Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Naomba msamaha kwa watanzania kwa kumsema kiongozi wetu kwa jambo hili

Mkuu kuna mambo mengi unajichanganya sana

Suala la uwajibikaji wa kiserikali na ofisi kwa ujumla
Naona Makonda na Makala kwa sasa aliyepaswa kuwa nje system nani?

Kosa la Makala ni la kawaida kulingana na makosa pamoja na tuhuma za Makonda?

Juzi mbona ulitwambia ndo mkuu wa mkoa bora?
Kuna nini cha ghafla?

Nini kinakupa kigugumizi kufanya maamuzi yanayohusu Makonda?

Britannica
Usilolijua ni sawa na usiku wa giza ,ni bora ukaendelea kulima vitunguu vyako na karanga ,"sirikali",unaeona anafaa kwake hafai ,na yule unaona hafai kwake anafaa sana ,na si kila jambo litawekwa wazi ,never at all
 
Mkuu, nawewe umekatwa mkia nini? Kwa muda mrefu ulikua ni mtu wa kupiga makofi na kusifia tu, nini kimekupata?

Mimi pia nimejiuliza sana, ila hawa ni kuwa wanatafuta kuongeza malipo, au malipo yamekatwa.
 
Naomba msamaha kwa watanzania kwa kumsema kiongozi wetu kwa jambo hili

Mkuu kuna mambo mengi unajichanganya sana

Suala la uwajibikaji wa kiserikali na ofisi kwa ujumla
Naona Makonda na Makala kwa sasa aliyepaswa kuwa nje system nani?

Kosa la Makala ni la kawaida kulingana na makosa pamoja na tuhuma za Makonda?

Juzi mbona ulitwambia ndo mkuu wa mkoa bora?
Kuna nini cha ghafla?

Nini kinakupa kigugumizi kufanya maamuzi yanayohusu Makonda?

Britannica
Makonda anafanya vizuri sana Dar es salaam.
Ni msimamizi mzuri sana wa mipango ya maendeleo katika jiji.
Mengine ya ujana hayana effect kwa wananchi wa Dar es salaam. Akikua ataacha.
 
Ni zaidi ya hiyo 'nepotism'.

Mtu anayetunza funguo za makabati yote sio wa kumkurupukia kirahisi. Akina Britannica wataimba kila aina ya nyimbo ...lakini inashangaza kidogo, kwa mtu kama 'Britannica' asielewe haya yote! Nadhani kuna 'disconnection' mahali fulani inayomfunika macho ili asione.
Mkuu hakuna disconnection, Mayalla aliwahi kusema kwamba unaweza kuwa unajua sababu au jambo ukaliibua kama swali bila kutaja ukijiacho ili uone mtazamo wa watuwengi je wanaujua ukweli,
Pascal Mayalla
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Huwezi kujua umepotea kama hujui unakoenda.
 
Kwa Mwalimu walikuwa wanaangalia utabiri wahali yahewa kwenye TV je nakwenu ilikuwa hivyo? Kama nihivyobasi nikweli mlikuwa sawa
Kwa mara ya kwanza niliona TV 1995 ya DTV kabla ya hapo kulikuwa na watu wana video zao. Mimi nisingeweza mudu hivyo vitu.
 
Salam wote,

Hoja yangu ya leo ni juu ya huyu dereva wetu...kwanza niseme wazi kabisa jamaa ni msanii, lakini pia ana Roho mbaya nafikiri tukitafuta duniani, anashika namba zenye digit Moja.

HAWA MAWAZIRI anao wateua, ni kama MBWA anayepewa NYAMA yenye SUMU! matokeo yake semeni wenyewe.

Mambo yote yanayoharibika hapa NCHINI kuanzia ukusanyaji MBOVU wa pesa, KUHARIBIKA kwa KOROSHO, kushuka kwa MAPATO, kufungwa kwa BIASHARA, watu kupotea kwenda KUSIKO JULIKANA, SIASA CHAFU na harakati chafu za kina MUSIBA......................


Yoote hayo, ni MATOKEO ya maamuzi mabovu ya MAGUFULI na sio MAWAZIRI anaojifanya KUWATUMBUA!!!!Kwanini?? Kwasbabu..

1. Ni nani aliyevuruga utaratibu wa wafanya biashara wa maika yote kununua KOROSHO na akatuma jeshi???

2. Ni nani aliyesema POLICE akiua asishitakiwe bali apandishwe cheo???

3. Ni nani aliyesema HAPANGIWI NA MTU YOYOTE CHA KUFANYA NA UKIMPANGIA NDO UMEHARIBU???

4. Ni nani aliyesema TRA watumie nguvu yoyote kukusanya mapato??

5. Ni nani aliyesema ole wake mkurugenzi atakaye mtangaza mpinzani kuwa mshindi????

Sikilizeni watanzania, POINT ya tatu ni msingi wa matokeo yote na mambo yote yanayoendelea hapa nchini... JIULIZE SWALI? WEWE NI BABA MWENYE NYUMBA NA USHASEMA NDANI YA NYUMBA YAKO HAKUNA WA KUKUPANGIA CHA KUFANYA..UNADHANI SIKU UKIVAA MKANDA UKAVUSHA TUNDU MOJA KUNA MTU ATAKUAMBIA?….Je utakapoenda ukaaibika huko nje unarudi KUWATANDIKA WATOTO kwa kutokukuambia umefunga mkanda VIBAYA??...HUO NI UONEVU..NA kwa level ya NCHI huo ni U-DICTATOR.

MZEE MAGU, MAMBO UMEYAHARIBU MWENYEWE, DANGANYA NYUMBU MIMI NIMEKATAA..TOKA HADHARANI UTUAMBIE una mkakati gani wa kututoa kwenye hili shimo? Wale wanufaikaji, mnakaribishwa pia, ila hapa ni mahali huru pa kujadili mustakabali wa MAMA TANZANIA.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom