Anayosema Kigwangalla kuhusu uaminifu wa Watanzania kuna tatizo?

Anayosema Kigwangalla kuhusu uaminifu wa Watanzania kuna tatizo?

Leo asb Hamisi Kigwangalla ameliamsha tena huko Instagram suala la uaminifu wa watanzania. Amehadithia alichofanyiwa na kijana aliyemuamini. Huko nyuma amewahi kuuliza WHAT IS TANZANIA'S COMPETITIVE ADVANTAGE -Akimaanisha nini ambacho tunaweza kusema hichi kinatutambulisha kitaifa.

Juzi kati I-SOKO mfumo wa kuwezesha wanawake kufanya biashara afrika mashariki imeanzishwa. Kilichojiri malalamishi kwamba watanzania hatuaminiki.

Kihehe tunasema sema we have a people problem. Tatizo ni kubwa lakini tunaogopa kulijadili kwakuwa ni kaa la moto. Au halipo


SOMA KISA HIKI KUTOKA KWA hamis Kigwangalla

NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 1:


Kama ukiona elimu ni gharama, ujue haujajaribu ujinga. Vile vile, kama ukiona kutafuta utajiri ni kazi, hebu jaribu umaskini uone.

Hakuna kitu kibaya kwenye maisha kama umaskini. Tuliouishi umaskini tunaujua. Tukipambana nao kwa kila hali msitushangae. Mara kadhaa tushawahi kurudi nyumbani for lunch na kukuta hakuna kilichopikwa tukaishia kunywa maji na kugeuza shule, maana hata wa kumuuliza chakula kiko wapi hayupo home.

Kutajirika ni katika vitu vigumu kabisa kufanya hapa duniani. Niliwahi kujaribu kutafuta utajiri sikuufikia, nikaishia hapa nilipo! Lakini bado napambana. Si haba, WALLAH sina malalamiko yoyote yale kwa Allah, zaidi zaidi narejesha shukrani tele. Nilipotoka napajua mwenyewe.

Kwenye safari ya kutafuta maisha, kwa kuwa nilikuwa na mbio ndefu na za spidi sana, nimejifunza mengi sana. Huwa najaribu kuandika andika hapa, wenye muda husoma na pengine hujifunza.

Niliwahi kuwa nalima ekari 500 - 600 kwa msimu, nikamuamini kijana wangu mmoja mahiri, mchapakazi, mwenye dini kweli kweli, mwenye elimu na passion ya farming; pamoja na kunifaidisha na kunipa tamaa ya kuwekeza zaidi, alinipiga kweli kweli!

Nikaamini wadogo zangu damu kabisa, wakanipiga. Nikazama. 😩!

Mtaji wa zaidi ya ekari 700 ukaporomoka mpaka ekari 100/200. Wakati unaporomoka, unadaiwa na benki ulipe mkopo wa mtaji uliochukua, unadaiwa na kampuni waliokukopesha matrekta, combine harvesters, planters, unadaiwa na suppliers wa pembejeo etc. Inaendelea…


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE. Part 2!

Wakati huo huo umeshushwa cheo na unaambiwa ukajibu hoja kwa CAG za dhambi ambazo hazikuhusu. Faida moja ya cheo ni kuwa kuna mikopo bankers wanakupa kwa kukuamini tu, tena kwa simu tu. Siku kikiondoka, wadai wote wanaanza kuhaha kukudai kama hawakujui vile. Wakubwa wote hawapokei simu zako. Unabaki peke yako kama siyo wewe vile. Marafiki waliokuwa wanakusalimia kila kukicha hawapokei simu zako wala hawajibu meseji zako.

Ukiwa na roho ndogo utasema umerogwa ama utaugua ugonjwa wa akili. Ama hata utaona maisha hayana maana tena.

Wakati unajaribu kutoka, bei za mazao zinaporomoka! Vita ya Ukraine inaanza na COVID inapandisha bei za mbolea etc.

Mwaka huu bei za mazao nzuri, wanatokea kwelea kwelea 😀.

Ili kusimama kwenye maisha, muombe sana Mungu akupunguzie masomo magumu ya kupitia, aidha usihangaike sana kuimarisha misuli ya mwili ili ukivaa suti upendeze, imarisha misuli ya moyo, ubongo na roho(kama nayo ina muscles!😀) ili uweze kukabiliana na nyakati za maanguko. Siku zote jua tu kwamba, baada ya maanguko kadhaa, na kama utaweza kuinuka kila unapoanguka, na kustahimili maumivu ya kila anguko, mwangaza huja na Mungu humuinua mja wake! (Graduation hiyo sasa!)

Maisha ni Marathon. Kutajirika siyo rahisi. Lakini kwani nani alisema umaskini ni raha?

Iendelee ama iishie hapa?


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 3.

Ukitenda wema, tenda kwa watu wengi sana, muhimu ni kuwa usingoje shukran. Kwa hakika wema, ni akiba isiyooza.

Pamoja na uwepo wa watu wengi wa hovyo kwenye maisha yetu, watu ambao hawawezi kukufanyia jambo jema, zaidi zaidi wanajipanga kukuangusha na kukudhuru kila kukicha, tena hawana sababu yoyote ile, huwa wapo watu wachache wema, pengine uliwahi kuwatendea wema basi wanakumbuka ama ni watu wenye tabia ya kupenda kutenda wema tu. Wapo!

Wabaya wengi wapo lakini wema wachache pia wapo. Jitahidi uwe miongoni mwa wema.

Kwenye maisha yako jitahidi kuwatendea watu wema, bila sababu, hujui nyuma ya tabasamu la mtu aliyekuja mbele yako kuna nini anapitia!

Kuna mtu mmoja alipataga kesi ya uhujumu uchumi, sikuwahi kuwa namjua, wala hakuwa rafiki yangu, na wala namba yake ya siku sikuwa nayo.

Nikaona mambo kwenye mitandao, nikafuatilia nikaona anaonewa tu, bila sababu. Nikaingilia kati kumtetea. Siyo kwa sababu yoyote ile, bali kwa kutamani kuona anatendewa haki.

