Anakorogea uji wa vitumbua na mkono wa mtoto aliyekufa

Anakorogea uji wa vitumbua na mkono wa mtoto aliyekufa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema wazee.

Yule Mama alikuwa muuza vitumbua, alikuwa maarufu Kwa vitumbua vyake kwani vilikuwa vitamu sana. Kwa siku alikuwa anauza ndoo Mbili.

Zikaja Stori kuwa Yule Bi.mkubwa ni mlozi, kikagula, jichawi lililoshindikana.

Bado nakumbuka, wakaitwa Wale watoa Uchawi, Kwa mliokuwepo enzi hizo kulikuwa na vikundi vya watu vilivyojipatia umaarufu Kwa kutoa Watu Uchawi legend wao akiwa Mzee MajiMarefu, kuna wale manyaunyau. Basi Watu wa namna hiyo wakaitwa ati wa mtoa Uchawi Yule Mama. Lile kundi maarufu Kutoka Shambalai liliwatoa Watu Uchawi makumi Kwa manma katika mji wetu.

" Wachawi wanawanga wanga ..wachawi(wanawanga wanga) × 3
Siondoki nangojea pembe siondokixl"
Ilikuwa moja ya nyimbo za kuongoza ibada ya kutoa Uchawi Watu.

Na wengi walitolewa uchawi. Lakini Taikon Baada ya kukua miaka mingi ikiwa imepita, najiuliza je ni kweli Yale matukio yanaukweli wowote?

Baada ya kukua nimegundua ule ulikuwa ni ushenzi mkubwa, na ulikuwa ni Uongo na uzushi unyanyasaji.

Ile hadithi ya kusema Yule Mama wa vitumbua alikuwa anakorogea uji wa vitumbua kwa Kutumia mkono wa mtoto Mdogo aliyekwisha Kufa ulikuwa ni Uongo Mkubwa.

Wivu na husda Kwa mahasimu wake wa kibiashara ndio waliomuundia njama ya kulichafua jina lake na kuiangusha biashara yake.

Hata wale Watu wa manyaunyau watoa Uchawi nao kumbe ilikuwa ni njama na mbinu za Watu wenye Chuki ambao walifanya hila kuwachafua baadhi ya Watu huku wakitumia mazingaombwe ya kitoto ya hila

Hayo mambo ili yakuingie akilini itakupasa uwe mjinga WA kiwango cha mwisho Kabisa au uwe mtoto Mdogo asiyeelewa mambo.

Nimekumbuka Zama za kale.

Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Ujinga kama huu nchi zenye viongozi wanaojitambua wasingekubali ufanyike.

Fikiria umeikuza biashara kwa jasho na damu anakuja punguani mmoja kavaa kaniki yake na mkononi kashika usinga anakuchafua kwa kuwaambia watu huyu anauza sana kwa sababu anakorogea uji kwa mkono wa mtoto.

Ukitoka hapo ushapoteza wateja ushapoteza heshima na huyo mjinga aliyefanya hivyo anatamba tu mtaani.
 
Tulosoma Mkwawa miaka ya 2003 kuna mama alikuwa maarufu kwa Supu na nyama za bei chee
Mia tatu unashiba siku nzima ee bwana wakajaga kina Maji marefu wakatoa Uchawi wanasema eti alikuwa anauza nyama za mizogaa na muda Anaanda huwa anakuwa Uchi,,ilivuma sana

Walikuwa wahuni tuu!
Waliharibu majina ya Watu na biashara zao. Kwa hadithi za kijinga zisizo na uhalisia.
Na Kwa vile jamii ya kijinga waliamini.

Sasa hivi wangeshtakiwa ili wakathibitishie hayo mambo Mahakamani
 
Ujinga kama huu nchi zenye viongozi wanaojitambua wasingekubali ufanyike...

Unauza Karanga alafu kuna mjinga mmoja kijiweni anasema unauza mavi ya mbuzi alafu wakibisha anatafutwa mganga, wengi wa waganga ni wahuni, matapeli na wakupangwa, anakuja anathibitisha kweli zile Karanga ni mavi ya mbuzi. Kwa kufanya Michezo Yao ya kiini macho
 
Unauza Karanga alafu kuna mjinga mmoja kijiweni anasema unauza mavi ya mbuzi alafu wakibisha anatafutwa mganga, wengi WA waganga ni wahuni, matapeli na wakupangwa, anakuja anathibitisha kweli zile Karanga ni mavi ya mbuzi. Kwa kufanya Michezo Yao ya kiini macho
Ujinga kama huu serikali ilikuwa inauruhusu tu.

Waganga wanapita nyumba kwa nyumba watu nyomi wanawafata nyuma eti unakuja kutolewa vitu.

Ukiwa hauna pesa za kuwapa waganga watu wanakuchangia(ili uaibike)

Binafsi nilikuwa nashangaa sana kivipi serikali inaruhusu watu kudhalilishana na kushushiana utu.
 
Kama ukila hivyo vyakula na hupati madhara basi ni salama.

Wakati naishi Mabibo hostel kuna mgahawa nilikuwa naenda kupata chakula, baadaye nikaja kusikia eti wanatumia maji ya hedhi kupikia chakula Chao kitamu.

Lakini sikujali wala nini, maana sikuwahi kupata shida yeyote ya tumbo wala nini? 😆

Mara nyingi huwa ni Fitina za washidani wa Kibiashara
 
Kama ukila hivyo vyakula na hupati madhara basi ni salama.

Wakati naishi Mabibo hostel kuna mgahawa nilikuwa naenda kupata chakula, baadaye nikaja kusikia eti wanatumia maji ya hedhi kupikia chakula Chao kitamu.

Lakini sikujali wala nini, maana sikuwahi kupata shida yeyote ya tumbo wala nini? 😆

Mara nyingi huwa ni Fitina za washidani wa Kibiashara

Ni kweli Kabisa. Fitna, husda, kijicho, Wivu.
Wakishindwa zaidi watasema freemason
 
Siamini mambo ya uchawi kabisa, ila Kuna mama alikua anapika chakula Hana mfanyakazi, aisee unakuta mibaba imepanga foleni inagombania chakula, afu sahani zikiisha unaosha mwenyewe unapanga foleni na hela kulipa ni cash, Kuna jamaa zangu wameosha sana sahani pale na ni watu na heshima zao, aisee hii kitu haijawahi kunitoka kichwani
 
Back
Top Bottom