SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #201
ANGA LA WASHENZI --- 09*
*Simulizi za series*
Fǎnzhèng wǒ yào tā sǐ!" (Nataka afe kwa njia yoyote ile!) Mwanaume mezani akasisitizia.
Mwanaume ndani ya suti akaitikia tena kwa kutikisa kichwa.
.
.
.
"Shì de xiānshēng!" (Ndio, mkuu!)
.
.
.
Haraka akatoka ndani ya chumba akiwa haamini kama ametoka na pumzi yake. Alihema kwanguvu jasho likimchuruza.
.
.
.
ENDELEA…
.
.
.
Aliendea gari lake akajiweka na kutoka ndani ya eneo hilo mpaka kwenye bangaloo iliyokuwa umbali wa kama kilomita tatu toka kwenye yale makazi alipofikishia taarifa.
Huko akakutana na wenzake wanne ambao alijumuika nao kwenye kunywa ulabu na kuvuta shisha iliyopo katikati ikiwa imezungukwa na kochi kubwa rangi nyekundu lililokuwa limejikunja kutengeneza umbo la ‘c’. Mwanaume mmoja alikuwa mwenye asili ya Uchina; nywele nyeusi, macho madogo na umbo dogo pia, alikuwa anajulikana kwa jina la Lee. Alikuwa mchangamfu na akiongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha kasoro tu lafudhi.
Wengine watatu walikuwa weusi ila wenye maumbo makubwa. Mmoja aliyekuwa amenyoa panki, pia akiwa na ndevu za duara, alikuwa anaitwa Mombo. Macho yake yalikuwa makubwa na sauti yake nzito.
Mwingine alikuwa ana nywele hafifu kichwani, vichengachenga vya ndevu vya hapa na pale kidevuni. Mdomo wake ulikuwa mpana, sauti yake ikikwaruza kana kwamba amekula chokaa. Jina lake Devi.
Wa mwisho yeye hakuwa na ndevu bali afro kubwa nyeusi ti! Alikuwa mwembamba mwenye macho mekundu malegevu. Mdomo wake mkavu mweusi kama kunguru. Aliitwa Nigaa. Alikuwa ndiye anayeshikilia bomba la shisha mara nyingi kuliko wenzake.
Walipeana salamu kwa kugusanisha mabega yao kabla mwanaume huyu aliyevalia suti nyeusi kuketi na kuanza kuwapasha wenzake habari namna mambo yalivyotukia. Kwenye haya maongezi, alitambulishwa kwa jina la Bigo.
.
.
“Una kazi nyepesi sana, Bigo,” akasema Devi na sauti yake inayotesa masikio. “Yani unahangaika na mchoraji?! Raha iliyoje. Si unammaliza ndani ya sekunde moja tu!”
Wenzake wakamuunga mkono.
.
.
“Yani kama ungeuawa kwasababu ya kushindwa kumuua mchoraji, kingekuwa ni kifo cha kizembe sana. Au una mpango wa kwenda mbinguni, Bigo?” Alisema Nigaa. Lee akaangua kicheko kikali wakati wenzake wakiishia kutabasamu.
Mchina huyu ungeweza kumdhania kama mtu mpole wa pendo, na asiye na tatizo na watu. Mkarimu, mtulivu na mwenye kupenda kufurahi. Ila kiuhalisia, hayo yote yangekuwa uongo kupitiliza.
Mwanaume huyu mwenye asili ya huko mashariki ya mbali mwa dunia, alikuwa ni miongoni mwa watu wauaji wakubwa kabisa kupata kutokea duniani. Alikuwa mkatili na mwenye upungufu wa huruma mwilini pindi awapo eneo la kazi.
Si tu kwa hapa Tanzania, bali hata huko kwao Uchina. Alishaua watu wengi kiasi kwamba hakumbuki tena idadi. Anaweza akamuua mtu lisaa limoja nyuma kisha akasahau hata uso wake!
Miaka ishirini na mitano huko nyuma, mchina huyu aliokotwa akiwa mdogo kabisa katikati ya jiji la Hongkong akiwa anazurura, hana makazi. Akalelewa katika familia ya Wu akichangamana na wenzake ambao nao pia waliokotwa ama kutekwa maeneo mbalimbali ya Uchina.
Takribani walikuwa mia mbili, wavulana kwa wasichana. Walihudumiwa vema kwa chakula na sehemu za kupumzikia. Ila walikuwa wanapewa mafunzo ya kupambana, mafunzo ya kufa ama kupona.
