Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola adaiwa kuwa chini ya ulinzi

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola adaiwa kuwa chini ya ulinzi

Imeandikwa ya kuwa hakuna ajuaye siku wala saa ya kuja mwana wa Joseph Pombe Magufuli,ole wako akute umeboronga.
 
Kwa sababu alizozitaja naye anapaswa kujiuzulu maramoja. Miradi mingi Bunge halijui. Yeye yuko juu ya sheria na katiba?
 
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola hivi sasa yupo chini ya ulinzi unaomfanya asiweze kusafiri sehemu yoyote bila Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuwa na taarifa.

Lugola alitenguliwa wadhifa wake baada ya kuhusishwa na mkataba wa kifisadi wa zaidi ya shilingi trilioni 1 wa ununuzi wa vifaa vuya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Hata hivyo, siku chache zilizopita wakati Rais Magufuli akiwaapisha mawaziri na mabalozi aliowateua alikabidhi suala hilo kwa TAKUKURU kwa hatua zaidi na kuisihi mamlaka hiyo kutowaonea huruma waliohusika.

Imeelezwa kuwa maagizo hayo yamekuwa mwiba zaidi kwa Lugola ambaye inaelezwa kuwa kwa sasa anafuatiliwa kwa karibu na vyombo vya usalama.

“Lugola yupo kwenye wakati mgumu sana, kwanza hajui hatma yake, yaani wale aliokuwa akiwapa amri hivi sasa ndiyo wanampa amri na kumchunguza”

“Yupo chini ya ulinzi kila anapokwenda na anachofanya ni lazima kijulikane, yale maisha ya kujimwambafai hayapo tena, sina hakika kama hata vikao vya bunge vilivyoanza jana atashiriki kikamilifu” chanzo kimoja kimelieleza Tanzania Daima.

Hata hivyo imeelezwa kuwa Kangi Lugola hakuonekana jana katika ufunguzi wa vikao vya bunge, jambo lililozua maswali kadhaa, mojawapo likiwa ni kama amekwenda Dodoma au yupo Dar kwa mahojiano na vyombo vya dola.

Siku chache zilizopita Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jen. John Mbung’o alisema uchunguzi huo umeanza kama sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais Magufuli.

Mbung’o alisema wataanza kupata nyaraka zinazohusu mkataba huo na kuhoji kila anayejua na aliyeshiriki katika mchakato wa mkataba huo, ikifuatiwa na kuwahoji watuhumiwa.

Chanzo: Tanzania Daima
Kilichomfanya atumbuliwe ni kupiga deal bila kumpa chochote yule doktari
 
Maaskari magereza wanamsubiri kwa hamu sana gerezani. Ndio atajua alikua hajui
 
Hili swala ni kama nyavu ya kokoro itawakusanya wengi huko mambo ya ndani na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.
Lakini ni kama upepo huvuma na kutulia.
Vilevile tusisahau meno ya mbwa hayaumani.
 
Chonde chonde nakuomba makufuli usimtumbue bashite, kwani yatakayo mkuta ni mara 10,000 yanayomkuta kangi, ingawaje yeye mwenyewe hajiurumii wengine tunamuonea huruma, cheo ni dhamana ya mda mchche sana!
 
Kangi kapige magoti kwa Mzee, mbona wenzako walikwenda na wamesamehewa!! ukizubaa unakwenda kuwa mbuzi wa Pasaka..

Kabla hujaenda kwa Mzee baba kuomba msamaha pita kwanza nyumbani kwa yule Kamanda uliyemtimua kama mbwa - kwa aibu kubwa pale kwenye kile kikao chako cha kwanza - anza kwa kumpigia magoti ya kuomba msamaha kwanza.

Vinginevyo Mzee kaka uanachama wako upo rehani....
...🤔🤔🤔..bora akatubu!
 
Wote waliojibizana na Musiba wanaisoma namba,alianza na wazee ,wakampigia kelele sauti zao zikawekwa mezani wameufyata hadi wakaomba msamaha,Lugola yeye alikuwa anajimwambafay kwa Musiba naye imekula kwakwe,mtashangaa kuona waziri wa kwanza kuwekwa ndani kwa uhujumu uchumi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani kangi Lugola aitwa na TAKUKURU kwa ajili ya mahojiano juu ya tuhuma za Kuingia mkataba wa kimangungo wa tsh zaidi ya Trillioni moja
Mungu kajibu maombi ya walokole alikuwa akiwanyanyasa tulimuonya humu. Lugola kaa mbali na kunyanyasa walokole akajitia kichwa ngumu yako wapi? Akaingia kunyanyasa mitume na manabii hadharani kilichomkuta halali yake.Nakala imfikie Sophia Mjema na mkurugenzi wa mji wa Babati .Lugora ananyolewa wao watie maji
 
Mungu kajibu maombi ya walokole alikuwa akiwanyanyasa tulimuonya humu.Lugora kaa mbali na kunyanyasa walokole akajitia kichwa ngumu yako wapi? Akaingia kunyanyasa mitume na manabii hadharani kilichomkuta halali yake.Nakala imfikie Sophia Mjema na mkurugenzi wa mji wa Babati .Lugora ananyolewa wao watie maji
Pole yake sisi tunashitaki kwa MUNGU tu
 
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani kangi Lugola aitwa na TAKUKURU kwa ajili ya mahojiano juu ya tuhuma za Kuingia mkataba wa kimangungo wa tsh zaidi ya Trillioni moja
Hii nchi ni maskini kwa sababu tuna deal na mambo ya kijinga. Hivi lugola angeweza kusaini huo mkataba bila magufuli kujua kweli?

Ama kweli trump hakukosea.

Na tukiendelea hivi tutabaki hapa hapa tulipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu kajibu maombi ya walokole alikuwa akiwanyanyasa tulimuonya humu.Lugora kaa mbali na kunyanyasa walokole akajitia kichwa ngumu yako wapi? Akaingia kunyanyasa mitume na manabii hadharani kilichomkuta halali yake.Nakala imfikie Sophia Mjema na mkurugenzi wa mji wa Babati .Lugora ananyolewa wao watie maji
AIBU yote hii ya Kangi Lugola ni ya Magufuli mwenyewe..
Angekuwa ni Rais makini anaefanya proper vetting kabla ya teuzi zake, Kangi hakupaswa kuwa kwenye cabinet kabisa.
 
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani kangi Lugola aitwa na TAKUKURU kwa ajili ya mahojiano juu ya tuhuma za Kuingia mkataba wa kimangungo wa tsh zaidi ya Trillioni moja
Mwasha uoshwa. Alikuwa anaosha sasa anaoshwa
 
Mbona Katibu Mkuu wake katunukiwa ubalozi?
 
Back
Top Bottom