Amini, Usiamini. Nimepona Magonjwa 100+ Kwa Jina la Yesu!

Amini, Usiamini. Nimepona Magonjwa 100+ Kwa Jina la Yesu!

Hakuna kitu kibaya kama kiburi cha uzima,it's as if hakuna Mungu,cha ajabu mtu huyo huyo anayebisha hapa kila Jumapili yuko kwenye ibada......
Umenena vema, mkuu. Jumapili wako ibadani; lakini kwakuwa macho ya mioyo yao yametiwa giza, hata wakisikia, hawaelewi
 
Kwamba umeponywa hautaumwa tena? Vipi wanaopana bila hata kuamini hayo mambo ya Mungu?
Yeye Yesu yuko wakati wowote na mahali popote. Siyo kwamba siumwi ila nikiumwa ninajua wa kumwendea kupata uponyaji. Yeye ni mponyaji wangu na atendelea kuniponya na siyo hayo tu amenikirimia mambo makubwa zaidi ambayo ni uzima wa milele. Siku zangu zikifika mwisho hapa dunani atanipokea kwenye ufalme wake wa milele. Hayo ndiyo makubwa zaidi ya uponyaji. Ninakushauri ukate shauri leo kumpokea huyu mwamba Yesu akupe uzima wa milele. Si unaona watu wanavyokufa ndugu yangu. Fanya haraka sana usije kuchelewa. Tafuta wachungaji wanaohubiri wokovu wakuombee na siyo manabii wa kukupa maji na mafuta. Watumishi wa kweli wanatumia neno la Mungu (biblia) tu kukuombea tena bure.
 
Yeye Yesu yuko wakati wowote na mahali popote. Siyo kwamba siumwi ila nikiumwa ninajua wa kumwendea kupata uponyaji. Yeye ni mponyaji wangu na atendelea kuniponya na siyo hayo tu amenikirimia mambo makubwa zaidi ambayo ni uzima wa milele. Siku zangu zikifika mwisho hapa dunani atanipokea kwenye ufalme wake wa milele. Hayo ndiyo makubwa zaidi ya uponyaji. Ninakushauri ukate shauri leo kumpokea huyu mwamba Yesu akupe uzima wa milele. Si unaona watu wanavyokufa ndugu yangu. Fanya haraka sana usije kuchelewa. Tafuta wachungaji wanaohubiri wokovu wakuombee na siyo manabii wa kukupa maji na mafuta. Watumishi wa kweli wanatumia neno la Mungu (biblia) tu kukuombea tena bure.
Huwa mna shida kubwa sana ya akili , sijakuomba uniletee mahubiri , kama hauna jibu ungepiga kimya tu
 
To name just a few....; Baada ya kuona hapo utagundua kwamba hakuna cha mapepo wala nini pengine ni uamuzi wako tu wa lishe..., Au kama unaamua kuachia mazalia ya mbu kwako basi usishangae malaria akiwa mgeni wako....
disease (and key nutrient involved)symptomsfoods rich in key nutrient
Source: Gordon M. Wardlaw, Perspectives in Nutrition (1999).
xerophthalmia (vitamin A)blindness from chronic eye infections, poor growth, dryness and keratinization of epithelial tissuesliver, fortified milk, sweet potatoes, spinach, greens, carrots, cantaloupe, apricots
rickets (vitamin D)weakened bones, bowed legs, other bone deformitiesfortified milk, fish oils, sun exposure
beriberi (thiamin)nerve degeneration, altered muscle coordination, cardiovascular problemspork, whole and enriched grains, dried beans, sunflower seeds
pellagra (niacin)diarrhea, skin inflammation, dementiamushrooms, bran, tuna, chicken, beef, peanuts, whole and enriched grains
scurvy (vitamin C)delayed wound healing, internal bleeding, abnormal formation of bones and teethcitrus fruits, strawberries, broccoli
iron-deficiency anemia (iron)decreased work output, reduced growth, increased health risk in pregnancymeat, spinach, seafood, broccoli, peas, bran, whole-grain and enriched breads
goitre (iodine)enlarged thyroid gland, poor growth in infancy and childhood, possible mental retardation, cretinismiodized salt, saltwater fish
We unajua "instant healing" au unaisikia tu? Hizo nutrients ukila unapata instant healing? Biology yako ulisoma wapi, mkuu. By the way, mpe mtu mwenye pepo bubu au kiziwi nutrients zote unazojua uone kama ataongea au kusikia. Lakini kwa jina la Yesu, ni instant healing. Hakuna kusubiri mtu ale eti saltwater fish/enriched breads. Jina la Yesu liko juu ya majina yote ya magonjwa. Ila shetani amewapofusha watu wasijue siri hii. Matokeo yake watu wanateswa na mapepo wanazunguka hospitali zote India, Uingereza na Marekani, wanarudi bila uponyaji.
Mathayo 9:32-33: Walipokuwa wakitoka, tazama, watu walimletea(Yesu) mtu aliyekuwa bubu mwenye pepo. Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena; makutano wakastaajabu, wakisema, 'Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli.'
 
