Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Ni mapema mno bado anarekebisha kuweka mambo sawa tuwe na subira
 
Huyu rais wetu amekuwa akijinasibu kuwa nchi hii ni tajiri na imechezewa kwa mda mrefu mbona anaharibu hata yale mazuri aliotuachia baba Riz wanafunzi wa Elimu ya juu watapata shida, Watumishi wa Umma vile vile waendesha dala dala kwa Dar, boda boda, hospitalini dawa shida
*Kubwa zaidi ni hili la kagera alishindwa kufika kule watu hawakutoa pesa zao ili zijenge miundo mbinu bali ilikuwa kuwachangia wahanga ile ilikuwa ni misaada ya kibinadamu wao wamebadilisha matumizi na kufanyia shughuli za kiserikali zile pesa ambazo mkuu amekuwa akijinasibu nazo zako wapi*
Yaani "ukimchoka" wewe basi ndio watanzania wote wamemchoka? Wewe ni mfuasi wa mamvi na ni dhahiri una mtazamo hasi. Subiri 2020.
 
kuna watu wanamchosha na kumbebesha lawama.
mtu mmoja, kazi na jina nahifadhi, akawa anatoa maoni yake katika basi. Alikosoa jambo kwamba badala ya elimu bure serikali ingeacha wanachi wakaendelea kulipa ada nayo serikali ikatoa chakula kwa wanafunzi kwani wengi wanatoka mazingra magumu. alisema maneno hana akili .. kumbe pembeni alikuwa amekaa mtumishi mlinda siri. Jamaa alimtokea na mwisho alifikishwa hadi gadirumu. sasa watua wanafikiria anawatuma kumbe wala!
Sasa hapo ndo unaona watu wanavotafsiri vibaya falsafa ya mkuu. waamharibia kwa watu wake.
 
Eeeti ni mapema mwaka mzima unasema ni mapema maana tumechoka kusikiliza hizi ngonjera za taifa changa wakati waasisi ni vikongwe
 
Wengi wamegundua kwamba ni janga la Taifa. Yuko busy kukandamiza katiba ya nchi kwa kuzuia mikutano na uendeshaji wa vyama vya upinzani na kutia ndani wapinzani ambao hawana hatia yoyote. Mambo muhimu yote nchini yanadorora.
Nimeota Baba Yako Atakufa Kwa Ajali Mbaya Sana Ya Gari Kabla Ya Mwisho Wa Mwaka Huu.
 
Huyu rais wetu amekuwa akijinasibu kuwa nchi hii ni tajiri na imechezewa kwa mda mrefu mbona anaharibu hata yale mazuri aliotuachia baba Riz wanafunzi wa Elimu ya juu watapata shida, Watumishi wa Umma vile vile waendesha dala dala kwa Dar, boda boda, hospitalini dawa shida
*Kubwa zaidi ni hili la kagera alishindwa kufika kule watu hawakutoa pesa zao ili zijenge miundo mbinu bali ilikuwa kuwachangia wahanga ile ilikuwa ni misaada ya kibinadamu wao wamebadilisha matumizi na kufanyia shughuli za kiserikali zile pesa ambazo mkuu amekuwa akijinasibu nazo zako wapi* huyu nchi imemshinda anaiendesha kama kampuni binafsi kodi kibao mtani hali ni mbaya mbwa kala mbwa mkuu yeye anajua sisi ni wavivu..... Huu mwaka mmoja naona kama miaka 10
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom