TANZIA Aliyekuwa Askofu Mkuu wa TAG, Prof. Rainwell Mwenesongole wa Upanga CCC ametwaliwa na Bwana!

Ni kweli kabisa.

Askofu mkuu wa sasa wa TAG ni Dr Barnabas Mtokambali
 
Unajua inachukua muda gani mpaka mtu anapata daraja la upadre?

Kila mtu huwa jobless kabla kuwa na kazi husika mkuu.

Kingine utaratibu wa kanisa katoliki huwezi linganisha na makanisa mengine.
 
Kusifia na kubariki yanayotendwa na watawala hapo wako sahihi??
Kubariki kivipi? Ulishaona bajeti ya serikali ikipelekwa kanisani kubarikiwa au katiba pendekezwa au iliyopo ulishawahi ona inapelekwa kanisani kubarikiwa?


Kushukuru sawa wanashukuru mfano serikali imetoa mchango jengo la kanisa hutaki washukuru? Au imekarabati barabara ya kwenda kanisani wasishukuru?
 
Hawa maaskofu hawanaga faida, wapiga dili tu sikuwahi kumsikia akihubiri haki
 
Unajua inachukua muda gani mpaka mtu anapata daraja la upadre?

Kila mtu huwa jobless kabla kuwa na kazi husika mkuu.

Kingine utaratibu wa kanisa katoliki huwezi linganisha na makanisa mengine.
Swala Sio muda mtu anatumia kufikia upadre issue ni kuwa kabla kuwa padre anakuwa jobless anaupata upadre akiwa jobless
 

Asante Mkuu kwa ufafanuzi
 
Acha kulinganisha mapadri wa Kanisa Katoliki na wachungaji wa ajabu ajabu!
 
Unajua inachukua muda gani mpaka mtu anapata daraja la upadre?

Kila mtu huwa jobless kabla kuwa na kazi husika mkuu.

Kingine utaratibu wa kanisa katoliki huwezi linganisha na makanisa mengine.
Usihangaike naye huyo halijui Kanisa Katoliki kwa hoja zake wote waliopo kazini walikuwa majobles Kanisa Katoliki huanza kuandaa mapadri tangu kidato cha kwanza kwenye shule zao zinazoitwa seminari ndogo wapo wachache sana wanaopata wito wa upadri ambao hawakupitia seminari ndogo lakini lazima wapitie seminari kusomea falsafa na teolojia upadri haupatikani kwa kujitangaza mwenyewe
 
Hiyo tafsiri yako kuwa Askofu ni mtumishi wa Mungu hivyo hapaswi kuwasemea na kuwatetea wanadamu ni tafsiri potofu kwa 100%.

Kama askofu hawezi kuwasemea na kuwatetea wanadamu wanaomzunguka huyo sio mtumishi wa Mungu bali ni tapeli wa kawaida sana kwa mgongo wa dini.

Wakati ule kanisa lake lilipokuwa linamsemea na kumpongeza Magufuli, halikujua kuwa Magufuli naye ni binadamu?

Utasemaje unampenda Mungu kama huwezi kumpenda jirani yako?
Kama kuna mamilioni ya watanzania wanateswa kwa dhuluma za Serikali, na wanakwenda kila jumapili kanisani kumlilia Mungu na kutoa sadaka zao, halafu wewe Askofu unapokea sadaka zao na kuzitafuna halafu hapo hapo unaogopa kufungua mdomo wako kuwasemea au kuwatetea watu hao dhidi ya serikali inayowatesa, wewe ni muovu mkubwa, na mbinguni unaweza usiingie.
 
Alianza safari ya utumishi akiwa kijana sana na aliacha kazi ili kuhudumu kwenye injili akiwa ofisa wa juu sana serikalini. Sasa Mtumishi ameondoka kwa Amani ya Bwana
 
Hakika mkuu.

Huduma yake ilianzia Kinondoni A miaka ile ya 1979 kisha akahamia Kisutu girls kabla ya kujenga Kanisa kubwa hapo Olympio opposite na Mzumbe.
Ni Askofu aliyewezesha wengi kumfuata Mungu, alianzisha program mbalimbali za vijana kujiendeleza kiroho na kijamii, bendi ya vijana pale CCC ect
 
Nafahamu kuwa alishastaafu hicho cheo cha uaskofu mkuu wa TAG, lakini hakuwahi kustaafu cheo cha uaskofu na wala hakuwahi kuacha kazi yake ya kuhubiri au kulisemea kanisa lake la TAG pale City Christian Centre. Hivyo maovu yaliyofanyika nchi hii na yeye akiwa anayaona lakini akaogopa na kukaa kimya yanamhusu kwa 100%.

Swali kuu, kwa miaka mitano ya utawala wa ukandamizaji wa Magufuli, yeye alikuwa anasema nini?
Ule uchafu uliokuwa unafanywa na wapontekoste wenzake (TAG ikiwa ni kinara) wa kumsifia na kumpamba Magufuli, yeye aliweza kuchukua hatua gani?

Ule ubunge wa wizi ambao mtoto wake alizawadiwa na CCM kule Songwe ilikuwaje akaubariki?
 
Alianza safari ya utumishi akiwa kijana sana na aliacha kazi ili kuhudumu kwenye injili akiwa ofisa wa juu sana serikalini. Sasa Mtumishi ameondoka kwa Amani ya Bwana
Kuondoka ameondoka lakini amani ya Bwana sina hakika kama ameenda nayo. Yaani watu wauawe, wateswe na kudhulumiwa mbele yako huku ukipiga makofi na kushangilia halafu ufe na uende na amani ya Bwana? How? Masihara haya.
 
Acha upumbafu wewe..manabii na mitume walikemea wazi wazi watawala wabovu na wala hawakuogopa..unadhani kichwa cha yohana mbatizaji kilikatwa kwasababu gani?.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swala Sio muda mtu anatumia kufikia upadre issue ni kuwa kabla kuwa padre anakuwa jobless anaupata upadre akiwa jobless
Naona huelewi unachokizungumza hasa kwa wakatoliki.
Kwa sisi wakatoliki kusomea upadri ni kama kusomea udaktari ama fani nyingine yoyote na hivyo huwezi kuzungumza habari ya jobless.
Vijana wanapokwenda seminarini wanakwenda kwa lengo la kuandaliwa kuwa mapadre,
Wengine wanaoshindwa wanaishia njiani na wanaofaulu ndio wanaokuwa mapadre.
Kanisa katoliki haliwezi kumchukua mtu mzima ambaye hajapitia kwenye utaratibu wa kanisa kwa kuwa tu ni jobless halafu akapewe upadre hiyo haipo kanisa Katoliki ya sayari hii.
Kwa hiyo tofautisha upadri na uchungaji kwa namna pekee wanavyopatikana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…