Aliyeolewa akaachika miaka 7 sasa imepita ila hakupewa talaka, Anataka nimuoe. Je, naweza kumuoa?

Aliyeolewa akaachika miaka 7 sasa imepita ila hakupewa talaka, Anataka nimuoe. Je, naweza kumuoa?

Uko sahihi mkuu. Akimuoa wakati ndoa ya awali haijafa basi ndoa yao mpya haitakuwa halali Kisheria.

Cha kufanya, mwanamke apeleke Mahakamani ombi la talaka. Lkn ombi la talaka haliwezi kusikilizwa Mahakamani bila mwanamke kuwa na hati ya Usuluhishi ya maswala ya ndoa kutoka kwenye mabaraza ya usuluhishi yaliyopo misikitini (bakwata), makanisani au kwenye kila kata. Haya mabaraza yatajaribu kuwasuluhisha, ikishindikana, itaandaliwa hati ambayo itaambatanishwa na maombi ya talaka yatakayopelekwa Mahakamani.

Hati ya usuluhishi halitakuwa takwa la lazima kama mwanaume atakataa kwenda kwenye hilo Baraza.

Moja ya sababu ambayo Mahakama itaizingatia kabla ya talaka kutolewa ni wanandoa kutengana kwa zaidi ya miaka mitatu. Mtoa mada anasema huyo mwanamke wake katengana na mume wake kwa miaka 7; so sababu ya msingi ipo.

Apeleke kesi Mahakama ya mwanzo au ya wilaya. Mahakama ikiamua kwamba waachanishwe ndiyo jamaa anaweza kufunga ndoa mpya halali ambayo itatambulika kisheria.

Kwa sasa ni hayo tu, namtakia kila la kheri.
Asante
 
Kiufupi hapo linatakiwa tamko tu la mwanaume wa mwanzo atoe talaka basi,
Ao mwanamke afanye khulus(ajivue ndoa irejeshwe mahari yake ndoa iishe,
Kama mwanaume atakataa basi nendeni kwa kadhi ataivunja ndoa hiyo....!
Ila hapo kumuoa huwezi maana bado mke wa mtu hata akae miaka 15 jamaa akirudi akihitaji mke wake huna ujanja
 
Ndoa ya kiislamu haivunjika kwa mwanaume kua mbali na mke wake miaka mingi na kisheria huyo mwanamke anamakosa yakuzini akiwa mke wa mtu...alichotakiwa kama alikua anaona hana mapenzi tena na huyo mwanaume basi awataarifu familia washenga au aliemuozesha kwakudai talaka na kama mwanaume hajaweza kutoa talaka basi aliruhusiwa kujivua kwakumrudishia mwanaume mahali yake na mwanamke kujivua eda yake ni mwezi mmoja baada hapo angeweza kuolewa tena.....lkn kwa kosa lililotendeka anaweza kurudi nyuma kwakurudi kwao na fanye toba ya zinaa kama alifanya kwakujua au kutokujua alf aendee na process zakujivua kwakuwafata hao niliowasema kwakudai talaka yake na kama hajatoa basi atajivua na kukaa eda ya mwezi ikiisha basi anaweza kuolewa tena na kama huyo mume akitoa talaka kwa hiyari basi eda ni miezi mi3 na baada ya hapo anakua yupo huru kuolewa tena
 
Mathematics!
Aliolewa akiwa na 17yrs, akaishi kwenye ndoa 8yrs, akaikimbia ndoa 7yrs, na wewe ukawa naye kwenye mahusiano 3yrs na anawatoto wawili.

Kwa haraka haraka saivi ana miaka 40, mbona unataka kuuziwa mbuzi kwenye gunia huyo si bibi kabisaaa! Yaani umekosa vijana wenzio mpaka ukaangukie penzi la kibibi? Shtuka mkuu.

N.B mtoto wake wa kwanza atakuwa na miaka 17/18. Kwamujibu wa maelezo yako.
Punguza chuki na ujuaji ye alieishi nae miaka mitatu hajaona uzee wake we fasta umeuona khaaa wanaume wa jf punguzeni kiherehere
 
Mtoa mada ni mdogo kuliko huyo mwanamke anayetaka kumuoa still yuko kwenye mid 20's ndio maana nashangaa sana!
Cha kushangaza kipi hapo mpe ushauri kutokana na alichoomba haya mengine kama ya umri sidhani kama ni muhimu kwetu kama ye muhusika yuko poa nalo
 
Mathematics!
Aliolewa akiwa na 17yrs, akaishi kwenye ndoa 8yrs, akaikimbia ndoa 7yrs, na wewe ukawa naye kwenye mahusiano 3yrs na anawatoto wawili.

