Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Mustakabali wa kinachoendelea kwa sasa utatoka ndani ya ccm yenyewe! Chama kimesurrender kwa mtu mmoja wote wanamsikiliza yeye tu! Anasema hadi 2020 serekali itakuwa imehamia dodoma kesho yake unasikia mawaziri kila mmoja anatamka tarehe ya karibu kuhamia dodoma kumshinda mwenzake, anasema sukari bei elekezi ni 1800 viongozi wote hadi Waziri mkuu nae anacheza wimbo huo bila hata kuhoji, anasema kuna watu walikuwa wanaimba tuna Imani na mtu fulani ningekuwa mimi mwenyekiti ningewapoteza watu wazima wanacheka kama mazuzu hata hawahoji ungewapotezaje? Anasema hapa kazi tu kila mtu anacheza hapa kazi tu wakati hamna kazi, anasema mikutano ya siasa hadi 2020 watu bila kuhoji wanacheza nyimbo yake hadi Waziri mkuu, hamna mwenye courage ya kumwambia umekosea, wakitoka njee ndio unasikia wanaulizana umemwelea muheshimiwa? Wengine ndio unasikia huyu jamaa haeleweki nakwambia hii nchi itamshinda. CCM ya sasa inaendeshwa na mtu mmoja wenye weledi wamebaki kushangilia ili wapate chakula cha kuishi!
Kwahiyo sasa wale wabunge wa ccm wanaishi Dar ambao huwa hawaendi majimboni kwao sasa wamepata kisingizio cha kutoitisha mikutano ya wananchi kuwapa milejesho!!

Na vyama vya mfukoni kama cha Dovutwa nadhani wanafurahia ili wasiwajibike kutumia pesa zao kuandaa mikutano mpaka 2020 ccm itakapowapa fungu lingine la kufanyia maigizo ya siasa.

Matokeo yake Dovutwa anagombea urais uzinduzi mbagala kampeni ni kubandika posters tu kamaliza pesa iliyobaki anaitafuna na familia yake.
 
Naomba mtoe Malecela, kwenye kuhamia Dodoma kasema yuko bega kwa bega na Rais, so sitegemei kama yuko sincerely katika kumshauri.

Yeye alikuwa right hand man wa Mwinyi hawakuhamia Dodoma, leo anamshabikia mwenzake kuingia katika huu mtego.

Inasikitisha sana Mh JPM katika awamu ya 4 katumia nguvu, akili, muda na jasho lake kuhangaika kusimamia kujenga nyumba za watumishi wa serikali DSM nyingi tu. Sasa tena kaamua serikali ihamie Dodoma pamoja na mambo mengine mengi atakayo fanya akanze tena kutumia nguvu na rasilimali kujenga nyumba mpya za watumishi wa serikali, so sad!!!
 
watanzania hatuko that special. ..yaliyotokea kwa wengine hayakutokea tu kwa bahati mbaya
 
This country is not a nation. It is a group of people living together.
 
Kikwete alikuwa mpole,matokeo yake kuitwa dhaifu na mnyika, na magufuli pia awe mpole basi umekuwa utoto. Alenselema alejaa, kanyaga twende,magufuli anatupeleka kwenye neema.
no....nchi inaongozwa kwa katiba na sheria tulizojitungia...sio matakwa ya mtu binafsi.

kama jk hakuchukua hatua za kisheria kama inavyotakiwa yes mnyika alikuwa sahihi

kama jpm hafuati sheria na katiba lissu yuko sahihi

nchi hii ni yetu sote
 
Naombea wakuu wa Chadema wasibadilishe msimamo ili tujue mbivu na mbichi
 
Wakulaumiwa ni wapinzani sio Magufuli.
Yule ni Mtawala kwa sasa na Katiba yetu ni ya Kikoloni inampa Mamlaka Yote kuliko hata Mungu.
Leo hii ni rahisi mtu kupita mitaa na kumkosoa Mungu na akasalimika lakini sio Viongozi wa Serikali.

Lakini pia tulitegemea nini tulipoirudisha CCM Madarakani kupitia Magufuli? Wengi tulisema tumemchagua Magufuli na sio CCM na wengi wakiwemo Wapinzani walimuunga mkono ikiwemo Mpigania Demokrasia namba moja Dr. Slaa . Hawa walijifanya hawajui kuwa tatizio la hii nchi sio mtu mmoja bali ni mfumo wa Kikoloni unaomsababisha rais kufanya nchi kuwa mali yake binafsi. Yani hatambui kuwa kuna watu wengi wenye mawazo mbadala juu ya taifa lao.

