Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini?

Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Baada ya Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa, sasa ni nderemo na vifijo nchi mzima!. Na mimi kama Mtanzania mzalendo wa taifa letu, pale linapofanywa jambo jema lolote la kheri kwa mustakabali mwema kwa taifa letu, sina budi kujiunga na wengine wote wanaolitakia mema taifa hili kwa kumpongeza Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mikutano ya siasa, kukubali kurekebisha sheria mbalimbali kandamizi na kubwa kuliko, kukubali kuendeleza mchakato wa katiba mpya.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa
, kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni kitu ambacho kimeruhusiwa na katiba, kitendo kile cha kuzuia mikutano hii, hakikuwa sawa!, huu ilikuwa ni ukwiukwaji wa wazi kabisa wa katiba ya JMT mchana kweupe!.

Kufanya mikutano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, hata lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?, naamini wengi mnajua nilijibiwa nini!.

Sasa leo Rais Samia, alichokifanya kwa kuruhusu mikutano ya siasa, ni kama leo ndio lile swali liameljibiwa kwa mtindo ule ule wa "anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!", jambo linalozuiliwa kwa utashi tuu wa mtu bila kifungu chochote, cha katiba au sheria, siku ya kuliruhusu jambo hilo, pia ni kwa utashi tuu, wa kiongozi aliyepo, bila kutumia kifungu chochote au sheria yoyote!. Jambo lolote lililozuiliwa, (regardless lilizuiwaje), linaporuhusiwa, hatua ya kwanza ni kushukuru kwa jambo hilo kurusiwa, hivyo Watanzania wote tujiunge pamoja na kusema kwa kauli moja, "Asante Sana Mama".

Baada ya kushukuru, sasa twende ndani kidogo zaidi ya jambo lenyewe lililoruhusiwa, kwa vile mikutano ya siasa ilizuiliwa kwa utashi tuu, na sasa imeruhusiwa kwa utashi tena, tukishukuru na kusema tuu asante bila kutia neno jingine lolote, hii inapelekea suala la mikutano ya siasa kuonekana ni kama jambo la hisani tuu ya rais aliyepo madarakani, JPM alizuia mikutano kwa utashi tuu, na leo Rais Samia ameruhusu mikutano hii kwa utashi na kwa hisani tuu!, swali linabaki ni jee mikutano ya vyama vya siasa ni haki ya vyama kufanya mikutano au ni hisani ya Rais wa JMT aĺlye madarakani?

Kitu kama ni haki, then haki ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini wakati haki zetu na stahili zetu zikigeuzwa kuwa hisani?.

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa, haipo!, imenyofolewa na kufinyangwa finyangwa hivyo kuonekana kama ipo ila kiukweli ni haipo na mimi mwenyewe ni shahidi wa hili!.

Kwenye issues za haki zetu za msingi za kikatiba, jee Watanzania tutaendelea kusubiri kuhisaniwa mpaka lini?.

Naendelea kusistiza mwaka huu wa 2023, Watanzania lazima tuamke tufanye kitu.

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema
asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!.

Wakati tukisubiria hisani ya Mama Samia kwenye hili, kupitia marekebisho ya sheria mbalimbali na kumruhusu kila Mtanzania kuchagua na kuchaguliwa, should we just sit and wait kusubiria hisani ya Mama kama vyama vya siasa vilivyosubiri hadi leo vilipohisaniwa, or should we do something?. Hiki ndicho nilicho anza nacho mwaka huu Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional not as a favour, hisani au fadhila!. Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, but only pale inapobidi, na ni katika kuipigania huku sometimes machozi, jasho na damu huweza kumwagika!.

Kwa vile Rais wetu Mama Samia, keshaonyesha utashi, kwa kauli na matendo, tuzidi kumuombea ili Mungu amuwezeshe ayaweze yote haya kabla hajamaliza awamu yake hii ya kwanza, ili hata ikitokea akaendelea kwa awamu ya pili, then hiyo itakuwa ni awamu ya shukrani na kumpa asante kwa aliyotatenda, na sio awamu ya kukamilisha ambayo hayakumamilika.

Mungu Mbariki Rais Samia
Mungu Ibariki Tanzania

Happy New Year.