Mkuu sio kwamba tunabisha tu ni kweli kwamba hayupo , akithibitika hakuna mtu anaweza kuhoji uwepo wake , hizo ni imani tu na zipo imani za uwepo wa Mungu zaidi ya 1000 na kila mmoja anadai Mungu wake ni sahihi zaidi ya mwingine, jinsi miaka inakwenda watu wanazidi kupata mashaka ya hizo imani zilizojengwa akilini kwa watu na vitisho na ahadi .
Hatushangai kusikia kwamba huamini. Hata Waisraeli, Yesu alikuja kwao, wakamuona "live" lakini hawakumwamini.
 
Huu ni ushuhuda wa kweli kabisa. Katika maisha yangu nimekuwa nikiugua magonjwa mengi ya aina mbalimbali. Kifuani, tumboni, miguuni, katika vidole, machoni, masikioni, puani, kichwani, nk, nk. Muda hautoshi kuyaeleza kwa kina. Kwa haraka haraka naweza kusema tangu ujana wangu nimeugua zaidi ya magonjwa 100. Namshukuru Mungu kwakuwa amekuwa akiniponya magonjwa kila yanaponiijia. Ninachokifanya, kila nikiumwa, namuomba Mungu aniponye kwa Jina la Yesu, kisha naweka mkono wangu juu ya sehemu inayoumwa na kuuamuru ugonjwa utoke kwa Jina la Yesu; kisha naamini kwamba imekuwa hivyo. Wakati mwingine inachukua muda kuona matokeo lakini wakati mwingine ugonjwa unatoweka saa hiyo hiyo. Maneno aliyosema Yesu ni kweli kabisa. Katika Mk 16:17-18 anasema: “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu(Yesu) watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.”

Huu ni uthibitisho kuwa Mungu yupo na anatenda miujiza hata leo kwa watu wanaomuamini. Kwa ushuhuda huu sikuambii usiende hospitali. La, hasha! Ukiwa na pesa, nenda. Nenda hata hospitali za nje ya nchi. Hata mimi kuna wakati huwa naenda hospitali kwa kuwa najua kwamba Mungu anaweza pia kuponya kwa kuwatumia madaktari. Hata hivyo ninapoenda hospitali bado naweka matumaini yangu kwa Mungu kwakuwa najua madaktari nao kuna magonjwa yako juu ya uwezo wao au elimu yao; na wakati mwingine nadhani huwa wanajisahau, badala ya kutia moyo wanakatisha tamaa. Kuna siku nilipungukiwa damu, nikaenda kumuona Daktari. Aliponipima na kuhakikisha damu imepungua, akaniuliza: “Damu umepeleka wapi wewe?” Usipokuwa na matumaini kwa Mungu ukiulizwa swali hilo la kuvunja moyo unaweza ukaugua mara mbili zaidi. Na kwa magonjwa niliyougua, kama kila ugonjwa ningekuwa nakimbilia hospitali, ningehitajika kuwa milionea maana ningepaswa kulipa pesa nyingi za matibabu. Namshukuru Yesu anaponya bila kulipa hata senti. Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka hizi za uzima.

Hata hivyo kuna vigezo na masharti ya kuzingatia ili mtu aone kikamilifu uponyaji wa Mungu kwa Jina la Yesu. Baadhi ya vigezo vimeelezwa katika Andiko hili: Kutoka 15:26. “Mungu akasema, ‘Kama mtaisikiliza kwa bidii sauti yangu mimi BWANA Mungu wenu na kuyafanya yaliyo sawa mbele yangu, kama mtayatii maagizo yangu na kuzishika amri zangu zote, sitaleta juu yenu ugonjwa wowote niliowaletea Wamisri, kwa kuwa Mimi ndimi BWANA, niwaponyaye.’” Uponyaji wa Mungu ni wa bure kwa wote wanaozingatia maneno hayo. Ukisikia Mtumishi anakuambia ulipe pesa kwanza ndio akuombee, jihadhari naye. Yesu alipowapa mamlaka wanafunzi wake ya kukemea pepo na kuweka mikono juu ya wagonjwa ili wapone, aliwaambia amewapa bure, hivyo wanapaswa kutoa huduma hiyo bure(Mathayo 10:8).