Nilipoingia nikaambiwa ni maelekezo kutoka juu. Juu kuna Rais, Makamu wake na Waziri Mkuu. Nikapiga moyo konde nikamuendea hewani bwana mkubwa; akaniuliza swali moja tu “umehongwa shilingi ngapi?” Nikamuambia Mhe. Rais, utakuwa umeshauriwa vibaya, kama unaniamini mimi mshauri wako unisikilize nikupe taarifa yangu kisha utume watu wako wafuatilie, mimi hata huyu mtu simjui na wala sijawahi kuwasiliana naye hata mara moja! Akakata simu.

Baada ya muda kidogo ukweli ulifika mezani kwa bwana mkubwa, akanipigia akasema ulisema kweli. Umenifurahisha. Yule bwana alikuja akaachiwa. Akaja akajua ushiriki wangu kwenye jambo lake. Akanishukuru sana. Akataka kunipa chochote nilikataa. Tukawa marafiki.

Siku moja baadaye kabisa, hapo nishatoka kwenye serikali, napambana na miradi yangu, hali yangu ngumu, sina kitu, naingiza kontena za kiwanda changu akajua akaniita, basi akalipia nusu ya gharama zote za kontena zangu!

Hakujua ni kiasi gani nilikuwa hoi! Usiku nilitafakari sana jambo lile hadi machozi yalinitoka. Niliswali rakaa mbili kumshukuru MUNGU…#HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 4.

Kila kitu kitapita. Hata uwe unapitia kipindi kigumu namna gani, jua tu kipindi hicho kitapita. Kama upo kwenye raha namna gani, jua tu zitaisha. Hakuna kinachodumu milele chini ya jua. Kila kitu kitapita. Kuna miamba, majabbar anidi, ilipita! Iko wapi leo hii?

Basi, maneno haya yatoshe kutunyenyekeza, kutushusha na kutukumbusha kuwa watu wema zaidi ya wabaya.
Mimi Nina kanuni moja kwenye maisha yangu; kama ni kuonewa, basi acha nionewe mimi, lakini siyo mimi nionee mtu mwingine. Kama ni kudhulumiwa, acha nidhulumiwe mimi lakini siyo mimi kumdhulumu mtu. Huwa naamini wema ni akiba isiyooza lakini ubaya ni deni lisilofutika! Ubaya utakurudia tu.

Watu kama mimi huchukuliwa kama watu imara na wagumu kweli kweli, na wenye mamlaka makubwa sana, kwamba tunaweza kufanya lolote na kumfanya mtu chochote, lakini amini nakuambia binafsi nimeonewa na kudhulumiwa mara nyingi na wengine kuliko unavyoweza kudhania.

Kuna kijana wangu mmoja, na wapo wengi, sema ntatolea mfano huyu mmoja, aliwahi kunipiga parefu sana. Kwa mara ya kwanza nililia machozi ya uchungu sana mbele ya wanangu. Na mbele ya mama yangu, nikiwa mtu mzima!

Tumelima, tumejaza stock kwenye magodown yetu na ya kukodi. Tumetazama soko tukajua bei zitapanda, tukanunua na mzigo mwingine kwa wakulima wengine tukatunza. Kwamba tutauza baadaye bei zikipanda. Biashara ya mazao siyo rocket science, ukiwa na mtaji tu, ukatunza stock siku bei zikipanda unauza kwa faida unatengeneza pesa nzuri.

Kumbe dogo ananiambia amepata mzigo wa kutosha, natuma hela, kumbe ananunua kidogo, anamhonga store keeper, wanaweka rekodi sawa, dogo anakula hela. Uko zako mjini, busy na majukumu ya serikali, unajenga nchi! Simu inaita tena baada ya siku tatu, unaambiwa kuna mkulima mwingine mkubwa anauza mzigo wake, unapiga kadhaa, unakopa hela unasukuma kwenye stock!

Kumbe unanunua Moet, VSOP etc. Dogo anafunga bar, anaagiza slay queens kutoka Dar, anawapa bata la hatari!

Dogo umempa gari, Nissan Patrol, matrekta, combine harvesters na mashine zote, na mamlaka ya kusimamia kampuni yako, basi anatukana na kuchimba mkwara kila mtu kwa jina lako! Inaendelea…#HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 5.


Anaogopwa kuliko hata unavyoogopwa wewe mwenyewe! Hakuna anayekupa taarifa na wewe uko busy na ujenzi wa Taifa!
Kumbe Taifa lako binafsi la Kigwangalla Corporation linaangamia! 😭💔

Wakati wa kulima, dogo anakupa hesabu ya kulimia ekari 400, kumbe amelima ekari 300. Ekari zako 100 amewakodishia watu wengine wanalima, halafu wewe anakuletea hesabu za mahitaji ya ekari zote 400 wakati wote - kuanzia mbegu, mashine za kulimia, kuvuruga, vibarua wa kupanda, madawa, mbolea, palizi, kuvunia, usimamizi.

Mwishoni kule anakupa hadi na idadi ya gunia alizovuna na kutunza godown. Hesabu yake na hesabu ya store keeper ziko sawa.

Bei zinaanza kupanda, wewe unachekelea unajua huu ndiyo ule mwaka wangu wa kupiga hela ndefu, ntanunua na G Wagon yangu (my dream car), ntajenga na ile lodge yangu, na zile apartments zangu! 😀. Ntalipa na madeni yangu yote ya mikopo, nitaongeza uwekezaji wangu kwenye hisa na T-bonds! Kumbe maskini unajenga zako magorofa hewani! 😭😪💔 ushapigwa!

Mtu mmoja akaniambia amekutana na ‘mdogo wangu’, yule anaitwa Kigwangalla, anayesimamia miradi yangu ya mashamba alikuwa club na warembo (ni maarufu sitowataja majina!) akampa offer! Nikashtuka.

Nikamcheki dogo, nikamuambia nimepata salamu zake. Nikaona nimtume kijana mmoja wa ofisini kwangu Dar, na mke wangu, wakakague stock. Akasikia kuwa wanakuja. Akaanza mbinu na wenzake, eti wachome godown ili kupoteza ushahidi! 💔😭😩

Anayetoa hizo taarifa ni mdada mmoja ambaye alikuwa rafiki wa mwamba, kumbe alimsikia akiongea kuhusu madumu ya petrol kumwagwa usiku kwa akili sana ili kupoteza ushahidi. Kwamba, kwanza wangetoa mpunga zaidi kutoka godown, wabakishe kidogo, halafu kwa kuwa huwa tunamwaga pumba za mpunga kwenye sakafu, wakinyunyiza petrol kidogo tu moto utakuwa mkali sana kiasi kwamba hautoweza kuzimika, kila kitu kitateketea!