Paskali
 
Happy New Year Brother,,,,,
Hatua moja muhimu imefanikiwa. Watanzania wenzetu wengi bado wanahitaji elimu kuhusu haki na wajibu wao kikatiba na hili linaweza kufanyika vema kupitia vyama vya siasa kwenye mikutano ya hadhara. Kupitia mikutano hii, wengi watendelea kujifunza kuhusu haki ya kuchagua na kuchaguliwa kama takwa la kikatiba. Nina imani ndani ya muda uliopo kabla ya uchaguzi kutakuwepo na mabadiliko makubwa.
 
Katiba hutafsiriwa kwa Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu. Hivyo basi, Mkuu Paskali, mwanahabari nguri, tafsiri yako ya uamuzi wa Rais SSH kuwa ni HISANI, ni potofu. Ungerejea sheria mbalimbali zinazohusu "mwenendo wa siasa" nchini na mapungufu yake, km Sheria ya Vyama vya Siasa (1992) na Marekebisho yake (2018)
 
Leo Mayalla niliyekuwa namjua amerudi jukwaani karibu Pasco
IMG_20221114_112805.jpg


Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Ameupiga mwingi, nzuri zaidi amegusia na suala la katiba mpya. Naona huyu mama anaweza kukamilisha mipanga mizuri ya JPM.
 
Wanabodi,
Baada ya Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa, sasa ni nderemo na vifijo nchi mzima!. Na mimi naomba nijiunge kupongeza Rais Samia kwa kuruhusu mikutano ya siasa, kukubali kurekebisha sheria mbalimbali kandamizi na kubwa kuliko, kukubali kuendeleza mchakato wa katiba mpya.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa imeruhusiwa na katiba, hivyo ni haki ya kikatiba ya vyama vya siasa kufanya mikutano kwa mujibu wa katiba, lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?.

Sasa leo Rais Samia, amelijibu lile swali kwa mtindo ule ule wa "anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!", jambo linalozuiliwa kwa utashi tuu wa mtu bila kifungu chochote, siku ya kuliruhusu pia ni kwa utashi tuu, bila kifungu chochote!. Hii inapelekea suala la mikutano ya siasa kuonekana ni kama Hisani tuu ya rais aliyepo madarakani, hivyo kuruhusiwa huku kwa mikutano ya siasa ni kwa hisani tuu ya Rais Mama Samia!. Swali ni jee mikutano ya vyama vya siasa ni haki ya vyama kufanya mikutano au ni hisani ya Rais wa JMT aĺlye madarakani?

Kitu kama ni haki, then ni stahili sio Hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini haki zetu na stahili zetu zikifanywa ni Hisani?.

Haki mbili kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!,
Kwenye issues za haki zetu za kikatiba, jee Watanzania tutaendelea kusubiri kuhisaniwa mpaka lini?.

Naendelea kusistiza mwaka huu wa 2023, Watanzania lazima tufanye kitu.

Asante Mama Samia kwa a political will kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama kujiona vimehisaniwa, nakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania kuchagua na kuchaguliwa.

Wakati tukisubiria hisani ya Mama Samia kwenye hili, la kumruhusu kila Mtanzania kuchagua na kuchaguliwa, should we just sit and wait kusubiria hisani kama vyama vya siasa vilivyosubiri hadi leo vilipohisaniwa, or we should do something?. Hiki ndicho nilicho anza nacho mwaka huu Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?

Happy New Year

Paskali
Kwa kweli nimeshangaa sana hata kuona wanasiasa wakishangilia kupongeza na kumshukuru rais wakiruhusiwa kufanya jambo ambalo wazuiaji walivunja KATIBA ya nchi.
Mimi nilikusudia zianze jitihada za kufungua kesi mahakamani ili kuhakikisha uvunjaji wa KATIBA namna hii haujirudii tena katika mipaka ya Tanzania bila kujali rais ni nani ana akili gani ni wa chama gani
 
Wanabodi,
Baada ya Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa, sasa ni nderemo na vifijo nchi mzima!. Na mimi naomba nijiunge kupongeza Rais Samia kwa kuruhusu mikutano ya siasa, kukubali kurekebisha sheria mbalimbali kandamizi na kubwa kuliko, kukubali kuendeleza mchakato wa katiba mpya.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa imeruhusiwa na katiba, hivyo ni haki ya kikatiba ya vyama vya siasa kufanya mikutano kwa mujibu wa katiba, lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?.

