Magufuli kasema mubashara kabisa kua alikua anabip tu URAIS mara kashangaa kapiga,kama alibip 2020 akigombea tena atasemaje?Mtu ambaye hakujiandaa kuwa raisi kufanya mambo kama yale siyo kosa lake .
Ulishaona wapi raisi wa nchi gani ?anateua watu wasiokuwa na taaluma kwenda kuwaongoza wananchi .
Unaona unavyozidi kujidanganyaMiaka kumi! Subiri 2020 ndiyo utajua majibu ya makorokoro ya mfalme na kumbuka wale wezi wa kura waliozoea kuwapa ushindi kwa bao la mkono nao wanaisoma
Watu mnatunza data kweli kweli.Punguza papara utatukana bure. Angalia unavyojiumbua mchana kweupee.
Ha ha ha, kamanda vipi tena?
Hoja gani?Watu mnatunza data kweli kweli.
Lakini hujajibu hoja yake??
dereva mpya kashabadili adi mafuta mambo badoJe inawezekana gari lenu limewekwa mafuta yaliyochakachuliwa?
Huna tofauti na abilia zuzu, aliyepanda gari akaona miti inarudi nyuma kwa kasi akashangilia eti "miti inatembea au kukimbia"Nyie tu ndo mmpepigwa opofu.
Sisi tumeshafika gairo tunaitafuta Dodoma.
Kaeni tu mnalalamika kuja kushituka 2020 hiyoooooooooo.
Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.
Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.
Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.
Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu
Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa?
Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.
Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Hapa hatuongelei Lowassa, Mbowe, wala Co.Tunaongelea Dira/direction ya JumaPondaMali Haipo bayana. Usitutoe kwenye mstari, anzisha Uzi mwingine. Hapa tunataka tujue tunaelekea wapi na JPM.Akupeleke kwani wewe umekuwa zombie? Raisi Magufuli hayuko hapa kukupeleka wewe popote pale, bali wewe ndiyo unatakiwa ujipeleke mahali kwingine, wewe ndiyo unatakiwa ujitoe hapo ulipo na kwenda sehemu nyingine, wewe ndiyo unatakiwa ujifungue minyonyoro uliyofungwa na fisadi Lowasa, Mbowe & Co. na kuwa mtu huru Raisi Magufuli hawezi kulifanya hilo na wala siyo kazi yake!