Huyo dada akasikia huruma sababu alijua wizi waliokwisha kunifanyia halafu wakichoma tena hicho kidogo, wachome na godown langu, na ndani humo Kuna mashine zangu zote - trekta kubwa3, stock ya mbolea, madawa… #HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 6.

…madawa ya mimea na combine harvester, itakuwa mbaya sana! Akamuambia ndugu yangu mmoja.

Ndugu akanitafuta toka asubuhi, wapi! Siku hiyo nilikuwa Ikulu kwenye cabinet, mule hamuingii na simu. Tumetoka, naingia kwenye gari, la kwanza kuwasha simu, nakutana na meseji Lukuki! Baada ya mimi kukosekana jamaa zangu waliamua kuripoti polisi, ulinzi ukawekwa!

Nilisikia kama nimechomwa kitu moyoni. Machozi yalinitoka bila kupigwa! Bila kutoa sauti. Sitokuja kusahau.

Nilifika nyumbani nikamkuta mama yangu sebuleni, niliangua kilio kama niliyefiwa na mtoto ama mzazi. Katika ukubwa wangu, nimewahi kufikwa na mambo mengi, lakini sijawahi kulia hata siku moja. Siku hii nililia bila kujali wanangu wanatazama wala nini. Mama yangu alinikumbatia kwa nguvu na kunituliza.

Nilijiuliza sana nimemkosea nini huyu dogo? Na wenzake? Mpaka leo sijawahi kupata majibu ya maswali yangu. Vijana wa kitanzania mna la kujifunza hapa. Huyu dogo na wenzake niliwapa gari ya kutembelea, mapikipiki, mashine ambazo wakimaliza kufanya kazi kwangu wanakodisha kwa wengine wanapata hela ya kula na matanuzi (ambayo mimi siichukui), kila kijana mmoja nalipia gharama ya kuanzia kumlimia na kumtunzia shamba lake; ekari 30 (huyo mkubwa wao), ekari 15 wale wasaidizi wake wawili. Kwenye ekari 15 unapata kati ya 30 - 40m kwa mwaka. Matukio ya hivi ni mengi kwenye story za wajasiriamali wengi hapa nchini.

Vijana wanadanganyika sana na maisha ya superstars, wanataka wayaishi bila jasho. Wengine wameishia kujidhalilisha na wengine wamefikia hata kushikishwa ukuta! Kama huna kipaji mdogo wangu, usitamani maisha ya wenye navyo. Fanya kazi kwa bidii, jipe muda wa kujitafuta, na wa kutafuta nafasi yako maishani. Ukifika utakula maisha yako ya halali kabisa.

Usikubali kuingia kwenye kundi la vijana wanaotafuta ajira lakini hawataki kufanya kazi. Wala usilikurubie kundi la vijana wanaotafuta ajira ili wakapige deal! Kila kijana anataka awekwe kitengo chenye ‘michongo’! Jamani nchi haijengwi namna hiyo. Hela haitafutwi namna hiyo. Nakuhakikishia, hela ya hivyo ukiipata haitokaa. Itakimbia tu.

Kama unahisi ‘nimefika mbali’ na unatamani…#HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIBA UBORA WAKE! Part 7.

Kama unahisi ‘nimefika mbali’ na unatamani kuwa kama mimi, basi nikuambie ukweli kuwa mimi najiona ‘Muomba Allah’ tu, sijafika popote na kiukweli hata hapa padogo nilipofikia, siyo kwa madili, dhulma, ubadhirifu na wala siyo kazi rahisi. Uwe tayari kutokwa machozi, jasho na damu!

Halafu; kwenye maisha yetu pesa, vitu, vyeo havileti furaha ya kweli, na wala havina thamani ya kweli. Vitu vyote vyenye thamani ya kweli kwenye maisha huwa havishikiki na havinunuliki. Usipoteze utu na imani yako kutafuta vitu vinavyoshikika.

Swali la ‘what did I do to deserve that?’ Halijawahi kunitoka. Usiulize huyu dogo mengine ya kijamii niliyowahi kumfanyia ni mangapi? Sema sipendagi kusema wema niliofanyia watu, Ila jua tu nilim-treat kwa heshima kupindukia, harusi yake niliwekeza na kuisimamia zaidi ya nilivyofanya kwa mdogo wangu niliyemuachia ziwa la mama!

Imagine rafiki zangu walivyojitoa, hata sijawahi kuwaambia dogo alivyoninyoosha! Dan La Kairo alitoa Range Rover yake mpya Autobiography kumpa dogo akajiendesha na mkewe! Miaka mitatu tu baadaye anataka kuchoma mali yangu! Dah! #HK #Fighter #NjeYaBox Iendelee ama tuishie hapa kwa sasa?


Kanipa somo zuri, ila mwanaume alii mbele ya watoto, Mama na Mke, hata kama anauliwa, Gambush blal glash.
 
Hapo sijaona tatizo la huyo kijana.
Tatizo halipo kwa vijana wa kitanzania.
Tatizo lipo kwa kigwangala. 100%

Mimi ni mjasiriamali pia.

Tatizo alikuwa anafanya biashara ya keyboard, unaletewa mahesabu mezani na unaweka pesa.

N:B nimetembelea wakulima wakubwa wa south africa,zambia,ukraine,dutch.

Mkulima ofisi yake ni shambani kwake anahandle kila kitu na ana accountant na kaajili. Sio hii upo mjini dar unatuma pesa kijijini wakulimie hujui miundombinu ya hapo matatizo ya day to day etc
 
Hata investor anayetuma pesa katika biashara hampi mtu pesa ,anaitoa katika proper and skilled management. Kama angekua ameajili :

1: Bwana shamba -2
2: farm meneja -1
3: accountant -1
4: Internal auditor -1
5: Sales/marketing executives- 5

So nafasi zote hizo kampa mtu mmoja na unamlaumu. Not fair angemuweka awe farm manager na angeajili hao wengine pia.
 
