Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II ---- 77*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Alipomaliza kusema hayo, wakahisi boti inapepesuka. Wakatazamana pasipo kusema jambo. Pengine wakahisi ni pepo ama maji ya bahari. Ila hapana, boti ikapepesuka zaidi na zaidi! Mmoja akalazimika kwenda kutazama.


Ila alipoenda hakurejea ndani ya muda. Mwenzake, yule aliyekuwa karibu na usukani, akapata shaka. Kabla hajaenda kutazama huko nje, Wales akamsimamisha na kumwambia, “Be careful.”


ENDELEA


Mwanaume yule hakujali sana, akaenda zake huko nje na kumfanya Wales akae tenge kuskiza nini kitakachotokea. Alitamani kwenda lakini majeraha aliyonayo yasingemruhusu kufanya hivyo. Alitega sikio pasi na kusikia jambo. Ikapita dakika moja, akaamua kuita.


Kimya.


Hapa akapata sababu ya kuwa na shaka. Akajikongoja kusimama aende huko nje. Mkononi alikuwa na bunduki ya kumlinda dhidi ya shambulizi. Kufika huko nje hakuona mtu! Akastaajabu. Kugeuka akajikuta amekitwa nyuma ya shingo, akadondoka chini kuzirai! Hakupata hata wasaa wa kumwona aliyemshambulia.


Alikuwa ni Miranda.


“Mpo sawa?” mwanamke huyo akawauliza wale makomandoo waliokuwako ndani wakiwa wamefungwa. Akawafungulia toka kwenye kamba kuwaweka huru.


“Wewe ni nani?” komandoo mmoja akauliza.


“Msijali, mtanijua. Siko mwenyewe.”


Baada ya muda mfupi, Lee naye akiwa ametokea upande wa pili wa boti, akajiri akiwa amelowana chepechepe kama ilivyokuwa kwa Miranda. Watu hawa ndiyo walikuwa wakiwavutia wale watu kwenye maji na kuwamaliza. Naye akajitambulisha kwa jina tu.


“Nanyi mlikuwapo kwenye ndege?” akauliza Komandoo.


“Ndio, tulikuwamo pamoja kwenye ndege kabla ya kuanguka,” akajibu Miranda.


“Vipi kuhusu mheshimiwa? Yupo wapi?” akauliza Komandoo.


Miranda akanywesha sura yake akisema, “Bahati mbaya alifariki safarini.”


“Vipi mwili wake? - upo wapi?”


“Msijali, upo. Utakuja hapa muda si mrefu bila shaka.”


Makomandoo wakatazamana na mmoja kuuliza, “Utakujaje na umesema amefariki?”


“Kuna mtu atauleta,” akajibu Miranda na kuongezea, “Kuna mwenzetu yupo huko nje. Yeye atakuja nao.”


“Anafanya nini huko?” Komandoo akaulizia.


“Anamalizia kazi kabla hatujandoka,” akasema Lee.


Lakini ilikuwa inaleta mantiki kwa Jona kuwapo huko nje? Pengine waweza kuona hii ilikuwa ni fursa adhimu kwake kujiondokea pamoja na wenzake baada ya kushikilia boti hii, ila kinyume na hapo yupo kule kisiwani! Msituni!


Atapambana na wanaume wale sita wenye silaha na ujuzi wa hali ya juu yeye mwenyewe?


Dakika nane nyuma …


“Nendeni,” alisema Jona baada ya kuchomoza nyuso zao toka kwenye maji, yeye pamoja na wenzake. Macho yao yaliyokuwa mekundu kwasababu ya kula chumvi ya bahari yalikuwa yanawashuhudia wanaume wale watano wakiwa wanazama msituni kisiwani kwenda kuwatafuta.


“Twende wapi?” akauliza Lee wakimtazama Jona.


“Nendeni kwenye boti,” Jona akasema. “Mimi nitarudi kule kisiwani kukabiliana nao.”


“Mwenyewe?” Miranda akadakia.


“Ndio, mwenyewe. Kuna haja gani ya kwenda wote kama kazi inaweza kufanyika na mmoja wetu?” Jona akasema akiwatazama wenzake kwa macho ya uhakika.


“Una uhakika?” akauliza Miranda. Uso wake ulikuwa na mashaka.


“Ndio, nina uhakika. Ikipita dakika arobaini na tano sijafika, basi nyie nendeni.”


“Hatuwezi kwenda tukakuacha, Jona,” aliteta Miranda kisha akamshika Jona mkono na kumwambia, “Please, be safe.”