Kwa haraka haraka saivi ana miaka 40, mbona unataka kuuziwa mbuzi kwenye gunia huyo si bibi kabisaaa! Yaani umekosa vijana wenzio mpaka ukaangukie penzi la kibibi? Shtuka mkuu.

N.B mtoto wake wa kwanza atakuwa na miaka 17/18. Kwamujibu wa maelezo yako.
Acha ushirikina, kwani anamwngilia kwenye mvi.
 
Naishi naye huu mwaka wa 3 bila ya ndoa.

Hadithi yake ya nyuma ipo hivi
" Alioelewa akiwa na miaka 17 baada ya kupewa ujauzito na uyo jamaa na wakaishi wote miaka 8 kwenye ndoa na kuzaa watoto wawili.

Sababu ya kuachana uyo jamaa alianza kula madawa ya kulevya ndugu wakampeleka sober akarudi kwa madai ameacha baada ya muda akarudia tena . Uyu mama akarud kwao jamaa akazama kwenye uteja tena .uyu mwanamke akarudi kwao kabisa. Sasa imepita miaka 7 tokea waachane

Mimi
" Anataka nimuoe kwaajili ya hii ramadhan .na nimeishi nae mwaka wa 3 sasa kama mke na mume

Karibuni
Akalete cheti cha talaka hakuna jingine
 
Naishi naye huu mwaka wa 3 bila ya ndoa.

" Anataka nimuoe kwaajili ya hii ramadhan .na nimeishi nae mwaka wa 3 sasa kama mke na mume

Karibuni

Kwahiyo Ramadhani zilizopita hazikuwa nzuri
 
Wengi wameniambia kuhusu taraka
Mimi
" Nimemwambia uyu mwanamke adai taraka
Akampigia mam mkwe wake ambae mama wa mme wake wa kipindi hicho akasema kwamba kwa sasa jamaa yupo jela maana madawa yamempanda na amepelekwa mahabusu yapata week sasa kwa kosa la kumshikia kisu mama yake mzazi
Yeye
Akawapigia tena familia yake uyu mwanamke kwao wanasema mwambie shem aje aoe tu.

Apo kitaaalamu imeekaaje
Pia nimezaa nae uyu mwanamke mtoto mmoja na kipindi na zaa nae bado alikuwa anaakaa kwako .
 
mbona huyo mkeo? mnamuoaje mkeo? miaka 3, ramadhani hii ndo Nini vile? mkeo huyooo bhana
 
Naishi naye huu mwaka wa 3 bila ya ndoa.

Hadithi yake ya nyuma ipo hivi
" Alioelewa akiwa na miaka 17 baada ya kupewa ujauzito na uyo jamaa na wakaishi wote miaka 8 kwenye ndoa na kuzaa watoto wawili.

Sababu ya kuachana uyo jamaa alianza kula madawa ya kulevya ndugu wakampeleka sober akarudi kwa madai ameacha baada ya muda akarudia tena . Uyu mama akarud kwao jamaa akazama kwenye uteja tena .uyu mwanamke akarudi kwao kabisa. Sasa imepita miaka 7 tokea waachane

Mimi
" Anataka nimuoe kwaajili ya hii ramadhan .na nimeishi nae mwaka wa 3 sasa kama mke na mume

Karibuni
Unataka kusema mpka Sasa huyo mwanamke Ana miaka 35??
 
Punguza chuki na ujuaji ye alieishi nae miaka mitatu hajaona uzee wake we fasta umeuona khaaa wanaume wa jf punguzeni kiherehere
Wanaume wa humu wengi wana wivu sana na wanawake nadhani wanatamani wangeumbwa wanawake ila ndo hivyo
 
Kwan yeye mleta mada umeujua umri wake?

Alaf swala la umri wa huyo mwanamke na watoto wake, vyote alivijua, na bado akaweza kuishi nae miaka mitatu, hadi wazo la kumuoa likamjia, hajakurupuka.

Na ndio maana ushauri anahitaji umelenga eneo jingine kabisa
Alafu pia hakujua kama jamaa anauliza ushauri wa namna gani, yeye alitaka kujua kisheria inakuwaje kama hawajapeana talaka na mumewe wa kwanza, na pia huyo ni kijana mdooogo kabisa anaamini ndoa ni za mabinti na vijana wadogo
 
Alafu pia hakujua kama jamaa anauliza ushauri wa namna gani, yeye alitaka kujua kisheria inakuwaje kama hawajapeana talaka na mumewe wa kwanza, na pia huyo ni kijana mdooogo kabisa anaamini ndoa ni za mabinti na vijana wadogo
😅😅😅 Hapo mwisho nimecheka sana. Bwana mdogo anaamini ndoa ni za vijana wadogo tu
 
Back
Top Bottom