Aliyewahi kupitia Changamoto za Nguvu za Giza katika harakati za ufugaji pitia hapa

Aliyewahi kupitia Changamoto za Nguvu za Giza katika harakati za ufugaji pitia hapa

Ibrahim HC

Member
Joined
Oct 8, 2021
Posts
56
Reaction score
88
Habari za wakati huu Wapendwa.
Binafsi nipende kuwashukuru wadau wote jamiiforum hakika nimejifunza mengi katika baadhi ya machapisho ya wadau nimekuwa motivated Sana kuingia kwa mara nyingine katika ufugaji.
Pamoja na kujifunza mengi Kuna baazi ya mambo Hadi hivi sasa yananitatiza ningependa kuwashirikisha, naimani ntasaidika kutokana na uzoefu wa watu wengi katika ufugaji.
Niende kwenye hoja ya msingi.
Mwaka 2017 niliingia katika ufugaji baada ya kumaliza chuo, nilikuwa ninaelimu kidogo juu ya maswala ya ufugaji na changamoto zake.
Nilianza na kuku 22 wakubwa kati ya 22 majogoo yalikuwa 3, lakini jirani yangu yeye alianza na kuku wawili tu mitetea na jogoo aliazima, baada ya miezi Kama minne jirani yangu alikuwa na kuku zaidi ya 40 pamoja na vifaranga, lakini Mimi walibaki wale wale 22 pamoja na kufanya kila kilichotakiwa kufanyika na sikuwahi kupoteza kuku kwa sababu ya ugonjwa, niliweza kuwatibu kwa dawa za asili na zilifanya vizuri.
Changamoto iliyonikuta
Kuku wangu walikuwa wanataga vizuri tu bila changamoto yoyote shida ilikuja walipoanza kuatamia mayai, wengi walikuwa wakiatamia baada Kama ya wiki ya pili wanaacha kuatamia, na walioweza kuangua vifaranga kiukweli baada ya wiki unakuta kuku Hana kifaranga hata mmoja vilikuwa vinakufa katika mazingira tata bila hata kuugua.
Kumbuka nilikuwa nafata kanuni zote za ufugaji na chakula nilikuwa nawapatia lakini jirani yangu yeye nikuwafungulia wanajitafutia na hata ikitokea changamoto ya ugonjwa kwake alikuwa hajisumbui kutibu kuku yeye ni mwendo wa kichinja tu na bado yeye alifanikiwa mara mbili zaidi ya Mimi ambaye niliamini nafaham kila kitu.
Baada ya hayo ilibidi kuwashirikisha wazee na wenyej wa mahali husika wakadai ya kuwa eti mifugo yangu halikuwa na ulinzi, wengine wakasema eti nilikuwa nakaribishwa na wenye mji japo nilifugia mashambani, nikaona isiwe tabu kuliko kukosa kabisa nikawauza wote nikaachana na ufugaji Hadi hivi leo naandika haya.
Niombe radhi kwa andiko refu, kifupi nimehamasika kurudi Tena katika ufugaji naona kabisa Kuna dhahabu iliyojificha ukiondoa changamoto ambazo zipo katika nyanja yoyote Ile katika maisha.
Jamani kwa yeyote aliyewahi kukutana na changamoto Kama yangu ningeomba tushirikishane uliitatua vipi ili nasi tujifunze, pia mnawezaje kulinda mali zenu dhidi ya mambo ya ulozi?
Natanguliza shukrani Wapendwa 🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻
 
Ndumba zipo ila sio mambo ya kuyaamini kwenye ufugaji ni sayansi kuku kuacha mayai ni kusumbuliwa na kuku wengine , kuhusu vifaranga walee peke yao na kuzingatia mahitaji muhimu hasa joto, dawa na chanjo ukiwa na uwezo usifuge kuku kidogo fuga kuku kuanzia mia kuendelea
 
Mkuu kwa sababu shetani yupo basi na uchawi upo vilevile asikudanganye mtu.
Mwaka 2013 nilienda pwani kwa ndg yangu yeye naye alikuwa mfugaji wa kukusana
na ni mzoefu sana.

cha ajabu baada ya kufika kule akajenga mabanda ili aanze ufugaji kisasa kwa kifupi tu hakufanikiwa.
Mimi nilipofika kwake na vile ananijua kwenye kuku ndo wameni somesha ilibidi tuanze upya mambo yakawa yale yale

Muda huo jamaa alikuwa mlokole sana kila kitu maombi. nami nikiwa kama mgeni sikutaka kumpa ushauri tofauti na imani yake.

