Aliyeng'atwa na Nyoka afia Kituo cha Afya kisa hana 150,000 Wilayani Babati

Ulipata bahati ya kugongngwa na nyoka asiye na sumu kali.
Kuna nyoka wana sumu kali balaa huyoboi kwenye dawa za ujanja ujanja.
Wasukuma Bagosha wanadawa za nyoka..

Kule mpaka Kuna majani yanaitwa MZIMA ukiweka mfukoni unakatiza msitu mzito hakuna Simba Wala nyoka wanakukwepa.
 
Wasukuma Bagosha wanadawa za nyoka..

Kule mpaka Kuna majani yanaitwa MZIMA ukiweka mfukoni unakatiza msitu mzito hakuna Simba Wala nyoka wanakukwepa.
Hahaha naufahamu mzima ila sikujua kuhusu hili...

Kuhusu dawa za nyoka ni kweli zipo, maeneo yale mtu akiumwa nyoka haendi hospitali.
 
Ulipata bahati ya kugongngwa na nyoka asiye na sumu kali.
Kuna nyoka wana sumu kali balaa huyoboi kwenye dawa za ujanja ujanja.
Basi ukienda Tabora utashangaa zaidi...

Pale kuna wakati inahitajika nguo ya mgonjwa tu inatibiwa na mgonjwa anapona huko aliko...
 
Mboni wamesema 150,000
Vyovyote vile lkn jua hiyo ndiyo range ya bei zake (100k-300k).

Na vinahitajika vichupa mpaka 4 sometimes...

So ukifikiria kimoja tu ndugu wameshindwa kulipia, inakuwa kisanga..

Na protocol za uuzaje kwenye hospitali zote ni "Pre-Paid".
 
Mkuu, kuna baadhi ya protocols huko utumishi wa umma huwa ni ngumu sana kwa wafanyakazi wa chini.

Hapana lawama zote zinaenda kwa MGANGA MFAWIDHI.

Case kama hii yeye ndiyo anapaswa atoe go ahead ili wale wa chini waweze kutoa hiyo dawa.

Anaposema yuko mbali, wale walioko kazini ndiyo wafanye maamuzi ni anawauzia msala ambao yeye ndiyo anapaswa ausovu.
 
Kuna wajinga flani wanatoka vyuoni na kuajiriwa then wanapewa kuwa incharge kwenye vituo hivi vya afya , ni wajinga sana ,hajai uongonzi ,kazi kujipendekeza kwa kwa MaDMO , mfano katika case hii, uyu alikua ni mgojwa wa kulazwa ,kulikua na ulazima gani kimbizana na pesa ilihali mgojwa yupo apo kituoni badala ya kumpa huduma, Mhimbili watu wanatibiwa na bili sembuse huku chini.

Ndio kifo kipo ila angalau onesha kujali uhai wa mtu awapo mikononi mwako katika critical condition. May be wangeanza muona mapema hata kama huduma pale ilikua haitoshi wangeweza kutoa referal mapema.

Ifike mda kwa uzembe kama huu , wawe wanashitakiwa kwa majina yao binafsi ndo iwe dawa
 
Anti -venon ndio 150k, ndugu yangu juzijuzi kang'atwa pale Kinyerezi akaenda hospitali akachomwa bure pale kituo cha afya. Alitoa hela ya dawa za maumivu na kadi tu.
 
Basi ukienda Tabora utashangaa zaidi...

Pale kuna wakati inahitajika nguo ya mgonjwa tu inatibiwa na mgonjwa anapona huko aliko...
Tabora na koboko wale? Sikubishii bali kama kuna antivenon za kiswahili za kutibu sumu ya koboko wazungu inatakiwa waende kujifunza huko Tabora,
Koboko ni moja ya nyoka wenye sumu kali sana
 
Tabora na koboko wale? Sikubishii bali kama kuna antivenon za kiswahili za kutibu sumu ya koboko wazungu inatakiwa waende kujifunza huko Tabora,
Koboko ni moja ya nyoka wenye sumu kali sana
Kwa Tabora, koboko atakuuwa kama umechelewa sana kwa mtaalamu...

Tena huwa wanaangalia nywele, koboko akikuuma baada ya mda flani ukivutwa nywele huwa zinang'oka...

Ikifika hali hiyo, inakua ngumu kukutibu...

Japo hao wazee wanakufaga na utaalamu wao.
 
Kwa hiyo huyo juliana alijuwa na i phone ya milioni nne mfukoni mwake? Huku akisumbuka vichakani kuokoteza vimboga vya kuilisha familia yake? Kweli ma ccm mna roho mbaya kuliko shetani,ila siku yenu yaja, mtakufa kwa uchungu mkuu, tunaomba mkono wa Mungu uwaguse ili mjutie ukatili wenu, Amen
 
Hospital ukiwa na huruma unaweza jikuta unatumia mshahara wako
Sio kweli hospital ngapi za Rufaa watu ambao hawana uwezo wanatibiwa bure kupitia kitengo cha social, je huduma za hospital za rufaa ni sawa na za vituo vya afya , hawa vijana wanaopewa endesha au simamia vituo wapuuzi tu, hata uongonzi hayajui, afya tz imeanza leo katika vituo vya umma?
 
Aya matukio ni mengi hawa vijana wana lilia ajira wakipata wanakua wangese sana uko kazini wana sahau kila kitu
Kuna watu wanaitwa maboss huko maofisini, Hawa ndio chanzo Cha uharibifu, vikao vyao na watumishi ni vitisho, kuvishana hofu na kutetemeshana, hili linasababisha watumishi wa chini kutokutumia akili na utu sababu mda mwingi Wana hofu
 
Wasanii wanatibiwa bure Jakaya Kikwete HI,Wakuu Mikoa,Wikaya ,wakurugenzi ,nk wanatembrlea magari ya Mil250+ ;Wananchi wanaichagua CCM kwa Asilimia 99πŸ˜’πŸ˜’πŸ₯΄
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Mbavu zanguuuuuuπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Huyo mganga mfawidhi hajitambui na ni mjinga kabisa.Ka kwepa kumsaidia mwananchi Kwa kumsukumizia awaombe wakati mwenye kutoa ruhusa ni yeye.Hawa watumishi wa Samia sijui anawaokota wapi?
 
Gentleman,
kifo cha mwendazake Juliana,
kiwe funzo na changamoto kwa kila mdau wa JF, hususani kuanzia mwaka mpya 2025, kuweka kipaumbele cha kua na Bima ya afya.

kulalamika au kulaumu hakusaidii chochote. Ni muhimu kugeuza changamoto kua fursa ya kujipanga na kuhakikisha una bima ya afya wewe na familia yako.

Epuka unafiki wa kujifanya una uchungu na mtu ambae tayari ameaga dunia na huna namna ya kumrejeshea uhai.

Bimba ya afya ni sehemu ya nusura ya maisha na uhai wako. Hakikisha una Bima ya afya na sio kumbwelambwela tu πŸ’ πŸ’
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…