Ancestral Curse: Ujerumani iliwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6, lakini ndio nchi yenye nguvu zaidi Ulaya. Je, hii dhana ya laana ya asili ipo sahihi?

Ancestral Curse: Ujerumani iliwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6, lakini ndio nchi yenye nguvu zaidi Ulaya. Je, hii dhana ya laana ya asili ipo sahihi?

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Ndugu zangu watanzania;

Ujerumani iliwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6, lakini ndio nchi yenye uchumi mkubwa zaidi barani Ulaya (European Powerhouse).

Kwanini wao hawajatafunwa na laana hii ya asili kutoka kwa babu zao? Je, hii dhana ya laana ya asili (Ancestral/Generational Curse) ipo sahihi kweli?

Kama ipo sahihi, kwanini iwepo Afrika tu na sio Ulaya?


Laana ya Asili kama inavyofafanulia na Mtumishi Joel Osteen (American Preacher & Televangelist)
=============
Laana ya vizazi inaaminika kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa sababu ya uasi dhidi ya Mungu. Ikiwa ukoo wako umepewa laana ya talaka, uchumba, umaskini, hasira au mifumo mingine isiyo ya kimungu, unaweza kuwa chini ya laana ya ukoo.

Familia zetu zina ushawishi mkubwa juu ya maendeleo yetu, pamoja na ukuzaji wa mifumo yetu ya dhambi. Watu wengine wanadai kwamba laana za kifamilia au kizazi hupitishwa kwa njia ya kizazi.

Imani hii inatokana na vifungu vya Agano la Kale ambavyo vinasema kwamba Mungu "huwaadhibu watoto na watoto wao kwa dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne" (Kutoka 34: 7).

Ikiwa familia zinarithi laana za kiroho au la, ni dhahiri kwamba mifumo ya dhambi hupitishwa kupitia familia. Kila mtu hutenda dhambi; lakini kama vile utamaduni, kabila, na jinsia zinavyoongoza mwelekeo wetu wa dhambi katika mwelekeo fulani, ndivyo pia familia zetu.

Tunarithi tabia nyingi na mapenzi ya kitu fulani kutoka kwa wazazi wetu ambao sio ushawishi mzuri kwetu au kwa wengine. Tunapopata tabia ya imani au imani ambayo inaathiri vibaya maisha yetu au wale wanaotuzunguka, hii inajulikana kama laana ya kizazi. Ni upande uliojificha wa tabia uliopitishwa kupitia vizazi.

KIINGEREZA KIDOGO: Many Africans, Christian or not, live in fear of generational curses. When misfortunes hit, they want to know who might have bewitched them.

Non-Christians may turn to the witchdoctor while believers seek a deliverance minister to diagnose their problem and prescribe necessary spiritual steps forward. But why is this so?

HISTORIA NDOGO YA MAUAJI YA WAYAHUDI BARANI ULAYA (HOLOCAUST)
==========
Holocaust, yalikuwa ni mauaji ya halaiki ya Vita vya pili vya dunia kwa Wayahudi wa Ulaya. Kati ya mwaka 1941 na mwaka 1945, Ulaya nzima ambayo ilikuwa inakaliwa na Wajerumani, Ujerumani ya wa Nazi na washirika wake waliwaua Wayahudi wapatao milioni sita, karibu theluthi mbili ya idadi ya Wayahudi wote wa ulaya kwa wakati ule.

Mauaji hayo yalifanywa kwa watu wengi kwa njia za upigaji wa risasi kwa halaiki ya watu;sera ya mauaji ya kutokomeza watu kupitia kazi katika kambi za mateso; na katika vyumba vya gesi na gari za gesi katika kambi za kuangamiza za Wajerumani, haswa Auschwitz, Belzec, Chelmno, Majdanek, Sobibór, na Treblinka katika Poland iliyokaliwa na Wajerumani.

UCHUMI WA UJERUMANI KWA UFUPI
=============
Pamoja na Pato la Taifa la zaidi ya Euro trilioni 3.4, uchumi wa Ujerumani ulikuwa mkubwa zaidi barani Ulaya mnamo mwaka 2019. Chumi zenye ukubwa sawa za Uingereza na Ufaransa zilikuwa chumi za pili na wa tatu kwa ukubwa barani Ulaya wakati wa mwaka jana, ikifuatiwa na Italia na Uhispania.

