Fasta fasta
JF-Expert Member
- Feb 15, 2011
- 1,125
- 725
Kabla hamjatoa hizi comment muwe mnaangalia hizo nchi mnazoshabikia zinafanya mabaya mangapi na hawaguswi na the so called Mahakama ya Kimataifa. Libya imefanywa nini na je walioifanya hivyo wamechukuliwa hatua gani? Iraq, Afghanstan na nchi nyingine nyingi tu wameziharibu lakini kimya. Huko huko Marekani watu weusi wanauwawa mchana kweupe lakini haya yanayojiita mashirika ya upuuzi yamekaa kimya wala darubini zao hazimuliki huko.
Kila nchi inautamaduni wao jinsi ya kuishi, wengine wanapenda kuwa wakimbizi, wangine kupigana risasi, wengine ubaguzi, wengine wanaishi kwa chuki kwa sababu wamekosa Uhuru, Amani, na upendo muda mrefu hawakuipata. Na yote haya yanatokana na kunyanyaswa, kukosa ajira, rushwa, uwongo, chuki, kutokuheshimiana n.k.
Afadhali leo tumepata watu wakutukumbusha kama hawa inamaana wanatupenda na sisi lazima tuone kwa nini kelele zimekuwa nyingi hivi?
Na hayo uliyoyataja hapo juu yatakuwa yametoka aidha kwa babu na bibi zao au kwa baba na mama zao. Wewe unafikiria maisha ya leo badala ya kesho. Mimi na wewe tunatakiwa tujenge nchi yetu sio tubaguane ili kizazi kinachotuangalia kituige.
Leo tunaweza kupambana mimi na wewe kwa mdomo lakini kesho vijana wetu watapigana kwa mapanga na risasi lwa akili ya madaraka. Roho yangu mimi na wewe itatusuta tutasema kwa nini hatukukaa tukawatengenezea hawa vijana maisha kama waliopita walivyotuandalia?
Ila inaonyesha una ubinafsi au ni mvivu wa kufikiri au unasoma kwa kukariri. Jaribu uwe na rafiki wa kizungu utabadilika.
Nakuombea hizo chuki zikutoke usije kupelekea kizazi chetu cha kesho maisha kama ya somalia.
Watanzania walishakubaliana ili kuondoa mzizi wa fitina nchi yetu hii katiba irekebishwe na kweli ikarekebishwa. Huyu aliyeificha anaitakia nini Tanzania au watoto wetu? Si anataka vita au?