Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Kama upo clear na utendaji wako wa kazi hofu ya nn? Hata waziri akiwa ana lala hapo bandalini haina shida.. ila kama una fanya madudu lazma upate jamba jamba
 
Huo muda wa kwenda kupekua uliposema sina.. Ila walioona wanakushangaa hapa unavyokataa.

Kama vipi nirudishe Ignore List tu ntakuboa..

Tena wahi fasta uje uweke hapa.

Ila usije tu na kituko kama cha wakati ule cha uthibitisho wako kuwa mimi naitwa Richard Mugizi.

Haya, wahi ukalete. Tena kimbia.
 
Pasco ,

Huyo Majaliwa anatumwa tu. Mwenyewe Magufuli.

Na kama hamjaweza kumsema Magufuli alipolipangia bunge jinsi ya kufanya tafrija, kitu ambacho hana mamlaka nacho kikatiba ( checks and balances haziruhusu, I haven't seen an article on this), huyo Waziri Mkuu kuvamia mashirika ya umma, kitu ambacho ana mamlaka nacho, hamtaweza hata pa kuanzia.



Unashangaa hilo la pesa za tafrija?
hujashangaa aliposema watu wote wafanye usafi tarehe 9 december?
na matamko ya watu wa chini yake yameshatoka kuwa ni 'lazima' kushiriki
vinginevyo hatua kali zitachukuliwa....
 
Weka hapa niliposema nina apartments Masaki na Msasani.

Sasa na hiyo namba ya simu ndo unataka kusema kuwa ni yangu?

Hahahaaa hebu ipige basi tuone....

Na maisha yangu wala huyajui kabisa.

Usitake kujifanya unayajua. Huyajui, mimi hunijui [wait...yeah naitwa Richard Muguzi:biggrin1:], na hujui chochote juu yangu zaidi ya kunisoma tu humu.

Na kwanza wala siishi Atlanta mimi. Uthibitisho mwingine kuwa hujui kitu.


Endelea kula Junk Foods huko wahed wewe...

teh teh teh teh teh hiyo dozi ya leo inakutosha..
 
Inaonekana wewe una upeo mdogo sana
hadi comments zako zingine nashindwa ku reply

Kama wewe mwananchi unapenda kinachoendelea basi ujue wapo wananchi wengine hatupendi pia kinachoendelea
hatupendi kusikia waziri mkuu kagundua makontena yamepotea kila siku
tungependa hilo tatizo liwe fixed for good....wezi wakamatwe wafungwe..system ibadilishwe
biashara ziendelee na tuzungumze mengine yenye umuhimu..

sio kila mtu ana enjoy kutazama tv na kukuta the never ending story ya makontena.....
wengine tungependa story tofauti huko bandarini ...success stories.....

sisi wengine hatumpongezi mtu kwa ku expose tatizo
tunapongeza watu kwa kuli fix tatizo for good....sio kila wiki habari ndo hiyo hiyo...

Mkuu nchi ina matatizo meng huwez kufix siku moja leo kawaambia wafunge mfumo kulipia ki electronics.kikubwa alichofuata bandari kukagua ule mfumo wa kupitishia mizigo na kuona inakuwaje kunatokea ubadhirifu?kingne ni kumuuliza meneja mbona kwenye ripot ya CAG waliochukuliwa hatua ni vidagaa 10 tu,mbona mapapa yameachwa?ubaya uko wap hapo?PM kukagua ofisi ya umma?
 
Hawa sio viongozi nadhani hawajui wanataka kuifanyia nchi hii yaani majaliwa anauliza makontena 2431 ya January to December 2014 kwenye serikali waliyokuwemo kwa kweli nimeamini hawana plan yakutuvusha haya mambo yakupachikwa kwenye uongozi tabu tupu

Mkuu Si Ungelala Tu Sasa Umekuja Kupost Nini Hiki Mnazalilisha ID Zenu tu
 
Ukweli utawaweka Uhuru .Wawe wanasema ukweli ili waliokuwa wanafanya wizi wakati wa serikali dhaifu wapewe stahili zao
 
Endelea kula Junk Foods huko wahed wewe...

teh teh teh teh teh hiyo dozi ya leo inakutosha..

Huna ujualo.

Umebaki kujitekenya na kucheka tu.

Unaweka namba za simu za ajabu ajabu tu ili uonekane unanijua.