Walifundishwa namna ya kuua, na wakapandikiziwa roho mbaya ya unyama. Walifundwa kutokujali wala kutokuwa na rafiki. Ilipogundulikana mtoto mmoja ana urafiki na mwingine, basi alijaribiwa kwa kupewa pambano apambane na mwenzake mpaka pale kifo kitakapo watenganisha.
Japokuwa walikula na kulala mahali pazuri, mazoezi haya yaliwafanya wawe wapweke kwa muda mwingi. Kutokuwa na furaha, wala amani. Ila kwa upande wa familia ya Wu, hiyo ilikuwa sherehe kubwa.
Lengo lao lilikuwa linatimia. Walifanikiwa kuwaandaa watoto waliokuja kurithi mikoba ya wauaji waliosambaa ulimwenguni kote wakifanya hili ama lile kwa manufaa ya familia ya Wu.
Miongoni mwa watoto mia mbili, ni watoto thelathini tu ndiyo ambao walifanikiwa kukua na kuungana na jeshi, wengine wakienda na maji! Miongoni mwa watoto hao waliofanikiwa, alikuwa ni huyu Lee Sun. Mtambo wa mauti wa familia ya Wu.
Kabla hata hajaenda kwenye uwanja wa mapambano, huko ‘duniani’, alikuwa tayari ameshanyofoa uhai wa binadamu kumi na tano. Wote wakiwa watoto wenzake ndani ya mafunzo.
Kazi yake ya kwanza ilikuwa ndani ya jiji la Hongkong, baadaye Bangkok, Thailand na kisha Rabat, Morocco. Kote huko akifanya kazi moja tu, kuua pasipo mjadala. Alikuwa anakabidhiwa picha ya mlengwa na makazi yake, kisha yeye anaenda kumaliza kazi.
Baada ya mafanikio ya shughuli zake hizo, ndipo akahamishiwa Dar es salaam kuipa nguvu makao yao mapya yaliyoanza kumea ndani ya Afrika ya mashariki.
.
.
.
"Si kwamba nimeshindwa kumuua, ila majira ya kumuua. Unadhani ningemmaliza pale mgahawani polisi alipokuwapo ingekuaje?” aliuliza Bigo, kisha akaendeleza soga: “Hata tuseme ningemmaliza na polisi pia, huoni kama ingekuwa msala mkubwa – kuchoma utambi mapema hivyo?”
.
.
Lee akatikisa kichwa.
.
.
“Ndiyo maana umeachwa hai la sivyo ungeshakuwa historia sasa, Bigo. Ila ndani ya siku hizo mbili hakikisha unamaliza hiyo kazi. Kama utakwama, usisite kututaarifu. Twaweza kutoa msaada.”
.
.
“Msijali,” Bigo akasema akitikisa kichwa. “Ni kazi ya mkono mmoja tu, sidhani kama nahitaji mkono mwingine wa ziada.”
.
.
.
***
.
.
.
Kwa mujibu wa saa ya mkononi ya Jona, ilikuwa ni saa moja na dakika nane jioni. Kwa kiasi kikubwa alikuwa amesogeza kazi zake ‘lukuki’ na sasa alikuwa akifunga ajirudishe nyumbani kwa ajili ya mapumziko.
Jumanne alikuwa tayari ameshaondoka, hivyo alikuwa mwenyewe. Kwenye mkono wake wa kuume alikuwa amebebelea mfuko mweupe wa Rambo wenye chapa nyekundu, ndani ukiwa umejazwa na baadhi ya vitu.
Alipanda bodaboda, kama ilivyo kawaida yake mara kwa mara, akaenda moja kwa moja mpaka kwenye bar karibu na makazi yake alipojiweka na kuagiza kinywaji laini kisicho na kilevi.
Akiwa anangojea kinywaji, alichomoa simu yake mfukoni akaitazama. Kulikuwa kuna ujumbe kwenye mtandao wa Facebook toka kwa mwanamke fulani ambaye hakumtambua kwa haraka.
Mwanamke huyo alikuwa anampa salamu akiambatanisha na vimdoli vitatu vinavyotabasamu.