Mimi kwenye dhehebu langu nilipata mwenyeji ambae ni mkulya kama mjuavyo mkikutana watu
sehemu tofauti na mmetoka ukanda mmoja mnakuwa kama ndg.

Katika kupeana ramani za maisha nikiwa pani huko akanikaribisha kwakwe.
kabla hata sijafika kwake sauti za kanga pamoja na kuku zilisika nyingi mnoo

Ile nafika nilikuta kanga wengi sana na kuku wengi mno.Ndipo nilipomuuliza siri ya mafanikio yake
kwanza aliniambia kanga wengi ni wa porini amekuwa akiletewa mayai na wachungaji wa ng'ombe wa kisukuma na mang'ati.

Ndipo aliposema wenyeji wanawivu sana kwa wageni kufanya miradi sio mifugo wala kilimo tu
lazima upite kushoto kidogo ndo mambo yako yakae sawa. Kwa sababu tuliendana sana na yule jamaa kwangu ni sawa baba kabisa alinipa mbinu nikaenda kufanya kisiri siri bila mwenyeji wangu kujua
.
Tulifanikiwa japo mimi siku za kuendelea kukaa huko ziliisha nikarudi.

baada ya kufika bara nilimtumia msg mwenyeji wangu shida yoyote ile ukiona mambo yako hayaendi onana na fulani usisite ndo aliyetusaidia.

Akasema kama ni hivyo ni bora aachane na ufugaji.


Ukija kwangu sasa kuniomba ushauri kama wewe nitakumbia mawili tu. kama unamwamini mungu
basi omba sana sana na kama upo huku kwa mizimu ya mababu basi fanya hivyo bila kusita.


hakuna mambo yanayojiendea yenyewe tu na ukafanikiwa yaani huna mungu wala kushoto uende na umilki kuku hata 700 nk basi wewe ni wakipekee sana. kwa uzoefu tangu 2009 nafuga kuku nimeona mengi na kujifunza mengi mno.
hapa najizungumzia mimi.
 
Kwenye kila kitu kuna kijicho sasa shauri yako kufuata njia ya kona au iliyonyooka.
 
Ni hatari kuhamasisha ulozi. Kuna mtu alifanya utafiti kwa wafugaji wakubwa wa kuku wa mayai wanaofuga kuku kuanzia 2000. Wafugaji wote walisema kuku wao wa kwanza walikufa!! Kila mmoja kwa sababu zake, haijalishi tahadhari kibwa na umakini waliokuwa nao Ila kuku walikufa!! wengi wa wafugaji wanaishia hapo!!!

Waloanza upya ndio wakatoboa, waliokata tamaa wanahubiri uchawi!!
Percevere children of God
 
Mkuu kwa sababu shetani yupo basi na uchawi upo vilevile asikudanganye mtu.
Mwaka 2013 nilienda pwani kwa ndg yangu yeye naye alikuwa mfugaji wa kukusana
na ni mzoefu sana.

cha ajabu baada ya kufika kule akajenga mabanda ili aanze ufugaji kisasa kwa kifupi tu hakufanikiwa.
Mimi nilipofika kwake na vile ananijua kwenye kuku ndo wameni somesha ilibidi tuanze upya mambo yakawa yale yale

Muda huo jamaa alikuwa mlokole sana kila kitu maombi. nami nikiwa kama mgeni sikutaka kumpa ushauri tofauti na imani yake.

Mimi kwenye dhehebu langu nilipata mwenyeji ambae ni mkulya kama mjuavyo mkikutana watu
sehemu tofauti na mmetoka ukanda mmoja mnakuwa kama ndg.

Katika kupeana ramani za maisha nikiwa pani huko akanikaribisha kwakwe.
kabla hata sijafika kwake sauti za kanga pamoja na kuku zilisika nyingi mnoo

Ile nafika nilikuta kanga wengi sana na kuku wengi mno.Ndipo nilipomuuliza siri ya mafanikio yake
kwanza aliniambia kanga wengi ni wa porini amekuwa akiletewa mayai na wachungaji wa ng'ombe wa kisukuma na mang'ati.

