Amsterdam and partners LLP wamlima barua Rais Magufuli na Jaji Mkuu, wabainisha njama zote zinazosukwa

Amsterdam and partners LLP wamlima barua Rais Magufuli na Jaji Mkuu, wabainisha njama zote zinazosukwa

Huyu Amsterdam alisikilizwa alipisema Tl asikamatwe akitua si ndio? Akisikilizwa tena ntaamini anayezungumza ni mtu tofauti kabisa na anavyojipambanua.
 
Ungewashauri wale waliompiga risasi hivi kwamba kwanini walifanya ungukuwa na maana Sana kuliko upumbavu ulioandika.
Hiyo barua ni kwa ajili ya mtu kama wewe usioweza kufikiri.

Tatizo lenu serikali ikisema itumie busara na kuachia tu watu wafanye mambo ata kama kinyume na sheria mnaanza kudai mnaogopwa sijui Amsterdam kasaidia etc with nonsense.

Wakichukua hatua mnaonewa ni shida tupu; ni mahakama gani kwa mfano huyo Amsterdam anaweza fungua kesi unadhani?
 
Capture.JPG

kama kweli magufuli na ccm yako mnapanga kufanya hiki kitu.... Mungu atawashughulikia ktk namna inayowafaa na mimi naomba mlaaniwe.
 
Amezuia mradi upi? Makinikia au? Au amelipwa zile trions?
Unaujua mradi wa gas lindi hadi ulipofanyiwa tathmini upya na watu kuliowa kulingana na thamani halisi?

Mradi wa madini ya uranium huko ruangwa pia aliusimamisha na tathmini bado inaendelea.

Pia alizuia usafirishaji wa madini kwa jina la makinikia na jamaa kupigwa faini. Kwa sasa hata kama wanasafirisha inajulikana madini ni yapi na makinikia ni yapi..umesahau mvutano kati ya serikali na maafisa waandamizi wa acacia na nyie ndio mlikuwa mkishangilia wale maofisa wa acacia kabla hawajapigwa na kurudi kwao.
 
ICC inafanya kazi kama ofisi za waendesha mashtaka wa serikali sawa sawa na ofisi ya DPP kwa Tanzania.

Kesi zao wanazitafuta wenyewe na wanakushitaki wenyewe hakuna mwanasheria independent anaweza kwenda kufungulia nchi au mtu kesi ICC.

Mambo mengine ni kufurahishana tu, kati ya Lissu na wafuasi wake lakini Amsterdam hana jurisdiction kwenye mambo ya ndani ya Tanzania.

Binafsi naomba Lissu asikatwe pamoja na kuvunja kanuni aachwe agombee baada ya kushindwa ndio watu wataelewa huyu mtu anahitaji psychological help.

Lissu kwa sasa anaamini yeye ni mtu untouchable, above the Tanzania laws, he has large support ready to rebel and that belief is growing as days go kwa sababu vyombo vya ulinzi wameamua ku entertain his thoughts tangia amerudi out of pity considering his plight but at some point he needs to come down to earth.

Baada ya kushindwa uchaguzi the extent of Lissu’s mental health problem will become obvious, to many people; time will tell.
Vipi Magu ,yupo juu ya sheria zetu?
 
Barua yenyewe ndio hiyo, jisomee mwenyewe.

Nimeisoma hii barua mpaka mwisho...

Barua imeandikwa kiweledi haswa na imebeba amri na maelekezo....

Halafu inaeleza mambo ya ndani hasa kiasi cha mtu kujiuliza nani anawataarifu hawa kinachoendelea ktk corridor za usalama za Ikulu ya Magufuli?...

Ukisoma barua hii NENO kwa NENO utagundua kuwa, hawa watu wana dhamira ya kweli kwa njia zozote kumlinda mteja wao....

Na ni kama Amsterdam & Partners LLP ni waanzisha varangati tu, lakini watendaji halisi wako sehemu wala hawajapanua mdomo....

Kwa akina sisi, tumejua hata ambayo tulikuwa hatuyajui kwa kweli katika sakata hili....

Kumbe kesi yake ya "sedition - uchochezi" ya trh 26/8 imepangwa hiyo tarehe kwa makusudi kabisa na ndani yake kukiwa na nia ovu au "collusion" kati ya Ikulu (serikali), Mahakama na NEC...!!

Na kumbe pingamizi la "Ugombea Urais wa Tundu Lissu" tayari lipo, lilikwisha kuandaliwa siku nyingi.....

Na kwamba, siku hiyo hiyo atakayokuwa mahakamani, ndiyo siku hiyo hiyo atatakiwa na NEC kuja kujitetea kwa nini asiondolewe sifa za ugombea Urais kwa sababu watakazokuwa nazo waweka pingamizi wake....

