Anahitajika msichana/mwanamke kwa ajili ya IVF

Anahitajika msichana/mwanamke kwa ajili ya IVF

Kinadada mnalalama hapa kua hela ndogo, sijui hamuwezi uza mtoto na blah blah kibao wakati mnatoa mimba, mnatupa watoto kwenye matundu ya vyoo, majalalani nk.

Si bora mchukue mpunga huo, lakini na jamaa nae moja ya sharti liwe ni kuhakikisha mtoto anaishi maisha mazuri. Kibongo bongo hii haipo sana hivyo ni kheri kumuondoa hofu mama mtoto.
 
Kwanza huu ni unyanyasaji.
Ujitolee kubeba mimba na usiruhusiwe kuwaona wanao baada ya kuwqkqbidhi.
Pili uhame kwako uje kukaa na mtu usiyempenda na sio mpenzi wako kivyovyote aqqh
Me nliandika tu kwa utani mbona
Kumzalia mtu kwaashart parefuu
 
Kinadada mnalalama hapa kua hela ndogo, sijui hamuwezi uza mtoto na blah blah kibao wakati mnatoa mimba, mnatupa watoto kwenye matundu ya vyoo, majalalani nk.

Si bora mchukue mpunga huo, lakini na jamaa nae moja ya sharti liwe ni kuhakikisha mtoto anaishi maisha mazuri. Kibongo bongo hii haipo sana hivyo ni kheri kumuondoa hofu mama mtoto.
Wewe mfano mie ni dume tu nitampatia Ila kama akifika 100 ml .
Na anunue gari Mercedes Benz hata toleo lakati mie nitamfikiria Nakadori unasemaje ??
 
Kinadada mnalalama hapa kua hela ndogo, sijui hamuwezi uza mtoto na blah blah kibao wakati mnatoa mimba, mnatupa watoto kwenye matundu ya vyoo, majalalani nk.

Si bora mchukue mpunga huo, lakini na jamaa nae moja ya sharti liwe ni kuhakikisha mtoto anaishi maisha mazuri. Kibongo bongo hii haipo sana hivyo ni kheri kumuondoa hofu mama mtoto.
Unadhani ni rahisi kubeba mimba miezi 9 kisha usijihusishe na mtoto?
 
Kinadada mnalalama hapa kua hela ndogo, sijui hamuwezi uza mtoto na blah blah kibao wakati mnatoa mimba, mnatupa watoto kwenye matundu ya vyoo, majalalani nk.

Si bora mchukue mpunga huo, lakini na jamaa nae moja ya sharti liwe ni kuhakikisha mtoto anaishi maisha mazuri. Kibongo bongo hii haipo sana hivyo ni kheri kumuondoa hofu mama mtoto.
Asante kwa maoni ndugu,
Nimeshatolea ufafanuzi jambo la malezi kwa mtoto/watoto kwenye baadhi ya comment kwamba mtoto/watoto watakua damu yangu hivyo malezi bora lazima yazingatiwe
 
Sio kama jela, ila kwa usalama wake.
Pia atakua kwa uangalizi ili asijihusishe tendo la ndoa na mtu mwingine kwa kipindi hicho sababu, kidogo itamsumbua kisaikolojia sababu hatoruhusiwa kujihusisha na tendo la ndoa na mwanaume kwa kipindi chote cha ujauzito na baada ya kujifungua
May I ask why, kwanini? Whats the logic behind this?
 
Wewe mfano mie ni dume tu nitampatia Ila kama akifika 100 ml .
Na anunue gari Mercedes Benz hata toleo lakati mie nitamfikiria Nakadori unasemaje ??
Kwakuwa ni swala linalohusisha uhai wa mtu na kuhusisha kiumbe chenye muunganiko kihisia na kidamu alitakiwa azingatie hilo na awake hela kubwa ili angalau iwe rahisi kwa wanaoweza kurisk.
Lakini pia atoe room ya second part ku bargain.
Ila mafuta akuwekee kwa miaka 5 na ajira ya kudumu akupatie mbali na hizo hela.
Access ya mtoto nayo upewe angalau ujue proceedings za mwanao...
 
IVF kirefu chake ni In Vitro Fertilization.
IVF ni jambo la kurutubisha kwa kuunganisha mbegu za uzazi za mwanamme na yai la uzazi la mwanamke maabara, baada ya hapo zoezi linalofatia ni kupandikiza ujauzito kwa mwanamke kwa njia ya sindano kisha ujauzito utaendelea kukua kama kawaida kwa mda wa miezi tisa kisha mwanamke atajifungua kawaida.

