Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Kama Waziri Mkuu kakosea, ashitakiwe.

Tuambiwe kavunja sheria ipi, apelekwe mahakamani, walioonewa waje hapa kutoa data zao, kama hawana fedha za kuendesha kesi tutawasaidia.

Sio mtu analaumu "mtindo" bila kuongelea sheria.

Mimi nilivyo m blast rais Magufuli kuingilia tafrija ya bunge, niliongelea "checks and balances" za kutoka katika katiba.

Pasco anapom critique PM, atupe msingi wa kisheria.

Kama hana msingi wa kisheria, asimlaumu PM. Ampigie simu mbunge wake sheria ibadilishwe.

Kukosea siyo lazima mtu avunje sheria.

Unaweza ukafanya jambo ambalo si kosa kisheria lakini likawa si la busara.

And just because one can, doesn't mean they should.

Kuna sehemu niliona umezungumzia tact. Hilo neno halipo kwenye msamiati wa Magufuli wala Majaliwa.

Hebu ona siku waziri mkuu alivyoenda hapo bandarini mara ya kwanza.

Hapo kwenye 0.33 mark anamwamuru IGP amkamate Bw. Masamaki...."IGP kamata huyu, ashiriki kwenye uchunguzi huu".



Hivi kweli hiyo unaona kuwa ni sawa?

Au watu tushakata tamaa kabisa na kufikia sehemu hatujali tena mambo ya tact ili mradi tunaona kuna kitu kinafanyika, hata kama hakina matokeo yoyote ya maana?
 
Last edited by a moderator:
Kukosea siyo lazima mtu avunje sheria.

Unaweza ukafanya jambo ambalo si kosa kisheria lakini likawa si la busara.

And just because one can, doesn't mean they should.

Kuna sehemu niliona umezungumzia tact. Hilo neno halipo kwenye msamiati wa Magufuli wala Majaliwa.

Hebu ona siku waziri mkuu alivyoenda hapo bandarini mara ya kwanza.

Hapo kwenye 0.33 mark anamwamuru IGP amkamate Bw. Masamaki...."IGP kamata huyu, ashiriki kwenye uchunguzi huu".



Hivi kweli hiyo unaona kuwa ni sawa?

Au watu tushakata tamaa kabisa na kufikia sehemu hatujali tena mambo ya tact ili mradi tunaona kuna kitu kinafanyika, hata kama hakina matokeo yoyote ya maana?


Pointi yangu ni kwamba, kwa sababu hii habari ya what is appropriate, tactful etc ni subjective, ili ku simplify mambo, tu operate kwa legal framework.

Waziri Mkuu anaweza kukosea kwa kupenga makamasi na kujifutoa na shati lake. That will be horribly tacky. But that is no legal ground to fault him.

We would do well to establish our legak framework so that it addresses all matters of import.

Haya mambo ya decorum na tact kwa watu wanaofuatilia intrigues za politics katika Washington Post na wale wanaofuatikia kwa Shigongo priorities ni tofauti.

Wewe unaweza kuwa refined ukaona kukaripiana karipiana live ni ujinga. Wengine washapotezewa mizigo yao hapo bongo wanaona ndio tunahitaji kukaripiana zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Pointi yangu ni kwamba, kwa sababu hii habari ya what is appropriate, tactful etc ni subjective, ili ku simplify mambo, tu operate kwa legal framework.

Kama ni hivyo basi kwa bongo itakuwa ni vigumu sana kumpata kiongozi, hususan rais na waziri mkuu, aliyefanya kosa kisheria.

Hao watu wana madaraka ya makubwa mno hadi inastaajabisha.

Juzi juzi hapa DC Makonda naye kafanya hivyo hivyo. Kaamrisha polisi mbele ya kadamnasi kuwakamata wale jamaa wawili kwa kosa la kuchelewa.

Anyway, labda ni mambo ya kiutamaduni pia.

Hebu ona hapa jinsi Rahm Emanuel alivyomfukuza kazi Police Chief wa Chicago kufuatia kuachiliwa kwa ile video inayomwonyesha polisi akimmiminia risasi yule dogo.

Mtu anafukuzwa kazi bila dramatics.

 
Last edited by a moderator:
Kama ni hivyo basi kwa bongo itakuwa ni vigumu sana kumpata kiongozi, hususan rais na waziri mkuu, aliyefanya kosa kisheria.