Yamkini unaumwa, umetibiwa kila mahali hujapona. Usikate tamaa. Ushuhuda huu ukutie moyo kuwa unaweza kupona kwa uwezo wa Jina la Yesu Kristo. Yote yawezekana kwake aaminiye(Mk 9:23). Amen.
Uliyapima kabla hayo magonjwa 100+?
 
We unajua "instant healing" au unaisikia tu? Hizo nutrients ukila unapata instant healing? Biology yako ulisoma wapi, mkuu. By the way, mpe mtu mwenye pepo bubu au kiziwi nutrients zote unazojua uone kama ataongea au kusikia. Lakini kwa jina la Yesu, ni instant healing. Hakuna kusubiri mtu ale eti saltwater fish/enriched breads. Jina la Yesu liko juu ya majina yote ya magonjwa. Ila shetani amewapofusha watu wasijue siri hii. Matokeo yake watu wanateswa na mapepo wanazunguka hospitali zote India, Uingereza na Marekani, wanarudi bila uponyaji.
Mathayo 9:32-33: Walipokuwa wakitoka, tazama, watu walimletea(Yesu) mtu aliyekuwa bubu mwenye pepo. Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena; makutano wakastaajabu, wakisema, 'Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli.'
Kama una matege kwanini ungojee kupata instant healing wakati unajua kabisa Vitamin D inahitajika ? Sasa unampa kiziwi nutrients ili aweze kusikia wakati huenda anahitaji hearing aids ?

Kwanini tuna complicate mambo ambayo yapo straight forward kabisa..., ila kama ni kitu Psychological na mind over matter works hata ukimwambia alete kuku mweusi na wewe ku recite Abracadabra za kutosha uneweza kumuaminisha kwamba all is well (Placebo); na mtu alikuwa anasikia maumivu ya kichwa akajiona amepona...
 
Uliyapima kabla hayo magonjwa 100+?
Nipoteze pesa za nini kupima, mkuu? Nikienda hospitali ndio wananipima. Lakini kama nilivyosema magonjwa mengi nimepona kwa muujiza baada ya kuyakemea kwa Jina la Yesu.
 
Nipoteze pesa za nini kupima, mkuu? Nikienda hospitali ndio wananipima. Lakini kama nilivyosema magonjwa mengi nimepona kwa muujiza baada ya kuyakemea kwa Jina la Yesu.
Aiseee..!!! Sasa naelewa kwanini umesema "amini usiamini".
 
Nipoteze pesa za nini kupima, mkuu? Nikienda hospitali ndio wananipima. Lakini kama nilivyosema magonjwa mengi nimepona kwa muujiza baada ya kuyakemea kwa Jina la Yesu.
Kwahio unashauri hata zile Hospitali tuzigeuze kuwa Makanisa, Mahekalu na Misikiti ?
 
Hakuna kitu kibaya kama kiburi cha uzima,it's as if hakuna Mungu,cha ajabu mtu huyo huyo anayebisha hapa kila Jumapili yuko kwenye ibada......
Yamkini mtoa mada ni muongo sana, uongo wake hautukatazi kwenda kusali
 
Huu ni ushuhuda wa kweli kabisa. Katika maisha yangu nimekuwa nikiugua magonjwa mengi ya aina mbalimbali. Kifuani, tumboni, miguuni, katika vidole, machoni, masikioni, puani, kichwani, nk, nk. Muda hautoshi kuyaeleza kwa kina. Kwa haraka haraka naweza kusema tangu ujana wangu nimeugua zaidi ya magonjwa 100. Namshukuru Mungu kwakuwa amekuwa akiniponya magonjwa kila yanaponiijia. Ninachokifanya, kila nikiumwa, namuomba Mungu aniponye kwa Jina la Yesu, kisha naweka mkono wangu juu ya sehemu inayoumwa na kuuamuru ugonjwa utoke kwa Jina la Yesu; kisha naamini kwamba imekuwa hivyo. Wakati mwingine inachukua muda kuona matokeo lakini wakati mwingine ugonjwa unatoweka saa hiyo hiyo. Maneno aliyosema Yesu ni kweli kabisa. Katika Mk 16:17-18 anasema: “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu(Yesu) watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.”