Hata hivyo naona ni bora Magufuli anayetumia katiba hii yenye kuweza kumpa mtawala mamlaka yote na ubabe wote kujenga nidhamu na maendeleo ya nchi kuliko wale waliomtangulia ambao walitumia mampaka hayo kufanya ujanja ujanja na kulitia taifa hasara huku wakiwadanganya wapinzani kwa chai za kushtukiza Ikulu.

Nafurahi sana ninapoona Rais Magufuli anaposoma maoni yangu na kuyafanyia kazi.

Tumempata Raisa wa kuinyosha nchi na bahati nzuri au mbaya hakuna wapinzani wabunifu zaidi ya kukariri aina moja tu ya kufanya siasa ,yaani maandamano tu na kubeba wabunge wote kwenda kwenye majimbo kuhamasisha watu kuwa wavunjifu wa sheria, uvivu na watu kuwa tegemezi kwa serikali kwa kila kitu.
Nilianza kuaona mwisho mbaya wa Chadema na wapinzani kuwa mbaya pale walipoanza kuchochea wananchi maandamano ya kumpinga Magufuli bila hata kumpongeza kwa hatua kadhaa alizochukua. Hii itamfanya ajenge chama chake kwa kasi kubwa kwani ndicho kitakachobaki kama msaada kwake na wale aliokua anawategemea kuibua madudu na kumpa moyo wa kupambana na ufisadi sasa wanageuka kuwa maadui wa kumkatisha tamaa.
Hili ni kosa kubwa wanalofanya wapinzani.
Siasa za CCM zilivyo kwa sasa ni kuteka akili za wananchi ambao wengi wao ni wale wasio na elimu. Na wamefanikiwa kupitia Magufuli na hawana haja tena ya kufanya siasa zaidi ya kuwatumia watawala na vyombo vya dola, ambavyo kimsingi jambo la kwanza kabisa ni kulinda amani na usalama wa nchi kwa nguvu zote.
Magufuli mara ya kwanza alionekana wazi kuwa alikua anavutuwa sana na siasa na misimamo ya vyama vya upinzani hasa chadema. Ndio maana alianza na yale waliyokuwa wanayapigania miaka nendarudi. Na asingeweza kubadili jambo lolote kuwa jema bila ya kutumbua majipu na mishipa yao michafu. Tulitakiwa wote tumuunge mkono ili asafishe kwanza nchi kwani kwenye majipu na ufisadi ndipo ilipo nguvu kubwa ya CCM.
Wapinzani wanakosea sana wanapofikiri kuwa CCM itaondoka madarakani kwa maandamano. CCM na wabunge wake na madiwani wake wengi na hata kwenye serikali za mitaa walikua wanapata madaraka kutokana na rushwa inayotokana na pesa walizokuwa wanazipata kutokana wizi na ujanja ujanja wa kila namna. Sasa amekuja kiongozi anayekata mizizi ya wizi jambo ambalo ni jema kwa wapinzani na wapenda maendeleo na demokrasia ya kweli.

Magufuli akiendelea nawendo huu na wapinzani wakakamuunga mkono Mwaka 2020 tutashuhudia uchaguzi huru na wa haki hasa kwa madiwani na wabunge.

Hivi kuna shida gani kwa Mwenyekiti wa Chadema na katibu wake kufanya vikao na mikutano ya ndani kama alivyoelekezwa ili kuepusha shari?

Kama sio akili za ajabu hiyo tarehe 01/09/2016 watu wa kuandamana Mbowe atawapata wapi chini ya mkwala mzito wa Magufuli wakati chadema hakijawaandaa wananchi kiimani,kifalisafa na kiitikadi.

Nasikitika sana ninapoona upinzani una wanachama wengi sana lakini inawatumia kufanya mambo ya ajabu ajabu badala ya kuwatumia kujijenga kiitikadi.
Kwa kweli kwa sasa hakuna mtawala chini ya katiba wala ijayo atakayeruhusu mamikutano ya hadhara ya kufuru kama yale ya kudeki barabara wakati uchaguzi umeisha.