Uchumi mdogo kabisa katika takwimu hii ni ule wa taifa dogo la Balkan la Montenegro, ambalo lilikuwa na Pato la Taifa la Euro bilioni 4.66 tu, karibu mara 74 ndogo kuliko uchumi wa Ujerumani.

Uchumi wa Ujerumani umekuwa ndio uchumi mkubwa zaidi barani Ulaya tangu mmwaka 1980, hata kabla ya kuungana tena kwa Ujerumani Magharibi na Mashariki. Uingereza, kwa kulinganisha, imekuwa na bahati wakati huo huo na ilikuwa na uchumi mdogo kuliko Italia mwishoni mwa miaka ya 1980.

Uingereza pia ilipata mapigo makubwa zaidi ya chumi zingine kubwa wakati wa anguko la uchumi wa mwishoni mwa miaka ya 2000, ikimaanisha uchumi wa Ufaransa ulikuwa wa pili kwa ukubwa barani kwa muda baadaye. Uchumi wa Uhispania ulikuwa wa tano kwa ukubwa Ulaya katika kipindi hiki cha miaka 38, na kutoka 2004 kuendelea umekuwa na thamani ya zaidi ya Euro trilioni moja.

Tazama takwimu kutoka chanzo sahihi hapo chini.

View attachment 1559175

Kwanini Ujerumani haijawahi kutafunwa na laana hii ya asili ya babu zao licha ya kuwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6 badala yake inazidi kuneemeka kiuchumi?

Mpaka Engineers bora wapo kwao>>> Kwanini wahandisi wazuri sana duniani (Magari, Mitambo) wanapatikana nchini Ujerumani? Siri yao ni ipi hasa?

Je, dhana hii ya laana ya asili ipo sahihi kweli?

ANGALIZO: Hii mada haizungumzii Wayahudi kama taifa teule la Mungu bali inazungumzia roho za binadamu wa asili ya Uyahudi. It's all about humanity and not ethnicity.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Nitatoa jibu langu kutoka kwenye perspective ya Biblia Takatifu. Ulimwengu wa roho una kitu kinaitwa madai ambayo lazima yalipwe ili hali fulani mbaya inayokabili mtu/ ukoo/ kabila/ nchi itulie. Sio kila uovu unatoka kwa kukemewa kwa jina au damu ya Yesu.

Kwa mfano kama ukoo wenu ulikuwa na miungu yake na mkaiacha kienyeji bila utaratibu sahihi wa kiroho kufuatwa, hiyo miungu ya ukoo itainua madai kwenye ulimwengu wa roho dhidi ya wanaukoo huo na madai hayo ni sahihi katika muktadha wa kiroho. Ikumbukwe kuwa ancestors wa ukoo huo walijikabidhi kwa hiari kwa miungu hiyo, hali ambayo iliunda agano halali la kiroho katika ulimwengu wa roho. Kwahiyo, ili kujiachanisha na miungu hiyo, kuna utaratibu wa kiroho lazima uufuate kwa usahihi kabisa, na ukikosea hata kama wewe ni mlokole kindakindaki, huwezi kujitoa katika vifungo au laana za miungu hiyo. Lazima uingie deep kwenye ulimwengu wa roho ujue tatizo lilipo ili ujue sehemu sahihi ya kupeleka damu ya Yesu kwa ajili ya kulipa fidia ya kukukomboa (ransom) kutoka kwa miungu hiyo na laana zote.

Kwenye agano la kale, wayahudi ndio taifa pekee ambalo lilikuwa na agano na Mungu wa mbinguni, agano ambalo lilikuwa na kifungo cha kiroho tangu Ibrahimu. Kila wakati walipomwasi Mungu walipata adhabu kali kwa kulivunja agano lao na Mungu. Mfano Mungu aliwauza wayahudi kwa falme za Babeli, Uajemi, na Rumi walipomwasi Mungu.