Hao watu wana madaraka ya makubwa mno hadi inastaajabisha.

Juzi juzi hapa DC Makonda naye kafanya hivyo hivyo. Kaamrisha polisi mbele ya kadamnasi kuwakamata wale jamaa wawili kwa kosa la kuchelewa.

Anyway, labda ni mambo ya kiutamaduni pia.

Hebu ona hapa jinsi Rahm Emanuel alivyomfukuza kazi Police Chief wa Chicago kufuatia kuachiliwa kwa ile video inayomwonyesha polisi akimmiminia risasi yule dogo.

Mtu anafukuzwa kazi bila dramatics.



Tatizo ni kwamba hatuko legalistic enough. Halafu mfumo wa sheria umekaa top down.

Huyo Makonda ka abuse sheria. Sheria inayomruhusu kukamata watu imetoa na justification za kutumia sheria hiyo. Ambazo zipo clear kwamba sheria itumike kunapokuwa na haki kama ya kuvunjika amani. Yeye kaitumia katika sehemu anbayo watu wanechelewa kuja kwenye kikao.

Hao watendaji wangeweza kumshiraki in theory, na hiyo hiyo sheria inayompa nguvu kutua ndani watu, inatoa hukumu atakapo i abuse. Lakini mtu anayetakiwa kupitisha kesi hiyo ni mtu wa system vile vioe ambaye by default ata side na Makonda. Kwa hiyo ni habari ya kesi ya nyani (no pun intended) umpe sokwe.

Mimi napenda viru viwe defined kisheria zaidi ili tuondokane na subjectivity.

Obviously huu u Sokoine mpya ni mabobish ambayo kwa watu wanaoangalia vitu systemic hauko far above empty populism.
 
Last edited by a moderator:
Hawajanikuta "mvuta bangi" kama mimi,ukiwa kwangu unataka free styles na kukawa na jambo linamuhusu rais au waziri aliyepita,ntamchana mbele ya media.yaani kama makontena yalipita kwa memo ya rais au waziri ni kuanika yoote halafu tuone.
 
Wanabodi,

Kwanza naomba kukiri, kuwa ninaunga mkono kwa asilimia 100% juhudi za serikali awamu ya 5 kupambana na rushwa, ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi, ili mtindo unaotumiwa na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kassim Majaliwa, sio!.

Baada ya kukisikia kisanga cha TRA kilichomng'oa Kamishna Mkuu na maofisa kadhaa kufuatia sakata la makontena, leo amerudi tena bandarini na nimekishuhudia kitu anachokifanya, japo anashangiliwa na umati wa watu, lakini anachokifanya ni kuviziana, kutishana, kudhalilishana na kunakwenda kinyume cha utawala bora, yaani good governance!.

Waziri Mkuu anafanya ziara za kushtukiza mahali, huku akiwa na karatasi lenye tuhuma specific, lakini amelificha!, anakwenda kumuuliza mhusika wa pale kuhusu utendaji wa mfumo fulani, anaelezwa kuwa mfumo uko perfect, kisha analiibua hilo karatasi lenye tuhuma na kuanza kumsomea mhusika mbele ya kadamnasi ya watu, abcd!, mhusika anashindwa kujibu, atasimamishwa kazi, na kama yuko juu ya mamlaka yake, atamchongea kwa Rais!.

Hata TRA siku hiyo alikwenda na nondo za makontena, alipomuuliza Bade, akamjibu details ziko kwa maofisa wangu, ndipo akaibua nondo lake na kumsomea kwenye kadamnasi ili aonekane mjinga!, huku ni kuaibishana, kudhalilishana na kinyume cha good governance!.

Baada ya kutoka bandaini, akaenda TRL na kumuuliza mkurugenzi mkuu, mlikopa bilioni 3 TIB za kufanyia nini?!, kwa nini hamkufanya kile mlichokopea?, akaambiwa tumelipia mishahara, nani aliwapa idhini ya kukopa?!, Mkurugenzi hana jibu na naamini kesho atatangazwa hana kazi!.

Top management angekaa nao ofisini na kuulizana kistaarabu ndio good governance!. Mimi hata home, wife alikuwa na tabia ya kuwafokea ma tx home, mbele ya watoto, nikamkataza!, nikamsisitiza if things are not right, muite pembeni ndipo umseme, sio kumdhalilisha mbele ya watoto!.

