Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Mchawi utamjua tu!
 
Lkn kumbuka sote yupo ktk jahazi moja!
 
Toka aingie madarakan alilofanikiwa ni lile la kutumia hela za covid kujenga madarasa,tofaut na hapo sjaona lingine zaidi ya kusafiri
Fungua ubongo ndigu. Sasa hivi ajira zimejaa kila Kona kwa sababu wawekezaji wameingia nchini kwa wingi. Vijana waliokuwa wanalanda land mtaani bila kazi kwa miaka mitano ya jpm sasa Wana Cha kufanya. Wafanyakazi wameongezeka mishahara kinyume na jpm ambaye miaka yake yote hajaongeza. Demokrasia imepanuka. Wakulima now wanaweza kupata masoko ya uhakika nje na ndani ya nchi
 
Usimuombee hivyo.... Tunaoumia ni sisi tabaka la wasakatonge...
 
Ingekuwa vema iwapo ungemutakia kinyume chake.

Hivi unafahamu kushindwa kwake ni kushindwa kwetu sote kama watanzania?

Matharani nchi iko gizani na Maji hakuna unazani Ikulu anapoishi kuna mgao wa Maji au umeme?

Na kushinda kwake vivyo hivyo ni kushinda kwetu sote kama Taifa.

Tafakari halafu badilisha namna yako ya kufikiri.

Tutakiane mema.

Kama uko na hoja za msingi au kumkosoa akosolewe kwa haki na sio wishes zisizo na maana.
 
Sababu kubwa ya vitu kupanda bei ni US Federal Reserve Bank (BOT ya US), uchumi wa dunia upo based kwenye dollars, miaka mingi interest rate ya dollar ilikuwa karibu na zero ndio maana pesa zetu zilionekana zina thamani kidogo ukilinganisha na dollar, sasa wameongeza interest rate ili kupambana na inflation kwa hiyo dollar imekuwa very expensive na kufanya pesa zetu kama shillings kuanguka na kupoteza thamani, na kumbuka uchumi wetu mkubwa unategemea importation kuanzia machinery za uzalishaji, mafuta, mbolea, vyakula, vipuri vya umeme etc, sasa shilingi imepoteza thamani kwa hiyo hivyo vitu vyote vimekuwa very expensive, sasa kila mtu anaumia na itachukua muda kurekebisha, jiandae na maumivu kwa muda mrefu na kiukweli Samia hana control na hii kitu ila kuna vitu vidogo serikali yake inaweza kufanya ambavyo navyo ni vigumu,kama kuwapunguzia makali ya chakula serikali inaweza kununua unga/mchele na kuuza kwa bei rahisi (subsidize) lakini nayo ni hatari inaweza kuua wakulima wa ndani
 
Sababu kubwa ya vitu kupanda bei ni US Federal Reserve Bank (BOT ya US), uchumi wa dunia upo based kwenye dollars, miaka mingi...
Mkuu, asante Kwa elimu hii, lakini ifahamike kuwa, hii inaweza kudhibitiwa vizuri kabisa

Umewahi kujiuliza ni Kwa nini serikali kila Leo inaagiza nagari yenye thamani kubwa saana m300+ Kwa kila gari kwenye mawizara, wakati huo huo inayauza kila unapoisha mwaka Kwa tsh m5?

Unadhani boss, Kwa serikali yenye watu makini, haiwezi Ku make kwenye haya mambo na kufanya maisha yawe ya kawaida kabisa Kwa Watanzanzia?

Mambo kama haya yatokeapo, serikali huwaza kweli namna ya kupunguza gharama za kuendesha nchi?
 
Watanzania wanapenda bure Sana...sasa umeme uwe elfu 27..na unadai kabisa ndo gharama halisi
Yaani gharama halisi.....aisee
 
Watanzania wanapenda bure Sana...sasa umeme uwe elfu 27..na unadai kabisa ndo gharama halisi
Yaani gharama halisi.....aisee
Kwa hio mboni 27elfu iliwezekana? Chini ya Medard Kaleman mwenye akili kubwa na ukafika mbali, hadi bibi yangu bush uko kawekewa umeme kwa 27elfu tu, wewe hujaliona hilo?

Mboni ahuhoji wanaojengewa Nyumba kwa mpango wa TASAF au sio bure ile?
 
Kosa kubwa sana la kwanza ni kumteua mtu mwenye historia ya wizi na ufisadi kuwa waziri wa fedha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…