Nilikuwa nawaza kuandika uzi wa namna hii kutokana na changamoto na uzoefu niliokutana nao katika harakati za kutaka kutengeneza maisha bora KWa familia yangu na jamii KWa ujumla. Lakini kwakuwa bwana kigwa kaandika ujumbe umewapata wahusika...

Nakumbuka katika harakati za maisha kuna biashara nilianzishisha,, nikamuweka mdogo wangu.. aiseh SAsa sijui alichoka au hakuitaka... Aliharibu sana aiseh...! Kwakuwa ni ndugu nikaona nipotezee tu nimepata elimu fulani katika hilo... Haya kuna ndugu wa pembeni alikuja kunitembelea akaniambia e bana nitakaa wiki 2 tu! Nikasema haina shida njoo... Alivyo kuja siku hiyo nilikuwa nasimamia biashara yangu mwenyewe.. alivyo fika akaona hakuamini maana alikuwaga na dharau sana... SAsa sijui iliwasa tu moyoni kuwa ana hakikisha ananifilisi... E bwana eeh! Ile mdogo wangu alivyo maliza dharula yake nami nikawa naendelea na mengine jamaa KILA day anakwenda pale ofisini atashinda asubuhi hadi jioni na atafosi atumie bajeti ya ofisi... Nilikuwa sijui kuja kugundua ni siku napitia hesabu nikajua nikashangaa wewe inakuaje unatumia chakula gharama hii namuuliza SAsa yule mdogo wangu nilie mwachia... Tumboni una mapipa ya lita 200? Kanyamaza tu SAsa hadi vicha unaweka KWa kutumia pesa ya ofisi kwani sikupagi pesa? Kanyamaza tu.... Nilimindi sana nikaona nikwambia ukweli hunikomoi tu mimi hadi wewe unajikomoa bila kujua mambo maana hayatoniharibikia tu mimi... BAdo wewe na wadogo zako na wazazi wetu maana kidogo mimi nina kahaueni badala muwe na bidii na uaminifu mnasikiliza ndugu wengine we haya... Kwakuwa baada ya kupiga hesabu nikaona hapa hadi nifanye haki itakuwa tete tu labda nikope... Nikaona niipotezee tu ijifie taratibu... Nilivyo ipotezea yule jamaa nae akawa ana kazana kwenda halafu ikifika jioni anasikia naongea na simu kama nimepagawa nakaripia watu hovyo KWa sababu ya mishe nilizo wapa nikawaamini na zikafeli yeye kumbe akisikia vile ana furahi.. na KWa upande wa pili wa mdogo wangu alivyo ona nimeicha biashara ijifie nae baadhi ya mambo yakawa magumu akaona amwambie mama kuwa yule ndugu ndo kasabisha yeye tokea aje kutwa hapa anafosi matumizi yake yaingizwe kwenye bajeti ya ofisi... Mama akamjibu kwanini ulinyamaza hana majibu... Mama kanitonya... Ikabidi nimchane tu jamaa kuwa aondoke kwangu maana SAsa ni miezi 3 na ulisema wiki 2.... Daahh! Nilisikitika sana..

Kuna mwengine nae kaomba chombo ya moto KWa ajili ya biashara akasema mimi nitakupa faida.. fulani yule hawezi sijui anakusumbua... Haya Sawa chukua chombo hii... Mwezi umepita mtu kimya unamuuliza vipi chombo mbovu hii namuuliza KWa nini usiniambie? Hana majibu yanayo elewaka( Hapo kuna mtu ananiambia chombo inapiga Kazi vibaya mno) nikamwambia leo jioni ilete(huwa ananielewa nikongeaga kitu huwana nahakikisha nakitekeleza au kinatekelezwa)... Imefika jioni naona muamala... Nikampigia hii ndo jioni ilete chombo majibu yake SAsa! Oohhh! Najua kwako hii biashara kwahiyo mambo yasiwe magumu nimeazima nikutumie... Nikamwambia hiyo si mbovu SAsa unakaa nayo ya nini? Ilete nikipata pesa nitairekebisha, jibu lake ooh! Nitairekebisha.... Nikaona isiwe tabu kesho irekebishe... SAsa sijui ndo alienda kuharibu? Ila hesabu anatuma lakini kumbe sijui anamipango yake... Imefika wakiti ananipa taarifa chombo ipo KWa Fundi naenda KWa Fundi chombo haitamaniki... Na sijui walipanga na Fundi? Nikapiga hesabu ya vifaa original pesa niliyo toa na ni zaidi hata ya hesabu aliyonipa KWa siku zote... Naye Fundi kama ilivyo destri ya Vijana wengi wa kitanzania pia kafanya udhulmati wake (aliyo yafanya itoshe tu kusema sio Fundi mtengenezaji ni Fundi muharibifu). Nikaona ataniumiza kichwa pamoja na kuingia hasara nikaona nichukue siklepa langu maana lishakuwa siklepa kwanguvu nikaondoka nalo likae tu home maana linafanya Kazi badala linipe faida linanitia hasara tu...

Nakubaliana na baadhi ya wanajamvi humu somo la maadili muhimu... Kokote kwenye mikusanyiko lisemwe, na Katika familia lisemwe na kutendwa na pia liwekwe mashuleni kuanzia chekechea hadi university.......

Japan wamefanikiwa sana katika hilo.. somo la maadili lipo mashuleni... Kuna jamaa mmoja mbongo alikuwa anafundisha shule ya Kati huko nchini japani unaweza sema KWa bongo huku ni kama sekondari... Siku kuna Mwanafunzi alisahau kamera darasani ile kamera ilikaa wiki nzima pale pale hadi yule Mwanafunzi anafika darasa lile anaikuta vile vile..... Bongo SAsa hata uangushe bahasha iliyo tuna watu hata hawajui kuna nini watatembea nayo... Watafungulia hukohuko... Kama wakikuta makaratasi ambayo hayana faida kwao watayatupa bila kujali wewe uliye yaangusha unafaida nayo hata kama wanakujua...
 