Sasa leo Rais Samia, amelijibu lile swali kwa mtindo ule ule wa "anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!", jambo linalozuiliwa kwa utashi tuu wa mtu bila kifungu chochote, siku ya kuliruhusu pia ni kwa utashi tuu, bila kifungu chochote!. Hii inapelekea suala la mikutano ya siasa kuonekana ni kama Hisani tuu ya rais aliyepo madarakani, hivyo kuruhusiwa huku kwa mikutano ya siasa ni kwa hisani tuu ya Rais Mama Samia!. Swali ni jee mikutano ya vyama vya siasa ni haki ya vyama kufanya mikutano au ni hisani ya Rais wa JMT aĺlye madarakani?

Kitu kama ni haki, then ni stahili sio Hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini haki zetu na stahili zetu zikifanywa ni Hisani?.

Haki mbili kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!,
Kwenye issues za haki zetu za kikatiba, jee Watanzania tutaendelea kusubiri kuhisaniwa mpaka lini?.

Naendelea kusistiza mwaka huu wa 2023, Watanzania lazima tufanye kitu.

Asante Mama Samia kwa a political will kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama kujiona vimehisaniwa, nakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania kuchagua na kuchaguliwa.

Wakati tukisubiria hisani ya Mama Samia kwenye hili, la kumruhusu kila Mtanzania kuchagua na kuchaguliwa, should we just sit and wait kusubiria hisani kama vyama vya siasa vilivyosubiri hadi leo vilipohisaniwa, or we should do something?. Hiki ndicho nilicho anza nacho mwaka huu Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?

Happy New Year

Paskali
Nimekupata P,

Mgombea binafsi ni HAKI ya KIKATIBA ya Kila mwananchi kuwa na HAKI ya kuchagua na kuchagulika!!


Kwa vile ndugu P, wewe ni mwanasheria Kwa Profession,

Unaonaje ukivaa VIATU vya MCHUNGAJI MTIKILA tukutane kwenye Court corridors???
 
Wanabodi,
Baada ya Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa, sasa ni nderemo na vifijo nchi mzima!. Na mimi naomba nijiunge kupongeza Rais Samia kwa kuruhusu mikutano ya siasa, kukubali kurekebisha sheria mbalimbali kandamizi na kubwa kuliko, kukubali kuendeleza mchakato wa katiba mpya.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa imeruhusiwa na katiba, hivyo ni haki ya kikatiba ya vyama vya siasa kufanya mikutano kwa mujibu wa katiba, lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?.

Sasa leo Rais Samia, amelijibu lile swali kwa mtindo ule ule wa "anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!", jambo linalozuiliwa kwa utashi tuu wa mtu bila kifungu chochote, siku ya kuliruhusu pia ni kwa utashi tuu, bila kifungu chochote!. Hii inapelekea suala la mikutano ya siasa kuonekana ni kama Hisani tuu ya rais aliyepo madarakani, hivyo kuruhusiwa huku kwa mikutano ya siasa ni kwa hisani tuu ya Rais Mama Samia!. Swali ni jee mikutano ya vyama vya siasa ni haki ya vyama kufanya mikutano au ni hisani ya Rais wa JMT aĺlye madarakani?

Kitu kama ni haki, then ni stahili sio Hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini haki zetu na stahili zetu zikifanywa ni Hisani?.

Haki mbili kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!,
Kwenye issues za haki zetu za kikatiba, jee Watanzania tutaendelea kusubiri kuhisaniwa mpaka lini?.

Naendelea kusistiza mwaka huu wa 2023, Watanzania lazima tufanye kitu.

Asante Mama Samia kwa a political will kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama kujiona vimehisaniwa, nakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania kuchagua na kuchaguliwa.

Wakati tukisubiria hisani ya Mama Samia kwenye hili, la kumruhusu kila Mtanzania kuchagua na kuchaguliwa, should we just sit and wait kusubiria hisani kama vyama vya siasa vilivyosubiri hadi leo vilipohisaniwa, or we should do something?. Hiki ndicho nilicho anza nacho mwaka huu Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?

Happy New Year

Paskali
ALIYEIZUIA ALIVUNJA KATIBA MAMA KARUHUSU ILI KATIBA IHESHIMIWE WALA SIO HISANI
 
Back
Top Bottom