Hii vita ya kiroho ya maagano ya kimungu iko very perfectly principled, bila kujali wazee wako walikuwa wakimuabu mungu yupi! Hoja ya msingi ni kwamba lazima agano lolote la kimungu cha shetani livunjwe kwa utaratibu sahihi wa kiroho na kulipa fidia sahihi kwa miungu unayotaka kuachana nayo kabla ya kuambatana na Mungu wa mbinguni. Walokole wengi wameshindwa kutegua huu mtego wa shetani, kwani wengi wao wanadhani kila roho ya shetani inatolewa kwa kukemewa kwa jina la Yesu, kumbe roho nyingine zinatolewa kwa kulipwa fidia kwanza.

Sasa tuje kwa Germany. Kama unasoma historia vizuri na kwa umakini, utagundua kwamba vita kuu ya pili ya dunia ambayo wajerumani waliianzisha, imechochewa na mambo makuu matatu.

Moja, ni dhuluma waliyofanyiwa na Uingereza na washirika wake wakati wa vita vya kwanza vya dunia, ambapo Ujerumani alilazimika kupigana ili kulinda maslahi yake Ulaya na duniani baada ya kupata mbinyo mkubwa kutoka Uingereza. Uingereza alikuwa na hofu kwamba masive expansion ya Germany ilikuwa inahatarisha usitawi wa maslahi yake duniani. Kwahiyo, ikabidi ianzishwe conspiracy ya kumdhibiti Germany mapema. Ndiyo vita ya kwanza ya dunia ikaanza, ambapo Germany alishindwa na kunyang'anywa makoloni yake yote, ikiwemo Tanganyika, Rwanda na Burundi. Kwahiyo, Germany ni kama alikatwa miguu yote miwili, kwahiyo ilibidi lazima apigane ili arudi kwenye chati tena.

Pili, Wajerumani walikuwa na chuki na wayahudi kwani walikuwa wamehodhi uchumi wao kwa kiasi kikubwa. Mbaya zaidi, wayahudi ni wabinafsi kwa asili yao, hali iliyowafanya wayahudi wajione watumwa ndani ya nchi yao. Kwahiyo, Hitler alikuwa na ndoto kubwa kuwashughulukia jews for that reason. Hata mauaji ya kimbari ya wayahudi wakati wa second world war, yalichochewa na chuki hii ya wajerumani kwa wayahudi.

Tatu, Hitler na genge lake waliwaaminisha wajerumani kwamba wao ni super race duniani, kwahiyo, wao wanapaswa kutawala na sio kutawaliwa na yeyote yule duniani. Huu ulaghai wa Hitler ndio ulimfanya Hitler na genge lake wawe na adhma ya kutaka kuitawala dunia wakati wa vita vya pili vya dunia.

Aidha, baada ya vita vya pili vya dunia, Germany alishindwa tena, na kupewa adhabu kali sana na mataifa washirika waliokuwa upande wa ushindi yaani USA, USSR, Uingereza na Ufaransa. Kwanza miundombinu yake yote ya viwandani ilikuwa sehemu ya vitu vilivyoporwa na mataifa hayo baada ya vita. Vilevile, wanasayansi wabobezi wa Ujerumani katika nyanja zote walichukuliwa mateka na mataifa yaliyoshinda vita. Ikumbukwe kuwa technology ya Ujerumani katika mambo kama silaha, ndege za kivita, U-Boats ili kuzamisha meli na nyambizi za Uingereza, na techhnology za uzalishsji mali kama viwanda zilikuwa tayari ziko juu sana kwa quality kipindi hicho. Pia Ujerumani iligawanywa vipande viwili: East Germany na West Germany, na kuasisi vita mpya ya dunia iitwayo Cold War. Vilevile, Ujerumani alilazimishwa kulipa fidia kwa nchi zote ambazo zilikuwa wahanga wa vita aliyoianzisha.

Ukisoma Daniel sura ya 9 na Maombolezo 5:7, utaona uovu na dhambi lazima vilipiwe ili kukomesha laana. Kwa kutazama adhabu alizopewa Ujerumani baada ya WW2, ni dhahiri kabisa kwamba alilipia uovu wake wote kwa zile adhabu alizopewa na mataifa washindi. Ukiisoma torati ya Musa utaona kwamba torati iliamuru kwamba aliyeua lazima naye auawe ili nchi isiinue uovu na laana. Ingawa sheria hii Yesu alikuja kuiondoa na badala akaleta sheria mpya ya rehema, toba, na kusameheana kupitia Agano Jipya la Kuokolewa kwa neema kupitia kwa Damu ya Yesu. Sina ushahidi wa dhahiri kwamba Wajerumani walitubia uovu wao wa WW2. Ila nnachojua ni kwamba waliadhibiwa sana kwa kusababisha vita ile.