Wapinzani hebu badilikeni kifikra muonyeshe kuwa mnaweza kukabidhiwa nchi!! Hivi kweli ni nani atakubali kumwacha Lowasa azunguke nchi nzima kujaza watu kwenye mikutano? Watu hawatafanya kazi ,miji na vijiji vitafurika mikutano na maandamano na shughuli kusimama bila sababu.
CCM imeshinda uchafuzi kama kawaida yake na tuipe muda iongoze kwa angalau miaka mitatu ili wananchi tuamue kama wanakwenda vizuri au wanafanya sanaa. Wakati huo wapinzani wawe wanajijenga kwenye majimbo na kata na vijijini kwa kuimarisha matawi yake. Hizo pesa wanazotumia kuzunguka na Helkopta wakati huu basi wazipeleke kule vijijini ili kujenga nguvu na uwezo wa wanachama wao.


Hivi Mbowe amekosa mbinu ya kuwafikia wanachi bila maandamano?
Ajabu kabiasa. Ni bora wavunjwe hata miguu kama hawana namna ya kuwafikia wanachama wao bila maandamano tena yenye lengo la kumpinga Rais aliyetumbua majipu yaliyoisumbua hii nchi kwa miaka nenda rudi. Siasa hizi zisizo na mipaka ndizo zilizotugharimu na kukosa kiongozi bora kama alivyokuwa waziri mkuu enzi za JK na Lowasa.

Lowasa alikua na maana kubwa sana alipowaambia Chadema sasa kifanye siasa na sio harakati. Aliona aina ya utawala uliopo wanaweza wote wakawa vilema. Na wananachama wao wakaishia.

Yani hata kisaikolojia hawa viongozi wa chadema hawaoni kuwa bado wananchi wana hamu na kipya kinyemi? Hata mwaka haujaisha bado ? Watu wanaimani kubwa na mategemeo makubwa na Magufuli. Wananchi bado wanafurahia neno hapa kazi tu. Chadema ingetulia kwanza angalau watu wawapime watawala kwa muda.
 
Hawana authority ya kulilia demokrasia wakati internally wanaigaragaza.

Huu msala ni wa Mbowe na Chadema (excluding chadema asilia? Ambao demokrasia yao iliminywa ndani ya chama chao). Wapinzani wengine kujiunga kwenye huu msala ni kujipendekeza wasipopendwa. Kama hawaamini wanatumika wajiulize ukawa imeishia wapi na nini utakua mwisho wa ukuta.
 
Hawa authority ya kulilia demokrasia wakati internally wanaogaragaza.

Huu msala ni wa Mbowe na Chadema (excluding chadema asilia? Ambao demokrasia yao iliminywa ndani ya chama chao). Wapinzani wengine kujiunga kwenye huu msala ni kujipendekeza wasipopendwa. Kama hawaamini wanatumika wajiulize ukawa imeishia wapi na nini utakua mwisho wa ukuta.
Rubbish
 
Nikimsikiliza Rais Magufuli napata picha ya mfanyabiashara mdogo wa duka la kaya aliyepewa mtaji na nduguze ili ajikimu yeye na familia yake lkn kabla hata hajaanza kufanya mauzo, anaamua kuanza kutafuna biskuti na kulamba sukari kiasi cha kufikia kula mtaji wote na hatimaye duka sasa kalifunga - Magufuli hakika ameamua kujihujumu na kuufanya Utawala wake kuwa mgumu pasi na sababu.

Basi natamani wapatikane wazee wenye busara (Maaskofu na Masheikh ) wakazungumze naye kwa upole wamkanye tu kwamba speed aliyo nayo ya kuelekea kupotea njia ni kubwa mno - ataivuruga nchi na atajivuruga mwenyewe, halafu wale wazee wa CCM akina Kikwete na akina Mkapa wataanza kumcheka.

Hakika kuna shida kubwa nafsini mwa Rais Magufuli - akikutana na Maaskofu na Masheikh naamini watamfanyia na maombi pia ili apone - Rais huyu anahitaji UPONYAJI.
kusema ukweli hao watu unaotaka wakamponye magufuli nawachukia kutoka moyoni.
usisahau huyohuyo Kikwete unayemponda alimuambia kupitia lugha ya kifalsafa kuwa acheni chama kiwe kwa wananchi. sijui wewe ulitakaje.
 
