Hatuamki asubuhi tukasema tunaenda kwenye viwanda, lazima tujiulize vilivyokuwepo kwa nini vilikufa. Tuna mioundombinu ya uhakika? tuna umeme? tuna malighafi? Leo tunalizwa na sukari, tumejiuliza kwa nini hatuwezi kuzalisha sukari ya kutosheleza mahitaji?
Kwani tawala zilizopita hazikuyaona yote unayoyasema wewe, je ni nini kilifanya mambo yawe shaghalabaghala mpaka tukafikia tulipofikia?
Je waliweka utaratibu gani wa kutimiza na kutekeleza ilani zao, kwanini hapakuwa na matokeo mazuri sana?
Kwa sisi tuliokula chumvi nyingi na kushuhudia tawala zote tangia uhuru, tunamuona Magufuli kama mtawala bora kabisa anayeweza kutuvusha kwa dhati toka sehemu tuliyokuwa tumenasa kama taifa.
Huu umangimeza wa kifisadi wa kufanya mambo kiuoga, ulianza kuota mizizi tangu awamu ya kwanza, ikiwa ni mbinu za kula kombe bila mwanaharamu kuona. Tawala zilizofuata zilipalilia na kulea sana mafisadi. Kulikuwa na kamsemo kao "chama hakimtaji mtu", huu msemo ndiyo ulio wapa kichwa mafisadi na kufanya waliyoyafanya bila hatua zozote za maana kuchukuliwa dhidi yao.
Tunafurahishwa sana na namna ambavyo awamu hii inavyoenda na mambo yote na kufanikiwa kuyakamilisha kwa wakati.
Miaka miwili na nusu tu ya utawala wao imekuwa kama wametawala miaka 10!
Kwa nini tuendelee kuhoji na kubeza mbinu zao walizoamua kuzitumia namna ya kulisikuma gurudumu?