Ally Kessy awashukia Zanzibar, Awataka Wabunge wa Zanzibar watoke nje kwa mambo yasiyo ya Muungano

Ally Kessy awashukia Zanzibar, Awataka Wabunge wa Zanzibar watoke nje kwa mambo yasiyo ya Muungano

Mbunge wa Nkasi Ally Kessy amewataka wabunge wa Zanzibar kuacha kung'ang'ania kupata nusu kwa nusu kila kitu na bara kwa kuwa wao ni 4% na wanastahili kupata 4% kwenye kila kitu na sio nusu kwa nusu, ameongezea pia gharama za nyingi kama za mabalozi wa nje Zanzibar haiwezi kumudu kulipia hata balozi mmoja ila na wanasaidiwa na bara kwa hiyo walipaswa kushukuru na sio kulalamika

Pia aliwaambia wasiwe wanachangia na watoke nje kwenye bajeti za wizara ambazo sio za Muungano kwa kuwa haziwahusu
 
Ally Kessy aliunga mkono au alipinga Rasimu ya Katiba iliyotokana na Tume iliyoongozwa na Jaji Warioba? Mambo haya yalijadiliwa na kuchambuliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

CCM wakakataa rasimu ambayo ingekuwa dawa ya mapungufu anayoyaeleza Kessy. Sasa kuja kusema Wabunge kutoka Zanzibar wawe wanatoka nje wakati wa kujadili mambo ambayo si ya muungano ni upunguani.
 
Mbunge wa Nkasi Ally Kessy amewataka wabunge wa Zanzibar kuacha kung'ang'ania kupata nusu kwa nusu kila kitu na bara kwa kuwa wao ni 4% na wanastahili kupata 4% kwenye kila kitu na sio nusu kwa nusu, ameongezea pia gharama za nyingi kama za mabalozi wa nje Zanzibar haiwezi kumudu kulipia hata balozi mmoja ila na wanasaidiwa na bara kwa hiyo walipaswa kushukuru na sio kulalamika

Pia aliwaambia wasiwe wanachangia na watoke nje kwenye bajeti za wizara ambazo sio za Muungano kwa kuwa haziwahusu


kwani Zanzibar ina balozi ? mnaodhani Zanzibar ni tegemezi kwa Tanganyika vunjeni Muungano..
Zanzibar ilikua na uchumi unaolingana na Mauritius..
ila baada ya bara kulazimisha mambo ya kiuchumi ya msingi ya Zanzibar kuingizwa kwenye Muungano ndio ikawa nuksi..

iachieni Zanzibar ijitawale..mbona hamkomi kupeleka mazombie nyakati za uchaguzi eti muendelee kuifanya Zanzibar koloni..

Zanzibar kumejaa Watanganyika wanakusanya kodi na kuzipeleka bara lakini bara hakuna mzanzibari anaekusanya kodi na kupeleka zanzibar...
 
Mimi naona tunauhitaji muungano japo wadau wa muungano wanapaswa kuamua wenyewe waungane kwa mfumo upi na sio yale mambo ya uchawi wa kuchanganya udongo.

Muungano huu umeingia mikikimikiki na bado upo,hii ni ishara kuwa unaweza pia kuhimili referendum.
Hatuna haja ya kuendelea kuuweka vidonda japo tuna fursa ya kuutazama upya.
Kama Nchi za Ulaya zenye nguvu zinaungana kwaajili ya usalama na uchumi, na sisi wachanga hatuwezi kukwepa.

Tuupinge ule uchawi wa kuchanganya udongo, tuanzishe muungano wa kisasa na wenye faida kwa pande zote.
 
Oneni siasa ilivyokua mbaya.Kessy akiwashambulia Zanzibar kwa maneno makali kambi yake wanamshangilia.Hao wanao mshangilia Kessy ndio wanasema ooo muungano ulindwe kwa gharama yoyote.

Kessy ametumia lugha ya kuudhi nashangaa Mhagama hajasimama
Akiulizwa kesi kuhusu muungano anaweza akasema uvunjwe kwakua amesema wanatunyonya bara.