Ndipo aliposema wenyeji wanawivu sana kwa wageni kufanya miradi sio mifugo wala kilimo tu
lazima upite kushoto kidogo ndo mambo yako yakae sawa. Kwa sababu tuliendana sana na yule jamaa kwangu ni sawa baba kabisa alinipa mbinu nikaenda kufanya kisiri siri bila mwenyeji wangu kujua
.
Tulifanikiwa japo mimi siku za kuendelea kukaa huko ziliisha nikarudi.

baada ya kufika bara nilimtumia msg mwenyeji wangu shida yoyote ile ukiona mambo yako hayaendi onana na fulani usisite ndo aliyetusaidia.

Akasema kama ni hivyo ni bora aachane na ufugaji.


Ukija kwangu sasa kuniomba ushauri kama wewe nitakumbia mawili tu. kama unamwamini mungu
basi omba sana sana na kama upo huku kwa mizimu ya mababu basi fanya hivyo bila kusita.


hakuna mambo yanayojiendea yenyewe tu na ukafanikiwa yaani huna mungu wala kushoto uende na umilki kuku hata 700 nk basi wewe ni wakipekee sana. kwa uzoefu tangu 2009 nafuga kuku nimeona mengi na kujifunza mengi mno.
hapa najizungumzia mimi.
Mkoa wa Pwani ni shida sana aisee ktk mambo ya ulozi. Haya mambo kila sehem yapo ila Pwani shida ni kwamba wenyeji hawafanyi kazi ipasavyo ila mgeni ukitia nanga ili ufanye jambo wanaona wivu na kuanza kukuletea mambo ya gizani.

Kuna ardhi nzuri sana yenye rutuba isiyokua na muendelezo wa kilimo.
 
Mkuu kwa sababu shetani yupo basi na uchawi upo vilevile asikudanganye mtu.
Mwaka 2013 nilienda pwani kwa ndg yangu yeye naye alikuwa mfugaji wa kukusana
na ni mzoefu sana.

cha ajabu baada ya kufika kule akajenga mabanda ili aanze ufugaji kisasa kwa kifupi tu hakufanikiwa.
Mimi nilipofika kwake na vile ananijua kwenye kuku ndo wameni somesha ilibidi tuanze upya mambo yakawa yale yale

Muda huo jamaa alikuwa mlokole sana kila kitu maombi. nami nikiwa kama mgeni sikutaka kumpa ushauri tofauti na imani yake.

Mimi kwenye dhehebu langu nilipata mwenyeji ambae ni mkulya kama mjuavyo mkikutana watu
sehemu tofauti na mmetoka ukanda mmoja mnakuwa kama ndg.

Katika kupeana ramani za maisha nikiwa pani huko akanikaribisha kwakwe.
kabla hata sijafika kwake sauti za kanga pamoja na kuku zilisika nyingi mnoo

Ile nafika nilikuta kanga wengi sana na kuku wengi mno.Ndipo nilipomuuliza siri ya mafanikio yake
kwanza aliniambia kanga wengi ni wa porini amekuwa akiletewa mayai na wachungaji wa ng'ombe wa kisukuma na mang'ati.

Ndipo aliposema wenyeji wanawivu sana kwa wageni kufanya miradi sio mifugo wala kilimo tu
lazima upite kushoto kidogo ndo mambo yako yakae sawa. Kwa sababu tuliendana sana na yule jamaa kwangu ni sawa baba kabisa alinipa mbinu nikaenda kufanya kisiri siri bila mwenyeji wangu kujua
.
Tulifanikiwa japo mimi siku za kuendelea kukaa huko ziliisha nikarudi.

baada ya kufika bara nilimtumia msg mwenyeji wangu shida yoyote ile ukiona mambo yako hayaendi onana na fulani usisite ndo aliyetusaidia.

Akasema kama ni hivyo ni bora aachane na ufugaji.


