Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Broda leo unageuka unakuwa wakili wa watendaji wabovu wa serikalini kama walituibia gizani wacha waumbuke mwangani
 
I find emotions in your post.
Are you and can you be rational?
Open up, I believe you are afraid of loosing your lucrative contracts from the present
corrupt leaders of public corporations.
Let Kassim and his boss JPM salvage whatever is salvageable.
MP's should help this new administration by enacting a law to question Presidents, past and present.

Yes their immunities should be waived if there is evidence of their complicity in economic sabotage and financial crimes. In this way we shall honour Baba wa Taifa and also instil discipline in public service.
 
tena majaliwa angetakiwa atembee na bakora awacharaze hao watumishi hadharani

agustino mrema alitumia mfumo wa kuwapelekesha watumishi jeshi la polisi likanyooka alipokuwa mambo ya ndani

MAJALIWA endelea hivyo hivyo na tena wapigishe na warushe hata kichura chura hao mameneja kama Mohamed Buhari 1978 ALIVYOFANYA NIGERIA
 
Sawa kwasababu tumekuwa na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea na sio ufanisi wa kazi
 
Target ni JK now naona
naona wanataka ashindwe hata kuitisha vikao vya kamati kuu...
mambo yote sio mapya...nini kifanyike ndo hawaji nacho...ni ku expose na ku expose tu...

Magufuli amewahi kuagiza ubomoaji zaidi ya mara mbili, Rais na PM wakamzuia kufanya hivyo, Magufuli aliwahi kupambana na watu wa mizani, wanaozidisha uzito, PM akaingilia, Magufuli alikuwa anachukia sana lakini kwa sababu hakuwa na madaraka juu yao alikaa kimya.

Leo ana madaraka, ana expose ubovu wa system, ana expose madudu yaliyofanyika kipindi hicho, ili unaposet system nyingine unakuwa unajua wapi pa kubana kwa sababu mbinu na loopholes zote umezifahamu.

Huwezi tu kuweka system haraka kabla hujajua mbinu zote/nyingi ambazo zinaweza kutumika kukuibia.

Hivyo mpeni muda tu, atafanya kitu.
 
Mkuu Pasco hayo ni maonyesho. PM angeweza kumwita mtu ofisini na kumweleza aliyogundua, kumpa muda wa kujieleza akishindwa chukua hatua. Sio lazima uite waandishi wa habari ili uonekane unafanya kazi.

Ukweli ni kuwa JPM anajua kuwa hakuchaguliwa na watanzania, na anajua watanzania waliikataa CCM sasa ili ku win watu ni lazima afanye hivyo, ili hata wale ambao hawakumpigia kura wamuunge mkono.

Jana nilimhurumia sana alipokuwa anaongea na wafanyabiashara, maneno "naomba mniunge mkono" ameyarudia kama mara 20 hivi na akahitimisha kwa maneno "yalitopita si ndwele tugange yajayo." Anajua aliokuwa anazungumza nao hawakumuunga mkono wala hawakumpigia kura, anajua jinsi alivyoupata huo urais ndiyo maana ni lazima a - plead huruma ya watu.

Harakati za PM ni jitihada hizo hizo za kutaka support ya wananchi. Anyway tuwape muda tuone jinsi watakavyotuvusha kutoka hapa tulipo.
 
Wenyewe siyo wastaarabu kwa uzembe, wizi na Ufisadi wa mali za umma ambazo zi zetu sote wewe na mimi. Sasa unataka wafanyiwe ustaarabu gani zaidi ya kuwaumbua ili wajirekebishe na kutoa somo kwa wengine wenye tabia kama za kwao.
 
ameniuzi sana ,ye hajui hii inchi tunakawaida ya kuvumiliana atuvumilie tule tukichoka tutaacha
 
Kuna watu makopo humu ndani ni kama huyu mtoa uzi upo kama mwanamke ambaye hataki kuolewa kila siku anakuja na hiki mara kile!!hivi sasa tulitaka uongozi wa aina gani????aisee mungu tusamehe kwa hawa wachache waliozoea kuturudisha nyuma wewe Pasco ni zaidi ya mnafiki!!good governance zilikuwepo na kuundwa tume ya uchunguzi matokeo yake yalikuwa nn!!si ndio nyie nyie mlipiga kelele tumechoka na kuundiwa tume!!leo unakuja na kuandika huu upopoma aisee umenipa hasira nataman kukutukana dah mungu anisamehe buree!!
 
Watanganyika wanapenda matukio......tunashangilia matukio. Matukio yakiisha tutaanza kulalamika.
 
siku mtu msafi atakapokwenda mahakamani na hukumu kutoka ndio tutajifunza-kama makonda alitakiwa kufunguliwa kesi na jamaa wangeshinda
 
anataka amfunike pinda ili yeye apate sifa na umaarufu zaidi


Kwa akili yako Pinda ni mtu? Angekuwa yeye bandarini angeanza kulia na kuongea porojo tu. Kale kajamaa kalikuwa hasara kwa taifa na hata Kikwete alijuwa na ndiyo maana alimkata mapemaaa kwenye jopo la urais. Nani anataka iongozi anayelia bila kujuwa wajibu wake? Majaliwa na JPM ni kiboko na ndiyo tunaowahitaji hapa Tanzania. Hii nchi ililiwa sana.
 
