Pre GE2025 Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM

Pre GE2025 Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mchungaji Peter Msigwa amejiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na amepokelewa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM NEC kinachoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Daktari Samia Suluhu Hassan

Alizaliwa Juni 8 1965, ni mwanasiasa Mtanzania aliyekuwa mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Iringa Mjini (2015-2020)

Kwa sasa Mchungaji Msigwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Hivi karibuni 30 Mei 2024 Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Sugu, alimshinda Mchungaji Peter Msigwa kwenye Cheo cha Uwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Nyasa.

Katika uchaguzi wa kanda hiyo uliofanyika ukumbi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Makambako, ambao ulikuwa na mchuano mkali, Sugu aliibuka kidedea baada ya kupata kura 52 sawa na asilimia 51 dhidi ya Mbunge wa zamani wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa aliyepata kura 51 (asilimia 49). Matokeo hayo Mchungaji Msigwa hakukubaliana nayo kwa kile alichodai haki haikutendeka na alikata rufaa.

====

Kuhusu Mchungaji Msigwa kutaka kupewa Uwaziri na Hayati Magufuli soma:

1. Kuelekea 2025 - Mchungaji Msigwa: Hayati Magufuli alitaka kunipa uwaziri na pesa lakini nilikataa

2. Kuelekea 2025 - Joseph Mbilinyi (Sugu) ashinda uchaguzi Kanda ya Nyasa, amgaragaza Mchungaji Msigwa
View attachment 3029802
Hakuna ubaya mwanampotevu kurudi nyumbani

Kidumu chama Cha Mapinduzi
 
Nilipoona zile mic za TBC, Channel 10 na za machawa wengine kwenye ile press yake nikajua tu ni swala la muda.

Ni haki yake pia kikatiba, kaokote okote na wewe Msigwa pesa za raia, ni aibu kuzidiwa mtonyo mpaka na Ally Hapi 😃
 
Lisu kapata salamu kutoka kwa Mbowe na team Lisu yao

Salamu za Mbowe ziwafikie Timu Lisu popote walipo ndani na nje ya nchi
Hakuna timu yoyote ile, mchungaji kajichanganya mwenyewe. Kila taasisi kubwa duniani lazima ijengwe kwa pillars ( nguzo) namojawapo ya nguzo kubwa sana ni nidhamu.
 
Toka Magufuli atake kumlipia hela ya kutoka gerezani, sikuwahi kuwa na imani na Msigwa. Na toka wakati ule nilishaona kuwa yuko cdm kimwili, lakini kimapato yuko ccm. Acha aende ccm akale hela za uchaguzi, na aandaliwe vipindi vya kutosha vya kuiponda cdm wiki hizi 2 tatu. Baada ya hapo aanze kufuatilia malipo yake kwa kukubali kurudi ccm.
Tofauti na hii comment ya leo, n lin uliwahi kusema huna imani na msigwa? Em leta uthibitisho ili tuamini mana isije ikawa unamsingzia kisa tayari amewakimbia
 
Wanasiasa wa upinzani wa Tanzania hawana nia ya dhati kutoka moyoni kulikomboa Taifa hili.

Wanasiasa hawa wanatafuta "maslahi yao na watoto wao". Siasa ni "fursa" kama fursa zingine.

Kwa kulitambua hili mapema ndiyo maana huwa napinga sana watu kutumiwa na wanasiasa kwenye maandamano.

Unaandamana, unapigwa, unaumizwa halafu mwisho wa siku yule yule aliyekuwa anakuhimiza kuandamana anaenda kujiunga na wale wale aliokuwa anawaita wana "akili ndogo".

Sisi Watanzania hatuandamani sababu sisi sio "waoga", sisi tuna akili, na hatuko tayari kutumiwa na wanasiasa uchwara kama condom au toilet paper.

Msigwa kaenda CCM, muda sio mrefu mtasikia kalamba uteuzi. Vijana mliokuwa mkishiriki maandamano pamoja na kina Msigwa miaka hiyo mnajisikiaje kutumiwa kama "condom"??

If you know you know
 
Kumbe watu wengine wengi mko tofauti na mimi kabisa. Kadiri CCM inavyovuta wanasiasa wengi basi ndivyo ukombozi unavyokaribia kwa haraka. Reason: wanasiasa wa aina hii wanakimbilia vyeo lakini jambo lililo dhahiri ni kuwa CCM hakuna nafasi za kuwatosha wote. Hili litasababisha anguko la CCM kwa haraka zaidi kwa sababu kutakuwa na mgongano mkubwa. Hapo wengi ya wanaoimba kumshangililia Msingwa wanaumia kichinichini kwa sababu wanajua kabisa ushindani unazidi vya kupata vyeo unazidi ndani ya CCM.
Sijui kama wengi watakuelewa. Kuna mwanasiasa mmoja alisema CCM ni kama kokoro, linavuta kila aina ya wanasiasa.
 
Tofauti na hii comment ya leo, n lin uliwahi kusema huna imani na msigwa? Em leta uthibitisho ili tuamini mana isije ikawa unamsingzia kisa tayari amewakimbia
Pitia post ya Msigwa kutaka kulipiwa hela ya kutoka gerezani na dhalimu Magu. Ndani ya cdm nina imani na Lisu tu, hao wengine naishi nao kwa akili.
 
Sitakaa nikaamini SIASA hii nchi. Mchaguane wenyewe.
 
Kuna mtu Twitter kasema msigwa kapewa advance ya dola laki tano hiyo ni advance tu bado Maokoto mengine yanakuja mifukoni mwake 🤣🤣. Hizo taarifa hazina uthibitisho ni tetesi tu. Labda huyo mtu wa Twitter ndio alete ushahidi wa hiyo dola laki tano kwenda kwa msigwa
Lowassa alipewa sh ngap kuhamia Chadema
 
Pitia post ya Msigwa kutaka kulipiwa hela ya kutoka gerezani na dhalimu Magu. Ndani ya cdm nina imani na Lisu tu, hao wengine naishi nao kwa akili.
Nataka comment yako ww kuonyesha huna imani na msigwa
 
Back
Top Bottom