Kwahiyo, kwa sheria ya kiroho, ni vigumu mno kuamini kwamba Ujerumani alipaswa kupata laana zaidi ya hizo adhabu alizopewa na nchi zilizoshinda vita, kwani hata mateka wao wa vita wengi wao waliishia kuuawawa na kuzikwa ugenini bila hata ndugu kujua marehemu wao walipo.

Mchumi mashuhuri wa Uingereza, John Maynard Keynes, alivyo-review paper inayohusu financial reparation ambazo Germany alipaswa kulipa kama fidia, aliikataa kabisa hiyo paper kwani ilikuwa haiwezekani katika parameter za kiuchumi hizo fidia kulipika kwa kiasi na muundo ulioamuliwa. Hata hivyo, bado Ujerumani alilazimishwa kulipa.

Clearly, unaweza kuona kwamba , Germany alilipia kabisa uovu wake hata katika muktadha wa kiroho.

Pamoja na kunyang'anywa kila kitu, Ujerumani walianza upya manufacturing technology yao from scratch, na hadi mwanzoni mwa miaka ya 70, West Germany ilikuwa tena on top in engineering technology, hali iliyosababisha hata watesi wao waanze tena kuiba Germany technology.
 
Tatu, Hitler na genge lake waliwaaminisha wajerumani kwamba wao ni super race duniani, kwahiyo, wao wanapaswa kutawala na sio kutawaliwa na yeyote yule duniani.
I think this guy was trying to instill patriotic mindset kwa wananchi wake. Huu ni uzalendo sana kwa kiongozi...
 
Nitatoa jibu langu kutoka kwenye perspective ya Biblia Takatifu. Ulimwengu wa roho una kitu kinaitwa madai ambayo lazima yalipwe ili hali fulani mbaya inayokabili mtu/ ukoo/ kabila/ nchi itulie. Sio kila uovu unatoka kwa kukemewa kwa jina au damu ya Yesu.

Kwa mfano kama ukoo wenu ulikuwa na miungu yake na mkaiacha kienyeji bila utaratibu sahihi wa kiroho kufuatwa, hiyo miungu ya ukoo itainua madai kwenye ulimwengu wa roho dhidi ya wanaukoo huo na madai hayo ni sahihi katika muktadha wa kiroho. Ikumbukwe kuwa ancestors wa ukoo huo walijikabidhi kwa hiari kwa miungu hiyo, hali ambayo iliunda agano halali la kiroho katika ulimwengu wa roho. Kwahiyo, ili kujiachanisha na miungu hiyo, kuna utaratibu wa kiroho lazima uufuate kwa usahihi kabisa, na ukikosea hata kama wewe ni mlokole kindakindaki, huwezi kujitoa katika vifungo au laana za miungu hiyo. Lazima uingie deep kwenye ulimwengu wa roho ujue tatizo lilipo ili ujue sehemu sahihi ya kupeleka damu ya Yesu kwa ajili ya kulipa fidia ya kukukomboa (ransom) kutoka kwa miungu hiyo na laana zote.

Kwenye agano la kale, wayahudi ndio taifa pekee ambalo lilikuwa na agano na Mungu wa mbinguni, agano ambalo lilikuwa na kifungo cha kiroho tangu Ibrahimu. Kila wakati walipomwasi Mungu walipata adhabu kali kwa kulivunja agano lao na Mungu. Mfano Mungu aliwauza wayahudi kwa falme za Babeli, Uajemi, na Rumi walipomwasi Mungu.