Ukija kwangu sasa kuniomba ushauri kama wewe nitakumbia mawili tu. kama unamwamini mungu
basi omba sana sana na kama upo huku kwa mizimu ya mababu basi fanya hivyo bila kusita.


hakuna mambo yanayojiendea yenyewe tu na ukafanikiwa yaani huna mungu wala kushoto uende na umilki kuku hata 700 nk basi wewe ni wakipekee sana. kwa uzoefu tangu 2009 nafuga kuku nimeona mengi na kujifunza mengi mno.
hapa najizungumzia mimi.
"hakuna mambo yanayojiendea yenyewe tu"either uwe kwa Mungu full au kwa shetan full👍👍👍👍,uchaguzi ni wako.
 
Mkoa wa Pwani ni shida sana aisee ktk mambo ya ulozi. Haya mambo kila sehem yapo ila Pwani shida ni kwamba wenyeji hawafanyi kazi ipasavyo ila mgeni ukitia nanga ili ufanye jambo wanaona wivu na kuanza kukuletea mambo ya gizani.

Kuna ardhi nzuri sana yenye rutuba isiyokua na muendelezo wa kilimo.
Mkuu Kuna sehemu panaitwa mto ruvu vizembe kama sijakosea Ile ardhi Ina rutuba sana. Jamaa mmoja alikuja akununua kama heka 100 heka 50 zote akafyeka na kung'oa visiki akachimba na mabwawa ya ufugaji samaki!


Alikuwa karibu na shamba nililokuwa nafanya kazi Mimi.

Katika Hela hizo alilima nyanya tikti na vitunguu

Vitunguu hakuvuna.
Nyanya alivuna ila chini ya target vibaya mno tikiti kama Mpira wa Watoto...

Samaki ndo kabisa hata sijui ilikuwaje. Alirudi dar Kwa shot ya mamilion na alikuwa amekopa mkopo

Akanunua tractor na akafungu pump kubwa ya kuvutia maji kutoa mtoni. Ni Hivi alikuwa hasara hata robo ya pesa yake aliyowekeza hakupata.


Mwingine huko uko vizembe kandokando ya mto kabisa
Tulivuna vitunguu Ile grade1 tulipata gunia 160. Grade iliyofata sikumbuki ila ndo vilkuwa vingi kulikuwa grade1


Alipofikisha dar ndani ya siku3 mzigo uliza wote! Haya mambo si ya kuzimuliwa nimeona mwenyewe

Panaitwa gwata vizembe huko mtoni ruvu. Huyo wa vitunguu ulikuwa mradi wa mwanamke Mme wake alikuwa anatembea Kila kikwete anakoenda wafanyakazi wake walikuwa wanasema ni muhasibu wa Jk.
 
Mkuu kwa sababu shetani yupo basi na uchawi upo vilevile asikudanganye mtu.
Mwaka 2013 nilienda pwani kwa ndg yangu yeye naye alikuwa mfugaji wa kukusana
na ni mzoefu sana.

cha ajabu baada ya kufika kule akajenga mabanda ili aanze ufugaji kisasa kwa kifupi tu hakufanikiwa.
Mimi nilipofika kwake na vile ananijua kwenye kuku ndo wameni somesha ilibidi tuanze upya mambo yakawa yale yale

Muda huo jamaa alikuwa mlokole sana kila kitu maombi. nami nikiwa kama mgeni sikutaka kumpa ushauri tofauti na imani yake.

Mimi kwenye dhehebu langu nilipata mwenyeji ambae ni mkulya kama mjuavyo mkikutana watu
sehemu tofauti na mmetoka ukanda mmoja mnakuwa kama ndg.

Katika kupeana ramani za maisha nikiwa pani huko akanikaribisha kwakwe.
kabla hata sijafika kwake sauti za kanga pamoja na kuku zilisika nyingi mnoo

Ile nafika nilikuta kanga wengi sana na kuku wengi mno.Ndipo nilipomuuliza siri ya mafanikio yake
kwanza aliniambia kanga wengi ni wa porini amekuwa akiletewa mayai na wachungaji wa ng'ombe wa kisukuma na mang'ati.

Ndipo aliposema wenyeji wanawivu sana kwa wageni kufanya miradi sio mifugo wala kilimo tu
lazima upite kushoto kidogo ndo mambo yako yakae sawa. Kwa sababu tuliendana sana na yule jamaa kwangu ni sawa baba kabisa alinipa mbinu nikaenda kufanya kisiri siri bila mwenyeji wangu kujua
.
Tulifanikiwa japo mimi siku za kuendelea kukaa huko ziliisha nikarudi.

baada ya kufika bara nilimtumia msg mwenyeji wangu shida yoyote ile ukiona mambo yako hayaendi onana na fulani usisite ndo aliyetusaidia.