Kwamaneno ya Kessy nikwamba wabunge wote watokao visiwani hata mtu awe waziri,au mwenyekiti wa bunge akae kwenye wizara za muunganotu.Je nyie CCM waumini wa muungano mmemuelewa Kessy vizuri au mmeshangiliatu.

Mimi sio mzanzibar lakini huo ni ubaguzi,unyanyapaa,udhalilishaji na nilugha ya kuudhi.

Je huyo mwenyekiti hapo sibora angeondokatu

Mhagama kwani unapo lalamika lugha ya kuudhi maranyingi unamaanisha nini?Angekuapo Zungu angemtuliza Kessy maana angalau yeye anaweza kukemea
 
Awataka wabunge wa Zanzibar kuanzia sasa wachangie Wizara zinazo wahusu, Awataka wawe wanatoka nje pale bunge linapojadili mambo yasiyo ya Muungano, sio wanatujazia foleni ya kuongea hata kwa mambo yasio ya Muungano.

Hivyo kasema Wanapaswa kutoka nje Zinapojadiliwa Wizara Zisizoihusu Zanzibar.

Ally Kessy Mbunge wa Nkasi, amesema Wazanzibar waache kuwanyonya Watanganyika. ameyasema hayo wakati wa kuchangia Wizara ya mambo ya Nje.

Amesema Wabunge kutoka Zanzibar wapo zaidi ya 54, wangekaa kule kwao hata Bunge lao lingeonekana dogo, wasingepata pa kukaa, hivyo wanapokuja wawe wapole.

Amedai wabunge wa Zanzibar wanataka haki sawa katika Uteuzi wa Mabalozi wakati wakati Mabalozi wenyewe ni 21 tu. Kasema kwa kuwa Zanzibar inachangia Asilimia 4, hivyo na mabalozi inabidi wawe asilimia nne. Hata kama wapo Manaibu Balozi wamependelewa tu.

 
Poor Kessy. "Nchi kubwa zinaungana vinchi vidogo vinawaza kutengana"J.K Nyerere
 
Ukweli una uma. Naungana na Kessy wawe wanatoka nje ya Bunge mambo yasiyo ya Muungano na posho isimame!! Na wawe waalikwa tu kwenye Wizara za Muungano.

Nakumbushia TANESCO huwa mnajidai mnatukatia sisi umeme tukichelewa kulipa. Bonyeza Switch ya OFF kwa Zanzibar kwa deni lenu.

Hawa majaa ni wavivu na wavuvi tu, kufanya kazi hawataki ila wanataka wakwee kupitia mgongo wa TANGANYIKA!! Mwaka huu inakula kwenu na MCC yenu!
 
Subiri majibu ya ngonjera na povu kutoka kwa Zbar! Amewachokora jichoni na pilipili! Inauma sana! Tusubiri!! Ila sababu ya njaa huwa wanakomaa hadi bunge lishe hawajaongea lolote na wal haiwahusu kuongea!!njaa mbaya sana! Koloni letu la mtu mweusi
 
Awataka wabunge wa Zanzibar kuanzia sasa wachangie Wizara zinazo wahusu, Awataka wawe wanatoka nje pale bunge linapojadili mambo yasiyo ya Muungano, sio wanatujazia foleni ya kuongea hata kwa mambo yasio ya Muungano.

Hivyo kasema Wanapaswa kutoka nje Zinapojadiliwa Wizara Zisizoihusu Zanzibar.

Ally Kessy Mbunge wa Nkasi, amesema Wazanzibar waache kuwanyonya Watanganyika. ameyasema hayo wakati wa kuchangia Wizara ya mambo ya Nje.

Amesema Wabunge kutoka Zanzibar wapo zaidi ya 54, wangekaa kule kwao hata Bunge lao lingeonekana dogo, wasingepata pa kukaa, hivyo wanapokuja wawe wapole.

Amedai wabunge wa Zanzibar wanataka haki sawa katika Uteuzi wa Mabalozi wakati wakati Mabalozi wenyewe ni 21 tu. Kasema kwa kuwa Zanzibar inachangia Asilimia 4, hivyo na mabalozi inabidi wawe asilimia nne. Hata kama wapo Manaibu Balozi wamependelewa tu.


Yaani hapo wabunge wa CCM wameona wamefanya kazi kweli kweli na kujipongeza
 
Back
Top Bottom