Kweli watanzania nani katuloga?? Hiyo good governance ndio imetufikisha hapa tulipo kama vip hama nchi Pasco. Hapa kazi tu!
 
Hayo ni maoni yako ni kwanini unataka uyalazimishe kwa WatanZania wote? Hayo ya utawala bora ni kulingana na tafsiri yako wewe na jinsi unavyoongoza familia nyumbani kwako usitake kutuletea kwenye nchi yetu, tumeshatoka huko, tumeshayafanya yote hayo ya kuitana faragha, kuundiana tume, kuonyana kwamba ninawajua wala rushwa msipojirekebisha mtakiona cha mtema kuni kote huko tumepita lkn matokeo yake ni kwamba makontena zaidi ya 2500 hayajalipiwa kodi, yaani yamekombolewa Bandarini bila kulipiwa sasa huu ni uhujumu Uchumi na kwa nchi nyingine adhabu yake ni sawa na Uhaini kwani unalinganishwa na uuwaji watu wote waliofia mapokezi kwa kukosa dawa hospitalini wameuliwa na hawa wezi!

Hivyo tuache na Magufuli wetu tumeshamkubali jinsi alivyo na vyovyote anavyofanya ana baraka zetu, na ndio maana ya kushinda Uchaguzi na kuwa Raisi vinginevyo basi kila mtu angejiongoza?
Wao wameshindwa hiyo good governance, wanaitaka ya nini tena? Majaliwa endelea!
 
Waziri mkuu hawezi kutembelea Ofisi zote za serikali nchini. Hivyo public punishment ni ujumbe tosha kwa ofis nyingine za serikali kufanya kazi bila mzaha.
 
Wanabodi,

Kwanza naomba kukiri, kuwa ninaunga mkono kwa asilimia 100% juhudi za serikali awamu ya 5 kupambana na rushwa, ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi, ili mtindo unaotumiwa na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, sio!.

Baada ya kukisikia kisanga cha TRA kilichomngoa Kamishna Mkuu na maofisa kadhaa kufuatia sakata la makontena, leo amerudi tena bandarini, na nimekishuhudia kitu anachokifanya, japo anashangiliwa na umati wa watu, lakini anachokifanya ni kuviziana, kutishana, kudhalilishana na kunakwenda kinyume cha utawala bora, yaani good governance!.

Waziri Mkuu anafanya ziara za kushtukiza mahali, huki akiwa na karatasi lenye tuhuma specific, lakini amelificha!, anakwenda kumuuliza mhusika wa pale kuhusu utendaji wa mfumo fulani, anaelezwa kuwa mfumo uko perfect, kisha analiibua hilo kaatasi lenye tuhuma na kuanza kumsomea mhusika mbele ya kadamnasi ya watu, abcd!, mhusika anashindwa kujibu, atasimamishwa kazi, na kama yuko juu ya mamlaka yake, atamchongea kwa rais!.

Hata TRA siku hiyo alikwenda na nondo za makomtena, alipomuuliza Bade, akamjibu details ziko kwa maofisa wangu, ndipo akaibua nondo lake na kumsomea kwenye kadamnasi ili aonekane mjinga!, huku ni kuaibishana, kudhalilishana na kinyume cha good governance!.

Baada ya kutoka bandaini, akaenda TRL na kumuuliza mkurugenzi mkuu, mlikopa bilioni 3 TIB za kufanyia nini?!, kwa nini hamkufanya kile mlichokopea?, akaambiwa tumelipia mishahara, nani aliwapa idhini ya kukopa?!, Mkuugenzi hana jibu na naamini kesho atatangazwa hana kazi!.

Top management angekaa nao ofisini na kuulizana kistaarabu ndio good governance!. Mimi hata home, wife alikuwa na tabia ya kuwafokea ma tx home, mbele ya watoto, nikamkataza!, nikamsisitiza if things are not right, muite pembeni ndipo umseme, sio kumdhalilisha mbele ya watoto!.

Anachofanya Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa ni kuviziana, kudhalilishana na kuabishana bila sababu za msingi!, hili la kuitana na kuanza kuhojiana mbele ya waandishi ili watu wamuone alivyo mkali, ni tabia za ma populist leaders!, Leo nimemuona Magufuli akiongea na wafanyabiashara yuko very humble even cracking some jokes!.

Kama kuna watu wako karibu na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, wamwambie anavyofanya sio vizuri, Sio Sawa, Sio Haki, Sio Good Governance!, Ni Udhalilishaji na Kuaibishana tuu!. Akumbushwe kuna kitu kinatwa 'karma' kisije kumshukia!.
Au wewe unaonaje?!, toa maoni yako ni sawa au sio sawa!.
Pasco
pm..jpg
 
Pasco unaijua karma lakini hapa hukupaangalia kwanini?

Kama ulifanya makosa unaijua njia ambayo Mungu atakuhukumu? Kama ulidhulumu wananchi na kusingizia kuwa pesa za serikali hayo ndio majibu yake.

Hawa watu Wanastahili hayo yanayowakuta ni wakati wao wa kuona machungu umefika.
 
Back
Top Bottom