Na huko mahakamani tarh 26/8 kumbe wamepanga kumuweka ndani (under detention) kwa siku kadhaa ili tu ashindwe kwenda kujitetea Dodoma kwenye NEC dhidi ya pingamizi lake, na muda uwe umekwisha kisha wanamwachia...

Baada ya muda kwisha wa kujitetea, NEC hawatakuwa na kizuizi tena kumwondoa ktk orodha ya wagombea kwa sababu watasema "hukuja kujitetea dhidi ya pingamizi lako"....

Loooh, huu ni ujinga na upumbavu wa kiwango cha juu sana ambao mamlaka za serikali ya Tanzania zinafanya eti kwa sbb ya mtu mmoja anayeitwa - Magufuli....

Nyuma ya mpango huu kwa kweli hakuna sababu zozote za kutaka kumzuia Tundu Lissu kutumia haki yake ya kiraia ya kuchaguliwa. Ni kwa sababu tu Magufuli hataki changamoto, hataki ushindani na hususani ushindani wa mtu sampuli ya Lissu....!!

Need we say more?

Absolutely nothing!!

Mimi sina shaka kuwa, hili jaribio nalo tayari limeshashindwa vibaya sana....!!!
 
Unaujua mradi wa gas lindi hadi ulipofanyiwa tathmini upya na watu kuliowa kulingana na thamani halisi?

Mradi wa madini ya uranium huko ruangwa pia aliusimamisha na tathmini bado inaendelea.

Pia alizuia usafirishaji wa madini kwa jina la makinikia na jamaa kupigwa faini. Kwa sasa hata kama wanasafirisha inajulikana madini ni yapi na makinikia ni yapi..umesahau mvutano kati ya serikali na maafisa waandamizi wa acacia na nyie ndio mlikuwa mkishangilia wale maofisa wa acacia kabla hawajapigwa na kurudi kwao.
Kwenye makinikia nani alipigwa faini?mwanaume au?
 
Vipi Magu ,yupo juu ya sheria zetu?
We umeona kuna mtu ameanza campaign mapema? Soma hiyo barua kama Lissu alikuwa anaona anachofanya sio kosa kwa kanuni za uchaguzi mbona anajihami leo kutokana na mambo aliyokuwa akifanya.

Ndio hayo watu walikuwa wanawaambia katika vyama 16 vilivyochukua form ni CDM peke yake ndio waliobaini loopholes za kanuni. Wengine wote mazoba.

NEC awajasema kitu mpaka sasa ni Lissu tu ndio anaeangaika na wasiwasi atakatwa kwa kuanza campaign mapema.
 
Wanachemka sasa..wameanza hadi kuingilia mhimili wa mahakama wakati wao wanajiita law firm..kweli hivi vikampuni vya kwenye mikoba vina shida sana.

Kisha wangejua ndio wanaharibu zaidi na wanamharibia mteja wao kwa kumtaja taja magufuli wangekaa kimya tu.

Maana magufuli huwa hajibizani na takataka. Huyo mteja wao mwenyewe kamtaja wee magufuli kwa majina yote na wala hajajibiwa hadi kaamua kujizungumzia yeye tu sasa.
Jitekenye halafu cheka mwenyewe.
 
We umeona kuna mtu ameanza campaign mapema? Soma hiyo barua kama Lissu alikuwa anachofanya sio kosa kwa kanuni mbona anajihami leo.

Ndio hiyo watu walikuwa wanawambia katika vyama 16 vilivyochukua form ni CDM peke yake ndio waliobaini loopholes za kanuni. Wengine wote mazoba.
Sheria inasemaje? Iweke hapa tuone inavyosema Kisha utuambie siku Magu anachukua form pale Dodoma alifanya nini na tbc walimuonesha live akiwa anafanya nini?
 
Sheria inasemaje? Iweke hapa tuone inavyosema Kisha utuambie siku Magu anachukua form pale Dodoma alifanya nini na tbc walimuonesha live akiwa anafanya nini?
Kila mtu alichukua fomu akaonekana hata lipumba na membe tuliwaona.

Je baada ya kuchukua fomu nini kiliendelea au nini kinaendelea?? Tunaanzia kutoka hapo.
 
Hiyo barua ni kwa ajili ya mtu kama wewe usioweza kufikiri.

Tatizo lenu serikali ikisema itumie busara na kuachia tu watu wafanye mambo ata kama kinyume na sheria mnaanza kudai mnaogopwa sijui Amsterdam kasaidia etc with nonsense.

Wakichukua hatua mnaonewa ni shida tupu; ni mahakama gani kwa mfano huyo Amsterdam anaweza fungua kesi unadhani?

The country could be an international pariah!!! Athari zake mnazijua lakini nchi ikipigwa spana au mnafurahia kusifia juhudi tu?
 
Back
Top Bottom