Anachofanya Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa ni kuviziana, kudhalilishana na kuabishana bila sababu za msingi!, hili la kuitana na kuanza kuhojiana mbele ya waandishi ili watu wamuone alivyo mkali, ni tabia za ma populist leaders!, Leo nimemuona Magufuli akiongea na wafanyabiashara yuko very humble even cracking some jokes!.

Kama kuna watu wako karibu na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, wamwambie anavyofanya sio vizuri, Sio Sawa, Sio Haki, Sio Good Governance!, Ni Udhalilishaji na Kuaibishana tuu!. Akumbushwe kuna kitu kinatwa 'karma' kisije kumshukia!.
Au wewe unaonaje?!, toa maoni yako ni sawa au sio sawa!.

Pasco




My Take:
Tuna tatizo kubwa la uelewa humu, ila pia kufuatia wengi kuchoshwa na kukinaishwa na rushwa na ufisadi, wamekata tamaa na kuhamaniko na mihemuko ya kuchukuliwa hatua kali sana na ikibidi hata wanyongwe!.

Nimenote wengi humu hawakunielewa!, japo nimeanza kwa utangulizi wa kuunga mkono hatua zozote zinazochukuliwa na awamu ya 5 kupiga vita rushwa na ufisadi, siungi mkono the means kwa kutumia populistic approach ya kufanya ili watu waone unafanya!.

Tanzania ni nchi inayofuata mfumo wa haki wa Uingereza, wa presumed innocent until proven guilt beyond reasonable doubt by the court of competant juisdiction!, kinachofanyia ni media trial kumuonyesha mtu ni mkosaji mbele ya camera!.

Sio wengi humu wanaojua kuwa hata mhalifu anahaki!, hata mlaushwa, fisadi, mwizi, pia ana haki!. Hata muuaji aliyehukumiwa kifo kwa kunyongwa naye pia ana haki zake, ananyongwa kwa heshima yake, na kabla hajanyongwa, anaitwa daktari kumpima afya yake, akikutwa na maadhi yoyote, hanyongwi!, bali anatibiwa mpaka apone ndipo adhabu hiyo itekelezwe!.

Japo kisheria hairuhusiwi kamera za waandishi kuingizwa mahakamani, Tanzania tunaingiza kamera mahakamani!, polisi nao wanawaparade wahalifu
kwa waandishi wa habari ili hali wako mikononi mwa polisi!, ni kama kuwahukumu kabla!. Kama Kova kila uchao, kwenye screen!, hilo baraza jipya likiishateuliwa, kama kila waziri nae atatembea na media team ili watu waone si itakuwa chaos?!.

Nilichokiona jana anachokifanya PM pia kinakwenda against the principles of Natural Justice
Vita dhidi ya uzembe, rushwa, ufisadi, na ukwepaji kodi yes!, means no!, haki sio tuu itendeke bali pia ionekane kutendeka!.

Pasco
Update.

Mkuu Kiranga, sio kila kitu ni sheria, vingine ni taratibu tuu na kanuni!, ndio maana kwenye ofisi za kizamani kuna vyumba vnawatenganisha ma bosi na wafanyakazi wao!, kuna chumba kinamtenganisha waziri na secretary wake, kuna ofisi ya boss, lengo ya yote hayo ni kuweka heshima na privacy!, nimefanya kazi na wazungu fulani nchini Uswiss, wenzetu wako kwenye full open government initiative, no secrets zozote ofisini, partition zote ni za kioo transparent, computers zote ziko linked kwenye network, desktop zote ni shared, ukipint chochote kuna back copy iko saved, all public communications ni shared.

Huwezi kumrepremand boss infront of his subordinates let alone infront of the media, mtu anaulizwa swali, hajapewa muda wa kujibu, linafuata na lingine na lingine!. Mimi sijasema mafisadi na wala rushwa wasishughulikiwe kikamilifu, nimesisitiza tuu, kuwepo fairness, respect, ustaarabu na sio kutegeana, kuumbuana na kuaibishana!. Wote walioangalia jinsi boss wa TRL alivyokuwa anahojiwa, kiukweli yule bosi amedhaaulika anaonekana ni li bosi lijinga ajabu!, limeshindwa kujibu simple questions kutoka kwa PM, wamekopa kwa idhini ya nani?!, baada ya tukio lile, kweli bosi kama huyu ana any respect left kwa wafanyakazi wake wa chini!, nahisi hata akipita, wananchungulia madirishani na kujisemea kimoyo moyo, angalia lijinga lile linapita!, ni huku tuu Afrika tunafanyiana mambo kama yale ile ni bullying of some kind!.