Kabla hajamjibu mwanamke huyo, akaenda kutembelea kwanza ‘profile’ yake. Kwa mujibu wa maelezo aliyoyakuta huko, mwanamke huyu alikuwa ni raia wa Afrika ya kusini. Mjasiriamali anayejihusisha na mauzo ya nguo akimiliki maduka kadhaa ndani ya jiji la Pretoria.
Hakufanikiwa kuona uso wake kwakuwa hakuwa ametuma picha yake hata moja, bali bidhaa zake anazoziuza. Kilichomfanya akajua kuwa ni mwanamke ni jina la mtu huyo na uchaguzi wa jinsia aliouteua kwenye ‘setting’ yake, ‘Female’. Akamjibu salamu yake kwa ufupi, kisha akaacha aone ni nini kitatokea. Punde kinywaji nacho kikaja akakinyaka na kuanza kunywa. Akaagiza pia na chakula ale hapo hapo ili amalize kila kitu kabla hajaenda zake nyumbani ambapo alilenga atajipumzisha moja kwa moja kutokana na uchovu aliokuwa nao.
Alikula na kunywa akisahau kabisa kuhusu simu. Alipomaliza akalipia chakula na kwenda zake nyumbani. Alioga kisha akaendea jokofu kuchomoa chupa kubwa ya kilevi na kuketi kitandani.
Hakuwa na mawazo mazito kichwani, alijitahidi kujipuuzisha. Alikunywa kileo chake taratibu macho yake yakiwanda wanda ndani ya nyumba yake pweke.
Haikupita muda mrefu, simu yake ikaita. Alikuwa ni mheshimiwa. Alisita kupokea akijiuliza. Ila akaamua kukata shauri na kuiweka sikioni.
.
.
“Kesho, majira ya saa tano asubuhi naomba tuonane nyumbani kwangu,” sauti ya mheshimiwa ilinguruma. Kabla Jona hajaongea, simu ikakata.
Jona akajikuta anatabasamu akitikisa kichwa chake. Akanywa mafundo matatu, kisha akajilaza kitandani.
.
.
“Mheshimiwa, bila shaka bado hatujafahamiana vizuri,” aliongea mwenyewe. “Tumeshayavulia nguo haya maji, hatuna budi kuyakoga.”
.
.
Kama maneno hayo angeliyasikia bwana Eliakimu Mtaja, basi bila shaka angezidi kuchochea hofu.
Kwa muda huu tu, akiwa ndani ya sebule yake mkononi akiwa amebebelea glasi yenye kiywaji chekundu, alikuwa tayari amepaliwa na mashaka.
Mkono wake uliobebelea kinywaji ulikuwa unatetemeka. Alikuwa ameubinua mdomowe kama upinde wa mshale. Uso wake ulikuwa mweusi, macho yake yakizama ndani ya fikira.
Pembeni yake alikuwa ameketi Nade akiwa amekunja nne, mapaja yake meupe yakiachwa wazi na kimini cheusi alichokuwa amevaa. Naye mkononi alikuwa amebebelea glasi kubwa ya kinywaji.
Mazingira yalikuwa tulivu.
Watu hawa wawili walikuwa wametekwa na mawazo. Walikuwa kimya ila sura zikiwa nzito. Kwa muda kidogo, tendo lililokuwa linafanyika ni kupeleka tu glasi ya kinywaji mdomoni kabla Nade hajauvunja ukimya kwa kuuliza:
.
.
“Kwahiyo sasa? – Kuna haja ya kummaliza?”
.
.
Mheshimiwa akashusha pumzi ndefu. Akanywa kwanza fundo moja.
.
.
“Hapana, Nade. Si haraka kiasi hiko.”
.
.
“Vipi sasa kama akiligundua ya chini ya zulia? Huoni tutakuwa tumeshachelewa?” Nade akauliza.
.
.
“Hapana,” mheshimiwa akajibu akitikisa kichwa. “Jona ni mtu mdogo sana kumhofia. Ataenda kush’taki wapi?”
“Mheshimiwa, ishu si wapi atashtakia, ila mambo yetu ya siri yataanza kuwa wazi. Inaweza ikakamata atensheni ya watu na mwishowe chombo kikaenda mrama. Tone moja la chumvi laweza kuharibu chakula.”
.
.
Mheshimiwa akanywa kwanza kinywaji. Fundo moja tena.
“Ila Nade, tukimmaliza sasa hivi, hatutampata Mariam. Tutampatia wapi yule mwanamke mzandiki? Mimi namhofia sana Mariam kuliko Jona. Mariam anajua vyetu vingi vya uvunguni.
Kadiri anavyoendelea kuwa mbali ya mikono yetu, ndivyo mambo yanavyozidi kuchacha. Mariam anajua mikataba, nyaraka, mipango, watu na mpaka washirika wangu.
Huko alipo hatujui anafanya nini, na yupo na nani. Nilitamani sana kumuagiza Jona ammalize mwanamke huyu pindi tu atakapomuona, ila niliona litazalisha maswali kichwani mwake.
Nakosa usingizi kumuwaza mwanamke huyu. Sina raha kabisa! Lengo langu la kwanza ni kumpata huyu mwanamke. Kuhusu Jona, sijali. Nataka tu kumtumia kwasababu najua ana uwezo wa kumpata huyo mwanamke.
Punde tu akapompata, ummalize upesi kabla hajaanza fyoko fyoko yoyote!”
.
.
“Mheshimiwa,” Nade akaita. “N’tajitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu, ila inabidi sasa niwe namfuatilia Jona kwa siri maana naona hatakuwa na mpango wa kunishirikisha kwenye mambo yake tangu aone namfuatilia kupitiliza.”
.
.
“Hakikisha haumtoi machoni mwako, sawa?”
.
.
“Bila shaka.”
.
.
Dakika tano mbele, mlango unagongwa. Mheshimiwa anatabasamu kidogo, ana habari na ujio huu. Anampa Nade ishara ya kichwa, Nade ananyanyuka na kuuendea mlango.
Mgeni alikuwa Miranda. Alikuwa amevalia koti dogo jeusi la ngozi, suruali ya jeans ya kumbana na viatu rangi ya kahawia vyenye visigino virefu.
.
.
.
.
*MIRANDA AMEKUJA KUFANYA NINI HAPA?*
.
.
*ANA MAHUSIANO GANI NA MHESHIMIWA?*
.
.
*NINI MHESHIMIWA NA NADE WANAFICHA?*
.
.
.
*JONA ANAFUATILIWA NA WATU WANGAPI SASA?*
.
.
.
*NANI ATAKUWA WA KWANZA KUZAMA KWENYE RADA ZAKE? – WAKINA MIRANDA, BIGO AMA NADE?*
*Simulizi za series*
Fǎnzhèng wǒ yào tā sǐ!" (Nataka afe kwa njia yoyote ile!) Mwanaume mezani akasisitizia.
Mwanaume ndani ya suti akaitikia tena kwa kutikisa kichwa.
.
.
.
"Shì de xiānshēng!" (Ndio, mkuu!)
.
.
.
Haraka akatoka ndani ya chumba akiwa haamini kama ametoka na pumzi yake. Alihema kwanguvu jasho likimchuruza.
.
.
.
ENDELEA…
.
.
.
Aliendea gari lake akajiweka na kutoka ndani ya eneo hilo mpaka kwenye bangaloo iliyokuwa umbali wa kama kilomita tatu toka kwenye yale makazi alipofikishia taarifa.
Huko akakutana na wenzake wanne ambao alijumuika nao kwenye kunywa ulabu na kuvuta shisha iliyopo katikati ikiwa imezungukwa na kochi kubwa rangi nyekundu lililokuwa limejikunja kutengeneza umbo la ‘c’. Mwanaume mmoja alikuwa mwenye asili ya Uchina; nywele nyeusi, macho madogo na umbo dogo pia, alikuwa anajulikana kwa jina la Lee. Alikuwa mchangamfu na akiongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha kasoro tu lafudhi.
Wengine watatu walikuwa weusi ila wenye maumbo makubwa. Mmoja aliyekuwa amenyoa panki, pia akiwa na ndevu za duara, alikuwa anaitwa Mombo. Macho yake yalikuwa makubwa na sauti yake nzito.
Mwingine alikuwa ana nywele hafifu kichwani, vichengachenga vya ndevu vya hapa na pale kidevuni. Mdomo wake ulikuwa mpana, sauti yake ikikwaruza kana kwamba amekula chokaa. Jina lake Devi.
Wa mwisho yeye hakuwa na ndevu bali afro kubwa nyeusi ti! Alikuwa mwembamba mwenye macho mekundu malegevu. Mdomo wake mkavu mweusi kama kunguru. Aliitwa Nigaa. Alikuwa ndiye anayeshikilia bomba la shisha mara nyingi kuliko wenzake.