Hata investor anayetuma pesa katika biashara hampi mtu pesa ,anaitoa katika proper and skilled management. Kama angekua ameajili :

1: Bwana shamba -2
2: farm meneja -1
3: accountant -1
4: Internal auditor -1
5: Sales/marketing executives- 5

So nafasi zote hizo kampa mtu mmoja na unamlaumu. Not fair angemuweka awe farm manager na angeajili hao wengine pia.
Unatafuta namna ya kumlaumu bwana kigwa... Mtu ndo anaanza SAsa hao watu atawalipaje na kasema kabisa ikifika kipindi anakopa.. pengine kapiga hesabu kaona hao wataalamu gharama yake tu ni tractors na skavetors kadhaa.... Be positive somtimes
 
Unatafuta namna ya kumlaumu bwana kigwa... Mtu ndo anaanza SAsa hao watu atawalipaje na kasema kabisa ikifika kipindi anakopa.. pengine kapiga hesabu kaona hao wataalamu gharama yake tu ni tractors na skavetors kadhaa.... Be positive somtimes
Ndio ukweli huo halisi nakuambia. Either uufuate ufanikiwe ama ubaki kulalamika.
Eg: crdb,nmb,tbl,tcc,nk kampuni hizo wanaofanya kazi ni vijana wazungu ama wajapani? No ni watanzania, ishu ni system hakuwa nayo. Kwa capital yake hakutakiwa kuwa mchuuzi. 100% blaming ni juu yake
 
Unatafuta namna ya kumlaumu bwana kigwa... Mtu ndo anaanza SAsa hao watu atawalipaje na kasema kabisa ikifika kipindi anakopa.. pengine kapiga hesabu kaona hao wataalamu gharama yake tu ni tractors na skavetors kadhaa.... Be positive somtimes
(, kila kijana mmoja nalipia gharama ya kuanzia kumlimia na kumtunzia shamba lake; ekari 30 (huyo mkubwa wao), ekari 15 wale wasaidizi wake wawili. Kwenye ekari 15 unapata kati ya 30 - 40m kwa mwaka. Matukio ya hivi ni mengi kwenye story za wajasiriamali wengi hapa nchini)

Kama ana uwezo wa kumlipia milioni 30-40 kwa msaidizi kwa mwaka, maana yake kwa watatu anatumia zaidi ya milioni 100.
Mwenye uwezo huo maana yake ana uwezo wa kuajiki professional (wataalamu wa kilimo,acxountant,sales and marketing)- 10 ,akawalipa take home laki 7 ambapo ni sawa na milioni 84 kwa mwaka na kazi yake ikaenda vizuri.
 
Leo asb Hamisi Kigwangalla ameliamsha tena huko Instagram suala la uaminifu wa watanzania. Amehadithia alichofanyiwa na kijana aliyemuamini. Huko nyuma amewahi kuuliza WHAT IS TANZANIA'S COMPETITIVE ADVANTAGE -Akimaanisha nini ambacho tunaweza kusema hichi kinatutambulisha kitaifa.

Juzi kati I-SOKO mfumo wa kuwezesha wanawake kufanya biashara afrika mashariki imeanzishwa. Kilichojiri malalamishi kwamba watanzania hatuaminiki.

Kihehe tunasema sema we have a people problem. Tatizo ni kubwa lakini tunaogopa kulijadili kwakuwa ni kaa la moto. Au halipo


SOMA KISA HIKI KUTOKA KWA hamis Kigwangalla

NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 1:


Kama ukiona elimu ni gharama, ujue haujajaribu ujinga. Vile vile, kama ukiona kutafuta utajiri ni kazi, hebu jaribu umaskini uone.

Hakuna kitu kibaya kwenye maisha kama umaskini. Tuliouishi umaskini tunaujua. Tukipambana nao kwa kila hali msitushangae. Mara kadhaa tushawahi kurudi nyumbani for lunch na kukuta hakuna kilichopikwa tukaishia kunywa maji na kugeuza shule, maana hata wa kumuuliza chakula kiko wapi hayupo home.

Kutajirika ni katika vitu vigumu kabisa kufanya hapa duniani. Niliwahi kujaribu kutafuta utajiri sikuufikia, nikaishia hapa nilipo! Lakini bado napambana. Si haba, WALLAH sina malalamiko yoyote yale kwa Allah, zaidi zaidi narejesha shukrani tele. Nilipotoka napajua mwenyewe.

Kwenye safari ya kutafuta maisha, kwa kuwa nilikuwa na mbio ndefu na za spidi sana, nimejifunza mengi sana. Huwa najaribu kuandika andika hapa, wenye muda husoma na pengine hujifunza.

Niliwahi kuwa nalima ekari 500 - 600 kwa msimu, nikamuamini kijana wangu mmoja mahiri, mchapakazi, mwenye dini kweli kweli, mwenye elimu na passion ya farming; pamoja na kunifaidisha na kunipa tamaa ya kuwekeza zaidi, alinipiga kweli kweli!

Nikaamini wadogo zangu damu kabisa, wakanipiga. Nikazama. [emoji30]!

Mtaji wa zaidi ya ekari 700 ukaporomoka mpaka ekari 100/200. Wakati unaporomoka, unadaiwa na benki ulipe mkopo wa mtaji uliochukua, unadaiwa na kampuni waliokukopesha matrekta, combine harvesters, planters, unadaiwa na suppliers wa pembejeo etc. Inaendelea…


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE. Part 2!

Wakati huo huo umeshushwa cheo na unaambiwa ukajibu hoja kwa CAG za dhambi ambazo hazikuhusu. Faida moja ya cheo ni kuwa kuna mikopo bankers wanakupa kwa kukuamini tu, tena kwa simu tu. Siku kikiondoka, wadai wote wanaanza kuhaha kukudai kama hawakujui vile. Wakubwa wote hawapokei simu zako. Unabaki peke yako kama siyo wewe vile. Marafiki waliokuwa wanakusalimia kila kukicha hawapokei simu zako wala hawajibu meseji zako.

Ukiwa na roho ndogo utasema umerogwa ama utaugua ugonjwa wa akili. Ama hata utaona maisha hayana maana tena.

Wakati unajaribu kutoka, bei za mazao zinaporomoka! Vita ya Ukraine inaanza na COVID inapandisha bei za mbolea etc.

Mwaka huu bei za mazao nzuri, wanatokea kwelea kwelea [emoji3].

