Pre GE2025 Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM

Pre GE2025 Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hizi projects za nani anahamia chama gani hazina tija yoyote kwa watanzania.
Tunataka maendeleo. Tunataka rushwa na wizi ukomeshwe. Tunataka uwajibikaji kwa wanaotuongoza na serikali nzima.
Sisi tukila na kushiba, mtacheza na siasa mpaka mchanganyikiwe
 
Huo ubinafsi ndio umelifikisha hapa lilipo taifa

Unaonekana nawe ukapata nafasi ya juu ya uongozi TANZANIA utaanza na huo ubinafsi wako kwa kufanya kile ambacho kina masilahi nawe

Badilika ndugu ubinafsi haufai kabisa
Ubinafsi ni huo wa kuteuana na kupeana mfereji wa pesa maisha yote huku wakidanganya vijana waeneze Ilani ya Chama

Ubinafsi ni kumchangia makamo Gari wakati jirani yako hana hela ya dagaa
 
Yaani Leo Lisu kingereza chote kitakuwa kimeisha hata kile cha zee zeze

Atakuwa anaporomosha tu matusi ya kinyiramba kwa kukosa vocabulary ya matusi ya kiingereza pamoja na yeye kujifanya ndie mtanzania pekee anayejua kingereza kuliko yeyote Tanzania

Leo kingereza hakitapanda wala kiswahili atakuwa anatukana na kulia kinyiramba tu
 
Mchungaji Peter Msigwa amejiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na amepokelewa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM NEC kinachoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Daktari Samia Suluhu Hassan

Alizaliwa Juni 8 1965, ni mwanasiasa Mtanzania aliyekuwa mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Iringa Mjini (2015-2020)

Kwa sasa Mchungaji Msigwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Hivi karibuni 30 Mei 2024 Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Sugu, alimshinda Mchungaji Peter Msigwa kwenye Cheo cha Uwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Nyasa.

Katika uchaguzi wa kanda hiyo uliofanyika ukumbi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Makambako, ambao ulikuwa na mchuano mkali, Sugu aliibuka kidedea baada ya kupata kura 52 sawa na asilimia 51 dhidi ya Mbunge wa zamani wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa aliyepata kura 51 (asilimia 49). Matokeo hayo Mchungaji Msigwa hakukubaliana nayo kwa kile alichodai haki haikutendeka na alikata rufaa.

====

Kuhusu Mchungaji Msigwa kutaka kupewa Uwaziri na Hayati Magufuli soma:

1. Kuelekea 2025 - Mchungaji Msigwa: Hayati Magufuli alitaka kunipa uwaziri na pesa lakini nilikataa

2. Kuelekea 2025 - Joseph Mbilinyi (Sugu) ashinda uchaguzi Kanda ya Nyasa, amgaragaza Mchungaji Msigwa
View attachment 3029802
Mchungaji Msigwa namkubali sana popote pale atakapokuwa. Nina imani kuwa ataendeleza moto wa kuichachafya serikali ya CCM hata akiwa ndani ya CCM. Namtakia kila la kheri ktk chama chake kipya.
 
Karibu sana nyumbani - siasa za Upinzani waachie waolikwisha jitoa maisha yao.

Kwetu ndani ya CCM maisha bwerere, jasho kidogo bahasha mzigo.

Ndoto zako kwamba Mwenyekiti na Makamu wake Lissu ugusanishe nyaya ili utokee mlipuko mkubwa hizo zimefeli.

Karibu sana mchungaji..naona humu kwetu mawazo na falsafa zako hasa za kudai katiba mpya na kwamba uchumi huwa hauombwewi - utaziendeleza.
 
Wampe ka cheo sasa! Ukuu wa Mkoa au UDC au ukurugenzi taasisi fulani.
Ila tukubaliane "Respect" atakosa. Kila la kheri kwenye maisha mapya ya kuwa "Doubtful" yaani ya kukana ulichokuwa unakisimamia awali.
Yaani leo aanze akane ile kauli ya Einstein aliyokuwa anaisimamia kwamba "Matatizo yetu hayawezi kutatuliwa na fikra ile ile iliyoyatengeneza" 😁
 
Mbona hajavalishwa sare!! Atalamba udc sku sio nyingi
Kuna mtu Twitter kasema msigwa kapewa advance ya dola laki tano hiyo ni advance tu bado Maokoto mengine yanakuja mifukoni mwake 🤣🤣. Hizo taarifa hazina uthibitisho ni tetesi tu. Labda huyo mtu wa Twitter ndio alete ushahidi wa hiyo dola laki tano kwenda kwa msigwa
 
Nasubiri huo muda.

Kanuni ni mbili tu weka akilini kwako na uishi nazo maisha yako ya hapa duniani

1. AKIPINGA = HAJAGAIWA
2. AKIPIGANIA (AKILINDA)= AMEGAIWA
Hizi ni kanuni za mtu asiye msomi, anayekaa nyumbani kusuburi viongozi wampiganie. Na ndiyo mawazo wa watanzania wengi. Watanzania sisi ni wavivu, tunataka short-cut, hivyo tunadhani wanasiasa ndiyo watatutatulia matatizo yetu wakati sisi tumekaa. Ni hivi: raia wote kwa umoja wetu leo hii tukamua kuikalia CCM kooni iwajibike na kuondoa viongozi wote wabovu tunaweza. Hili lina maana gani? Kiongozi hawezi kuwajibika bila msukumo wa wananchi.
 
Back
Top Bottom