Wanabodi,
Kwanza naomba kukiri, kuwa ninaunga mkono kwa asilimia 100% juhudi za serikali awamu ya 5 kupambana na rushwa, ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi, ili mtindo unaotumiwa na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kassim Majaliwa, sio!.
Baada ya kukisikia kisanga cha TRA kilichomng'oa Kamishna Mkuu na maofisa kadhaa kufuatia sakata la makontena, leo amerudi tena bandarini na nimekishuhudia kitu anachokifanya, japo anashangiliwa na umati wa watu, lakini anachokifanya ni kuviziana, kutishana, kudhalilishana na kunakwenda kinyume cha utawala bora, yaani good governance!.
Waziri Mkuu anafanya ziara za kushtukiza mahali, huku akiwa na karatasi lenye tuhuma specific, lakini amelificha!, anakwenda kumuuliza mhusika wa pale kuhusu utendaji wa mfumo fulani, anaelezwa kuwa mfumo uko perfect, kisha analiibua hilo karatasi lenye tuhuma na kuanza kumsomea mhusika mbele ya kadamnasi ya watu, abcd!, mhusika anashindwa kujibu, atasimamishwa kazi, na kama yuko juu ya mamlaka yake, atamchongea kwa Rais!.
Hata TRA siku hiyo alikwenda na nondo za makontena, alipomuuliza Bade, akamjibu details ziko kwa maofisa wangu, ndipo akaibua nondo lake na kumsomea kwenye kadamnasi ili aonekane mjinga!, huku ni kuaibishana, kudhalilishana na kinyume cha good governance!.
Baada ya kutoka bandaini, akaenda TRL na kumuuliza mkurugenzi mkuu, mlikopa bilioni 3 TIB za kufanyia nini?!, kwa nini hamkufanya kile mlichokopea?, akaambiwa tumelipia mishahara, nani aliwapa idhini ya kukopa?!, Mkurugenzi hana jibu na naamini kesho atatangazwa hana kazi!.
Top management angekaa nao ofisini na kuulizana kistaarabu ndio good governance!. Mimi hata home, wife alikuwa na tabia ya kuwafokea ma tx home, mbele ya watoto, nikamkataza!, nikamsisitiza if things are not right, muite pembeni ndipo umseme, sio kumdhalilisha mbele ya watoto!.
Anachofanya Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa ni kuviziana, kudhalilishana na kuabishana bila sababu za msingi!, hili la kuitana na kuanza kuhojiana mbele ya waandishi ili watu wamuone alivyo mkali, ni tabia za ma populist leaders!, Leo nimemuona Magufuli akiongea na wafanyabiashara yuko very humble even cracking some jokes!.
Kama kuna watu wako karibu na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, wamwambie anavyofanya sio vizuri, Sio Sawa, Sio Haki, Sio Good Governance!, Ni Udhalilishaji na Kuaibishana tuu!. Akumbushwe kuna kitu kinatwa 'karma' kisije kumshukia!.
Au wewe unaonaje?!, toa maoni yako ni sawa au sio sawa!.
Pasco
My Take:
Tuna tatizo kubwa la uelewa humu, ila pia kufuatia wengi kuchoshwa na kukinaishwa na rushwa na ufisadi, wamekata tamaa na kuhamaniko na mihemuko ya kuchukuliwa hatua kali sana na ikibidi hata wanyongwe!.
Nimenote wengi humu hawakunielewa!, japo nimeanza kwa utangulizi wa kuunga mkono hatua zozote zinazochukuliwa na awamu ya 5 kupiga vita rushwa na ufisadi, siungi mkono the means kwa kutumia populistic approach ya kufanya ili watu waone unafanya!.
Tanzania ni nchi inayofuata mfumo wa haki wa Uingereza, wa presumed innocent until proven guilt beyond reasonable doubt by the court of competant juisdiction!, kinachofanyia ni media trial kumuonyesha mtu ni mkosaji mbele ya camera!.
Sio wengi humu wanaojua kuwa hata mhalifu anahaki!, hata mlaushwa, fisadi, mwizi, pia ana haki!. Hata muuaji aliyehukumiwa kifo kwa kunyongwa naye pia ana haki zake, ananyongwa kwa heshima yake, na kabla hajanyongwa, anaitwa daktari kumpima afya yake, akikutwa na maadhi yoyote, hanyongwi!, bali anatibiwa mpaka apone ndipo adhabu hiyo itekelezwe!.
Japo kisheria hairuhusiwi kamera za waandishi kuingizwa mahakamani, Tanzania tunaingiza kamera mahakamani!, polisi nao wanawaparade wahalifu kwa waandishi wa habari ili hali wako mikononi mwa polisi!, ni kama kuwahukumu kabla!. Kama Kova kila uchao, kwenye screen!, hilo baraza jipya likiishateuliwa, kama kila waziri nae atatembea na media team ili watu waone si itakuwa chaos?!.
Vita dhidi ya uzembe, rushwa, ufisadi, na ukwepaji kodi yes!, means no!, haki sio tuu itendeke bali pia ionekane kutendeka!.
Pasco