Ili kusimama kwenye maisha, muombe sana Mungu akupunguzie masomo magumu ya kupitia, aidha usihangaike sana kuimarisha misuli ya mwili ili ukivaa suti upendeze, imarisha misuli ya moyo, ubongo na roho(kama nayo ina muscles![emoji3]) ili uweze kukabiliana na nyakati za maanguko. Siku zote jua tu kwamba, baada ya maanguko kadhaa, na kama utaweza kuinuka kila unapoanguka, na kustahimili maumivu ya kila anguko, mwangaza huja na Mungu humuinua mja wake! (Graduation hiyo sasa!)

Maisha ni Marathon. Kutajirika siyo rahisi. Lakini kwani nani alisema umaskini ni raha?

Iendelee ama iishie hapa?


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 3.

Ukitenda wema, tenda kwa watu wengi sana, muhimu ni kuwa usingoje shukran. Kwa hakika wema, ni akiba isiyooza.

Pamoja na uwepo wa watu wengi wa hovyo kwenye maisha yetu, watu ambao hawawezi kukufanyia jambo jema, zaidi zaidi wanajipanga kukuangusha na kukudhuru kila kukicha, tena hawana sababu yoyote ile, huwa wapo watu wachache wema, pengine uliwahi kuwatendea wema basi wanakumbuka ama ni watu wenye tabia ya kupenda kutenda wema tu. Wapo!

Wabaya wengi wapo lakini wema wachache pia wapo. Jitahidi uwe miongoni mwa wema.

Kwenye maisha yako jitahidi kuwatendea watu wema, bila sababu, hujui nyuma ya tabasamu la mtu aliyekuja mbele yako kuna nini anapitia!

Kuna mtu mmoja alipataga kesi ya uhujumu uchumi, sikuwahi kuwa namjua, wala hakuwa rafiki yangu, na wala namba yake ya siku sikuwa nayo.

Nikaona mambo kwenye mitandao, nikafuatilia nikaona anaonewa tu, bila sababu. Nikaingilia kati kumtetea. Siyo kwa sababu yoyote ile, bali kwa kutamani kuona anatendewa haki.

Nilipoingia nikaambiwa ni maelekezo kutoka juu. Juu kuna Rais, Makamu wake na Waziri Mkuu. Nikapiga moyo konde nikamuendea hewani bwana mkubwa; akaniuliza swali moja tu “umehongwa shilingi ngapi?” Nikamuambia Mhe. Rais, utakuwa umeshauriwa vibaya, kama unaniamini mimi mshauri wako unisikilize nikupe taarifa yangu kisha utume watu wako wafuatilie, mimi hata huyu mtu simjui na wala sijawahi kuwasiliana naye hata mara moja! Akakata simu.

Baada ya muda kidogo ukweli ulifika mezani kwa bwana mkubwa, akanipigia akasema ulisema kweli. Umenifurahisha. Yule bwana alikuja akaachiwa. Akaja akajua ushiriki wangu kwenye jambo lake. Akanishukuru sana. Akataka kunipa chochote nilikataa. Tukawa marafiki.

Siku moja baadaye kabisa, hapo nishatoka kwenye serikali, napambana na miradi yangu, hali yangu ngumu, sina kitu, naingiza kontena za kiwanda changu akajua akaniita, basi akalipia nusu ya gharama zote za kontena zangu!

Hakujua ni kiasi gani nilikuwa hoi! Usiku nilitafakari sana jambo lile hadi machozi yalinitoka. Niliswali rakaa mbili kumshukuru MUNGU…#HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 4.

Kila kitu kitapita. Hata uwe unapitia kipindi kigumu namna gani, jua tu kipindi hicho kitapita. Kama upo kwenye raha namna gani, jua tu zitaisha. Hakuna kinachodumu milele chini ya jua. Kila kitu kitapita. Kuna miamba, majabbar anidi, ilipita! Iko wapi leo hii?

Basi, maneno haya yatoshe kutunyenyekeza, kutushusha na kutukumbusha kuwa watu wema zaidi ya wabaya.
Mimi Nina kanuni moja kwenye maisha yangu; kama ni kuonewa, basi acha nionewe mimi, lakini siyo mimi nionee mtu mwingine. Kama ni kudhulumiwa, acha nidhulumiwe mimi lakini siyo mimi kumdhulumu mtu. Huwa naamini wema ni akiba isiyooza lakini ubaya ni deni lisilofutika! Ubaya utakurudia tu.

Watu kama mimi huchukuliwa kama watu imara na wagumu kweli kweli, na wenye mamlaka makubwa sana, kwamba tunaweza kufanya lolote na kumfanya mtu chochote, lakini amini nakuambia binafsi nimeonewa na kudhulumiwa mara nyingi na wengine kuliko unavyoweza kudhania.

Kuna kijana wangu mmoja, na wapo wengi, sema ntatolea mfano huyu mmoja, aliwahi kunipiga parefu sana. Kwa mara ya kwanza nililia machozi ya uchungu sana mbele ya wanangu. Na mbele ya mama yangu, nikiwa mtu mzima!

Tumelima, tumejaza stock kwenye magodown yetu na ya kukodi. Tumetazama soko tukajua bei zitapanda, tukanunua na mzigo mwingine kwa wakulima wengine tukatunza. Kwamba tutauza baadaye bei zikipanda. Biashara ya mazao siyo rocket science, ukiwa na mtaji tu, ukatunza stock siku bei zikipanda unauza kwa faida unatengeneza pesa nzuri.

Kumbe dogo ananiambia amepata mzigo wa kutosha, natuma hela, kumbe ananunua kidogo, anamhonga store keeper, wanaweka rekodi sawa, dogo anakula hela. Uko zako mjini, busy na majukumu ya serikali, unajenga nchi! Simu inaita tena baada ya siku tatu, unaambiwa kuna mkulima mwingine mkubwa anauza mzigo wake, unapiga kadhaa, unakopa hela unasukuma kwenye stock!

Kumbe unanunua Moet, VSOP etc. Dogo anafunga bar, anaagiza slay queens kutoka Dar, anawapa bata la hatari!