Akasema kama ni hivyo ni bora aachane na ufugaji.


Ukija kwangu sasa kuniomba ushauri kama wewe nitakumbia mawili tu. kama unamwamini mungu
basi omba sana sana na kama upo huku kwa mizimu ya mababu basi fanya hivyo bila kusita.


hakuna mambo yanayojiendea yenyewe tu na ukafanikiwa yaani huna mungu wala kushoto uende na umilki kuku hata 700 nk basi wewe ni wakipekee sana. kwa uzoefu tangu 2009 nafuga kuku nimeona mengi na kujifunza mengi mno.
hapa najizungumzia mimi.
Huo ndio uhalisia wa maisha yetu watoto wa kishua wanaona ni hadithi za kufikirika ila katika utafutaji mauzauza mengi Sana lazima kuwa na Nguvu ya kukulinda wewe pamoja na mali zako.
Well said mkuu
 
Mkuu Kuna sehemu panaitwa mto ruvu vizembe kama sijakosea Ile ardhi Ina rutuba sana. Jamaa mmoja alikuja akununua kama heka 100 heka 50 zote akafyeka na kung'oa visiki akachimba na mabwawa ya ufugaji samaki!


Alikuwa karibu na shamba nililokuwa nafanya kazi Mimi.

Katika Hela hizo alilima nyanya tikti na vitunguu

Vitunguu hakuvuna.
Nyanya alivuna ila chini ya target vibaya mno tikiti kama Mpira wa Watoto...

Samaki ndo kabisa hata sijui ilikuwaje. Alirudi dar Kwa shot ya mamilion na alikuwa amekopa mkopo

Akanunua tractor na akafungu pump kubwa ya kuvutia maji kutoa mtoni. Ni Hivi alikuwa hasara hata robo ya pesa yake aliyowekeza hakupata.


Mwingine huko uko vizembe kandokando ya mto kabisa
Tulivuna vitunguu Ile grade1 tulipata gunia 160. Grade iliyofata sikumbuki ila ndo vilkuwa vingi kulikuwa grade1


Alipofikisha dar ndani ya siku3 mzigo uliza wote! Haya mambo si ya kuzimuliwa nimeona mwenyewe

Panaitwa gwata vizembe huko mtoni ruvu. Huyo wa vitunguu ulikuwa mradi wa mwanamke Mme wake alikuwa anatembea Kila kikwete anakoenda wafanyakazi wake walikuwa wanasema ni muhasibu wa Jk.
Alafu maeneo Kama hayo unapoenda kuwekeza wenyeji hawakusanui, wanakuchora tu ukiangukia pua ndio wanakwambia njia za kupita, kwa kifupi maeneo ya pwani Kuna uswahili mwingi na wanapenda watu waishi maisha ya kufanana, ukijifanya mpambanaji wanakuvuta shati urudi nyuma kimaendeleo
 
Alafu maeneo Kama hayo unapoenda kuwekeza wenyeji hawakusanui, wanakuchora tu ukiangukia pua ndio wanakwambia njia za kupita, kwa kifupi maeneo ya pwani Kuna uswahili mwingi na wanapenda watu waishi maisha ya kufanana, ukijifanya mpambanaji wanakuvuta shati urudi nyuma kimaendeleo
Sana mkuu Bahati nzuri nilifanikiwa kuwa na urafiki na wenyeji hasa walio okoka walikuwa wananiambia hivihivi kuwa watu wa huku Wana wivu sana. Hawapendi maendeleo ya wageni
 
Huo ndio uhalisia wa maisha yetu watoto wa kishua wanaona ni hadithi za kufikirika ila katika utafutaji mauzauza mengi Sana lazima kuwa na Nguvu ya kukulinda wewe pamoja na mali zako.
Well said mkuu
Hao wanaopinga hata Huwa sibishani nao. Ukiona mtu anapinga kwanza hajawahi tembelea maeneo mengi ama kafanikiwa Mali za kukuta (kurithi) ila sisi wa mguu Kwa mguu taabu na mauza uza tunayajua vizuri mno.
 