Walipeana salamu kwa kugusanisha mabega yao kabla mwanaume huyu aliyevalia suti nyeusi kuketi na kuanza kuwapasha wenzake habari namna mambo yalivyotukia. Kwenye haya maongezi, alitambulishwa kwa jina la Bigo.
.
.
“Una kazi nyepesi sana, Bigo,” akasema Devi na sauti yake inayotesa masikio. “Yani unahangaika na mchoraji?! Raha iliyoje. Si unammaliza ndani ya sekunde moja tu!”
Wenzake wakamuunga mkono.
.
.
“Yani kama ungeuawa kwasababu ya kushindwa kumuua mchoraji, kingekuwa ni kifo cha kizembe sana. Au una mpango wa kwenda mbinguni, Bigo?” Alisema Nigaa. Lee akaangua kicheko kikali wakati wenzake wakiishia kutabasamu.
Mchina huyu ungeweza kumdhania kama mtu mpole wa pendo, na asiye na tatizo na watu. Mkarimu, mtulivu na mwenye kupenda kufurahi. Ila kiuhalisia, hayo yote yangekuwa uongo kupitiliza.
Mwanaume huyu mwenye asili ya huko mashariki ya mbali mwa dunia, alikuwa ni miongoni mwa watu wauaji wakubwa kabisa kupata kutokea duniani. Alikuwa mkatili na mwenye upungufu wa huruma mwilini pindi awapo eneo la kazi.
Si tu kwa hapa Tanzania, bali hata huko kwao Uchina. Alishaua watu wengi kiasi kwamba hakumbuki tena idadi. Anaweza akamuua mtu lisaa limoja nyuma kisha akasahau hata uso wake!
Miaka ishirini na mitano huko nyuma, mchina huyu aliokotwa akiwa mdogo kabisa katikati ya jiji la Hongkong akiwa anazurura, hana makazi. Akalelewa katika familia ya Wu akichangamana na wenzake ambao nao pia waliokotwa ama kutekwa maeneo mbalimbali ya Uchina.
Takribani walikuwa mia mbili, wavulana kwa wasichana. Walihudumiwa vema kwa chakula na sehemu za kupumzikia. Ila walikuwa wanapewa mafunzo ya kupambana, mafunzo ya kufa ama kupona.
Walifundishwa namna ya kuua, na wakapandikiziwa roho mbaya ya unyama. Walifundwa kutokujali wala kutokuwa na rafiki. Ilipogundulikana mtoto mmoja ana urafiki na mwingine, basi alijaribiwa kwa kupewa pambano apambane na mwenzake mpaka pale kifo kitakapo watenganisha.
Japokuwa walikula na kulala mahali pazuri, mazoezi haya yaliwafanya wawe wapweke kwa muda mwingi. Kutokuwa na furaha, wala amani. Ila kwa upande wa familia ya Wu, hiyo ilikuwa sherehe kubwa.
Lengo lao lilikuwa linatimia. Walifanikiwa kuwaandaa watoto waliokuja kurithi mikoba ya wauaji waliosambaa ulimwenguni kote wakifanya hili ama lile kwa manufaa ya familia ya Wu.
Miongoni mwa watoto mia mbili, ni watoto thelathini tu ndiyo ambao walifanikiwa kukua na kuungana na jeshi, wengine wakienda na maji! Miongoni mwa watoto hao waliofanikiwa, alikuwa ni huyu Lee Sun. Mtambo wa mauti wa familia ya Wu.
Kabla hata hajaenda kwenye uwanja wa mapambano, huko ‘duniani’, alikuwa tayari ameshanyofoa uhai wa binadamu kumi na tano. Wote wakiwa watoto wenzake ndani ya mafunzo.
Kazi yake ya kwanza ilikuwa ndani ya jiji la Hongkong, baadaye Bangkok, Thailand na kisha Rabat, Morocco. Kote huko akifanya kazi moja tu, kuua pasipo mjadala. Alikuwa anakabidhiwa picha ya mlengwa na makazi yake, kisha yeye anaenda kumaliza kazi.
Baada ya mafanikio ya shughuli zake hizo, ndipo akahamishiwa Dar es salaam kuipa nguvu makao yao mapya yaliyoanza kumea ndani ya Afrika ya mashariki.
.
.
.
