Amos Makalla: Chanzo cha moto wa soko la Karume ni mshumaa uliowashwa na mateja

Amos Makalla: Chanzo cha moto wa soko la Karume ni mshumaa uliowashwa na mateja

Tumesikia taarifa ya Tume iliyoundwa kwa ajili ya uchunguzi wa chqnzo cha moto Soko la Karume Dsm.....almaarufu mchikichini.
Kwa Taarifa hii
(1) Ninamuomba Madame President ikimpendeza YAANI IKIMPENDEZA WAJUMBE WA HII TUME WASILIPWE KWA KWELI SABABU WAMETUMIA MUDA MWINGI KU PROVE MANENO YA MLINZI
(2) MLINZI AHOJIWE TENA VIZURI KUHUSU UPATIKANAJI WA MISHUMAA KWA AJILI YA KUCHOMA SOKO/ MASOKO USIKU
NI HAYO TU....ILA MBONA BWANA ZUNGU HAFUNGUI MDOMO WAKATI HILI LIMETOKEA JIMBONI MWAKE ? AU ANA JADILI KUUPATA UNDUNGAI ?
Yuvisisiemu mmekubaliana na hili au mtapinga? Mana RC katembea na maneno yote ya yule kijana aliehojiwa Clouds lakini sijui mnatuonaje wananchi wa hii nchi?
 
Hahahaha[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji81][emoji81]
 
Miongoni mwa Maoni na Mapendekezo ya Kamati hiyo Ni pamoja Ujenzi wa Soko jipya linaloendana na Hali ya Sasa na vizimba kutolewa kwa kipaombele kwa wazawa, Je kuna watu wa nje wanaofanya biashara hapo? au ndo tunaambiwa kwamba wameshakaribishwa?
 
"Miongoni mwa Maoni na Mapendekezo ya Kamati hiyo Ni pamoja Ujenzi wa Soko jipya linaloendana na Hali ya Sasa na vizimba kutolewa kwa kipaombele kwa wazawa, uwepo wa mfumo mzuri wa kuzuia Moto, Barabara za kuingia na kutoka, Ujenzi wa Majengo ya Muda mfupi, Kila mfanyabiashara kuwa na bima."

Hiki ndicho walichokuwa wanakitaka. Hao wafanyabiashara hawatarudi tena kwani ilikuwa trick ya kuwaondoa, halafu unasema umati umeshangilia? Hao wanarudije wakati mitaji hawana tena?


Hii nchi ina mambo mengi ya kushangaza.



Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kufuatia soko la wamachinga la Karume kuunguzwa moto na "watu wasiojulikana" na serikali kuunda tume ya kuchunguza chanzo cha moto huo, hatimaye mbivu na mbichi zimejulikana baada ya kamati kubaini mhalifu aliyefanya uharamia huo wa kuunguza mali za wateja na miundombinu yao ya biashara. Akitoa majibu mbele ya waandishi wa habari, mwenyeketi wa kamati iliyochunguza tukio hilo Engineer Justin Lukaza amemtaja hadharani mtu aliyehusika kusoma soko hilo kwa makusudi (arson). Bila kuwapotezea muda wala kufanya mambo kuwa mengi, hebu msikilize mwenye mubashara hapo chini 👇 👇 👇

 
SERIKALI YARUHUSU WAFANYABIASHARA KUREJEA KARUME KWA MPANGO MZURI.

- Umati walipuka kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan.

- RC Makalla apokea taarifa ya ripoti ya Kamati iliyoundwa kuchunguza Chanzo Cha Moto.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameruhusu Wafanyabiashara wa Soko la Karume kurejea na kuendelea na Biashara kwa kuwekewa Mpango mzuri ambapo Wafanyabiashara wa Soko hilo wamepongeza uamuzi huo na kuishukuru Serikali.

Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara na Wafanyabiashara hao Mara Baada ya kupokea Taarifa ya ripoti iliyoundwa kuchunguza chanzo Cha Moto, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amesema Rais Samia ameelekeza pia uwepo utaratibu mzuri wa kuzuia Moto, kuhakikisha hakuna atakaedhulumiwa eneo lake na kutoa ruhusa kwa Wafanyabiashara kujenga Vibanda kwa gharama zao.

Kuhusu Ripoti ya chanzo Cha Moto, RC Makalla amesema Kamati imebaini Moto huo ulitokana na Mshumaa uliowashwa kwenye kibanda walichokuwa wanajihifadhi watumiaji wa dawa za kulevya "Mateja".

Aidha RC Makalla amesema Baada ya kupokea ripoti hiyo ataikabidhi kwenye Mamlaka za juu kwaajili ya utekelezaji wa maoni na Mapendekezo yote ya Kamati.

Miongoni mwa Maoni na Mapendekezo ya Kamati hiyo Ni pamoja Ujenzi wa Soko jipya linaloendana na Hali ya Sasa na vizimba kutolewa kwa kipaombele kwa wazawa, uwepo wa mfumo mzuri wa kuzuia Moto, Barabara za kuingia na kutoka, Ujenzi wa Majengo ya Muda mfupi, Kila mfanyabiashara kuwa na bima.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo Eng. Justin Lukaza amesema hasara iliyotokana na Kuungua Hilo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 7.2 ambapo idadi ya Wafanyabiashara waliokumbwa na janga Hilo Ni 3,090.

Pia soma:

- Shuhuda: Chanzo cha moto soko la Karume ni mateja, waliangusha mshumaa wakati wanatengeneza mihadarati (18/01/2022)
View attachment 2094094
 

Attachments

  • twitter_20220120_101600.mp4
    77.2 KB
Mmmmmmmh!Hii ngumu kumeza!

Moto kusambaa kona zote za Soko Kutokana na mshumaa Mmoja? Msiwe wavivu wa kufikiri!! Kariakoo nako ni hao hao mateja? Mnapenda sana majibu ya rahisi rahisi.
 
Back
Top Bottom