Habari za wakati huu Wapendwa.
Binafsi nipende kuwashukuru wadau wote jamiiforum hakika nimejifunza mengi katika baadhi ya machapisho ya wadau nimekuwa motivated Sana kuingia kwa mara nyingine katika ufugaji.
Pamoja na kujifunza mengi Kuna baazi ya mambo Hadi hivi sasa yananitatiza ningependa kuwashirikisha, naimani ntasaidika kutokana na uzoefu wa watu wengi katika ufugaji.
Niende kwenye hoja ya msingi.
Mwaka 2017 niliingia katika ufugaji baada ya kumaliza chuo, nilikuwa ninaelimu kidogo juu ya maswala ya ufugaji na changamoto zake.
Nilianza na kuku 22 wakubwa kati ya 22 majogoo yalikuwa 3, lakini jirani yangu yeye alianza na kuku wawili tu mitetea na jogoo aliazima, baada ya miezi Kama minne jirani yangu alikuwa na kuku zaidi ya 40 pamoja na vifaranga, lakini Mimi walibaki wale wale 22 pamoja na kufanya kila kilichotakiwa kufanyika na sikuwahi kupoteza kuku kwa sababu ya ugonjwa, niliweza kuwatibu kwa dawa za asili na zilifanya vizuri.
Changamoto iliyonikuta
Kuku wangu walikuwa wanataga vizuri tu bila changamoto yoyote shida ilikuja walipoanza kuatamia mayai, wengi walikuwa wakiatamia baada Kama ya wiki ya pili wanaacha kuatamia, na walioweza kuangua vifaranga kiukweli baada ya wiki unakuta kuku Hana kifaranga hata mmoja vilikuwa vinakufa katika mazingira tata bila hata kuugua.
Kumbuka nilikuwa nafata kanuni zote za ufugaji na chakula nilikuwa nawapatia lakini jirani yangu yeye nikuwafungulia wanajitafutia na hata ikitokea changamoto ya ugonjwa kwake alikuwa hajisumbui kutibu kuku yeye ni mwendo wa kichinja tu na bado yeye alifanikiwa mara mbili zaidi ya Mimi ambaye niliamini nafaham kila kitu.
Baada ya hayo ilibidi kuwashirikisha wazee na wenyej wa mahali husika wakadai ya kuwa eti mifugo yangu halikuwa na ulinzi, wengine wakasema eti nilikuwa nakaribishwa na wenye mji japo nilifugia mashambani, nikaona isiwe tabu kuliko kukosa kabisa nikawauza wote nikaachana na ufugaji Hadi hivi leo naandika haya.
Niombe radhi kwa andiko refu, kifupi nimehamasika kurudi Tena katika ufugaji naona kabisa Kuna dhahabu iliyojificha ukiondoa changamoto ambazo zipo katika nyanja yoyote Ile katika maisha.
Jamani kwa yeyote aliyewahi kukutana na changamoto Kama yangu ningeomba tushirikishane uliitatua vipi ili nasi tujifunze, pia mnawezaje kulinda mali zenu dhidi ya mambo ya ulozi?
Natanguliza shukrani Wapendwa 🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻
Ungejitahidi kuwa karibu na jirani yako update elimu au somo zaidi kipi kinafanya eye anafanikiwa na wewe hufanikiwi. Tunajifunza kwa waliofanikiwa Tena ni jirani yako ambabo mazingira na Hali ya hewa karibu ni Ile Ile.
Usipiteza muda na mambo ya ushirikina wengi wao ni matapeli wanakula vya wajinga.
 
Hao wanaopinga hata Huwa sibishani nao. Ukiona mtu anapinga kwanza hajawahi tembelea maeneo mengi ama kafanikiwa Mali za kukuta (kurithi) ila sisi wa mguu Kwa mguu taabu na mauza uza tunayajua vizuri mno.
Mimi sijawahi kuingia kw undani kwenye kilimo....ila Nina ushahidi ,kwenye kilimo kuna ushirikina mwingi Mno! Unaweza ukalima.,kwa mfano hekari 5 za mahindi ukitarajia Magunia pengine 100 utashangaa unapata 50! Kwenye mazingira ya utata! Naungana na wewe ..
Kama unabisha nenda huko.mashambani ukaingie kichwakichwa uone upande wa pili wa Dunia!
 
Back
Top Bottom