Hii vita ya kiroho ya maagano ya kimungu iko very perfectly principled, bila kujali wazee wako walikuwa wakimuabu mungu yupi! Hoja ya msingi ni kwamba lazima agano lolote la kimungu cha shetani livunjwe kwa utaratibu sahihi wa kiroho na kulipa fidia sahihi kwa miungu unayotaka kuachana nayo kabla ya kuambatana na Mungu wa mbinguni. Walokole wengi wameshindwa kutegua huu mtego wa shetani, kwani wengi wao wanadhani kila roho ya shetani inatolewa kwa kukemewa kwa jina la Yesu, kumbe roho nyingine zinatolewa kwa kulipwa fidia kwanza.

Sasa tuje kwa Germany. Kama unasoma historia vizuri na kwa umakini, utagundua kwamba vita kuu ya pili ya dunia ambayo wajerumani waliianzisha, imechochewa na mambo makuu matatu.

Moja, ni dhuluma waliyofanyiwa na Uingereza na washirika wake wakati wa vita vya kwanza vya dunia, ambapo Ujerumani alilazimika kupigana ili kulinda maslahi yake Ulaya na duniani baada ya kupata mbinyo mkubwa kutoka Uingereza. Uingereza alikuwa na hofu kwamba masive expansion ya Germany ilikuwa inahatarisha usitawi wa maslahi yake duniani. Kwahiyo, ikabidi ianzishwe conspiracy ya kumdhibiti Germany mapema. Ndiyo vita ya kwanza ya dunia ikaanza, ambapo Germany alishindwa na kunyang'anywa makoloni yake yote, ikiwemo Tanganyika, Rwanda na Burundi. Kwahiyo, Germany ni kama alikatwa miguu yote miwili, kwahiyo ilibidi lazima apigane ili arudi kwenye chati tena.

Pili, Wajerumani walikuwa na chuki na wayahudi kwani walikuwa wamehodhi uchumi wao kwa kiasi kikubwa. Mbaya zaidi, wayahudi ni wabinafsi kwa asili yao, hali iliyowafanya wayahudi wajione watumwa ndani ya nchi yao. Kwahiyo, Hitler alikuwa na ndoto kubwa kuwashughulukia jews for that reason. Hata mauaji ya kimbari ya wayahudi wakati wa second world war, yalichochewa na chuki hii ya wajerumani kwa wayahudi.

Tatu, Hitler na genge lake waliwaaminisha wajerumani kwamba wao ni super race duniani, kwahiyo, wao wanapaswa kutawala na sio kutawaliwa na yeyote yule duniani. Huu ulaghai wa Hitler ndio ulimfanya Hitler na genge lake wawe na adhma ya kutaka kuitawala dunia wakati wa vita vya pili vya dunia.

Aidha, baada ya vita vya pili vya dunia, Germany alishindwa tena, na kupewa adhabu kali sana na mataifa washirika waliokuwa upande wa ushindi yaani USA, USSR, Uingereza na Ufaransa. Kwanza miundombinu yake yote ya viwandani ilikuwa sehemu ya vitu vilivyoporwa na mataifa hayo baada ya vita. Vilevile, wanasayansi wabobezi wa Ujerumani katika nyanja zote walichukuliwa mateka na mataifa yaliyoshinda vita. Ikumbukwe kuwa technology ya Ujerumani katika mambo kama silaha, ndege za kivita, U-Boats ili kuzamisha meli na nyambizi za Uingereza, na techhnology za uzalishsji mali kama viwanda zilikuwa tayari ziko juu sana kwa quality kipindi hicho. Pia Ujerumani iligawanywa vipande viwili: East Getmany na West Germany, na kuasisi vita mpya ya dunia iitwayo Cold War. Vilevile, Ujerumani alilazimishwa kulipa fidia kwa nchi zote ambazo zilikuwa wahanga wa vita aliyoianzisha.

Ukisoma Daniel sura ya 9 na Maombolezo 5:7, utaona uovu na dhambi lazima vilipiwe ili kukomesha laana. Kwa kutazama adhabu alizopewa Ujerumani baada ya WW2, ni dhahiri kabisa kwamba alilipia uovu wake wote kwa zile adhabu alizopewa na mataifa washindi. Ukiisoma torati ya Musa utaona kwamba torati iliamuru kwamba aliyeua lazima naye auawe ili nchi isiinue uovu na laana. Ingawa sheria hii Yesu alikuja kuiondoa na badala akaleta sheria mpya ya rehema, toba, na kusameheana kupitia Agano Jipya la Kuokolewa kwa neema kupitia kwa Damu ya Yesu. Sina ushahidi wa dhahiri kwamba Wajerumani walitubia uovu wao wa WW2. Ila nnachojua ni kwamba waliadhibiwa sana kwa kusababisha vita ile.

