kambi wala sio kumkataa! Alitakiwa agome kuwa nae toka Chugga huko!
Ndo mnapokoseaga maisha na msaada ni zaidi ya ngono aka zinaa kitu kiko ndani ya uwezo wako why usitoe msaada kwa mtu. Toa msaada then sepaga huyo dada ndo atapata revenge nzuri bila kumrudia
 
kama shida yake haikugharimu sana wewe hebu msaidie mkuu uokoe kizazi chake, kukoseana kwenye mapenzi kusikufanye usimsaidie shida za kibinadamu
 
Ngoja sasa nikuambie Jambo rafiki. Huyo dada alikuacha baada ya kujihakikishia hana anachohitaji toka kwako. Na alipokuambia hakupendi hakuwa anatania, alikuambia ukweli. Ndo maana akakupa ruhusa uwaambie ndugu zako na rafiki zako.

Usithubutu kusogeza tena karibu yako. Kama yeye hakujal hisia zako, wewe kwann uanze kuwaza sana juu yake.
Acha ujinga na utegemezi wa kihisia.
Ili hakuheshimu na kuwaheshimu wanaume wajao kwake mfungie vioo.
 
Back
Top Bottom