Hahahaaa una hamu kweli ya kutaka kunijua wewe eeh?
 
watu kuonyeshwa udhaifu wao sio good governance ila "kupotea" kwa makontena 2341 ndio good governance? you can't be serious Pasco.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nchi ina matatizo meng huwez kufix siku moja leo kawaambia wafunge mfumo kulipia ki electronics.kikubwa alichofuata bandari kukagua ule mfumo wa kupitishia mizigo na kuona inakuwaje kunatokea ubadhirifu?kingne ni kumuuliza meneja mbona kwenye ripot ya CAG waliochukuliwa hatua ni vidagaa 10 tu,mbona mapapa yameachwa?ubaya uko wap hapo?PM kukagua ofisi ya umma?

Inawezekana tunabishana sana hadi tunashindwa kujua nini tunabishania
watu hatupingi nia nzuri ya Waziri mkuu au Rais
ishu hapa sio nia nzuri ,ishu hapa ni njia nzuri ya ku fix tatizo
kuna ulazima wa waziri mkuu kwenda bandarini ghafla mara mbili in a week?
hawezi toa maagizo yakatekelezwa?
kama hilo haliwezekani basi tatizo lipo kubwa somewhere...
 
Zamani hizo vijijini ambako kipindi cha utandawazi na mitandao hakuna, watu waliokwenda kinyume na taratibu walizojiwekea kwenye vijiji vyao walipongundulika wamekengeuka walitungiwa nyimbo za kuwasema na kuwasuta. Hivyo kila mmoja alijua ni nani anazomewa.

Hivi kweli tunataka kuaminishwa kwamba hii ni mara ya kwanza duniani eti viongozi wa Tanzania tu ndio wanavunja taratibu!!!!

Nafikiri tunahitaji kujikumbusha tu kwamba cheo ni dhamana.
 
Inawezekana tunabishana sana hadi tunashindwa kujua nini tunabishania
watu hatupingi nia nzuri ya Waziri mkuu au Rais
ishu hapa sio nia nzuri ,ishu hapa ni njia nzuri ya ku fix tatizo
kuna ulazima wa waziri mkuu kwenda bandarini ghafla mara mbili in a week?
hawezi toa maagizo yakatekelezwa?
kama hilo haliwezekani basi tatizo lipo kubwa somewhere...

You would think angeweza tu kuwaita wahusika ofisini kwake na kujieleza kuliko kwenda bandarini na makamera lukuki.

Kwenda yeye mwenyewe huko bandarini na kuanza kuhoji watumishi wa hapo kunaweza kukatafsiriwa vibaya kuwa wanatafuta sifa tu.
 
Wanabodi,

Kwanza naomba kukiri, kuwa ninaunga mkono kwa asilimia 100% juhudi za serikali awamu ya 5 kupambana na rushwa, ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi, ili mtindo unaotumiwa na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, sio!.

Baada ya kukisikia kisanga cha TRA kilichomngoa Kamishna Mkuu na maofisa kadhaa kufuatia sakata la makontena, leo amerudi tena bandarini, na nimekishuhudia kitu anachokifanya, japo anashangiliwa na umati wa watu, lakini anachokifanya ni kuviziana, kutishana, kudhalilishana na kunakwenda kinyume cha utawala bora, yaani good governance!.

Waziri Mkuu anafanya ziara za kushtukiza mahali, huki akiwa na karatasi lenye tuhuma specific, lakini amelificha!, anakwenda kumuuliza mhusika wa pale kuhusu utendaji wa mfumo fulani, anaelezwa kuwa mfumo uko perfect, kisha analiibua hilo kaatasi lenye tuhuma na kuanza kumsomea mhusika mbele ya kadamnasi ya watu, abcd!, mhusika anashindwa kujibu, atasimamishwa kazi, na kama yuko juu ya mamlaka yake, atamchongea kwa rais!.

Hata TRA siku hiyo alikwenda na nondo za makomtena, alipomuuliza Bade, akamjibu details ziko kwa maofisa wangu, ndipo akaibua nondo lake na kumsomea kwenye kadamnasi ili aonekane mjinga!, huku ni kuaibishana, kudhalilishana na kinyume cha good governance!.