Kwahiyo, kwa sheria ya kiroho, ni vigumu mno kuamini kwamba Ujerumani alipaswa kupata laana zaidi ya hizo adhabu alizopewa na nchi zilizoshinda vita, kwani hata mateka wao wa vita wengi wao waliishia kuuawawa na kuzikwa ugenini bila hata ndugu kujua marehemu wao walipo.

Mchumi mashuhuri wa Uingereza, John Maynard Keynes, alivyo-review paper inayohusu financial repation ambazo Germany alipaswa kulipa kama fidia, aliikataa kabisa hiyo paper kwani ilikuwa haiwezekani katika parameter za kiuchumi hizo fidia kulipika kwa kiasi na muundo ulioamuliwa. Hata hivyo, bado Ujerumani alilazimishwa kulipa.

Clearly, unaweza kuona kwamba , Germany alilipia kabisa uovu wake hata katika muktadha wa kiroho.

Pamoja na kunyang'anywa kila kitu, Ujerumani walianza upya manufacturing technology yao from scratch, na hadi mwanzoni mwa miaka ya 70, West Germany ilikuwa tena on top in engineering trchnology, hali iliyosababisha hata watesi wao waanze tena kuiba Germany technology.
Madini mazito sana haya kaka mkubwa.
 
Ulimwengu wa roho una kitu kinaitwa madai ambayo lazima yalipwe ili hali fulani mbaya inayokabili mtu/ ukoo/ kabila/ nchi itulie. Sio kila uovu unatoka kwa kukemewa kwa jina au damu ya Yesu.
asante mkuu...
 
Mdogoangu aliyehesabu hizo maiti milioni6, specifically za Jews ni nani??

Wewe tuuzie tu vitabu vya kijerumani, propaganda zao za kibeberu achana nazo...

Kuanzia IBM, mpaka experiments za pharmaceuticals za uzazi wa mpango zilifaidika sana na hii vita..
A lot of scientific discovery na research zilifaidika kwa hili..

Ni sawa tu na twende DRC.

Everyday is Saturday............................ 😎
 
Kama hoja yako haitokani na porojo za ukiifanyia ubaya Israel unalaaniwa, suala lako la kwamba kuua roho za watu kunaleta laana umelitoa wapi?!

Kama hoja yako haitokani na porojo za Israel ni Taifa Teule, kwanini hukumtaja Stalin ambae anaaminika kuwa ndie ameua rohho nyingi zaidi pengine kuliko hata huyo Hitler?! Kwanini isiwe Wajapan ambao na wenyewe waliua mamilioni ya roho?! Kwanini wasiwe Wachina, hususani kipindi cha Mao ambao waliua mamilioni ya Wachina wenzao?
Mao The Don uyu ndo anaongoza 70+ million waliteketea

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Huchukua muda kidogo kwa mfano dola ya kirumi ilikuwa ndio yenye nguvu ikitawala dunia lakini baada ya askari wake wa kirumi kumuua Yesu dola ya kirumi ilisambaratika na sasa Italia ni kiinchi kidogi tu cha hovyo

Pili kuna mjerumani mtu wa Mungu Martini Luther aliyeanzisha imani ya kiprotestanti duniani kazi yake yaweza kuwa sababu ya ujerumani kutopigwa na laana hadi sasa
Ulutheri imo pote duniani
Roma ilianguka kwa sababu ilikwisha andikwa. Na siyo kwa sababu ya kumwua Yesu.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Kwa hapa sina comment kwa maana kila shetani ana mbuyu wake. Unayemuona hana maana kwako anaweza akawa ni mtu wa muhimu kwa mwingine...
Bwana mkubwa Mbowe kama unapita hapa nakuomba ikiwezekana tembea kwa magoti hadi chamwino ukaombe radhi kwa Rais Magufuli la sivyo mtakufa tu mtakuwa mmekaidi sauti ya Mungu.
 
Back
Top Bottom