IVF haihusishi kukutana kimwili kati ya mwanamke na mwanaume bali mwanaume anatoa mbegu kwa kujichua au punyeto na mwanamke anatolewa yai lililopevuka maabara na wataalamu baada ya hapo ndio ujauzito unapandikizwa kwa mwanamke,
Ni njia safi na salama na haihusishi operation kubwa na haina hatari yeyote kwa mwanamke.

Sasa anahitajika mwanamke au msichana katika zoezi hilo,

MALIPO
Moja malipo ni milioni 25 ambayo yatasainiwa kisheria mahakamani na ustawi wa jamii.
Pili kila mwezi atalipwa milioni moja kama malipo ya motisha kwa mda wa miezi tisa ya ujauzito, malipo hayo ni nje ya ile milioni 25.
Tatu kila siku atalipwa elfu ishirini kama gharama ya chakula kulea mimba kwa mda wa miezi tisa ya ujauzito.
Nne atalipwa shilingi elfu hamsini kila siku kama gharama ya chakula baada ya kujifungua kwa mda wa mwaka mmoja kipindi ananyonyesha.
Tano gharama zote za hospital kwa mama kipindi cha ujauzito, mama na mtoto baada ya kujifungua zitagharamiwa na baba wa mtoto/watoto

MASHARTI
Moja ujauzito utalelewa sehemu aliyopo baba wa watoto.
Mbili hauruhusiwi kisheria kutangaza kwa mtu yeyote kama una ujauzito labda wazazi wako tu, na wazazi wakiambiwa nao wataelimisha kuhusu hili sharti.
Tatu baada ya kujifungua, mtoto/watoto wakifikisha mwaka mmoja utawakabidhi kwa baba yao.
Nne baada ya kukabidhi mtoto/watoto hautoruhusiwa kisheria na kibinadam wewe ndugu zako au rafiki zako kuwaona mtoto/watoto kwa namna yeyote kipindi chote cha maisha yenu hapa duniani.
Tano hautoruhusiwa kuwa na mahusiano ya aina yoyote na baba wa watoto kabla na baada ya kujifungua mtoto/watoto.
Sita awe tayari kulea ujauzito akiwa jijini dar es salaam.

SIFA ZA MWANAMKE/MSICHANA ANAEHITAJIKA.
Moja awe na afya nzuri, asiwe na magonjwa ya akili, pili asiwe na magonjwa ya zinaa ikiwemo ukimwi.
Pili awe mtanzania kutoka kabila na dini yeyote.
Tatu awe mrefu, mrefu sana atapewa upendeleo.
Nne awe mwembamba, akiwa mnene isiwe unene mkubwa sana.
Tano awe na umri wa kati ya miaka 25 hadi 35.
Sita awe mweupe au maji ya kunde asiwe mweusi sana.

Asanteni.
Pia kwa mwana Jamii Forum mwenye ndugu, rafiki au jirani mwenye hizo sifa naomba mnisaidie kusambaza hili tangazo.
Asante tena.

Vigezo na masharti kuzingatiwa
Unatafuta surrogate mother for you child.
 
May I ask why, kwanini? Whats the logic behind this?
Logic ni kupata mtoto/watoto bila mama na baba kukutana kimwili, pili mama kutojihusisha na mtoto/watoto kwa namna yeyote maisha yake yote hapa duniani ikiwemo kutowaona mtoto/watoto na baba yao kisheria baada ya mwaka tangu huyo mama kujifungua
 
Logic ni kupata mtoto/watoto bila mama na baba kukutana kimwili, pili mama kutojihusisha na mtoto/watoto kwa namna yeyote maisha yake yote hapa duniani ikiwemo kutowaona mtoto/watoto na baba yao kisheria baada ya mwaka tangu huyo mama kujifungua
Nlikuwa nauliza kwanini asiruhusiwe kufanya sex pindi ana mimba au akishajifungua.?
 
So utalea mwenyewe bila mama?
Unique Flower
Ndio ndugu, na inawezekana vizuri sana pia kumbuka itakua damu yangu.
Kuna watoto wapo vituo vya watoto yatima wapo chini ya mwaka mmoja na wanalelewa hadi kua watu wazima.
Hivyo kwa watoto wangu inawezekana nikawalea kwa mazingira bora zaidi na kumbuka nitaanza kuwalea baada ya kunyonya kwa mwaka mmoja toka kwa mwanamke atakaewazaa
 
Back
Top Bottom