Dogo umempa gari, Nissan Patrol, matrekta, combine harvesters na mashine zote, na mamlaka ya kusimamia kampuni yako, basi anatukana na kuchimba mkwara kila mtu kwa jina lako! Inaendelea…#HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 5.


Anaogopwa kuliko hata unavyoogopwa wewe mwenyewe! Hakuna anayekupa taarifa na wewe uko busy na ujenzi wa Taifa!
Kumbe Taifa lako binafsi la Kigwangalla Corporation linaangamia! [emoji24][emoji174]

Wakati wa kulima, dogo anakupa hesabu ya kulimia ekari 400, kumbe amelima ekari 300. Ekari zako 100 amewakodishia watu wengine wanalima, halafu wewe anakuletea hesabu za mahitaji ya ekari zote 400 wakati wote - kuanzia mbegu, mashine za kulimia, kuvuruga, vibarua wa kupanda, madawa, mbolea, palizi, kuvunia, usimamizi.

Mwishoni kule anakupa hadi na idadi ya gunia alizovuna na kutunza godown. Hesabu yake na hesabu ya store keeper ziko sawa.

Bei zinaanza kupanda, wewe unachekelea unajua huu ndiyo ule mwaka wangu wa kupiga hela ndefu, ntanunua na G Wagon yangu (my dream car), ntajenga na ile lodge yangu, na zile apartments zangu! [emoji3]. Ntalipa na madeni yangu yote ya mikopo, nitaongeza uwekezaji wangu kwenye hisa na T-bonds! Kumbe maskini unajenga zako magorofa hewani! [emoji24][emoji25][emoji174] ushapigwa!

Mtu mmoja akaniambia amekutana na ‘mdogo wangu’, yule anaitwa Kigwangalla, anayesimamia miradi yangu ya mashamba alikuwa club na warembo (ni maarufu sitowataja majina!) akampa offer! Nikashtuka.

Nikamcheki dogo, nikamuambia nimepata salamu zake. Nikaona nimtume kijana mmoja wa ofisini kwangu Dar, na mke wangu, wakakague stock. Akasikia kuwa wanakuja. Akaanza mbinu na wenzake, eti wachome godown ili kupoteza ushahidi! [emoji174][emoji24][emoji30]

Anayetoa hizo taarifa ni mdada mmoja ambaye alikuwa rafiki wa mwamba, kumbe alimsikia akiongea kuhusu madumu ya petrol kumwagwa usiku kwa akili sana ili kupoteza ushahidi. Kwamba, kwanza wangetoa mpunga zaidi kutoka godown, wabakishe kidogo, halafu kwa kuwa huwa tunamwaga pumba za mpunga kwenye sakafu, wakinyunyiza petrol kidogo tu moto utakuwa mkali sana kiasi kwamba hautoweza kuzimika, kila kitu kitateketea!

Huyo dada akasikia huruma sababu alijua wizi waliokwisha kunifanyia halafu wakichoma tena hicho kidogo, wachome na godown langu, na ndani humo Kuna mashine zangu zote - trekta kubwa3, stock ya mbolea, madawa… #HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIKA UBORA WAKE! Part 6.

…madawa ya mimea na combine harvester, itakuwa mbaya sana! Akamuambia ndugu yangu mmoja.

Ndugu akanitafuta toka asubuhi, wapi! Siku hiyo nilikuwa Ikulu kwenye cabinet, mule hamuingii na simu. Tumetoka, naingia kwenye gari, la kwanza kuwasha simu, nakutana na meseji Lukuki! Baada ya mimi kukosekana jamaa zangu waliamua kuripoti polisi, ulinzi ukawekwa!

Nilisikia kama nimechomwa kitu moyoni. Machozi yalinitoka bila kupigwa! Bila kutoa sauti. Sitokuja kusahau.

Nilifika nyumbani nikamkuta mama yangu sebuleni, niliangua kilio kama niliyefiwa na mtoto ama mzazi. Katika ukubwa wangu, nimewahi kufikwa na mambo mengi, lakini sijawahi kulia hata siku moja. Siku hii nililia bila kujali wanangu wanatazama wala nini. Mama yangu alinikumbatia kwa nguvu na kunituliza.

Nilijiuliza sana nimemkosea nini huyu dogo? Na wenzake? Mpaka leo sijawahi kupata majibu ya maswali yangu. Vijana wa kitanzania mna la kujifunza hapa. Huyu dogo na wenzake niliwapa gari ya kutembelea, mapikipiki, mashine ambazo wakimaliza kufanya kazi kwangu wanakodisha kwa wengine wanapata hela ya kula na matanuzi (ambayo mimi siichukui), kila kijana mmoja nalipia gharama ya kuanzia kumlimia na kumtunzia shamba lake; ekari 30 (huyo mkubwa wao), ekari 15 wale wasaidizi wake wawili. Kwenye ekari 15 unapata kati ya 30 - 40m kwa mwaka. Matukio ya hivi ni mengi kwenye story za wajasiriamali wengi hapa nchini.

Vijana wanadanganyika sana na maisha ya superstars, wanataka wayaishi bila jasho. Wengine wameishia kujidhalilisha na wengine wamefikia hata kushikishwa ukuta! Kama huna kipaji mdogo wangu, usitamani maisha ya wenye navyo. Fanya kazi kwa bidii, jipe muda wa kujitafuta, na wa kutafuta nafasi yako maishani. Ukifika utakula maisha yako ya halali kabisa.

Usikubali kuingia kwenye kundi la vijana wanaotafuta ajira lakini hawataki kufanya kazi. Wala usilikurubie kundi la vijana wanaotafuta ajira ili wakapige deal! Kila kijana anataka awekwe kitengo chenye ‘michongo’! Jamani nchi haijengwi namna hiyo. Hela haitafutwi namna hiyo. Nakuhakikishia, hela ya hivyo ukiipata haitokaa. Itakimbia tu.

Kama unahisi ‘nimefika mbali’ na unatamani…#HK #Fighter #NjeYaBox


NJE YA BOX: MAISHA KATIBA UBORA WAKE! Part 7.

Kama unahisi ‘nimefika mbali’ na unatamani kuwa kama mimi, basi nikuambie ukweli kuwa mimi najiona ‘Muomba Allah’ tu, sijafika popote na kiukweli hata hapa padogo nilipofikia, siyo kwa madili, dhulma, ubadhirifu na wala siyo kazi rahisi. Uwe tayari kutokwa machozi, jasho na damu!