“I will be safe,” akasema Jona na kabla mtu mwingine hajaongeza neno lingine, mwanaume huyo akazamia kwenye maji asionekane ameelekea upande upi wa dunia. Basi Miranda na Lee wakafanya kama vile walivyoambiwa, wao waende botini. Jona yeye ataenda kukabiliana na wale wanaume walioenda kule msituni mpaka arudi na kitambulisho, gate-pass (kama itakuwapo) na chombo cha mawasiliano alichobebelea yule mkuu wa kikosi kilichokuja kumwokoa Wales.


Walijua mwanaume huyo alikuwa navyo kwani walishawafuatilia watu hao kwa muda fulani huko msituni. Yaani siri ilikuwa sirini. Wakati wanaume hao wakiwa wanajificha na kufanyia siri kwenye mashambulizi yao, na wao sirini walikuwa wanatazamwa ama kufuatwa!


Kifuani mwa mwanaume yule aliyekuwa kamanda mkuu wa wenzake, kulikuwa kunaning’inia karatasi fulani iliyokuwa ‘laminated’. kwenye karatasi hiyo kulikuwa na picha ndogo na pembeni ya picha hiyo taarifa kadhaa.


Ilikuwa ni jambo linaloleta maana masikioni kuona wakina Jona wanawinda namna ya mawasiliano ya mkuu huyu. Walijua watu hawa wametoka kutumwa na hivyo basi mawasiliano yao na makaoni huwa yenye nguvu na tija kuliko yale ya Wales. Walijua watu hawa watakuwa na cha ziada. Cha ziada ambacho kitawasaidia kuangusha ngome mbeleni.


Lakini wote twajua kuwa kupata vitu hivyo haitakuwa nyepesi. Tena ikifanywa na mtu mmoja ambaye silaha yake ni mikono pekee.



**



Alipochomoza toka kwenye maji alipanda haraka ardhini. Alikuwa kwenye ubavu wa magharibi wa kisiwa. Alitazama huku na kule kabla upesi hajakimbia na kuzamia kwenye miti.


Na basi akiwa amebeba tahadhari zote, akatazamia ardhi na kuona alichokuwa anakitaka baada ya hatua kadhaa, nacho si kingine bali alama za watu anaowatafuta. Majani yalikuwa yametawanyika mahali walipopita, na pengine ambapo hapakuwa na majani akaona nyayo za viatu.


Akafuatilia kwa muda wa dakika sita. Akajibana kwenye kwenye mti baada ya kusikia sauti ya wanaume wakiongea. Aliporusha macho yake, akaona watu wawili. Ni wale ambao walipewa kukagua upande wa magharibi.


Akaendelea kunyata kuwajongea. Ilikuwa ni hatari kwake kuwaonyesha alipo mapema maana walikuwa na silaha za moto, wangeweza kuzitumia kummaliza kabla hajatimiza adhma yake.


Basi alipoona sasa amekaribia vya kutosha, akanyanyua tawi moja la mti lililo kavu, lakini kabla hajamaliza kunyanyuka, tawi lile likameguka kuvunjika! Likatoa sauti iliyowashtua wanaume wale na kuangazia upande huo upesi!


Jona akatulia tuli nyuma ya mti akihema taratibu. Wanaume wale wakatazama eneo hilo kwa sekunde kadhaa. Na wasipuuzie jambo, wakatazamana na kupeana ishara ya kwenda kutazama kupata uhakiki. Taratibu wakajongea, ila ghafla wakasikia sauti ya kitu upande wao wa kushoto. Haraka wakageukia huko!


Kutazama wakaona ni kipande cha tawi la mti. Kilikuwa ni kipande ambacho Jona amekirusha. Kabla hawajarejewa na akili, Jona akawa ameshawafikia. Kurejesha nyuso zao kule walipokuwa wanaelekea, bunduki zikakamatwa na kuviringitwa duara kamili, mikono yao ikachina, sasa haraka silaha hizo zikavutwa pasipo kipingamizi.


Hawajakaa vema, silaha zao zikatumika kuwabondea vichwa na kuwaangusha chini wakiwa hawana fahamu. Jona akachojoa vyombo vyao vya mawasiliano na kuzihifadhi silaha zao kwa ajili ya matumizi ya baadae.


“ … thirteen … fourteen … Fifteen!” alisema Jona kisha akapiga ngumi kiganjani mwake. Mpaka muda huo alikuwa ametumia robo saa. Hivyo ana nusu saa tu kutimia dakika arobaini na tano za kumaliza kazi yake. Muda ambao amewaambia wenzake kuwa ukifika na bado hajarudi, basi wawashe boti kwenda zao.



**


“Sure? … ok, we’re coming!” alisema yule kamanda mkuu wa kikosi kisha akamtazama mwenzake aliyekuwa anashirikiana naye kwenye ukaguzi wa kisiwa eneo la katikati. “They’ve got them in the West!” akamwambia kisha akawasiliana na wale wengine wa upande wa Mashariki kuwa hawana haja ya kuendelea kusaka kwani watu wao wamepatikana.


Basi wakaanza funga safari kuelekea kule upande wa magharibi. Walikuwa wanatembea kasi wakiwasiliana. Baada ya dakika kama kumi na moja, wakawa wamefika upande huo wa magharibi wakiwa wote wanne.


“Hey, where exactly are you?” akauliza kamanda mkuu. Punde akajibiwa, akawatazama wenzake na kuwapa ishara ya kichwa kuwataka wasonge mbele zaidi. Wakasonga kwa dakika mbili. Ila ghafla kamanda akawataka wasimame kwani alihisi kitu! Wote wakasimama!


Kwa utulivu mkubwa akaskiza. Macho yake yalienda kushoto na kulia. Juu na chini. Hamaki! Akatokea Jona mbele yao toka nyuma ya mti mkubwa uliopo hatua nane tangu walipo.


Mwanaume huyo alikuwa amebebelea bunduki kwenye mikono yake yote miwili na tayari tunduze ameshawaelekezea maadui. Basi kamanda kuona vivyo, kabla Jona hajabinya vitufe vya bunduki, upesi mno akamkamata mmoja wa wenzake na kumweka mbele yake kujikinga.


Basi risasi zikanyesha haswa!! Ilikuwa ni ti!-ti!-ti!-ti!-ti!-ti!-ti!-ti! Wanaume wale wakizungu wote wakala za kutosha isipokuwa yule kamanda mkuu ambaye akiwa amejikinga, akawa anasonga kumfuata Jona.


Aliposonga karibu kidogo, akamrushia Jona mtu yule aliyekuwa anamkingia. Jona kumkwepa mtu huyo na kukaa vema, kamanda akawa ameshamfikia akatengulia bunduki zake kando. Akachomoa bunduki yake ndogo, ila Jona naye akawahi mkono wake na kuutengua, bunduki ikadondokea chini. Sasa wote wakawa hawana bunduki mikononi.


Wakatupiana mikono, ila wote wakafanya ustadi kujilinda. Wakakaa tenge kutazamana kana kwamba majogoo. Kamanda akauliza, “So you are the dangerous one?”


Jona hakujibu akamvamia. Alikuwa hana muda. Alikuwa anakimbizana na muda na mpaka muda huo alikuwa amebakiza dakika kumi na mbili tu.




**
Mkuu shkamoo
 
Miranda hawezi mwacha Jona porini tena kisiwa kigeni kabisa
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 78*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Wakatupiana mikono, ila wote wakafanya ustadi kujilinda. Wakakaa tenge kutazamana kana kwamba majogoo. Kamanda akauliza, “So you are the dangerous one?”


Jona hakujibu akamvamia. Alikuwa hana muda. Alikuwa anakimbizana na muda na mpaka muda huo alikuwa amebakiza dakika kumi na mbili tu.


ENDELEA


Wakatupiana makonde ya nguvu. Wote walikuwa wana nguvu za kupambana na ustadi wa aina yake. Ilikuwa ni mapambano ya mafahali wawili ambayo yaliumiza majani. Waliparangana kwa muda wa dakika kadhaa asionekane nani aliye mwamba. Wakasimama tena kutazamana.


“Anything left?” akauliza yule kamanda. Jona akatazamia muda. Sasa amebaki na dakika tano tu! Akapiga kelele kwanguvu na kumvamia kamanda kwa mashambulizi makali.


Kamanda akajizuiza, akatupa pia na yake, Jona akajikinga na upesi akambana kamanda miguu kumwangusha chini. Kabla kamanda hajafurukuta, Jona akawahi kunyanyua silaha na kumtwanga nayo risasi tatu kifuani! Kamanda akaenda na ubabe wake.


Jona akamkagua na kuchukua kila alichokiona kinastahili alafu akaanza kukimbia kwenda kuikuta boti waliyomo wenzake.


Kupiga hatua mbili, akadakwa mguu na kuanguka chini. Kumbe kulikuwa na adui mmoja aliyebakia na uhai. Aling’ang’ania mguu wa Jona na upesi akavuta silaha yake iliyokuwa pembeni apate kumuua, ila Jona kwa haraka akatumia mguu wake uliokuwa huru, akatengua mkono wa adui uliobebelea bunduki na kisha akammaliza mtu huyo kwa kummiminia risasi nne za uhakika.


Akanyanyuka na kuendelea kukimbia kwa kasi. Sasa alikuwa amebakiza dakika mbili tu kwenye muda wake. Hakutazama nyuma wala pembeni bali mbele aelekeapo!



**



“Tuondoke,” alisema Lee akimtazama Miranda aliyekuwa anaangalia msitu wa kisiwa.


“Hapana,” Miranda akatikisa kichwa. “Hatuwezi kuondoka tukamwacha.”


“Alisema ikifika daki ya arobaini na tano twende kama atakuwa hajafika,” Lee akakumbushia. Japo uso wake nao ulikuwa na huzuni kuyasema haya.


“Najua alisema hivyo, ila hatutaondoka pasipo yeye,” Miranda akasisitizia. Muda si mrefu macho yake yakaanza kujawa na machozi. Jicho lake la kushoto likadondosha maji.


“Najua atarudi,” akasema kwa sauti ya chini. Alikuwa anatazama miti kama vile mtu asomaye ramani. “Najua hatafia huko … atarudi tu.” akamtazama Lee na kumwambia, “Atarudi, si ndio?”


Lee akashusha pumzi ndefu. Akatazama saa ya mkono wake, ilikuwa ni dakika ya sitini sasa na Jona hajaonekana. Akakosa cha kusema.


“Atarudi, si ndio?” Miranda akauliza tena akiwa ameng’ata meno. “Na kama hatorudi, basi hapahapa nitawangoja waliomuua na kuwaadhibu.”


Wakakumbatiana Miranda akiegamisha kichwa chake kwenye bega la Lee. Machozi yaliendelea kumtoka. Hakuwa anataka kuamini kwamba msitu ule umemmeza Jona.


Basi punde wakiwa vivyo wamekumbatiana, wakasikia sauti, “Heey!”


Miranda akasema, “ni Jona!” akaangaza kule msituni na akamwona mwanaume akiwa anakuja akikimbia, mikononi mwake alikuwa amebebelea mwili wa Raisi. Akamtazama Lee kwa furaha kubwa na kumwambia tena. “Ni Jonaa!”


Basi wakaruka na kwenda kumlaki, Lee akapokea mwili wa Raisi na kuutanguliza botini. Miranda akafurahi sana kumwona Jona, hata akambusu mwanaume huyo shavuni na kumwambia, “Nilijua utarudi tu,” akasema akiwa na tabasamu pana. Akamkumbatia tena Jona kabla hawajakwenda botini.


“Umepata kitu?” Lee akamuuliza.


“Nimepata kila kitu,” Jona akajibu. “Sasa ni muda wa kwenda kumaliza kazi.”


Basi wakatia moto boti na kuondoka zao. Wakiwa njiani Jona akawasiliana na makao makuu na taarifa ikawa ni kwenda kwenye ‘bay’ kama ilivyokuwa awali. Huko watakutana na ‘helicopter’ ya kuwachukua na kuwarejesha makaoni.


Basi safari yao ikadumu kwa mwendo wa saa moja na nusu mpaka kufika ‘bay’ ya barafu kuu. Hapo kulikuwa na wanaume wawili ndani ya helicopter ambao walikuwa wanawangoja.


Basi kwakuwa haikutakiwa wanaume hao wagundue mapema kuwa si wenyewe waliokuja hapo, wakawataarifu kwa njia ya mawasiliano kuwa kuna majeruhi wa kuja kuwasaidia kuwabeba, hivyo waje kuwapatia mkono.


Wanaume wale wakashuka pasi na hiyana na kusonga kwenye boti. Tena walikuwa hawana hata silaha mikononi mwao. Wakajikuta wakiwekwa chini ya ulinzi na kuamriwa waanike mikono yao juu upesi! Kwa woga wakatii amri. Lee na Miranda wakawaswaga kwenda kwenye helicopter wakimwacha Jona peke yake na wale makomandoo.


“Nadhani sasa mtarudi nyumbani kupeleka mwili wa mheshimiwa. Sisi tunaenda England kumaliza mzizi wa yote haya,” Jona aliwaambia wale makomandoo, watatu kwa idadi, watano wakiwa waliuawa kule msituni.


“Tumekubaliana ataenda huko mmoja, na sisi wawili tutaongozana na nyinyi kwenda huko kupambana,” akasema yule kamanda wa kile kikosi cha makomandoo.


Basi kwakuwa tayari ndege yao iliyokuwa inawasiliana nayo ilikuwa njiani, wakawasiliana nayo kuwaelekeza walipo, kisha walipofanya hivyo makomandoo wawili wakaondoka na wakina Jona wakitumia ile helicopter waliyoiteka. Wakadaka anga kwenda kuwatafuta na kuwamaliza washenzi.



**



Saa tano asubuhi …



Baada ya mlango kufunguka, walitangulia wanaume wawili ambao ni wale waliokuwa madereva wa ile helicopter iliyotekwa. Wanaume hawa wazee waliokuwa wamevalia makoti meusi ya ngozi na jeans zilikoza kwa rangi ya bluu, walikuwa wamenyoosha mikono juu na nyuso zao zikiwa zimejawa na hofu.


Nyuma yao alikuwapo Jona na wenzake, Miranda, Lee na Makomandoo wawili. Basi wakaketi na Jona akawauliza wale mateka juu ya taarifa zao. Wakajitambulisha kuwa ni madereva waliokodiwa kwa ajili ya usafirishaji. Hakuna kingine wanachokijua.


Jona na wenzake wakafanya msako ndani ya makazi ya wanaume hao na wakabahatika kupata nyaraka na picha kadhaa ambazo zilithibitisha kuwa mateka walitoa taarifa za uongo. Walikuwa ni miongoni mwa wafanyakazi wa taasisi ya siri ya Uingereza, ila kwenye kitengo cha usafirishaji.


“So you were lying, unh?” Jona akamnyooshea mmoja wao tundu la bunduki kichwani. “So choose one, to speak or die?”


Mwanaume huyo akatetemeka kwa hofu. Jasho likamchuruza. Akabanwa na kigugumizi asijue nini aseme.


“I’m gonna count up to five seconds!” Jona akafoka kisha akafungua bunduki yake na kutoa risasi nne, akabakiza risasi moja tu ndani ya bunduki alafu akaifunga na kumwekea mateka wake kichwani.


“One …” Jona akahesabu kisha akafyatua kitufe cha bunduki. Bunduki ikalia kak! Kumaanisha imekosa risasi.


“Two …” akahesabu tena na kufyatua kitufe cha bunduki, bunduki ikalia kak! Kumaanisha imekosa tena tundu la risasi.


“Three! …” akahesabu tena na kufyatua kitufe. Tena, kak! Bunduki ikalalamika kwa kukosa risasi! Hapo mwanaume yule mateka akawa amelowana jasho ndembendembe. Alikuwa kwenye vuli la umauti. Pengine kwenye wakati mgumu zaidi tangu aingie duniani.


Jona aliposema “Four! …” kabla hajafyatua, mateka akapiga kelele, “I’ll speak! … damn! I’ll speak!”


Jona akafungua bunduki na kutazama, tundu lenye risasi ndilo lilikuwa limekaa tenge. Kwahiyo endapo angebonyeza kitufe basi mateka yule alikuwa anapasuliwa ubongo na kulazwa mfu!


“Okay, one after another,” akasema Jona akiketi. “Tell us about your boss.”


Mateka akamtazama na kumuuliza, “What do you want to know about him?”


“Important things,” akajibu Jona. “Let’s start with where he lives, where he likes to go and what he likes to do.”


Basi mateka akasema kila alichoulizwa, kwa ufasaha na kwa uoga. Ofisi za bosi ziko wapi, makazi yake yapo wapi na viwanja anavyopenda kutembelea. Pia pasipo kusahau nini huwa anapendelea kufanya.


Sasa Jona na wenzake wakawa wana kazi ya kuanza kusuka mipango ya kutekeleza na kumaliza. Ila Lee akapata wazo, akaita,


“Jona,” na kisha akasema kwa uhakika, “nadhani kuna mtu tunamhitaji kuturahisishia kazi yetu.”


“Nani huyo?” Jona akauliza.


“Mwanamke mmoja aitwa Glady,” Lee akajibu akimtazama Jona machoni.


“Glady? Ni nani huyo na atatufaa vipi?”



***
 
Back
Top Bottom