Huu ni uthibitisho kuwa Mungu yupo na anatenda miujiza hata leo kwa watu wanaomuamini. Kwa ushuhuda huu sikuambii usiende hospitali. La, hasha! Ukiwa na pesa, nenda. Nenda hata hospitali za nje ya nchi. Hata mimi kuna wakati huwa naenda hospitali kwa kuwa najua kwamba Mungu anaweza pia kuponya kwa kuwatumia madaktari. Hata hivyo ninapoenda hospitali bado naweka matumaini yangu kwa Mungu kwakuwa najua madaktari nao kuna magonjwa yako juu ya uwezo wao au elimu yao; na wakati mwingine nadhani huwa wanajisahau, badala ya kutia moyo wanakatisha tamaa. Kuna siku nilipungukiwa damu, nikaenda kumuona Daktari. Aliponipima na kuhakikisha damu imepungua, akaniuliza: “Damu umepeleka wapi wewe?” Usipokuwa na matumaini kwa Mungu ukiulizwa swali hilo la kuvunja moyo unaweza ukaugua mara mbili zaidi. Na kwa magonjwa niliyougua, kama kila ugonjwa ningekuwa nakimbilia hospitali, ningehitajika kuwa milionea maana ningepaswa kulipa pesa nyingi za matibabu. Namshukuru Yesu anaponya bila kulipa hata senti. Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka hizi za uzima.

Hata hivyo kuna vigezo na masharti ya kuzingatia ili mtu aone kikamilifu uponyaji wa Mungu kwa Jina la Yesu. Baadhi ya vigezo vimeelezwa katika Andiko hili: Kutoka 15:26. “Mungu akasema, ‘Kama mtaisikiliza kwa bidii sauti yangu mimi BWANA Mungu wenu na kuyafanya yaliyo sawa mbele yangu, kama mtayatii maagizo yangu na kuzishika amri zangu zote, sitaleta juu yenu ugonjwa wowote niliowaletea Wamisri, kwa kuwa Mimi ndimi BWANA, niwaponyaye.’” Uponyaji wa Mungu ni wa bure kwa wote wanaozingatia maneno hayo. Ukisikia Mtumishi anakuambia ulipe pesa kwanza ndio akuombee, jihadhari naye. Yesu alipowapa mamlaka wanafunzi wake ya kukemea pepo na kuweka mikono juu ya wagonjwa ili wapone, aliwaambia amewapa bure, hivyo wanapaswa kutoa huduma hiyo bure(Mathayo 10:8).

Yamkini unaumwa, umetibiwa kila mahali hujapona. Usikate tamaa. Ushuhuda huu ukutie moyo kuwa unaweza kupona kwa uwezo wa Jina la Yesu Kristo. Yote yawezekana kwake aaminiye(Mk 9:23). Amen.
Nimeshaandika sana humu kama mnaleta shuhuda za uponyaji leteni shuhuda za amputees (waliokatwa mikono au miguu) walioponywa. Hayo mengine mazingaombwe tu!
 
Ah, I see you're unleashing quite the tapestry of whimsical observations. Allow me to reciprocate in kind: Your penchant for theatrical declarations could rival the most eccentric of dramatists, but alas, it appears that your rhetorical compass has wandered far afield. Perhaps a recalibration of your logic processor is in order, lest you remain adrift in this sea of imaginative conjecture.
Nimefurahia kiingereza chako japo sijui kama mtoa mada amekuelewa. Seems like you was whistling the wind!😆
 
We unajua "instant healing" au unaisikia tu? Hizo nutrients ukila unapata instant healing? Biology yako ulisoma wapi, mkuu. By the way, mpe mtu mwenye pepo bubu au kiziwi nutrients zote unazojua uone kama ataongea au kusikia. Lakini kwa jina la Yesu, ni instant healing. Hakuna kusubiri mtu ale eti saltwater fish/enriched breads. Jina la Yesu liko juu ya majina yote ya magonjwa. Ila shetani amewapofusha watu wasijue siri hii. Matokeo yake watu wanateswa na mapepo wanazunguka hospitali zote India, Uingereza na Marekani, wanarudi bila uponyaji.
Mathayo 9:32-33: Walipokuwa wakitoka, tazama, watu walimletea(Yesu) mtu aliyekuwa bubu mwenye pepo. Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena; makutano wakastaajabu, wakisema, 'Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli.'
Narudia kuuliza tena hii imani yenu ya uponyaji imeishia hapo tu? Vipi kuhusu kuwaponya amputees? Mbona hamjibu??? Maana hapo ni kama Mungu wenu hawezi!
 
Hii ni delusion
Wahi kwa psychologist kabla haujapelekwa kwa psychiatrist
I acknowledge your perspective but dissent; what you designate as a 'delusion' epitomizes my profound existential encounter with faith and divine intercession—domains beyond the purview of psychology or psychiatry to adequately delineate or encapsulate.
 
Back
Top Bottom