Halafu; kwenye maisha yetu pesa, vitu, vyeo havileti furaha ya kweli, na wala havina thamani ya kweli. Vitu vyote vyenye thamani ya kweli kwenye maisha huwa havishikiki na havinunuliki. Usipoteze utu na imani yako kutafuta vitu vinavyoshikika.

Swali la ‘what did I do to deserve that?’ Halijawahi kunitoka. Usiulize huyu dogo mengine ya kijamii niliyowahi kumfanyia ni mangapi? Sema sipendagi kusema wema niliofanyia watu, Ila jua tu nilim-treat kwa heshima kupindukia, harusi yake niliwekeza na kuisimamia zaidi ya nilivyofanya kwa mdogo wangu niliyemuachia ziwa la mama!

Imagine rafiki zangu walivyojitoa, hata sijawahi kuwaambia dogo alivyoninyoosha! Dan La Kairo alitoa Range Rover yake mpya Autobiography kumpa dogo akajiendesha na mkewe! Miaka mitatu tu baadaye anataka kuchoma mali yangu! Dah! #HK #Fighter #NjeYaBox Iendelee ama tuishie hapa kwa sasa?
Imani za dini zinatupumbaza mno watanzania. Mno. Wewe mtu anakutendea uovu huo, unamwacha. Ni dhambi kwa sababu unapomwacha hujamsaidia. Mhalifu ni mhalifu tuu, peleka kwenye vyombo vya sheria aadhibiwe, akirudi mpokee. Atakuwa GM mzuri kabisa maana amefundishwa huko maana ya kufanyakazi na uadilifu. Watanzania wengi wanadhani kumfunga mtu jela ni dhambi. Hamna. Gereza ni vyombo vya Mungu pia kuifanya dunia mahala pa amani. Ona sasa, mtu anafikia hatua ya kutaka kuteketeza mali za mamia ya mamilioni! Kweli? Huyo anakuua pia, tena mchana kweupee!
Nina mtoto alijifanya ameshindikana; Peleka shule, tena hizi za gharama, wapi! Geuza na kugeuza, wapi! Wananchi wakanishauri kuwa nisimlazimishe hataki shule, kwani wote lazima wasomee? Nikawaelewa. Nikampeleka kusomea udereva, nikampatia motokaa, akashirikiana na mafundi anaiba vipuri, gari mwisho wa siku likakaa juu ya mawe. Navumilia ila moyo unaniuma kwelikweli. Akakwiba kwa mtu akafungwa, Nikamtoa. Si unajua Bongo ukiwa na "kitu kidogo" hakuna jambo gumu. Nikamweka dukani, akapora. Aah, akili zikanirudi. Utu wangu ukanirudia. Utu wa ndani kabisa. Nikahisi kuwa na hatia kwa kuendelea kumdekeza wakati Serikali imeajiri vyombo vyenye vijana wasomi waliosomeshwa hadi shahada juu ya kurekebisha tabia za watu. Nikampeleka gerezani. Mapolisi, mahakimu, maafisa magereza walinipongeza sana, walisema, Bongo tungekuwa na wazazi kama wewe tungetengeneza kizazi cha vijana kilicho bora bora kabisa. Kijana alifundishwa adabu kule. Watu wamesomea mambo haya bwana. Tena alikaa miezi mitatu tu. Aliporudi sikuamini. Jambo la kwanza alitubu kwa machozi mengi Nimsamehe. Nilimsamehe. Ni mtoto, kama mzazi sikuwa namwadhibu ili ateseke bali a-reform. Baada ya hapo Akaokoka. Aliomba shamba, nikampatia na vitendeakazi vyote. To cut story short, sasa hivi ni kijana mzuri, mzuri mno na ndiyo tegemeo langu.
Mhe: Kigwangala, ulikosea kijana huyo ulitakiwa kumpeleka jela. Ange-reform na kuwa chombo chenye kufaa. Kwa kumwacha ataendeleza ujinga wake. Polisi, mahakama, na gereza, vipo kwa ajili ya watu kama hao, ukimwacha atakufa ktk dhambi zake na akifa anakwenda Jehanamu. Damu yake mwenyezi Mungu ataitaka mikononi mwako mhe. Kigwangala.
Over.
 
Ukileta emotion ama undugu katika biashara basi hutoboi.
Biashara ina rules zake. Ni either ufanye 100% ama achana nayo.
Wananifata wengi ambao wameajiliwa nachowashauri msiingie ktk biashara sababu kuna vitu vingi sana underground. Nawashauri wajenge nyumba za kupangisha kama hawana akili nzuri zitawalipa in the long run.
 
Huyo dogo aliemliza kigwangala aka kigwafix anaitwa

TOMMY
Ukipita usangu mbarali wanamjua sana
Alikuwa anatembelea nissan patrol
Anapiga bata za hatari
Tumewahi zinguana pale DS makambako
Afu anajifanya mdg ake kigwangala

Alikuwa anaonea wanyonge sana
Mara apore mademu zao
Ila sisi tulimkokesha

Sijui kwa sasa kapotea wapi

Oyaa, Tommy km unasoma huu Uzi
Wambie wadau kilichokukuta pale DS hotel mpk ukakimbia ukaacha gari

Dadeeki
Tom alikuwa mjinga sana alipora mke wa mtu pale chimala anaitwa d akawa anatanua naye
Baada ya kigwa kumfunga pale gereza la uhamila na kutoka,akaja mbeya life likampiga amechoka yupo mwanza,huko
Tom alichezea tshs chooni

Sent from my SM-N960U using JamiiForums mobile app
 
Tom alikuwa mjinga sana alipora mke wa mtu pale chimala anaitwa d akawa anatanua naye
Baada ya kigwa kumfunga pale gereza la uhamila na kutoka,akaja mbeya life likampiga amechoka yupo mwanza,huko
Tom alichezea tshs chooni

Sent from my SM-N960U using JamiiForums mobile app
Anafanya shughuli gani nowdays

Yule dogo kigwangala ilitakiwa akaze kamba ampige gerezan hata miaka 10
ili aisome namba
 
Back
Top Bottom