Baada ya kutoka bandaini, akaenda TRL na kumuuliza mkurugenzi mkuu, mlikopa bilioni 3 TIB za kufanyia nini?!, kwa nini hamkufanya kile mlichokopea?, akaambiwa tumelipia mishahara, nani aliwapa idhini ya kukopa?!, Mkuugenzi hana jibu na naamini kesho atatangazwa hana kazi!.

Top management angekaa nao ofisini na kuulizana kistaarabu ndio good governance!. Mimi hata home, wife alikuwa na tabia ya kuwafokea ma tx home, mbele ya watoto, nikamkataza!, nikamsisitiza if things are not right, muite pembeni ndipo umseme, sio kumdhalilisha mbele ya watoto!.

Anachofanya Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa ni kuviziana, kudhalilishana na kuabishana bila sababu za msingi!, hili la kuitana na kuanza kuhojiana mbele ya waandishi ili watu wamuone alivyo mkali, ni tabia za ma populist leaders!, Leo nimemuona Magufuli akiongea na wafanyabiashara yuko very humble even cracking some jokes!.

Kama kuna watu wako karibu na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, wamwambie anavyofanya sio vizuri, Sio Sawa, Sio Haki, Sio Good Governance!, Ni Udhalilishaji na Kuaibishana tuu!. Akumbushwe kuna kitu kinatwa 'karma' kisije kumshukia!.
Au wewe unaonaje?!, toa maoni yako ni sawa au sio sawa!.
Pasco

Naandika kwa ujasiri kuunga mkono ukurupushaji wa waziri mkuu! Hawa watendaji wa mashirika hawna huruma na nchi yao ndo maana wanaiba hata zaidi ya wazungu.


Tena wangekamtwa palepale na kupelekwa keko kwa miezi minne kwanza.

Pasco katika hili sikuungi mkono hawa jamaa ni makatili kwa uchumi wetu.

Wangenyongwa hata nina hasira na mfumo huu tena kwenye hili usianze kuzungumzia hizo good governance coz this is management
 
Huna ujualo.

Umebaki kujitekenya na kucheka tu.

Unaweka namba za simu za ajabu ajabu tu ili uonekane unanijua.

Hahahaaa una hamu kweli ya kutaka kunijua wewe eeh?


Sasa si ushasema mimi mzushi, sikujui, muongo, namba si yako etc.. Aya nimekubali..

Sasa nirudishe Ignore list, ila I already ring out your bell :hurt:
 
Bwaha ha ha ha haaa, Pasco bhana, kama vile umekasirika kweli!
 
Mh, pasco, ni wewe kweli wasema hayo! Hayo yanayoandikwa humu JF na kushangiliwa! Hayo yanayowekwa kwenye magazeti ya udaku! VIOJA vinavyofanywa na viongozi! Ufisadi uliokubuhu! Udanganyifu na uzembe uliotukuka. Enough is enough.

CHEO NI DHAMANA

TAFAKARI CHUKUA HATUA

Yesssss enough is enough. Waliaibika wametaka wenyewe .tuliwapa nchi wakajaza matumbo yao .leo mnaona wanadhalilishwa ???
Hebu angalia hutba ya JK aliposema magufuli kaenda kwenye wizara na anacheka kwa kukejeli .walifikiria wamepata watakaye muendeshaaaa lakini kiumbe mzitooooo. Na uzuri wake hajali ukawa wala ccm anajali ichapaji kazi. Wote watanzania
 
Hayo Mapigo Uliyotoa Ni Kama Ya Ninja Assasin, Picha Limekwisha

Mkuu si unamwona anavyoweweseka hapo.. Alafu mi namwacha tu aendelee kulia lia..

Unaweza kuuficha ukweli kwa kipindi fulani, lakini hutaweza kuuficha ukweli kipindi chote..
 
You would think angeweza tu kuwaita wahusika ofisini kwake na kujieleza kuliko kwenda bandarini na makamera lukuki.

Kwenda yeye mwenyewe huko bandarini na kuanza kuhoji watumishi wa hapo kunaweza kukatafsiriwa vibaya kuwa wanatafuta sifa tu.

Ndo maana wengine tunaona hizi ni bongo movies tu
manake mtu kama unajua ABC hadi Z ya ku fix tatizo huhitaji media...
watu watajikuta tu bandari inafanya kazi vizuri....
kuna nchi unakuta airport inafanya kazi vizuri,bandari pia,barabara zinsafishwa
na hujawahi kuona hata siku moja kuna waziri 'kaja kutingisha'....
 
Back
Top Bottom