"Si kwamba nimeshindwa kumuua, ila majira ya kumuua. Unadhani ningemmaliza pale mgahawani polisi alipokuwapo ingekuaje?” aliuliza Bigo, kisha akaendeleza soga: “Hata tuseme ningemmaliza na polisi pia, huoni kama ingekuwa msala mkubwa – kuchoma utambi mapema hivyo?”
.
.
Lee akatikisa kichwa.
.
.
“Ndiyo maana umeachwa hai la sivyo ungeshakuwa historia sasa, Bigo. Ila ndani ya siku hizo mbili hakikisha unamaliza hiyo kazi. Kama utakwama, usisite kututaarifu. Twaweza kutoa msaada.”
.
.
“Msijali,” Bigo akasema akitikisa kichwa. “Ni kazi ya mkono mmoja tu, sidhani kama nahitaji mkono mwingine wa ziada.”
.
.
.
***
.
.
.
Kwa mujibu wa saa ya mkononi ya Jona, ilikuwa ni saa moja na dakika nane jioni. Kwa kiasi kikubwa alikuwa amesogeza kazi zake ‘lukuki’ na sasa alikuwa akifunga ajirudishe nyumbani kwa ajili ya mapumziko.
Jumanne alikuwa tayari ameshaondoka, hivyo alikuwa mwenyewe. Kwenye mkono wake wa kuume alikuwa amebebelea mfuko mweupe wa Rambo wenye chapa nyekundu, ndani ukiwa umejazwa na baadhi ya vitu.
Alipanda bodaboda, kama ilivyo kawaida yake mara kwa mara, akaenda moja kwa moja mpaka kwenye bar karibu na makazi yake alipojiweka na kuagiza kinywaji laini kisicho na kilevi.
Akiwa anangojea kinywaji, alichomoa simu yake mfukoni akaitazama. Kulikuwa kuna ujumbe kwenye mtandao wa Facebook toka kwa mwanamke fulani ambaye hakumtambua kwa haraka.
Mwanamke huyo alikuwa anampa salamu akiambatanisha na vimdoli vitatu vinavyotabasamu.
Kabla hajamjibu mwanamke huyo, akaenda kutembelea kwanza ‘profile’ yake. Kwa mujibu wa maelezo aliyoyakuta huko, mwanamke huyu alikuwa ni raia wa Afrika ya kusini. Mjasiriamali anayejihusisha na mauzo ya nguo akimiliki maduka kadhaa ndani ya jiji la Pretoria.
Hakufanikiwa kuona uso wake kwakuwa hakuwa ametuma picha yake hata moja, bali bidhaa zake anazoziuza. Kilichomfanya akajua kuwa ni mwanamke ni jina la mtu huyo na uchaguzi wa jinsia aliouteua kwenye ‘setting’ yake, ‘Female’. Akamjibu salamu yake kwa ufupi, kisha akaacha aone ni nini kitatokea. Punde kinywaji nacho kikaja akakinyaka na kuanza kunywa. Akaagiza pia na chakula ale hapo hapo ili amalize kila kitu kabla hajaenda zake nyumbani ambapo alilenga atajipumzisha moja kwa moja kutokana na uchovu aliokuwa nao.
Alikula na kunywa akisahau kabisa kuhusu simu. Alipomaliza akalipia chakula na kwenda zake nyumbani. Alioga kisha akaendea jokofu kuchomoa chupa kubwa ya kilevi na kuketi kitandani.
Hakuwa na mawazo mazito kichwani, alijitahidi kujipuuzisha. Alikunywa kileo chake taratibu macho yake yakiwanda wanda ndani ya nyumba yake pweke.
Haikupita muda mrefu, simu yake ikaita. Alikuwa ni mheshimiwa. Alisita kupokea akijiuliza. Ila akaamua kukata shauri na kuiweka sikioni.
.
.
“Kesho, majira ya saa tano asubuhi naomba tuonane nyumbani kwangu,” sauti ya mheshimiwa ilinguruma. Kabla Jona hajaongea, simu ikakata.
Jona akajikuta anatabasamu akitikisa kichwa chake. Akanywa mafundo matatu, kisha akajilaza kitandani.
.
.
“Mheshimiwa, bila shaka bado hatujafahamiana vizuri,” aliongea mwenyewe. “Tumeshayavulia nguo haya maji, hatuna budi kuyakoga.”
.
.
Kama maneno hayo angeliyasikia bwana Eliakimu Mtaja, basi bila shaka angezidi kuchochea hofu.
Kwa muda huu tu, akiwa ndani ya sebule yake mkononi akiwa amebebelea glasi yenye kiywaji chekundu, alikuwa tayari amepaliwa na mashaka.
Mkono wake uliobebelea kinywaji ulikuwa unatetemeka. Alikuwa ameubinua mdomowe kama upinde wa mshale. Uso wake ulikuwa mweusi, macho yake yakizama ndani ya fikira.
Pembeni yake alikuwa ameketi Nade akiwa amekunja nne, mapaja yake meupe yakiachwa wazi na kimini cheusi alichokuwa amevaa. Naye mkononi alikuwa amebebelea glasi kubwa ya kinywaji.
Mazingira yalikuwa tulivu.
Watu hawa wawili walikuwa wametekwa na mawazo. Walikuwa kimya ila sura zikiwa nzito. Kwa muda kidogo, tendo lililokuwa linafanyika ni kupeleka tu glasi ya kinywaji mdomoni kabla Nade hajauvunja ukimya kwa kuuliza:
.
.
“Kwahiyo sasa? – Kuna haja ya kummaliza?”
.
.
Mheshimiwa akashusha pumzi ndefu. Akanywa kwanza fundo moja.
.
.
“Hapana, Nade. Si haraka kiasi hiko.”
.
.
“Vipi sasa kama akiligundua ya chini ya zulia? Huoni tutakuwa tumeshachelewa?” Nade akauliza.
.
.
“Hapana,” mheshimiwa akajibu akitikisa kichwa. “Jona ni mtu mdogo sana kumhofia. Ataenda kush’taki wapi?”
“Mheshimiwa, ishu si wapi atashtakia, ila mambo yetu ya siri yataanza kuwa wazi. Inaweza ikakamata atensheni ya watu na mwishowe chombo kikaenda mrama. Tone moja la chumvi laweza kuharibu chakula.”
.
.
Mheshimiwa akanywa kwanza kinywaji. Fundo moja tena.
“Ila Nade, tukimmaliza sasa hivi, hatutampata Mariam. Tutampatia wapi yule mwanamke mzandiki? Mimi namhofia sana Mariam kuliko Jona. Mariam anajua vyetu vingi vya uvunguni.
Kadiri anavyoendelea kuwa mbali ya mikono yetu, ndivyo mambo yanavyozidi kuchacha. Mariam anajua mikataba, nyaraka, mipango, watu na mpaka washirika wangu.
Huko alipo hatujui anafanya nini, na yupo na nani. Nilitamani sana kumuagiza Jona ammalize mwanamke huyu pindi tu atakapomuona, ila niliona litazalisha maswali kichwani mwake.
Nakosa usingizi kumuwaza mwanamke huyu. Sina raha kabisa! Lengo langu la kwanza ni kumpata huyu mwanamke. Kuhusu Jona, sijali. Nataka tu kumtumia kwasababu najua ana uwezo wa kumpata huyo mwanamke.
Punde tu akapompata, ummalize upesi kabla hajaanza fyoko fyoko yoyote!”
.
.
“Mheshimiwa,” Nade akaita. “N’tajitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu, ila inabidi sasa niwe namfuatilia Jona kwa siri maana naona hatakuwa na mpango wa kunishirikisha kwenye mambo yake tangu aone namfuatilia kupitiliza.”
.
.
“Hakikisha haumtoi machoni mwako, sawa?”
.
.
“Bila shaka.”
.
.
Dakika tano mbele, mlango unagongwa. Mheshimiwa anatabasamu kidogo, ana habari na ujio huu. Anampa Nade ishara ya kichwa, Nade ananyanyuka na kuuendea mlango.
Mgeni alikuwa Miranda. Alikuwa amevalia koti dogo jeusi la ngozi, suruali ya jeans ya kumbana na viatu rangi ya kahawia vyenye visigino virefu.
.
.
.
.
*MIRANDA AMEKUJA KUFANYA NINI HAPA?*
.
.
*ANA MAHUSIANO GANI NA MHESHIMIWA?*
.
.
*NINI MHESHIMIWA NA NADE WANAFICHA?*
.
.
.
*JONA ANAFUATILIWA NA WATU WANGAPI SASA?*
.
.
.
*NANI ATAKUWA WA KWANZA KUZAMA KWENYE RADA ZAKE? – WAKINA MIRANDA, BIGO AMA NADE?*