Pasco

Honestly! Sioni hoja hapo mkuu zaidi ya malalamiko tuu na majuto ya mtu aliekumbwa na adhabu. Unataka PM aheshimu misingi ya haki, sheria na kanuni za utawala bora ambayo hao unaosema wameonewa waliamua kuivunja kwa makusudi kabisa?
Kama wao walikuwa wanajua kuwa kuna makontena yamepotea walikuwa wapi kulipoti hiyo issue mpaka PM aje awaumbue? Hata kama ulilazimishwa kutumia bilioni 200 kinyume cha utaratibu ulichukua hatua gani? Walifanya jitihada za makusudi kuvunja sheria na utawala bora ili kutuibia kodi zetu bila aibu, Leo unataka PM awafichie aibu yao..Sorry BUT this is insane.

Siku zote "Aliyesalimika Serikalini ni yule ALIYEANDIKA" Ukilazimishwa kufanya kitu ANDIKA kwa upole tu kutokulizika kwako na ueleze kwanini hujalizika na maamuzi na matokeo ya kutofata ushauri wako kisha ungana nao, likibumburuka unarecall kwamba ulionya juu ya hilo.

Tuwaache JPM na Majaliwa wafanye kazi, Sikuwapigia kura ila nafurahia kazi yao.
 
ukimchekea nyani katika shamba la mahindi utavuna mabua

Hahahaha! Naona ndicho anachotaka Pasco tuvune mabua kwa kuitana chemba kuulizana eti uliiba? Kisha tuundiane tume itakayotumia mabilioni hahahaha.
 
pasco roho inamuuma baada ya kula pesa za watu kufanya promo ili mamvi ashinde
 
Nawashangaa sana watu wanaosema jamaa Waziri mkuu anakiuka taratibu za utawala bora. Je hao waliotusabishia fedheha kwa miaka yote walizingatia utawala bora?
Katika sheria huwa tuna maxim inayosema kwamba "He who comes to equity must come with clean hands" Tafsiri isiyo rasmi ya maxim hiyo ni kwamba mtu unapokwenda kudai haki lazima uwe umetimiza wajibu wako ipasavyo.
Eti wanadai waziri anawadhalilisha watu kwa kuwakemea mbele ya hadhara na kamera?? Shiiiiiit, what kind of honour does this person deserve??!! A person who caused our hospitals to have no facilities for years, our schools to have no desks and text books, our girls and boys from poor families to miss education for lack of loans, our citizen to face disgrace abroad, leo unataka uniambie we have to treat this culprit with respect. Which respect?? The only respect is to let them die in jail mercilessly and their families starve as our poor family did....
 
Mkuuu Pasco hebu soma hilo gazeti la Sweden

Ndugu zangu,
Dagens Nyheter ni gazeti kubwa kushinda yote nchini Sweden, ndio 'Daily News' lao kwa maana ya jina la gazeti.
Katika toleo lake la jana Desemba 4, habari za John Magufuli zimepamba pia gazeti hilo. Amemwagiwa sifa, na ikaandikwa pia, kuwa Magufuli amewaweka katika wakati mgumu marais wenzake wa nchi jirani kwa vile wapiga kura wao wameonyesha wivu wao kwa Watanzania kupata Rais wa aina ya Magufuli.
Hata hivyo, kwenye gazeti hilo, imeandikwa pia, kuwa hata kabla ya kuingia milango ya Ikulu, Magufuli tayari ameshajipatia maadui wakiwamo wa ndani ya chama chake kwa hatua zake anazozichukua, hususan za kubana matumizi ya Serikali.
Hapa chini ni kipande cha habari za gazeti hilo na link ya habari nzima kwa lugha ya Kisweden. ( Picha iliyotumika gazetini humo ni ya Mpiga picha Halfan Said, ana malipo yake mazuri tu, akiyadai!)
"DAR ES SALAAM. Den nyvalde presidenten John Magufuli hann knappt flytta in i Tanzanias presidentpalats innan han fick sina f'rsta fiender" medlemmarna i det egna partiet CCM"
link Nyheter - DN.SE
Maggid Mjengwa
0754 678 252
==========
TAFSIRI YA GAZETI HILO KWENYE LUGHA YA KIINGEREZA

Nimekopi na kupaste kutoka kwenye uzi humuhumu Jamii Forum
 
Yaani anachokifanya ni zaidi ya sahihi. Kujifichaficha na kuongea pembeni ndio kufuga mianya ya rushwa. Mambo yaanikwe tu, kama utawajibishwa kwa makosa hukumu itabatilishwa na, ikilazimu, utalipwa fidia!
(WATU MLIOKUWA MNATAKA MAAMUZI MAGUMU NDIO WA KWANZA KULALAMIKA, MLITAKA YAMHUSU NANI?)
JAMANI TUJIANDAE TU, MAANA HATUJUI KAMA NI LEO AU KESHO!

 
Mkuu pasco siyo good governance sawa,lakini na hawa watendaji ni kama hawajielewi hivi,yaani libaba lizima linaulizwa maswali linaanza kutetemeka ,,lol

Jamani musiwacheke wenzenu hayajawafika. Unajua kushtukizwa namna hiyo kwa aina fulani hivi ya kukomoana (samahani lugha yangu) siyo vizuri hata kidogo, kwani unaweza kuua mtu hapo.

Nakubaliana na Pasco kwa hili, siyo good governance.
 
Kwa kuwa nchi ilioza na kwa kuwa hawezi kwenda kwenye kila ofisi ya umma anatisha ili maofisa wengine waogope na wawe kwenye mstari hata kama hata enda. Akija kwa kushtukiza ofisini kwangu nitaendelea na ratiba yangu ya kazi
 
Viongozi wetu wamezidi kuwa waongo. Hivi Majaliwa angemfanyaje MTU kama yule anaulizwa maswali mbele ya kamera na kumdanganya waziri Mkuu. DAWA YA MOTO NI MOTO. AMEMDANGANYA HADHARANI NAYE AMEPEWA MAJIBU HADHARANI
 
ndo dawa yao;asieweza kazi asepe.kila zama na kitabu chake na spidi yake.wamdate aliekuwa anawalea uozo wao:
 
Pasco sijaweza malizia hata kusoma. Ni hivi ndugu kitaa watu tunahamu na damu. Kuna msemo wasema the end justifies the means....nikuulize wajua watu wangapi waki 6ft under sbb yakukosa dawa? Wangapi wanamaisha magumu sababu ya kukosa fursa? Demokrasia and stupid good governance pull out cards wont help this country....mie nasema bado Mhe. Majaaliwa na Mhe. Rais wako wapole ...waongeze kasi...kitaa tunataka damu za waliotuibia by any means possible.
 
If anything yule Mkurugenzi wa TRL anatakiwa kufukuzwa kazi kabisa kwa kile tulichokiona na sidhani kama waziri mkuu alikurupuka lazima kuna tips za ndani alipata kila mwaka ikija ripoti ya CAG tunasoma mambo ya ubadhirifu, misstament and all sort of unaccounted usage of public monies.

Nani ndani ya shirika mwenye kibali cha kuidhinisha kuomba mkopo surely sio kila mtu anaweza omba mkopo TRL sasa kama umeomba mkopo kwa sababu A halafu umetumika kwa sababu B huo ndio mwanzo wa ubadhirifu wenyewe unaulizwaa legit query halafu auna majibu (sio kwamba hajui anaelewa kama ni makosa kutumia hela tofauti na alivyopewa ndio sababu za ubabaishaji wake) yaani humo ndani wakija auditors ni kasheshe na uzembe unapoanzia kila mtu ameona.

Bado kuwepo katika nafasi yake huyu mtu kunawezekana Tanzania tu nchi zingine vyombo vya habari vingerudi nyuma kuidhinisha ni uzembe gani mwingine chanzo chake ni mkurugenzi kama swala jepesi anashindwa kulitolea ufafanuzi waandishi wa habari wangeta kuakikisha huyu mtu anafutwa ajira kabisa sio wanamtetea kama mwafudenge anavyofanya that was unacceptable kama sehemu ya internal financial control ya shirika na ndio mwanzo wa fraud zenyewe tunazopigia kelele kila ripoti ya CAG inapokuja.
 
Back
Top Bottom