Inasikitisha na inahuzunisha sana kwa Tanzania kuwa na Rsis wa aina ya Magufuli!
Tangu ameingia madarakani mheshimiwa JPM amekuwa ni mtu wa kutoa matamko yasiyo zingatia Katiba na Sheria na hii ni hatari sana! Rais anayeongoza Taifa lenye takribani watu milioni 50 kwa kuongozwa na hisia au mihemko ni janga kwa Taifa!
Kila kitu au mtu kuna sehemu ya uzuri na ubaya na huo uzuri au ubaya unapimwa kwa kuangalia upande upi unaoelemea mwingine!
Pamoja na sifa ya JPM kupambana na Ufisadi na kusaidia vijana wetu kielimu katika machache mazuri mizani inaelemea kwenye Wingi wa ubaya. Kitendo cha kuendesha nchi bila kufuata Katiba au Sheria ndiyo inabeba ubaya wa JPM kwa asilimia kubwa kama ni kwa aslimia basi ni 60-80%!
Kwa kiwango hichi cha ubaya wa JPM anajitengenezea kaburi lake na la chama chake cha CCM! Laiti JPM angelikaa siku moja na kutafakari kura alizopata mwaka jana 58%(8m votes) zidi ya UKAWA/Lowassa aliyepata 40%(6m votes) kati ya Watz milioni 40 alitakiwa kuwa mpole na kuwaheshimu wale 6m na wengine zaidi ya 25-30m ambao hawakupiga kura kabisa!
Kwanza Rais anapotamba na kuanza kuzuia mikutano ya siasa kwa kisingizio cha Hapa Kazi Tu siyo sawa! Rais anapozuia Bunge la JMT kuonyeshwa LIVE siyo sawa! Rais anapotumbua/fukuza/simamisha kazi watu bila kufuata taratibu na sheria za kazi hiyo si sawa!
Rais anapotisha wanachama tena wa Chama chake watakaompinga kuwapoteza hiyo si sawa!
Rais anapowatisha Wapinzani kuwa yeye Hajaribiwi na atakayejaribu ataona siyo sawa hata kidogo! Hawa Wapinzani wana haki na wana nguvu ya Kikatiba kufanya hivo na si kumjaribu JPM! Wana haki kuwatembelea na kufanya mikutano na wapiga kura wao zaidi ya 6m!Sasa unapozuia wasikutane eti tu kwa sababu hawakupata kura za kuingia Ikulu si sawa! Kwa maana hii JPM hatakiwi kufanya mikutano kwenye Majiji,miji na Majimbo yanayoobgozwa na wapinzani maana hawakumchagua! Je, hiyo ni sawa????
Nimalize kwa kusema kuwa OGOPA SANA MTU ANAYETANGULIZA UMIMI/UBINAFSI kwenye maswala ya kitaifa kana kwamba Tanzania ni nyumbani kwake,mkewe na watoto!
Sina hakika kama JPM amebahatika kusikiliza hotuba za wagombea Urais wa Marekani wa Demokratiki na Republican hasa mama Hillary Clinton ambsye Hotuba yake imesheheni "WE BELIEVE IN....." yaani Tuna amini na tutafanya 123,tuta...tuta....n.k! Na siyo NITA...... na majigambo kibao kama ya"Tanzania ya Magufuli,Serikali ya Magufuli n.k,n.k. Huo ni uzuzu wa kisiasa kutaka kuonyesha kuwa wewe peke yako unaweza na cyo Katiba ya nchi!
Kwa sheria na Katiba hizi anazotunga Rais majukwaani na kuungwa mkonon na Majeshi ya Ulinzi na Usalama ni hatari sana kwa mstakabari wa nchi!
Watu waombe na kusali sana ili Mungu aondoe moyo wa kiburi na jeuri ndani ya Rais wetu vinginevo.........!!!!!????
Mbowe kuandamana jimbo la hai usiku na mchana ili kudumisha democrasia ni kinyume cha katiba ??

Mbowe njoo Moshi ,tuandamane , maana ndio ulichotuahidi wakati wa uchaguzi kwamba ukishinda utatuletea maandamano.

Tunahitaji maandamano
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom