Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Nchi aliipindisha Kikwete, ambaye ndiye aliyemteua kuwa mgombea...yaani ndie aliyempa urais
 
Amani iwe nanyi ndugu zangu,hii kauli si njema hata kidogo,najiuliza waliopindisha ni kina nani?nchi mupindishe wenyewe kisha muinyoshe wenyewe itawezekana kweli? Yangu macho ila kumbukeni taabu na dhiki zinaongezeka kila uchao nyinyi mnakula bata. Tena zile million 10 mlizogawana km ni kweli mungu awapige mapigo alompiga firauni.Acheni kulindana naomba mseme nani aliipindisha?
M 7 unazo mkuu?
 
tafadhali wajuzi hasa wa masuala ya uchumi, hizi hesabu zinatatanisha kidogo nahitaji kujua kitaalamu.

Kiukweli kumekuwa na malalamiko na binafsi naona hela imepotea mtaani, kifupi mzunguko wa hela umekuwa mdogo, wenye nchi na makada wanatuambia ufisadi aka wizi na upigaji haupo sasa kwa hiyo ile hela iliyozagaa haipo tena...

Swali la msingi, sasa kama hela haipo inakuwaje bei za vitu zipo palepale? na hata vingine kupanda maradufu.
Mfano cement twiga plus 12500/=.
Dangote cement. 11500/=
Kifupi hakuna iliyo chini ya 10000/=.
Nauli za ndege, bei ipo palepale.
Sukari ndio hivyo tena.
Unga umepanda kidogo.

Wataalamu wa uchumi na sio wanasiasa mtuambie tafadhali hii inaashilia nini??? maana kama hela hamna hata vitu vilitakiwa vishuke bei..
 
Kunyoosha - ni neno la kishwahili na tafsiri yake ni
kuhakikisha kilichopinda kinakaa.
sawa.
Lakini pia mnyooshaji anaweza kutumia tendo la kunyoosha vibaya kwa sababu labda anaweza kuwa na kinyongo au donge/gere akiwaona watu wakiishi maisha ambayo yeye hataki waishi.

Unaweza ukawa na hela lakini zikawa zinakutesa mwenyewe inawezekana ni za uganga na ikakupasa ulale chini, nguo chafu hata kula yako pia. Kifupi unakuwa hohehahe ujitambui na ukifa unaacha shida kwa wengine, sasa watu wanamna hii wakiona unaishi vizuri ni tatizo kwao watatamani hata wakutoe roho na mwisho wa siku ndio utanyooshwa

Speed without control kills, Power without knowledge is nothing.
 
Anapindisha, ndie anaenyoosha, anaebomoa, ndie anaejenga, waacheni CCM wainyoshe Nchi wenyewe ndio walipindisha
 
Kinachonitisha mimi ni pale aliposema anaweka katiba pembeni anataka kunyoosha nchi, hii maana yake ni kuwa anatumia akili yake na sio katiba iliyomuweka hapo
 
Nchi ilipindishwa na mwinyi na si rahisi kwa vijana wa hivi karibuni kulitambua hilo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom